Uhusiano wa Chagga na Kikuyu

Uhusiano wa Chagga na Kikuyu

Wewe unayesema hakuna kabila la Wachagga kwanza kabisa naamini wewe si Mchagga maana ungekuwa Mchagga usingeongea hivyo

Kwa kukusaidia tu ni kwamba Wachagga wanafanana kwa kila kitu, hiyo tofauti iliyopo ni maeneo tu wanayotoka lakini mambo mengine yote wanaenda sawa

Kwanza mila na desturi za Wachagga wote ni moja yaani kuanzia vyakula vya asili, vinywaji vya asili, majani na miti ya asili, uchumba, ndoa, uongozi, majina ya machifu, imani za kidini kila kitu ni kimoja

Pili Wachagga huwezi kuwatenganisha kwani muingiliano wao ni wa kindugu zaidi hapa namaanisha koo au familia za kichagga zinapatikana maeneo yote ya uchagga, kwa mfano utakuta Massawe anapatikana Rombo, Kilema, Kirua Vunjo, Old Moshi, Uru, Kibosho na Machame
Ukikuta Temba anapatikana KIbosho, Uru, Old Moshi, Marangu
Ukikuta Ngowi anapatikana, Kibosho, Uru, Old Moshi, Marangu, Rombo
Ukikuta Kimaro anapatikana Machame, Kibosho, Uru, Old Moshi, Marangu, Rombo
Sasa kwa akili yako watu hawa unawatofautisha vipi?

Yani unaanzaje kunishawishi kwamba Urassa aliyeko Machame na Urassa aliyeko Rombo sio ndugu, wakati hatujasikia Urassa aliyepo Tanga?

Pia Wachagga wanafahamiana, wanatambuana na wanafahamu kwamba wao ni wachagga na mtu ambaye si mchagga wanajua si mwenzao na wanamuita kyasaka au (mndu o nuka) wakimaanisha mtu wa porini, kwa mfano unaweza kuulizwa huyo mtu ni mchagga?, unasema ee ni mchagga kutoka Rombo au Uru au Sanya Juu, lakini kama si mchagga utasikia tu hapana si mchagga ni kyasaka yaani hatokei sehemu yoyote ya uchagga

Mfumo wa Umangi na lugha zote zinafanana ila kuna kuwepo utofauti mdogo unasababishwa na ule umbali wa kijiografia kutoka sehemu moja mpaka nyingine

Ni kawaida kutokea utofauti kidogo wa lugha pale jamii zinapokuwa zimegawanyika kiuongozi hata kama ni jamii moja

Naamini mpaka hapo nimekusaidia kwa kiasi kama unataka kufahamu zaidi vipo vitabu vingi sana vinavyowahusu Wachagga katika maktaba karibu zote za vyuo vikuu nchini upitie utafahamu zaidi

Kwa maelezo zaidi nifuate inbox

Karibu sana
Nilitaka niongee ila bandiko lako limetosha... kuna watu hawalitaki hili kabila ila ndo ivo lishakuwa bora hamna namna
 
Mm naona headline ina uhusiano mdogo sana na habari yenyewe
Kutokana na Ramani ya Afrika ku fitinishwa mwaka 1884-1885,kuna Fitna baridi iliwekwa makusudi ili kukidhi VIU vya maharamia waliohusika katika mambo hayo.

Bila kujijua na kuendelea kuabudu fikra za maharamia hao bado tunaendelea kufuata mipaka waliyotuwekea kwa sababu zao.

Kwa mfano wamakonde wapo Tz na pia wapo Mzqe Je mpaka pale ulitakiwa uwe wapi? Hata hili sakata la Ziwa nyasa chanzo ni kuendelea kuabudu mipaka iliyowekwa na wale wezi zama hizo.

Angalia wamasai wapo Kenya na wapo TZz, kama hiyo haitoshi cheki wajaluo:Wanyambo je? hawasikilizani na wanyarwanda na wabaganda? Pia waha na watu wa fasi ya Kongo kina papaa wanasikilizana bila shaka.Pande za Mkoa wa Rukwa na Zambia huelewana bila taabu.

