Msuruhishi
Senior Member
- Jun 18, 2008
- 103
- 38
Katika hotuba ya 'kuahirisha' kupitisha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini'u Waziri Mkuu Pinda alitumia lugha ambayo siyo yake tunayoifahamu; hasa pale alipozungumza kuhusu barua ya Jairo iliyoibuliwa na Mh. Beatrice Shelukindo. Kwa lugha rahisi, Waziri Mkuu alisema Katibu Mkuu Jairo ni wa kufukuzwa tu ila yeye hana madaraka na hilo. Alituaminisha kuwa kama Rais Kikwete 'asingekuwa hewani", njiani kwenda Sauzi, angempa taarifa tu na Raisi angetamka amri ya kumfuta kazi Jairo. Tukumbuke kuwa kabla ya kumteua Jairo kuwa Katibu Mkuu, Jairo huyo alikuwa mtu wa karibu sana na Rais huyo, kama Msaidizi wake mkuu katika Ofisi Binafsi (Private Office) ya Rais. Sasa Rais yuko njia panda. Amfukuze Jairo mtu wake wa karibu kiasi hicho? Asipomfukuza, Pinda atawaambia nini Watanzania?