Uhusiano wa Chagga na Kikuyu

Uhusiano wa Chagga na Kikuyu

Swali langu kwako, kwa nini Wameru hawaitwi Wachaga kama wanasikilizana na Wamachame ambao wanajiita Wachaga? Au kwa nini Wamachame hawasikilizani na Warombo au Wakibosho wakati wote wanaitwa/wanajiita Wachaga?
Kwa kifupi wameru wametokea uchagani walipohamia maeneo ya mlima meru inasemekana walichanganyika na wamasai ndipo wameru wakapatikana...wajuzi waje
 
Kwa kifupi wameru wametokea uchagani walipohamia maeneo ya mlima meru inasemekana walichanganyika na wamasai ndipo wameru wakapatikana...wajuzi waje


Mchaga ni nani? na ni nani aliamua huyu aitwe Mchaga na yule asiitwe Mchaga? Kama Wameru wametokea Uchagani kama unavyodai ni nani aliamua kwamba, kuanzia sasa wao siyo Wachaga tena?
 
Ok. Jibu haya:-
1. Kichaga ni lahaja ipi?
2. Nani aliyesanifisha lahaja hiyo kuwa kichaga?
Ebu rudia kusoma vizuri.

Ni kwamba nilitoa mfano wa kiswahili kuwa na lahaja nikarelate na kichaga chenye vikundi ving vinavyoshea matamshi, muundo wa sentensi,msamiati,sarufi ndio maana kikibosho, kisiha, kimarangu n. k ni kichaga kwa sababu vinashea hiyo mifano niliyokutajia.

Sijasema kichaga kina lahaja.
 
Kwa kifupi wameru wametokea uchagani walipohamia maeneo ya mlima meru inasemekana walichanganyika na wamasai ndipo wameru wakapatikana...wajuzi waje
Si kweli, kusikilizana kidogo kwa lugha hakuna uhusiano na wameru kuwa wachaga. Hata mila hazifanani ila zinakaribiana kama ilivyo kwa kabila nyingi za Afrika. Tafuta historia yao utajua origin yao iko vipi.
 
Si kweli, kusikilizana kidogo kwa lugha hakuna uhusiano na wameru kuwa wachaga. Hata mila hazifanani ila zinakaribiana kama ilivyo kwa kabila nyingi za Afrika. Tafuta historia yao utajua origin yao iko vipi.
Umejitahidi kujenga hoja lakini historia ndivyo ilivyo...nimejaribu kuhoji wazee wa kimeru kuhusu uhusiano wao na wamachame,, majibu niliyopata ni kuwa babu zao wameru wametokea uchagani yaani wamachame, hata kijiografia wamepakana kiasi flani
Mimi nakisikia au hata kuzungumza maneno machache ya kimeru, vivyo hivyo mmachame akizungumza namsikia kiasi.
Utafiti wangu sio wa jumla mkuu.
Mfano..mmeru husalimia ..kwantwa...mmachame..nantwa maana yake habari za asubuhi wakati za mchana mmeru..kwasindiswa..mmachame nesindiswa...na mengine mengi, kwa uthibitisho tafuta uzi humu unahusu uhusiano wa wameru na wamachame
 
Ebu rudia kusoma vizuri.

Ni kwamba nilitoa mfano wa kiswahili kuwa na lahaja nikarelate na kichaga chenye vikundi ving vinavyoshea matamshi, muundo wa sentensi,msamiati,sarufi ndio maana kikibosho, kisiha, kimarangu n. k ni kichaga kwa sababu vinashea hiyo mifano niliyokutajia.

Sijasema kichaga kina lahaja.
Sasa huoni mfano wako haulingani? Kiswahili ni lahaja ya kiunguja iliyosanifishwa. Hadi mwaka wa kusanifishwa upo. Sasa kichaga ni kipi, na kimesanifiwa na nani? Hapo unachanganya.