Wameru wapo kenya na Tanzania na wanasikilizana vizuri sana WaChagga katika maongezi yao kuna vitu husikilizana na vichache hutofautiana kutokana na kwamba wewe ni Mchagga wa wapi,kwa mfanno mRombo au mMachame Vivyo hivyo wa KIkuyu ni jamii hii hii ya wa Chagga,mbali na lugha kuzikilizana hata mambo yao ya kiasili kwa mfano ndoa zao,taratibu za ndoa zao ni zilezile za wa Chagga jaribu kufuatilia Star Tv(kwenye kipindi cha bridal blah blah).

Je ni lini Afrika itaweka tofauti zao pembeni na kuamua kuungana kuwa nchi moja?
Search Results
View attachment 399322
Bob Marley- Africa Unite (live) - YouTube
 
Sijakataa kama hakuna watu wanaojiita/wanaoitwa Wachaga, usichanganye mambo ila nimepinga kama kama kuna ,,Kabila" la Wachaga, hayo ni mambo mawili tofauti, kusema Wachaga ni kama vile kusema Watanzania tafiti zote za Wazungu na Waafrika zinasema kuna Watanzania, lkn Je kuna kabila la Watanzania? Jibu ni hakuna, vivyo hivyo kwa wanoijiita Wachaga, Wanyamwezi au sijui Wahaya na wengineo wote hawa ni matokeo ya Ukoloni kabla ya Ukoloni wa Wazungu na Waarabu wengi wao wanaojiita Wachaga leo hawakujiita hivyo, vivyo hivyo Wanyamwezi kabla ya Biashara ya Utumwa kulikuwa hakuna watu walioitwa Wanyamwezi au sijui Wagogo, ndicho nilichomaanisha, hivyo narudi kwenye basics ni nini maana ya ,,Kabila" kwanza halafu ndiyo tuanzie hapo!

Sidhani kama nina cha kuzungumza na wewe unayetaka kuniaminisha kwamba Kimaro aliyeko Machame na Kimaro aliyeko Kibosho ni makabila tofauti, yani unataka kuniambia kwamba Massawe na Mushi walioko Machame, Kibosho, Uru, Old Moshi na Rombo ni makabila tofauti

Yani unataka kuniaminisha kwamba Assenga aliyeko Rombo Mashati na Assenga aliyeko Kibosho Kirima ni makabila mawili tofauti na ni jamii tofauti imetokea tu kama ajali wakakutana

Kwa maana nyingine unataka kuniambia kwamba Ngowi aliyeko Kibosho ni kabila lingine, halafu Ngowi aliyeko Uru ni kabila lingine, halafu Ngowi aliyeko Old Moshi ni kabila lingine, halafu Ngowi aliyeko Marangu ni kabila lingine

Au tuseme unataka kusema kwamba Lyimo aliyeko Uru sio ndugu na Lyimo aliyeko Old Moshi ambaye naye sio ndugu na Lyimo aliyeko Marangu
Au tuseme Njau wa Uru, Njau wa Old Moshi, Njau wa Marangu na Njau wa Rombo imetokea wamejikuta hivyo lakini ni watu ambao hawana undugu wowote ni makabila tofauti kabisa

Au unataka kusema Temba ya Mangare Kibosho, Temba ya Mangare Uru na Temba ya Mangare Old Moshi imetokea tu wote wakawa Temba halafu yote ikawa ya Mangare lakini hawana undugu wowote wala hawafahamiani yani ni ajali tu

Yani unamaanisha Urassa na Swai walioko Rombo ni tofauti na wale Urassa na Swai walioko Machame, au Moshi na Kiwelu waliopo Old Moshi ni tofauti na Moshi na Kiwelu waliopo Marangu japo hakuna Urassa na Swai waliopo Iringa

Aisee, nirudie kukwambia hakuna namna unaweza kuwatenganisha Wachagga, Wachagga wote ni ndugu wa damu na wanafanana kwa kila kitu, hayo unayong'ang'ania ni makabila yao sio bali ni maeneo wanayoishi tu
Wewe si mchagga na huwajui Wachagga, sisi Wachagga tunafahamiana vizuri na tunajua kwamba sisi ni ndugu wa damu na hakuna anayeweza kututenganisha, ni ndugu ambao waliunda nchi moja, Taifa moja
 
Hongera mchaga, lakini urais mtausikilizia kwenye bomba!
Anayetawala biashara na uchumi ndie anayetawala nchi, wachagga wametapakaa kila kona wakimiliki biashara ndogo (a. k. a duka la mchagga) hadi kubwa.
 
