Mbalamwezi
JF-Expert Member
- Sep 30, 2007
- 800
- 171
Wafanya biashara wengi wakubwa wa mafuta ni wajumbe wa kamati ya madini na nishati, ambao inaonekana wana nguvu kubwa kisiasa ya kuweza kuyumbisha hata uchumi wa nchi. Kwa kuwa wamebanwa sana na wanashindwa kupata faida haramu kwenye uchakachuaji, kuiba mafuta yasiyolipiwa kodi, kupungua kwa wigo mkubwa wa faida na kuanza kwa uagizaji mafuta wa pamoja basi wanaamua kutibua soko ili kutafuta kisingizio bungeni ambako wana nguvu kubwa. Ifike wakati suala la mgongano wa maslahi liangaliwe upya ili kuwa na kamati murua?