Kifupi ni kuwa kibosho ni kibosho, kimarangu ni kimarangu, ki uru ni ko uru na kimachame vivyo hivyo. Katika lugha zote hizo, ipi tuiite ndiyo kichaga? Na kwa mantiki hiyo, yupi ni mchaga?
 
Kwa hiyo kwa maelezo yako unakubalina na mimi na kile ninachoamini siku zote kwamba HAKUNA kitu kama Kabila la Kichaga Dunia hii? Na badala yake kilichopo ni makundi mbalimbali ya watu yaliounganishwa na Wageni na hapa Wazungu kwa lengo la kututawala Waafrika?
Na hapa ni Tanzania nzima vivyo hivyo kama vile hakuna kitu kama Kabila la Wahaya au sijui Wasukuma au sijui Wanyakyusa wote hawa ni matokeo ya Ukoloni aidha Waarabu au Wazungu!



Wewe unayesema hakuna kabila la Wachagga kwanza kabisa naamini wewe si Mchagga maana ungekuwa Mchagga usingeongea hivyo

Kwa kukusaidia tu ni kwamba Wachagga wanafanana kwa kila kitu, hiyo tofauti iliyopo ni maeneo tu wanayotoka lakini mambo mengine yote wanaenda sawa

Kwanza mila na desturi za Wachagga wote ni moja yaani kuanzia vyakula vya asili, vinywaji vya asili, majani na miti ya asili, uchumba, ndoa, uongozi, majina ya machifu, imani za kidini kila kitu ni kimoja

Pili Wachagga huwezi kuwatenganisha kwani muingiliano wao ni wa kindugu zaidi hapa namaanisha koo au familia za kichagga zinapatikana maeneo yote ya uchagga, kwa mfano utakuta Massawe anapatikana Rombo, Kilema, Kirua Vunjo, Old Moshi, Uru, Kibosho na Machame
Ukikuta Temba anapatikana KIbosho, Uru, Old Moshi, Marangu
Ukikuta Ngowi anapatikana, Kibosho, Uru, Old Moshi, Marangu, Rombo
Ukikuta Kimaro anapatikana Machame, Kibosho, Uru, Old Moshi, Marangu, Rombo
Sasa kwa akili yako watu hawa unawatofautisha vipi?

Yani unaanzaje kunishawishi kwamba Urassa aliyeko Machame na Urassa aliyeko Rombo sio ndugu, wakati hatujasikia Urassa aliyepo Tanga?

Pia Wachagga wanafahamiana, wanatambuana na wanafahamu kwamba wao ni wachagga na mtu ambaye si mchagga wanajua si mwenzao na wanamuita kyasaka au (mndu o nuka) wakimaanisha mtu wa porini, kwa mfano unaweza kuulizwa huyo mtu ni mchagga?, unasema ee ni mchagga kutoka Rombo au Uru au Sanya Juu, lakini kama si mchagga utasikia tu hapana si mchagga ni kyasaka yaani hatokei sehemu yoyote ya uchagga

Mfumo wa Umangi na lugha zote zinafanana ila kuna kuwepo utofauti mdogo unasababishwa na ule umbali wa kijiografia kutoka sehemu moja mpaka nyingine

Ni kawaida kutokea utofauti kidogo wa lugha pale jamii zinapokuwa zimegawanyika kiuongozi hata kama ni jamii moja

Naamini mpaka hapo nimekusaidia kwa kiasi kama unataka kufahamu zaidi vipo vitabu vingi sana vinavyowahusu Wachagga katika maktaba karibu zote za vyuo vikuu nchini upitie utafahamu zaidi

Kwa maelezo zaidi nifuate inbox

Karibu sana
 
Swali langu kwako, kwa nini Wameru hawaitwi Wachaga kama wanasikilizana na Wamachame ambao wanajiita Wachaga? Au kwa nini Wamachame hawasikilizani na Warombo au Wakibosho wakati wote wanaitwa/wanajiita Wachaga?
Swali zuri sana
 
