Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,693
- 20,453
Wakati wa shamrashamra za kubeba ubingwa, kocha wa Yanga, Nasredine Nabi alionekana akipiga picha huku akishikilia bendera ya nchi yake yenye rangi nyekundu na nyeupe.
Rangi hizo zilikwishapigwa marufuku kuonekana katika hadhira ya Yanga, na msimamo huo umeshatolewa mara kadhaa na uongozi wa Yanga, na kwa mifano michache ni pale uongozi ulipokataa kwa nyakati tofauti nembo za wadhamini wa ligi na klabu ya Yanga, kama vile Vodacom, GSM na NBC ambazo zote zilikuwa na rangi nyekundu na nyeupe inayodhaniwa kuwa inavutia kibiashara katika makampuni mengi.
Uongozi wa Yanga ulikwishaweka wazi msimamo kwamba rangi hizo haziendani na 'utamaduni' wa timu yao. Je, kocha Nabi hakujua hilo au alijua akapuuzia? Je, uongozi wa klabu ya Yanga utamchukulia hatua za kinidhamu iwapo itabainika alifanya makusudi kuvunja utamaduni wa klabu?
Uzi
Rangi hizo zilikwishapigwa marufuku kuonekana katika hadhira ya Yanga, na msimamo huo umeshatolewa mara kadhaa na uongozi wa Yanga, na kwa mifano michache ni pale uongozi ulipokataa kwa nyakati tofauti nembo za wadhamini wa ligi na klabu ya Yanga, kama vile Vodacom, GSM na NBC ambazo zote zilikuwa na rangi nyekundu na nyeupe inayodhaniwa kuwa inavutia kibiashara katika makampuni mengi.
Uongozi wa Yanga ulikwishaweka wazi msimamo kwamba rangi hizo haziendani na 'utamaduni' wa timu yao. Je, kocha Nabi hakujua hilo au alijua akapuuzia? Je, uongozi wa klabu ya Yanga utamchukulia hatua za kinidhamu iwapo itabainika alifanya makusudi kuvunja utamaduni wa klabu?
Uzi