UJENZI na shilingi 252 bilioni

Sasa mlitaka madeni yasilipwe? hivi nyie watu vipi ? Halafu wakandarasi wangegoma mngemlaumu nani?

Umerukia treni kwa mbele, what does it take for someone to become a great thinker? Soma habari yote kwanza mkuu, vinginevyo kama kweli umesoma na bado unaleta post hii, moja kati ya yafuatayo au yote ni sahii.
1. Wewe ni gamba original na umekosa jibu
2. Wewe ni mtoto wa gamba na unamtetea mama/baba yako
3. Wewe ni mke/mme wa gamba na unamtetea mme/mke wako
4. Wewe ni mjukuu wa gamba na unamtetea babu/bibi yako
5. Wewe ni mamluki wa ile ndoa ya mseto kule zenji
****HATUKATAI MAWAZO YAKO, BILA KUJARI UBORA, UOZO AMA UTOTO ULIOJAA, HII NDIYO JF*******
 
kweli CCM kiboko, yaani wanalidanganya hadi Bunge? hawna hata aibu machoni?
 

Nakubaliana na wewe kua mfumo wa Nchi yetu unalinda maovu! Sasa Mh Zitto na na wengine wenye nafasi ya uongozi waangalie namna Ingine ya kuweza kutengeneza mfumo wa kuweza kuzibiti Haya mambo au kuwafikisha kwenye sheria! Kwasababu kutoa ripoti ni sawa lakini swali ni kwamba ripoti zitatolewa mpaka lini?
 
ahsante Mhe Zitto kwa taarifa mhimu sana haswa tunapoelekea 2015, hapo ni kutonesha tu watu hoi.
 

Anza kupiga kelele wewe uone Kama utasikika....! Zitto ajaribu kuangalia namna ingine pamoja na wenzake kuyashughulikia Haya mambo kisheria! Itafutwe mbinu ingine au mfumo mbadala wa kushughulikia Haya mambo! Lakini kuja na hizi ripoti kila Mara huku mafisadi wakiendelea kupeta tu hakusaidii kitu!
 
Sasa mlitaka madeni yasilipwe? hivi nyie watu vipi ? Halafu wakandarasi wangegoma mngemlaumu nani?

Sio unaandika porojo ili kuhakikisha hiyo buku 7 kama una uhakika wa kulipwa hao wakandarasi lete ushaidi humu. Pia kummbuka wanachoshitakiwa hawa mawaziri ni kulidanganya Bunge wewe unakuja na viroja humu.
 
Bongo kila kitu kinakanushwa tu kwa maslahi ya kisiasa.Hakuna uzalendo.Hata CAG?
Ngoja nizame kwenye kamusi nitafute maana ya "bongo-bongo land..."
 
Tatizo hili si la kwanza wala la pili, kuna viporo vingi kama hivi vimefichwa kwa jina la 'tume' n.k.
Wanoafanya hivi wanatujua vema Watanzania na wala hawana wasi wasi.
Matatizo yapo wapi?

1. MTAZAMO , kwa bahati mbaya taifa hili halina watu wa taaluma ya uandishi. Kila mmoja anaweza kuwa mwandishi.Habari hizi zilitakiwa ziandikwe kwa lugha rahisi na inayoeleweka kwa mwananchi.
Hakuna wa kufanya hilo, tuna reporters hatuna journalists. Pasco prove me right or wrong

2. Ujinga wa Wananchi.
a) Wananchi hasa wanachama wa CCM ni kikwazo katika kupata suluhu. Suala la linalogusa maisha yao watalifanya la kisiasa. Utawasikia wakiimba nyimbo za kubariki uozo huu, kwa bahati mbaya wao si sehemu ya mgao.Mwisho wa siku watalala kama nguruwe pale muhimbili, wakiamka na afadhali wanatudi kuisaga lami

b)Wananchi kudhani kazi yao imeisha baada ya uchaguzi na mbunge anakuwa kiongozi wa taifa na si wao.
Endapo wananchi wangesimama bila kujali itikadi za kisiasa leo kila jimbo lingemwita mbunge wake na kumwambia ima atoe majibu au atokomee kabisa wasimuone tena. Wananchi wa Tanzania uzezeta umetujaa

c)Sisi sote ni sehemu ya tatizo: Tunadhani kuwa mwenye uwezo ni Zitto au wapinzani.
Ukisoma maoni ya wengi wameacha sualalishughulikiwe na Bunge.