(Unajua nini...Wa Rombo na Wakibosho hawasikilizani lakini wote wanajinasibu kuwa ni wachagga,,,lipi jema?Wote kuitwa Wameru ilhali hamsikilizani au muitwe majina tofauti na huku mwasikilizana?)
Tatizo la hawa Wanajifanya kabila kubwa ilhali ni muunganiko wa koo
 
Swali langu kwako, kwa nini Wameru hawaitwi Wachaga kama wanasikilizana na Wamachame ambao wanajiita Wachaga? Au kwa nini Wamachame hawasikilizani na Warombo au Wakibosho wakati wote wanaitwa/wanajiita Wachaga?
Mkuu ipo hivi

Machame = kibosho,
Kibosho = uru,
Uru = old moshi,
Old moshi = vunjo,
Vunjo = horombo.

Lugha nyingine zinazofanana na chagga ni meru na gweno.
 
Chaga na kikuyu wamefanana kitu kimoja tu.WIZI
Picture this "Bukoba bway"

Epa scandal wahusika wakubwa ni wahaya.

Escrow scandal wahusika wakuu ni wahaya, tena mpaka mapadri na maaskofu ndani.

Iptl mmiliki wake ni mhaya, ambaye alishiriki kuingizia serikali katika mikataba mibovu.

Wizi na mafisadi ni wahaya.
 
Wewe unayesema hakuna kabila la Wachagga kwanza kabisa naamini wewe si Mchagga maana ungekuwa Mchagga usingeongea hivyo

Kwa kukusaidia tu ni kwamba Wachagga wanafanana kwa kila kitu, hiyo tofauti iliyopo ni maeneo tu wanayotoka lakini mambo mengine yote wanaenda sawa

Kwanza mila na desturi za Wachagga wote ni moja yaani kuanzia vyakula vya asili, vinywaji vya asili, majani na miti ya asili, uchumba, ndoa, uongozi, majina ya machifu, imani za kidini kila kitu ni kimoja

Pili Wachagga huwezi kuwatenganisha kwani muingiliano wao ni wa kindugu zaidi hapa namaanisha koo au familia za kichagga zinapatikana maeneo yote ya uchagga, kwa mfano utakuta Massawe anapatikana Rombo, Kilema, Kirua Vunjo, Old Moshi, Uru, Kibosho na Machame
Ukikuta Temba anapatikana KIbosho, Uru, Old Moshi, Marangu
Ukikuta Ngowi anapatikana, Kibosho, Uru, Old Moshi, Marangu, Rombo
Ukikuta Kimaro anapatikana Machame, Kibosho, Uru, Old Moshi, Marangu, Rombo
Sasa kwa akili yako watu hawa unawatofautisha vipi?

Yani unaanzaje kunishawishi kwamba Urassa aliyeko Machame na Urassa aliyeko Rombo sio ndugu, wakati hatujasikia Urassa aliyepo Tanga?

Mfumo wa Umangi na lugha zote zinafanana ila kuna kuwepo utofauti mdogo unasababishwa na ule umbali wa kijiografia kutoka sehemu moja mpaka nyingine

Ni kawaida kutokea utofauti kidogo wa lugha pale jamii zinapokuwa zimegawanyika kiuongozi hata kama ni jamii moja

Naamini mpaka hapo nimekusaidia kwa kiasi kama unataka kufahamu zaidi vipo vitabu vingi sana vinavyowahusu Wachagga katika maktaba karibu zote za vyuo vikuu nchini upitie utafahamu zaidi

Kwa maelezo zaidi nifuate inbox

Karibu sana


Vitabu vipo vingi

Katherine stahl, "The history of Chagga People of Kilimanjaro", 1964, mouton publisher.

Charles Dundas, "Kilimanjaro and Its people", 1924, 1st edition, cass london.


Pia kuna website hii www.ntz.info
 
Tatizo la hawa Wanajifanya kabila kubwa ilhali ni muunganiko wa koo
Sio tu walijifanya kuwa kabila kubwa bali pia ni kabila lenye watu wakini, wenye maendeleo, wenye upeo, utajiri, elimu, utamaduni, mila na desturi bora katika taifa.

