Boniphace Kichonge
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 1,606
- 1,956
FEBRUARI 7 2020.
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kipande cha Dar es Salaam- Morogoro chenye urefu wa kilomita 300 umekamilika kwa asilimia 70.
Amesema hatua hiyo ni miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa bajeti ya Serikali iliyopitishwa na Bunge.
Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Februari 7, 2020 wakati akiahirisha mkutano wa 18 wa Bunge la 11 mjini Dodoma.
Amesema ujenzi kwa sehemu ya Morogoro – Makutupora (kilometa 422) unaendelea.
Ametaja mafanikio mengine kuwa ni kuendelea na ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa maji wa Julius Nyerere ambako kazi zilizokamilika ni pamoja na ujenzi wa daraja la muda, utafiti wa miamba na udongo na uchimbaji wa mtaro wa chini kwa chini wenye urefu wa mita 147.6.
Amebainisha kuwa Serikali imefanikiwa kuendeleza mradi wa umeme vijijini (REA), kwamba hadi Desemba 2019 vijiji 8,236 kati ya 12,268 vya Tanzania Bara vilikuwa vimeunganishwa na umeme, sawa na asilimia 67.1.
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kipande cha Dar es Salaam- Morogoro chenye urefu wa kilomita 300 umekamilika kwa asilimia 70.
Amesema hatua hiyo ni miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa bajeti ya Serikali iliyopitishwa na Bunge.
Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Februari 7, 2020 wakati akiahirisha mkutano wa 18 wa Bunge la 11 mjini Dodoma.
Amesema ujenzi kwa sehemu ya Morogoro – Makutupora (kilometa 422) unaendelea.
Ametaja mafanikio mengine kuwa ni kuendelea na ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa maji wa Julius Nyerere ambako kazi zilizokamilika ni pamoja na ujenzi wa daraja la muda, utafiti wa miamba na udongo na uchimbaji wa mtaro wa chini kwa chini wenye urefu wa mita 147.6.
Amebainisha kuwa Serikali imefanikiwa kuendeleza mradi wa umeme vijijini (REA), kwamba hadi Desemba 2019 vijiji 8,236 kati ya 12,268 vya Tanzania Bara vilikuwa vimeunganishwa na umeme, sawa na asilimia 67.1.