Hawa mawaziri ni wabunge na Wabunge wetu mnawajua viwango vyao, leo unamkabidhi nyani kesi ya tumbiri kula mahindi yako.Hawa walioshindwa kutetea Simcard. wazungumzie ulaji wao kweli!
i)Tuwasaidie wanaofichua maovu .kwa pamoja tutie shinikizo hadi wahusika wawajibishwe
ii)Tuwabane wabunge majimboni waache kutudanganya'wanaleta maendeleo', kodi zetu wanaziteteaje!
iii)Kuishinikiza serikali itupe majibu hela zimetoka kwa utaratibu gani, zimelipa madeni gani
 

Naomba tupitie hizi cli za video kwa mtililiko huu ili pia kuona nani ni mkweli katika hili:

1. HOJA ILIYOKUFA YA MH.ZITTO VS DR.MAGUFULI NA UPOTEVU WA TSH 252 BILION (SOURCE : YOUTUBE)

HOJA ILIYOKUFA YA MH.ZITTO VS DR.MAGUFULI NA UPOTEVU WA TSH 252 BILION - YouTube

2. WIZARA YA MAGUFULI YAMJIBU ZITTO KABWE(SOURCE:JF)

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UJENZI



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Yah: USAHIHI WA MATUMIZI YA KASMA MAALUM YAUJENZI WA MIRADI YA BARABARA NCHINI SHS. 252,975,000,000.00


Tarehe 22/08/2013, Wizara ya Ujenzi ilikutana na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwa ajili ya kujadili Hesabu zilizokaguliwa za Fungu 98 kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012. Kikao hicho kilifanyikia katika Ofisi Ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam chini ya Uenyekiti wa Mhe. Gaudence Cassian Kayombo Mbunge wa Mbinga Mashariki, ambaye alitoa maamuzi na maelekezo rasmi ya Kamati.

Katika kikao hicho hoja kadhaa zilijadiliwa ikiwamo hoja kuhusu Matumizi ya Kasma Maalun ya Ujenzi wa Miradi ya Barabara nchini ambayo ilitengewa kiasi cha Shs. 252,975,000,000.00.

Katibu Mkuu (Afisa Masuhuli) wa Wizara ya Ujenzi alikiarifu kikao hicho kuwa fedha za Mradi huo Maalum zilitumika kwa ajili ya kulipia madai ya Makandarasi na Wahandisi Washauri kwa miradi ya ujenzi wa barabara inayoendelea katika mipango na bajeti ya Serikali. Katika ujenzi wa barabara; jukumu la msingi kwa Wizara ni kulipa madai ya Makandarasi na Wahandisi Washauri.

Aidha, alifafanua kwamba Mradi huu umekuwa na matokeo mazuri kwani ulifanikisha shughuli za ujenzi wa barabara nchini. Afisa masuhuli aliendelea kufafanua kwamba mradi huu wa barabara haukuwa mradi kivuli bali ulikuwa ni mradi maalum kwa lengo la kufanikisha programu ya barabara na maendeleo ya wananchi kwa ujumla.

Tarehe 22/08/2013 na tarehe 23/08/2013 zimetolewa taarifa za upotoshaji na baadhi ya vyombo vya habari kuhusu ukweli wa suala hili ambapo baadhi ya vyombo hivyo vilinukuliwa kusema kuwa kumekuwepo na ufisadi, matumizi tata na ubadhirifu katika mradi huu.

Wizara inapenda kuudhibitishia umma kwamba katika utekelezaji wa mradi huu hapakuwepo na ufisadi, ubadhilifu, au matumizi tata.