Wachagga ni kioo cha mtanzania kama wewe.
 
Sio tu walijifanya kuwa kabila kubwa bali pia ni kabila lenye watu wakini, wenye maendeleo, wenye upeo, utajiri, elimu, utamaduni, mila na desturi bora katika taifa.

Wachagga ni kioo cha mtanzania kama wewe.
Hongera mchaga, lakini urais mtausikilizia kwenye bomba!
 
Tatizo la hawa Wanajifanya kabila kubwa ilhali ni muunganiko wa koo
sijui kwanini mnaumia sana kila jambo linalogusa wachaga.
Acheni husda na wivu, hawa jamaa hata wakibaki mia 5 lakini wataendelea kuwa maarufu tu. Pia tukumbuke kuwa hawa jamaa wana vitu viwili muhimu sana.
1. Wajanja kimaisha
2. Kupenda na kujali kwao

Na hizo ndizo tabia za binadamu yeyote aliyekamilika kiakili. Kama wazungu wanavyothamini kwao.

Mchaga haachi kwenda kwao kila mwaka., mluguru anamaliza miaka 10 yupo dar bila kufika kwao matombo.

Pia chunguza makabila yanayojitambua utakuta ni tofauti na wengine.

Angalia Muhaya na Mnyakyusa walivyo wajanja kimaisha na wanavyothamini na kupapenda kwao ni tofauti na wengine
 
Sasa huoni mfano wako haulingani? Kiswahili ni lahaja ya kiunguja iliyosanifishwa. Hadi mwaka wa kusanifishwa upo. Sasa kichaga ni kipi, na kimesanifiwa na nani? Hapo unachanganya.

Kifupi ni kuwa kibosho ni kibosho, kimarangu ni kimarangu, ki uru ni ko uru na kimachame vivyo hivyo. Katika lugha zote hizo, ipi tuiite ndiyo kichaga? Na kwa mantiki hiyo, yupi ni mchaga?

Wewe mtu unakosea sana, kwanza unapaswa kujua Kichagga cha kuanzia Marangu Mwika yote mpaka Mamba, Marangu Mtoni, Kirua Vunjo, Kilema, Old Moshi yote mpaka Uru ni lugha moja kwa almost 100% tofauti ni matamshi machache ambayo unaweza kuzungumza na mtu hata lisaa lizima mkiwa bado hamjataja hayo maneno yanayotofautiana na hata mkiyataja utakuta tofauti labda ni herufi o na e, au r na d
Kwa hiyo Wachagga wa Marangu, Uru na Old Moshi wanaelewana 100%, ukija Kibosho nao wanaelewana na hawa wa Marangu, Uru na Old Moshi kwa almost 95%, yani naweza kusikiliza wimbo umeimbwa na mtu wa Kibosho na kuuelewa kila kitu au kuna sehemu naweza nisielewe vizuri kumbe kuna namna tu neno lilipindishwa kidogo, tofauti iliyopo ni kuna baadhi ya vocabulary chache sana unaweza kukuta wanatamka tofauti au salamu wanaitaja tofauti japo unaelewa, kwa mfano mtu wa Kibosho anaweza kusema Kida lo Assenga?, Mtu wa Marangu, Uru na Old Moshi anajua Kida maana yake ni Vp au Inakuwaje, lakini wao hawasalimiani hivyo

Ukija Machame na Rombo nao utakuta bado unawaelewa kwa more than 80% tofauti na kwamba kuna vocabularies kadhaa ziko tofauti, lakini pia mchaagga yeyote akimsikiliza mchagga mwingine yeyote kwa makini anaweza kumuelewa almost kila kitu
Kitu kilicholeta utofauti mdogo uliopo ni ule umbali wa kijiografia and nothing else!
Karne nyingi zilizopita kutokana na uhasama wa baadhi ya machifu ulisababisha mwingiliano kupungua na ndio ukazaa utofauti mdogo uliopo
 
Back
Top Bottom