Ujasiri wa Jakaya kikwete : Rais wa Tanzania.

Azimio Jipya

JF-Expert Member
Nov 27, 2007
3,362
1,131
Ujasiri na Uadilifu wa uongozi, Ungempelekea Rais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania Kuawachukulia hatua za dhati kabisa mafisadi waliokuwa wamewekwa hadharani na kufahamika waziwazi. Lakini akawa mnyonge, akasita na mdhaifu hadi sasa ameshindwa kuchukua hatua muafaka na sasa umoja wa kitaifa unayumba.

Jamii ya Watanzania ingehemuheshimu Kikwete na kumuenzi kama angechukua hatua hizo za dhati dhidi ya mafisadi na ingejisikia Upendo, Matumaini, kujaliwa na kuwa wamoja na kundeleza mshikamano wa Taifa jambo ambalo ni Mila na desturi ya watanzania, lakini sasa linahatarishwa na mafisadi na kulindana kwao kwa nguvu zote.

Umoja wa kitaifa ambao ungejijenga kwa Hatua za kuridhisha dhidi ya Ufisadi na suala lote la rushwa dhidi ya rasilimali za Taifa ungepelekea uimara na mshikamano wa kiutu, kibinaadamu ambao ndio Utanzania wenyewe!

Ndani ya Umoja huo, mshikamano huo, uzalendo huo, utanzania na utu wa kitaifa mgawanyiko wa KIDINI na KIKABILA ungetoka wapi?

Kwanini tunaelekeza nguvu zetu kwingine na si kwa mafisadi na mbinu zao chafu za kututenga kama jamii iliyoshikana ya Kitanzania kwa faida yao?

Watanzania tuamke tufumbue macho yetu, tutizame na kuona kinachotakiwa kuona... tuone kuwa UFISADI uliokomaa na kujisokota kwenye uongozi wetu ....Unatuyumbisha unhatarisha amani na kuligawa taifa.

Inabidi kuchukulia hatua jambo hili na wala si lingine. Tufanye hivyo sasa!!!
 
Kuwanadi watuhumiwa wa ufisadi ni ujasiri? kama ipo maana hiyo ndio inajenga matabaka ndani za jamii.
 
Huyu jamaa alikula kura yangu 2005, yaani najuta kumweka mtu wa aina hii. Lakini sikuwa na jinsi nilikuwa na fikira kama za huyu jamaa, watu walisema ana nguvu ya soda pale alipotembelea maliasili Temeke na kwawajibisha jamaa fulani. kumbe ilikuwa nguvu ya soda kweli.

Mwaka huu ndugu sidanganyiki kutenda dhambi ya aina hii
mtu asiyewajibika kwa nafasi yake. mwenye uwezo wa ku"hire" bila ku"fire" swahiba wa mafisadi
jamaa kapoteza kabisa credibility.
hana uadilifu wala mtizamo, ana sura nzuri lakini roho ya korosho ya kibaguzi
Kwa kifupi ana ngozi ya kondoo hali yeye ni mbwa mwitu.
 
Huyu jamaa alikula kura yangu 2005, yaani najuta kumweka mtu wa aina hii. Lakini sikuwa na jinsi nilikuwa na fikira kama za huyu jamaa, watu walisema ana nguvu ya soda pale alipotembelea maliasili Temeke na kwawajibisha jamaa fulani. kumbe ilikuwa nguvu ya soda kweli.

Mwaka huu ndugu sidanganyiki kutenda dhambi ya aina hii
mtu asiyewajibika kwa nafasi yake. mwenye uwezo wa ku"hire" bila ku"fire" swahiba wa mafisadi
jamaa kapoteza kabisa credibility.
hana uadilifu wala mtizamo, ana sura nzuri lakini roho ya korosho ya kibaguzi
Kwa kifupi ana ngozi ya kondoo hali yeye ni mbwa mwitu.
 
Ujasiri na Uadilifu wa uongozi, ungempelekea Rais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania Kuawachukulia hatua za dhati kabisa mafisadi waliokuwa wamewekwa hadharani na kufahamika waziwazi.

Jamii ya Watanzania ingeheshimu na kuenzi hatua hizo na kujisikia upendo, matumaini, kujaliwa na kuwa wamoja na kundeleza mshikamano wa Taifa jambo ambalo ni Mila na desturi ya watanzania.

Umoja wa kitaifa ambao ungejijenga kwa Hatua za kuridhisha dhidi ya Ufisadi na suala lote la rushwa dhidi ya rasilimali za Taifa ungepelekea uimara na mshikamano wa kiutu, kibinaadamu ambao ndio Utanzania wenyewe!

Ndani ya Umoja huo, mshikamano huo, uzalendo huo, utanzania na utu wa kitaifa mgawanyiko wa KIDINI na KIKABILA ungetoka wapi?

Sijakuelewa boss.

Kwani siku hizi uoga = ujasiri??
 
Sijakuelewa boss.