Ukweli huu umethibitishwa kwa maandishi na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwamba hoja ya ukaguzi huu haikuhusu ubadhirifu au matumizi mabaya yoyote ya fedha bali ni suala la uandishi wa vitabu vya fedha uliohitaji kuboreshwa.

Wizara ya Ujenzi inapenda kutoa ufafanuzi huu na kuudhibitishia tena umma kwamba hakuna upotevu wowote wa fedha kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari vimetaka ieleweke.

Taarifa hii imetolewa na;


Balozi Herbert E. Mrango
KATIBU MKUU (AFISA MASUHULI)
WIZARA YA UJENZI


3. CAG AKANUSHA MADAI YA KUWEPO UFISADI KATIKA MRADI MAALUM WA WIZARA YA UJENZI (SOURCE: YOUTUBE & Michuzi)

CAG LUDOVICK UTOUH BIL.252/- ZA WIZARA YA UJENZI - DR.MAGUFULI ALISHUTUMIWA KUZITUMIA VIBAYA - YouTube

MICHUZI BLOG: CAG AKANUSHA MADAI YA KUWEPO UFISADI KATIKA MRADI MAALUM WIZARA YA UJENZI

4. MBOWE ALIPOMSIFU JK (SOURCE: YOUTUBE & JF)

Mbowe Clip - YouTube

5. CHEYO ALIPOISIFU WIZARA YA UJENZI (SOURCE: YOUTUBE & JF)

JOHN CHEYO AKIMSIFU DR.MAGUFULI - MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI - YouTube

6. MKOSAMALI AUNGA MKONO HOJA YA SERIKALI (SOURCE: YOUTUBE & JF)

MKOSAMALI AIPONGEZA BAJETI YA UJENZI NA KUUNGA MKONO HOJA - YouTube

Hizi clips zinasdambazwa sana humu JF????!!

Nawalkilisha
 

Kweli kabisa mkuu,

CAG kapiga siasa pia.Anasema hakuna ufisadi kwenye hili simply ameamua kutumia vizuri maana halisi ya neno ufisadi kupindisha ukweli wa makosa ya msingi kabisa juu ya jinsi fedha hizi zilivyoombwa na kuja kutumika (Misappropriation).

Ilipaswa waziri akubali haya makosa na watuambie kwanini watumie mbinu hiyo kuomba fedha Bungeni bila kusema wazi makusudi halisi ili wabunge wahoji vizuri.

CAG kanishangaza zaidi anasema ni makosa ya kiuhasibu tu!!!! Siasa hizi hadi kwa watu professional!! Waandishi wetu kama kawaida habari zao ni CAG awasafisha akina magufuli blah blah!!! Hakuna aliandika kwa kuchambua udhaifu wa wazi juu ya hili wanasubiri akina Zitto waandike makala kufafanua basi!!!

Swali la msingi madeni yametoka wapi while fedha za ujenzi wa barabara zote zilitengewa bajeti? Kama kulikuwa na madeni kwanini hakuomba fedha za hayo madeni ili bunge lihoji vizuri?
 
Kumbe kiwango cha ujinga wa wananchi wa Tanzania kinaweza kuwa kikubwa kuliko inavyodhaniwa!
 
Ungesoma hadi mwisho na kuelewa, sidhani kama ungeibuka na post ya hivi. Kuna tatizo.

Kwa fungu lenye kiasi kikubwa kama hicho cha Shs. 252 bilioni kwamba limepitishwa na Bunge makini bila ya kujua miradi husika iliyomo ndani ya fungu hilo ni jambo la kujiuliza.
 
Mkuu Nguruvi3, kusema Tanzania hatuna waandishi, sio kututendea haki, kwa sababu waandishi tupo, maripota pia wapo na maanalist pia wapo, ila tatizo ni level tuu!.

I can't prove you right or wrong kutokana na views zako kwa sababu huo ni mtazamo na its relative!.Kitu ambacho nakubaliana na wewe, Tanzania waandishi tupo ila level yetu na uwezo wa kuchanganua mambo mazito ni limited kwa sababu hatuna kada ya waandishi waliospecialize kwenye technical issues kama hizi.

