Ujasiriamali gani huu wa kuvunja ndoa za watu……………………!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Huyu kijana amegeuka kuwa hatari hapa mtaani ninapoishi. Mpaka sasa kuna ndoa kama saba hivi ambazo inaonekana jahazi linaelekea kuzama kutokana na ushushushu wa huyu kijana anayedai eti amejiajiri ili kujikimu na maisha.

Anachofanya ni kumfuatilia mume wa mtu ambaye anamhisi ni mkware, akishagundua ana nyumba ndogo mahali atahakikisha anajuana na hiyo nyumba ndogo ili apate taarifa za jamaa na ikiwezekana anampiga picha huyo nyumba ndogo kisha anamfuata mke wa jamaa na kujenga naye urafiki na wakizoeana anamweleza kwamba anayo siri kubwa na anaomba ahakikishiwe usalama wake.

Akihakikishiwa usalama wake anamuuliza mke wa muhusika, kama akimpa taarifa kuwa mumewe anayo nyumba ndogo pamoja na ushahidi atamlipa kiasi gani……………Mke akikubali dili, anamwaga siri zote pamoja na picha na details nyingi tu alizokusanya ili mke aweze kumulika mwizi.

Akishakabidhi ushahidi anakunja mkwanja wake kisha anasepa na kuacha timbwili nyuma………………Wanawake hapa mtaani wanampenda kweli na wanapeana namba zake za simu. Sasa hivi huyu kijana anatengezeza mkwanja ile mbaya. Ila nimesikia wanaume wanamuwinda ili wamfanyie kitu mbaya……………………..
 
Huyo kuna kitu anatafuta huyo! Subiri uone!

Hiyo fani ni kama amesomea ni intelijensia wa nguvu ..............maana amenunua hata Bodaboda ili imrahisishiea misele yake ya kutaduta data za wanaume wanaosaliti ndoa zao apate kuishi................
 
Huyu kijana amegeuka kuwa hatari hapa mtaani ninapoishi. Mpaka sasa kuna ndoa kama saba hivi ambazo inaonekana jahazi linaelekea kuzama kutokana na ushushushu wa huyu kijana anayedai eti amejiajiri ili kujikimu na maisha.

Anachofanya ni kumfuatilia mume wa mtu ambaye anamhisi ni mkware, akishagundua ana nyumba ndogo mahali atahakikisha anajuana na hiyo nyumba ndogo ili apate taarifa za jamaa na ikiwezekana anampiga picha huyo nyumba ndogo kisha anamfuata mke wa jamaa na kujenga naye urafiki na wakizoeana anamweleza kwamba anayo siri kubwa na anaomba ahakikishiwe usalama wake.

Akihakikishiwa usalama wake anamuuliza mke wa muhusika, kama akimpa taarifa kuwa mumewe anayo nyumba ndogo pamoja na ushahidi atamlipa kiasi gani……………Mke akikubali dili, anamwaga siri zote pamoja na picha na details nyingi tu alizokusanya ili mke aweze kumulika mwizi.

Akishakabidhi ushahidi anakunja mkwanja wake kisha anasepa na kuacha timbwili nyuma………………Wanawake hapa mtaani wanampenda kweli na wanapeana namba zake za simu. Sasa hivi huyu kijana anatengezeza mkwanja ile mbaya. Ila nimesikia wanaume wanamuwinda ili wamfanyie kitu mbaya……………………..

Mtambuzi, mi nina mtazamo tofauti kidogo. Ingawa kazi yake inaleta majuto na kuhatarisha usalama wa ndoa, lakini pia nahisi kwa kiasi inaweza kusaidia kupunguza ukware wetu sisi vidume wenye kupenda nyumba ndogo.

Natafakari, labda huyo kijana angetusaidia na sisi wanaume kwa kutupigia uchunguzi wa kina kwa wake zetu ili tuwe na uhakika kuwa hatuibiwi! Mke wangu, kupitia kijana huyo akiwa na uhakika kuwa sina nyumba ndogo na mimi kupitia kwa huyo kijana kujihakikishia kuwa wife hagawi huoni hapo amani itatawala nyumbani? Au aanzishe kampuni kabisa tumlipe kuondoa ukware mtaani ambao ungeweza kutusababishia magonjwa, ugomvi na umaskini? Kuumbuliwa kwa kupenda nyumba ndogo si haki yangu ninayoistahili??! Just joking!!!
 
Mtambuzi, mi nina mtazamo tofauti kidogo. Ingawa kazi yake inaleta majuto na kuhatarisha usalama wa ndoa, lakini pia nahisi kwa kiasi inaweza kusaidia kupunguza ukware wetu sisi vidume wenye kupenda nyumba ndogo.