Kwani siku hizi uoga = ujasiri??

fail.jpg
 
Huyu jamaa alikula kura yangu 2005, yaani najuta kumweka mtu wa aina hii. Lakini sikuwa na jinsi nilikuwa na fikira kama za huyu jamaa, watu walisema ana nguvu ya soda pale alipotembelea maliasili Temeke na kwawajibisha jamaa fulani. kumbe ilikuwa nguvu ya soda kweli.

Mwaka huu ndugu sidanganyiki kutenda dhambi ya aina hii
mtu asiyewajibika kwa nafasi yake. mwenye uwezo wa ku"hire" bila ku"fire" swahiba wa mafisadi
jamaa kapoteza kabisa credibility.
hana uadilifu wala mtizamo, ana sura nzuri lakini roho ya korosho ya kibaguzi
Kwa kifupi ana ngozi ya kondoo hali yeye ni mbwa mwitu.

we ujui ulisemamalo,kura yako aijalishi k2 ni sawa sawa na,punje ya sukari kwenye gunia ccm itashinda tena kwa kishindo vuvuzela mkubwa we
 
Kuwanadi watuhumiwa wa ufisadi ni ujasiri? kama ipo maana hiyo ndio inajenga matabaka ndani za jamii.

Tz J,

Kuwanadi watuhumiwa wa ufisadi sio ujasiri, na sisemema Rais ni jasiri kwa hilo... kama unavyosema huo ni msingi wa Ufisadi unaopelekea MATABAKA NDANI YA JAMII kama udini, ukabila, matabaka kwenye huduma za elimu, huduma za tiba, huduma za haki nk... Na suluhu ya hili si waislam kupamabana na wakristu au kabila moja kupambana na lingine...vita vingeelekezwa kwa mafisadi!! Ni Ujinga kuwaacha wananawiri huku misikiti na makanisa yakiwa vitani...infact ni upuuzi!!
 
Ujasiri na Uadilifu wa uongozi, ungempelekea Rais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania Kuawachukulia hatua za dhati kabisa mafisadi waliokuwa wamewekwa hadharani na kufahamika waziwazi.

Jamii ya Watanzania ingeheshimu na kuenzi hatua hizo na kujisikia upendo, matumaini, kujaliwa na kuwa wamoja na kundeleza mshikamano wa Taifa jambo ambalo ni Mila na desturi ya watanzania.

Umoja wa kitaifa ambao ungejijenga kwa Hatua za kuridhisha dhidi ya Ufisadi na suala lote la rushwa dhidi ya rasilimali za Taifa ungepelekea uimara na mshikamano wa kiutu, kibinaadamu ambao ndio Utanzania wenyewe!

Ndani ya Umoja huo, mshikamano huo, uzalendo huo, utanzania na utu wa kitaifa mgawanyiko wa KIDINI na KIKABILA ungetoka wapi?


Naamini mwandishi anajaribu kuonyesha matumaini yetu ambayo hayakutimizwa. NI KWELI.

KUna wakati mgombea huyu alidai kisha kamata mali zao. leo hii hataji kama ni moja ya mafanikio yake. Bull shit, dog shit!
 
Sijakuelewa boss.

Kwani siku hizi uoga = ujasiri??

Mkuu

Naona umefanya mahesabu na jibu ....

Ni kweli kuwa Uoga ulitawala kushughulikia swala zima la ufisadi na hiyo sio quality sahihi ya uadalifu katika uogozi. Kiongozi muoga bila kujali chama anachotoka, kabila ua dini hataweza kushugulikaia ufisadi ambao ndo DONDA KUU la usatawi wa taifa hili kwa sasa. Ni ufisadi ulio msingi wa MGAWANYIKO MKUU TAIFA LA TANZANIA LINALOUPITIA TANGU UHURU WAKE!...Ni magawanyiko huo ambao sasa unatupatia vijimgawanyiko vidogovidogo vingi vya kidini, kikabila, kimadhehebu, rangi nk.

Kimahesabu umesema ni WOGA...

Lakini badala ya kuushugulikia woga wa viongozi wetu...Tunaacha wanachi wetu wanyukana na kuumizana kwenye kampeni zinazoendeshwa kidini, kikabila kifamilia nk!

Jibu la haya yote ni kushughulika udhaifu uliopelekea ufisadi kushamiri nchini vinginevyo ....Taifa halitabakia kwnye sifa ya uasisi wake!!
 
Huyu jamaa alikula kura yangu 2005, yaani najuta kumweka mtu wa aina hii. Lakini sikuwa na jinsi nilikuwa na fikira kama za huyu jamaa, watu walisema ana nguvu ya soda pale alipotembelea maliasili Temeke na kwawajibisha jamaa fulani. kumbe ilikuwa nguvu ya soda kweli.