Kwa hiyo kwa maelezo yako unakubalina na mimi na kile ninachoamini siku zote kwamba HAKUNA kitu kama Kabila la Kichaga Dunia hii? Na badala yake kilichopo ni makundi mbalimbali ya watu yaliounganishwa na Wageni na hapa Wazungu kwa lengo la kututawala Waafrika?
Na hapa ni Tanzania nzima vivyo hivyo kama vile hakuna kitu kama Kabila la Wahaya au sijui Wasukuma au sijui Wanyakyusa wote hawa ni matokeo ya Ukoloni aidha Waarabu au Wazungu!
Siyo kuunganishwa na wazungu na waarabu ni chiefdoms za waafrika wenyewe kulikuwa na nyanyembe ,buhaya chiefdoms na wengineo waliojiunga wenyewe
 
Sina hakika saana, kama wana matatizo ya masikio,ila kazi ya masikio ni kusikia.(Unajua nini...Wa Rombo na Wakibosho hawasikilizani lakini wote wanajinasibu kuwa ni wachagga,,,lipi jema?Wote kuitwa Wameru ilhali hamsikilizani au muitwe majina tofauti na huku mwasikilizana?)
Wanasikilizana kwa asilimia 70
 
Ok. Jibu haya:-
1. Kichaga ni lahaja ipi?
2. Nani aliyesanifisha lahaja hiyo kuwa kichaga?
Tafuta kitabu kilichoandikwa na Chief Mareale. kinaitwa Mila na Desturi za Wachaga utapata jibu la chimbuko la wachaga
 
Kuwa kabila moja ni zaidi ya lugha.. kuna mila n.k...

Nadhani kila kabila kuna vikundi vidogovidogo ambavyo vinatenganishwa na Dialect... mfano wagogo kuna wanyambwa na wanyaogogo japokuwa wote wagogo ila kuna utofauti wa matamshi katika lugha hiyo ya kigogo ...

Angalia koo za kichagga utakuta Watu wanaitwa Mosha, massawe, Mmassy wapo kotekote kibosho, Machame au sehemu nyinginezo huku wakifanya mila ambazo hazitofautiani sanaa
 
Nashukuru umethibitisha utofauti uliopo na hivyo nahitimisha tu kuwa mko tofauti. Suala la msamiati kuingiliana ni la kawaida sana kwa watu walio majirani ambao lugha zao ni tofauti.

Ukisema mmetofautiana kwa sababu ya umbali kijiografia, haikubaliki kwa sababu zifuatazo:-

1. Wasukuma ni kabila kubwa kuliko wote tanzania. Wamesambaa mikoa kadhaa hapa nchini na walikuwa na utawala wa kichifu kama mlivyo watu wa kilimanjaro. Lkn msukuma wa shinyanga anaongea sawa tu na wa mwanza na wa geita na wa simiyu.

Iweje kaeneo kadogo kiasi hicho ndo kawe na tofauti ta lugha hadi kwa 80%?

2. Kabila la wanyamwezi kwa usiyejua utasema ni wasukuma, karibia kila kitu wanefanana lkn hawajiiti wasukuma bali wanajitambua ni wanyamwezi. Pia wanyantuzu japo wengine tunawaita ni wasukuma lkn wenyewe wanakataa. Iweje kwa watu wa moshi, hai, siha kaeneo kadogo tu?

Mko tofauti na mnajipambanua kwa lugha zenu. Na hamwezi kuongea lugha hadi ujue unaongea na wa wapi. Halafu wapo wanaojitwalia ukuu wa kichaga kuwa wao ndio wenyewe wengine mamluki. Na kila mmoja anamwita mwenzake wa kuja.