Kwa miaka 4 mfulilizo, nimekuwa nikiwaletea humu ripoti za CAG ile siku zinatoka tuu!, lakini sii wengi wenye uwezo wa kuzisoma kuzielewa na kuzichambua ipasavyo, ndio itakuwa sisi waandishi?!. Angalia CNN, kukiwa na technical issues, wanamuita pro. Wakati wa vita vya Gulf, CNN walimuajiri retired joint chief of staff kuwa war commentator!.
Media yetu ipi ina jeuri ya kumuajiri Mboma, Sarakikya au Sayore?!.

Siku ya bajeti ambayo ni moja kwa Tanzania, Kenya na Uganda, soma magazeti ya Kenya na Uganda wanavyoripoti bajeti zao!. Hata Bajet yetu, inachambuliwa vizuri zaidi kwenye gazeti la The East Africa kuliko gazeti la Daily News!.

Ili tuwe na specialization, inabidi mtu aliyesoma uchumi to degree level, then akasoma journalism, then anakuwa na uwezo wa kuandika uchambuzi wa kina!.

Hili la kusema Tanzania hatuna hiki au kile sii haki, unamaanisha waandishi wote hawa humu Tanzania huwaoni?!. Hivi ni kweli wote tunaoandika hata humu tuu, wote ni maripota tuu?!, hakuna waandishi?!, au angalau hata wachambuzi?!.

Pasco



 
Mkuu Pasco , niseme nilitambua hili litaku provoke kidogo pengine kukukihiri. Tumekuwa tunajadiliana kuhusu hili si mara moja au mbili sometime tunakuwa page moja na wakati mwingine tofauti, jambo zuri ni kuwa huwa tuna hoja za kujenga.

Mwaka 2011 niliandika kuwa si lazima kuwa na mwandishi wa habari wa taaluma, kinachotakiwa ni mwandishi wa habari mwenye kuelewa(weledi) wa mambo. Huyu ataweza kujua habari gani ifafanuliwe na nani. Kilichopo ni maripota ambao hawajui right source za info. Journalist waliopo nao wameingia katika mkumbo wa sensational news badala ya kufanya 'analysis' kutafuta habari zaidi na kuziandika katika lugha nyepesi.
Ni kwasababu hizo wao hawaonekani, tunaona maripota

Kuna uwezekano kabisa wa vyombo kuajiri wataalam kama part time, kwamba kila anapohitajika analipwa.
Tatizo siyo kupata wenye taaluma, tatizo hao waliopo wanajiendeleza na kupanua wigo wao wa ufahamu?

Watanzania hasa vijana wana tatizo. Wao wanategemea kusoma ajira za magazetini.
Wanashindwa kuwa aggressive na wanadhani taaluma zao zinazungumza zenyewe.

Miaka ya 70 na 80 watu walikuwa wanatumiwa barua za scholarship kama wanataka.
Form 6 akimaliza tu ajira kabla ya kwenda chuo. Siku hizi mambo sivyo, competition ni kubwa sana tena yenye ''technical know who na si know how''

Unaweza kuwa na digriii zako za nguvu zenye GPA ya haja. Digrii hazizungumzi wala hazielezi wewe ni nani katika free market. Soko linatawali na wewe nina, una nini na unaleta nini mezani.
Soko la ajira ni biashara kwamba inabidi utangaze kama wanavyotangaza wafanyabiashara.

Katika upande wa journalism soko lipo huru na wazi kabisa. Wewe kama Engineer, Lawyer, Mchumi n.k. kwanini usijitolee muda wako kufanya kazi za kufafanua, kuandika kuhusu taaluma yako ukiomba msaada wa mwandishi mkongwe kuweka habari zako katika hali inayokubalika?

Katika soko overcrowded kama hili la leo nani atakuona kama hutafanya jitihada za kuonekana?



Atakayeona kitu ni PM.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…