Natafakari, labda huyo kijana angetusaidia na sisi wanaume kwa kutupigia uchunguzi wa kina kwa wake zetu ili tuwe na uhakika kuwa hatuibiwi! Mke wangu, kupitia kijana huyo akiwa na uhakika kuwa sina nyumba ndogo na mimi kupitia kwa huyo kijana kujihakikishia kuwa wife hagawi huoni hapo amani itatawala nyumbani? Au aanzishe kampuni kabisa tumlipe kuondoa ukware mtaani ambao ungeweza kutusababishia magonjwa, ugomvi na umaskini? Kuumbuliwa kwa kupenda nyumba ndogo si haki yangu ninayoistahili??! Just joking!!!

Labda tumshauri awe anachunguza pande zote...........!
 
Huyu kijana soon tutamuona kwenye mitandao mbalimbali akiwa anachezewa na wahuni. Tabia ya ufitini ni mbaya sana.
Huyu kijana amegeuka kuwa hatari hapa mtaani ninapoishi. Mpaka sasa kuna ndoa kama saba hivi ambazo inaonekana jahazi linaelekea kuzama kutokana na ushushushu wa huyu kijana anayedai eti amejiajiri ili kujikimu na maisha.

Anachofanya ni kumfuatilia mume wa mtu ambaye anamhisi ni mkware, akishagundua ana nyumba ndogo mahali atahakikisha anajuana na hiyo nyumba ndogo ili apate taarifa za jamaa na ikiwezekana anampiga picha huyo nyumba ndogo kisha anamfuata mke wa jamaa na kujenga naye urafiki na wakizoeana anamweleza kwamba anayo siri kubwa na anaomba ahakikishiwe usalama wake.

Akihakikishiwa usalama wake anamuuliza mke wa muhusika, kama akimpa taarifa kuwa mumewe anayo nyumba ndogo pamoja na ushahidi atamlipa kiasi gani……………Mke akikubali dili, anamwaga siri zote pamoja na picha na details nyingi tu alizokusanya ili mke aweze kumulika mwizi.

Akishakabidhi ushahidi anakunja mkwanja wake kisha anasepa na kuacha timbwili nyuma………………Wanawake hapa mtaani wanampenda kweli na wanapeana namba zake za simu. Sasa hivi huyu kijana anatengezeza mkwanja ile mbaya. Ila nimesikia wanaume wanamuwinda ili wamfanyie kitu mbaya……………………..
 
Ggggrrrrhhh! Mbona kaniwahi huyu! Mi nataka nisajili kampuni kabisa ya cheaters hunters. Mbona hata ulaya zipo hizi dingi? Acheni ukware muwe na amani, usilaumu microscope kwa kukutwa na malaria! Tumia chandarua yenye ngao!
 
Afungue kampuni ili iwe biashara rasmi, Mtambuzi unaogopa kumulikwa?????

Hahahahaaaa
Wenzetu majuu walirasimisha hii biashara long time,wanaitwa 'private investigators' wana leseni kabisa.Hii njemba ifungue na ofisi kabisa,tena ngoja nimwambie mtambuzi anipe namba ya simu ya mbunifu huyu,kuna mtu anamendea mtu wangu wa karibu humu mmu.
 
Huyo Jamaa huwa anaweza kufuatilia wanawake na kukusanya data zao kama wana mafiga ya ziada pia?
 
Huyu mwanaume ana hatarii.... Ana hatari kwake mwenyewe na hata walomzunguka. Kakazana anatafuta taarifa za waume wanaotoka nje.... nani kamwambia wanawake hua hawatoki kabisa? Anatumia vigezo gani na inamhusu nini? Hata hio nyumba ndogo lazima itatoa details sababu wengi hawana busara na ujinga wake anaweza fikiria kuachika kwa nyumba ndogo ni gurantee ya yeye kuolewa. Huyo hafai kabisaa!
 
Ggggrrrrhhh! Mbona kaniwahi huyu! Mi nataka nisajili kampuni kabisa ya cheaters hunters. Mbona hata ulaya zipo hizi dingi? Acheni ukware muwe na amani, usilaumu microscope kwa kukutwa na malaria! Tumia chandarua yenye ngao!

Huyu mimi simfagilii, maana anafanya kama udaku................Kama ingekuwa anafanya hivyo baada ya kuombwa, basi isingekuwa ni jambo la kushangaza.................Lakini huyu anaangalia familia ambazo kipato kipo.........hasa kama mke anafanya kazi aua ni mjasiriamali, hapo anajua kuna dili.............lakini sisi ambao wake zetu ni wauza maandazi na chapati uswazi tumesalimika..............
 