Utasikia mtu anatamba, mie wa old moshi ndo mchaga halisi, wengine wakuja tu.
 
Nashukuru umethibitisha utofauti uliopo na hivyo nahitimisha tu kuwa mko tofauti. Suala la msamiati kuingiliana ni la kawaida sana kwa watu walio majirani ambao lugha zao ni tofauti.

Ukisema mmetofautiana kwa sababu ya umbali kijiografia, haikubaliki kwa sababu zifuatazo:-

1. Wasukuma ni kabila kubwa kuliko wote tanzania. Wamesambaa mikoa kadhaa hapa nchini na walikuwa na utawala wa kichifu kama mlivyo watu wa kilimanjaro. Lkn msukuma wa shinyanga anaongea sawa tu na wa mwanza na wa geita na wa simiyu.

Iweje kaeneo kadogo kiasi hicho ndo kawe na tofauti ta lugha hadi kwa 80%?

2. Kabila la wanyamwezi kwa usiyejua utasema ni wasukuma, karibia kila kitu wanefanana lkn hawajiiti wasukuma bali wanajitambua ni wanyamwezi. Pia wanyantuzu japo wengine tunawaita ni wasukuma lkn wenyewe wanakataa. Iweje kwa watu wa moshi, hai, siha kaeneo kadogo tu?

Mko tofauti na mnajipambanua kwa lugha zenu. Na hamwezi kuongea lugha hadi ujue unaongea na wa wapi. Halafu wapo wanaojitwalia ukuu wa kichaga kuwa wao ndio wenyewe wengine mamluki. Na kila mmoja anamwita mwenzake wa kuja.

Utasikia mtu anatamba, mie wa old moshi ndo mchaga halisi, wengine wakuja tu.
 
Jibu kisha nipe reference ya kitabu hicho
Kifupi wachaga ni wahamiaji kama makabila mengine asili yao ni Ethiopia sehemu inaitwa wolo pia koo nyingine za wachaga asili yake ni wamasai,wakamba na kikuyu kutoka Kenya Wabondei n k kama ilivyo makabila yote ya Tz
 
Kifupi wachaga ni wahamiaji kama makabila mengine asili yao ni Ethiopia sehemu inaitwa wolo pia koo nyingine za wachaga asili yake ni wamasai,wakamba na kikuyu kutoka Kenya Wabondei n k kama ilivyo makabila yote ya Tz
Ref. Tafura hicho kitabu ukisome cha zamani sana sina uhakika uki google utakipata pengine tafuta encyclooedia nafikiri Britanica
 
Ref. Tafura hicho kitabu ukisome cha zamani sana sina uhakika uki google utakipata pengine tafuta encyclooedia nafikiri Britanica
Kifupi mimi ni mchaga na nimeshafuatilia asili yangu na ilikuwa rahisi sana baada ya kusoma hicho kitabu
 
Nikikutana na wachaga nawaambia live hakuna kabila la wachaga. Ila kuna machame, kibosho, uru, marangu n.k. na hakuna lugha ya kichaga daima
Yaani hakuna kabila linajulikana tanzania kama Wachaga. Duh hadi mnajua warombo, kibosho,machame. Utadhani lilishawahi kutoa Rais Wa nchi.
 
Yaani hakuna kabila linajulikana tanzania kama Wachaga. Duh hadi mnajua warombo, kibosho,machame. Utadhani lilishawahi kutoa Rais Wa nchi.
Rais hawezi kutoka si kwa wanaojiita wachaga tu bali kaskazini nzima haitakuwa na rais. Labda marais wa Civil Society's tu kama vyama vya siasa na NGO nyingine.

