Timu ya Wataalam wa Wizara ya Nishati pamoja na TANESCO wakiongozwa na Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga imefanya ziara ya kukagua Ujenzi wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa MW 14 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Kagera.
Mradi huo wa Murongo Kikagati unatekelezwa mpakani mwa Nchi za Tanzania na Uganda katika Vijiji vya Murongo kwa upande wa Tanzania na Kikagati kwa Upande wa Uganda.
Akizungumzia maendeleo ya Mradi Huo, Mhandisi Luoga amesema kwamba Timu yake imeridhishwa na kasi ya Ujenzi wa Mradi husika "na Serikali ya Tanzania ipo tayari kutoa ushirikiano unaohitajika ili kuhakikisha mradi unakamilika kabla ya wakati"
Utekelezaji wa Mradi huo ulianza mwezi Oktoba 2017 na utarajiwa kukamilika Juni 2020.
Kamishna Luoga ambaye yupo katika ziara ya kikazi ya siku Tatu Mkoani Kagera ameongozana na Maafisa Waandamizi kutoka wizarani, Pascal Mduma na Suleiman Mtunzi.
Mradi huo wa Murongo Kikagati unatekelezwa mpakani mwa Nchi za Tanzania na Uganda katika Vijiji vya Murongo kwa upande wa Tanzania na Kikagati kwa Upande wa Uganda.
Akizungumzia maendeleo ya Mradi Huo, Mhandisi Luoga amesema kwamba Timu yake imeridhishwa na kasi ya Ujenzi wa Mradi husika "na Serikali ya Tanzania ipo tayari kutoa ushirikiano unaohitajika ili kuhakikisha mradi unakamilika kabla ya wakati"
Utekelezaji wa Mradi huo ulianza mwezi Oktoba 2017 na utarajiwa kukamilika Juni 2020.
Kamishna Luoga ambaye yupo katika ziara ya kikazi ya siku Tatu Mkoani Kagera ameongozana na Maafisa Waandamizi kutoka wizarani, Pascal Mduma na Suleiman Mtunzi.