Mtambuzi, mi nina mtazamo tofauti kidogo. Ingawa kazi yake inaleta majuto na kuhatarisha usalama wa ndoa, lakini pia nahisi kwa kiasi inaweza kusaidia kupunguza ukware wetu sisi vidume wenye kupenda nyumba ndogo.

Natafakari, labda huyo kijana angetusaidia na sisi wanaume kwa kutupigia uchunguzi wa kina kwa wake zetu ili tuwe na uhakika kuwa hatuibiwi! Mke wangu, kupitia kijana huyo akiwa na uhakika kuwa sina nyumba ndogo na mimi kupitia kwa huyo kijana kujihakikishia kuwa wife hagawi huoni hapo amani itatawala nyumbani? Au aanzishe kampuni kabisa tumlipe kuondoa ukware mtaani ambao ungeweza kutusababishia magonjwa, ugomvi na umaskini? Kuumbuliwa kwa kupenda nyumba ndogo si haki yangu ninayoistahili??! Just joking!!!

Kwamba itapunguza Ukware? hio ni kudanganyana HP.... Hio ndoa itavunjika.... ikiwezekana mwanaume ataoa tena na atacheat vile vile.... na kwa upande mwingine siamini kua ndoa zote ambazo anachonganisha kweli zavunjika. Ingekua anapeleleza wanawake na kupelekea waume zao sawa! Katka ndoa ambazo zipo hadi sasa ni aslimia zaidi ya 60 ambayo wake imewatokea kujua kua mume wake alichepuka/anachepuka nje ya ndoa.....
 
Huyu mwanaume ana hatarii.... Ana hatari kwake mwenyewe na hata walomzunguka. Kakazana anatafuta taarifa za waume wanaotoka nje.... nani kamwambia wanawake hua hawatoki kabisa? Anatumia vigezo gani na inamhusu nini? Hata hio nyumba ndogo lazima itatoa details sababu wengi hawana busara na ujinga wake anaweza fikiria kuachika kwa nyumba ndogo ni gurantee ya yeye kuolewa. Huyo hafai kabisaa!
Nakwambia Da' AshaDii huyu kijana kalizua balaa hapa mtaani wanume hawa amani na ndoa zaop zimeingia Kidamisi.........Hata zile ndoa zilizokuwa zikipigiwa mfano nazo zimetikiswa maana kidudu mtu keshatia fitna..........Hivi unaweza vipi kukanusha wakati kuna data zote.........Kuanzia picha za huyo hawara, na kama ulipaki gari eneo hilo, utakuta limefotolewa na kama uliwahi kumnunulia vitu mbalimbali zikiwemo samani za ndani kutoka home shopping centre wakati kwako una samani chakavu kutoka keko.................Lazima hapo timbwili liibuke.....................
 
Wenzetu majuu walirasimisha hii biashara long time,wanaitwa 'private investigators' wana leseni kabisa.Hii njemba ifungue na ofisi kabisa,tena ngoja nimwambie mtambuzi anipe namba ya simu ya mbunifu huyu,kuna mtu anamendea mtu wangu wa karibu humu mmu.

Huyu ni wa wanawake tu, wanaume hatuna nafasi.................!
 
Kwamba itapunguza Ukware? hio ni kudanganyana HP.... Hio ndoa itavunjika.... ikiwezekana mwanaume ataoa tena na atacheat vile vile.... na kwa upande mwingine siamini kua ndoa zote ambazo anachonganisha kweli zavunjika. Ingekua anapeleleza wanawake na kupelekea waume zao sawa! Katka ndoa ambazo zipo hadi sasa ni aslimia zaidi ya 60 ambayo wake imewatokea kujua kua mume wake alichepuka/anachepuka nje ya ndoa.....

Huyu aliangalia jinsia ambayo itapokea idea yake haraka...............wanaume huchukuwa muda kukubaliana na jambo lolote..............Hivi AshaDii kama anakujia mtu kama huyu na mapicha kibao ya hubby wako akijivinjari na nyumba ndogo..........utamsikiliza au utamtimua? (Siombei litokee hilo.........I am just thinking)
 
Huyu mwanaume ana hatarii.... Ana hatari kwake mwenyewe na hata walomzunguka. Kakazana anatafuta taarifa za waume wanaotoka nje.... nani kamwambia wanawake hua hawatoki kabisa? Anatumia vigezo gani na inamhusu nini? Hata hio nyumba ndogo lazima itatoa details sababu wengi hawana busara na ujinga wake anaweza fikiria kuachika kwa nyumba ndogo ni gurantee ya yeye kuolewa. Huyo hafai kabisaa!
Ukosefu wa ajira balaa...unatia kichefu chefu kweli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom