Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Huyu kijana amegeuka kuwa hatari hapa mtaani ninapoishi. Mpaka sasa kuna ndoa kama saba hivi ambazo inaonekana jahazi linaelekea kuzama kutokana na ushushushu wa huyu kijana anayedai eti amejiajiri ili kujikimu na maisha.
Anachofanya ni kumfuatilia mume wa mtu ambaye anamhisi ni mkware, akishagundua ana nyumba ndogo mahali atahakikisha anajuana na hiyo nyumba ndogo ili apate taarifa za jamaa na ikiwezekana anampiga picha huyo nyumba ndogo kisha anamfuata mke wa jamaa na kujenga naye urafiki na wakizoeana anamweleza kwamba anayo siri kubwa na anaomba ahakikishiwe usalama wake.
Akihakikishiwa usalama wake anamuuliza mke wa muhusika, kama akimpa taarifa kuwa mumewe anayo nyumba ndogo pamoja na ushahidi atamlipa kiasi gani……………Mke akikubali dili, anamwaga siri zote pamoja na picha na details nyingi tu alizokusanya ili mke aweze kumulika mwizi.
Akishakabidhi ushahidi anakunja mkwanja wake kisha anasepa na kuacha timbwili nyuma………………Wanawake hapa mtaani wanampenda kweli na wanapeana namba zake za simu. Sasa hivi huyu kijana anatengezeza mkwanja ile mbaya. Ila nimesikia wanaume wanamuwinda ili wamfanyie kitu mbaya……………………..
Anachofanya ni kumfuatilia mume wa mtu ambaye anamhisi ni mkware, akishagundua ana nyumba ndogo mahali atahakikisha anajuana na hiyo nyumba ndogo ili apate taarifa za jamaa na ikiwezekana anampiga picha huyo nyumba ndogo kisha anamfuata mke wa jamaa na kujenga naye urafiki na wakizoeana anamweleza kwamba anayo siri kubwa na anaomba ahakikishiwe usalama wake.
Akihakikishiwa usalama wake anamuuliza mke wa muhusika, kama akimpa taarifa kuwa mumewe anayo nyumba ndogo pamoja na ushahidi atamlipa kiasi gani……………Mke akikubali dili, anamwaga siri zote pamoja na picha na details nyingi tu alizokusanya ili mke aweze kumulika mwizi.
Akishakabidhi ushahidi anakunja mkwanja wake kisha anasepa na kuacha timbwili nyuma………………Wanawake hapa mtaani wanampenda kweli na wanapeana namba zake za simu. Sasa hivi huyu kijana anatengezeza mkwanja ile mbaya. Ila nimesikia wanaume wanamuwinda ili wamfanyie kitu mbaya……………………..