Wataishia kugombea tu. Maana wanaongoza kwa kutoa wagombea wengi zaidi wa urais kwa nchi hii
 
Naona kila nikijaribu kukueleza kwa hoja zenye mashiko na mifano hai jinsi gani Wachagga ni wamoja na huwezi kuwatenganisha wewe unaendele kuleta maneno ya mitaani

Labda nikusaidie ni kwamba Wachagga ni watu wenye asili ya mapinduzi na harakati, Wachagga kwa historia au hata ukijaribu ku-observe kwa makini ni jamii moja ila imekaa maeneo tofauti na mwanzo walikuwa na mtawala mmoja lakini kutokana na kutoridhishwa na baadhi ya maamuzi ya uongozi yalianza kutokea mapinduzi mbalimbali yaliyozaa kingdom ndogo ndogo ambazo ndio zilileta huo utofauti unaouona

Lakini hata hivyo baadaye baada ya kuishi karne kadhaa wakiwa wamegawanyika kwa kingdom ndogo ndogo wali-reunite na kurudi tena kuwa Kingdom moja baada ya kutambua umuhimu wa kuwa Wamoja na ulifanyika uchaguzi wakaweza kuchagua kiongozi mkuu wa Wachagga wote kidemokrasia kabisa kabla nchi ya Tanganyika haijakuwepo
Kulikuwa kuna chama cha siasa kinaitwa Chagga Democratic Party

Wewe unasema Wachagga kama kabila hawapo, lakini research zote zinazofanyika zinahusu Wachagga, hata vitabu vilivyoandikwa na Wachagga wenyewe zamani vimeandikwa na Wachagga vinahusu Wachagga kama Wachagga

Mangi Petro Itosi Marealle mwaka 1946 aliandika kitabu "Maisha ya Mchagga Hapa Duniani na Ahera" huyo alikuwa ni Mangi Mwitori wa Vunjo, kungekuwa ni makabila tofauti angeandika Maisha ya Mmarangu lakini yeye anajua hakuna kitu kinaitwa Mmarangu bali kuna sehemu inayoitwa Marangu ambayo ni moja kati ya maeneo wanaoishi Wachagga

Katika kitabu chake Mangi Petro Itosi Marealle 1946 amezungumzia lifestyle ya Wachagga na kuelezea mila na desturi karibu zote za Wachagga kwa karne nyingi zilizopita na hakuna sehemu amesema Mkibosho alifanya vile au vile, amezungumzia Wachagga huku akijua Kibosho, Old Moshi au Machame ni moja kati ya maeneo wanayotokea Wachagga lakini sio jamii tofauti

Ukitaka kuwatofautisha Wachagga hutaweza, maana hauwatofautishiki na ni jamii ambayo ni ndugu wote wa moja kwa koo zao ziko maeneo yote ya Uchagga kitu ambacho kinaashiria ni Wamoja wanaoishi maeneo tofauti kwani hamuwezi wote mkaishi eneo moja litakalotajwa kwa jina moja

Hoja kwamba hawa wana tabia hii na wale wana tabia ile ni dhaifu sana kwani hakuna watu wanaowezakuishi kama jamii kukaacha kuwa na utofauti mdogo lakini kukawa na ufanano mkubwa, Wachagga ufanano mkubwa kuliko viutofauti vidogo, wote ni watafutaji, wote ni wapenda maendeleo na wote ni optimists sana, na wana-appreciate each other pale anapotokea mtu wa tofauti na wao
Mkuu hao wanatamani wachagga tusiwe wamoja lakini hawataweza.. Ukitoa tofauti ndogo sana iliyopo kwenye lugha zetu tamaduni na mila zetu wote ni zile zile, vyakula vya asili ni vile vile, pombe yetu ya asili ni ile ile.. Mfano; Mtoto wa kwanza wa kike katika familia ya Ngowi ataitwa Mangowi, wa pili wa kike ataitwa Manka na watatu na kuendelea wataitwa Kyekue. Na hiyo ni kwa wachagga wote, mipaka ya viamba pia ni Masale kwa wachagga wote. Hizi porojo zinapigwa na watu fulani kuaminisha wajinga kwamba wachagga ati hatupendani au si damu moja. Huo ni uzandiki tu na wivu wa kike..

Kabla ya Uhuru wa Tanganyika tayari wachagga tulikuwa na serikali yetu iliyotuunganisha, tulikuwa na bendera yetu na ofisi za serikali zilikuwa pale Moshi mjini..
 
Back
Top Bottom