Mwaka huu ndugu sidanganyiki kutenda dhambi ya aina hii
mtu asiyewajibika kwa nafasi yake. mwenye uwezo wa ku"hire" bila ku"fire" swahiba wa mafisadi
jamaa kapoteza kabisa credibility.
hana uadilifu wala mtizamo, ana sura nzuri lakini roho ya korosho ya kibaguzi
Kwa kifupi ana ngozi ya kondoo hali yeye ni mbwa mwitu.

MTWA,

Hukujadili wala kujibi swali la msingi...

jipange tena na kelekeza hoja hapa!..

"Ndani ya Umoja huo, mshikamano huo, uzalendo huo, utanzania na utu wa kitaifa mgawanyiko wa KIDINI na KIKABILA ungetoka wapi?"

 
usiwe unaongea pumba..kikwete mwenyewe fisadi then atawafanya nini mafisadi wenzie????
wote tumeona anawanadi mafisadi theni wewe unatwambia nini hapo??
 
usiwe unaongea pumba..kikwete mwenyewe fisadi then atawafanya nini mafisadi wenzie????
wote tumeona anawanadi mafisadi theni wewe unatwambia nini hapo??

Paty read between the line;

Sijamsifu Kikwete.... Soma hapa ukiwa umetulia, ukimaanisha na usiwe una mumunya kitu mdomoni...

....Ujasiri na Uadilifu wa uongozi, ungempelekea Rais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania Kuawachukulia hatua za dhati kabisa mafisadi waliokuwa wamewekwa hadharani na kufahamika waziwazi



Kwa kutokuwa na Ujasiri na uadilifu ...that means alishindwa kuwachukulia hatua...matokeo? Nchi imegawanyika matabaka ya udini, ukanada, ukabila nk....

did you get ma point son?
 
Azimio na Bwanashamba hamna hadhi ya kuwa great thinkers. How did u get in here? Hoja za kitoto. Chakavu. Zilipauka.
Ndio Jk jasiri kwa:
1. Nawajua ila mawapa mda wajirekebishe
2. Hela za ali mashauri zinaliwa na wajanja
3. Ya lowasa ni ajari ya kisiasa
4. 30% ya budget huliwa na wajanja na mwaka huu tunategemea 33% kuliwa. (openin of Takukuru buildin)
5. Siitaj kura 350,000 zao
6. Sijui kwanin nchi hii maskin...
Yataka ujasiri kutamka haya kweli
 
Azimio na Bwanashamba hamna hadhi ya kuwa great thinkers. How did u get in here? Hoja za kitoto. Chakavu. Zilipauka.
Ndio Jk jasiri kwa:
1. Nawajua ila mawapa mda wajirekebishe
2. Hela za ali mashauri zinaliwa na wajanja
3. Ya lowasa ni ajari ya kisiasa
4. 30% ya budget huliwa na wajanja na mwaka huu tunategemea 33% kuliwa. (openin of Takukuru buildin)
5. Siitaj kura 350,000 zao
6. Sijui kwanin nchi hii maskin...
Yataka ujasiri kutamka haya kweli

Mheshimiwa soma post namba 17 Kwa kuelwa zaidi na nivizuri usome poast za wenzio pia.

Kiwete sio jasiri ndio maana kashindwa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi so? Udini na ukabila unashamiri!

Make no mistake... Am a serious and a noble Thinker!!!

That is why i real think we have only one major problem that of president failing to deal with Mafisadi and hence ...mgawanyiko mkubwa wa Kitabaka kwa Taifa zima sio kidini na kikabila tu! EVERYTHING...!! hali ambayo haijawahi kutokea tangu tupate uhuru...But Dr slaa kamaliza kila kitu leo... Kasema tena with details... atakavyo washughulikia mafisadi na kurudisha mshikamano na uzalendo wa nchi. That means hakuna haja ya kupigana kati ya muiskam na mkristu, kati ya kabila lako na langu...No tupigane na MAFISADI!
 
Mheshimiwa soma post namba 17 Kwa kuelwa zaidi na nivizuri usome poast za wenzio pia.

Kiwete sio jasiri ndio maana kashindwa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi so? Udini na ukabila unashamiri!

Make no mistake... Am a serious and a noble Thinker!!!

That is why i real think we have only one major problem that of president failing to deal with Mafisadi and hence ...mgawanyiko mkubwa wa Kitabaka kwa Taifa zima sio kidini na kikabila tu! EVERYTHING...!! hali ambayo haijawahi kutokea tangu tupate uhuru...But Dr slaa kamaliza kila kitu leo... Kasema tena with details... atakavyo washughulikia mafisadi na kurudisha mshikamano na uzalendo wa nchi. That means hakuna haja ya kupigana kati ya muiskam na mkristu, kati ya kabila lako na langu...No tupigane na MAFISADI!

Pole ndugu yangu. wewe mwenyewe umechemsha kuandika kichwa cha habari yako. ndo maana unaposema "Ujasiri wa Jakaya kikwete : Rais wa Tanzania" WATU WANAKUELEWA KUWA UNATAKA KUSEMA KUWA JAKAYA KIKWETE ANA UJASIRI.
 
Back
Top Bottom