Uhakiki wa taarifa za wateja benki bila National ID ni kutupotezea muda

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
May 14, 2010
2,182
307
Benki Kuu ya Tanzania imezitaka benki zote nchini kuhakiki taarifa za wateja wao, sote tunajua jinsi ilivyo rahisi kwa mtu kuchonga muhuri feki mtaani na jinsi watendaji wa kata na mitaa wasivyo makini katika kuwathibitisha watu wanaokwenda kwao kuomba utambulisho.
Naamini Benki Kuu (kupitia UWT) wanayajua yote haya na kama ningekuwa Gavana nisingepoteza muda kuziomba benki zihakiki wateja wao badala yake ningeiomba serikali iharakishe mchakato wa kuleta vitambulisho vya uraia, pamoja na zoezi la kuhakiki anwani za makazi ya watu.

Naamini zoezi hili litafanyika na pesa haramu zitaendelea kuingia kwenye mfumo wa benki zetu bila wahusika kugundulika, kama kweli lengo ni kudhibiti fedha haramu serikali ianze kwanza na uhakiki wa vyanzo vya mapato vya wamiliki wa magorofa yanayoota kila uchao mitaani.
 
Hili swala mimi naliona la kipuuzi na la kisiasa.Katika hali halisi hakuna mtu anaenda ofisi za bank anapewa tu account bila kujaza particulars zake,hizo information wanazozihitaji leo ni zipi?Inakuaje kitu kama hicho watu wanakubaliana kifanyike ndani ya mwezi mmoja tu?I know kuna watu wapo nje ya nchi au safarini hata kama ni ndani ya nchi,nadani ya huo mwezi wanawapata vipi?Nahisi hizi ni agenda za kutekeleza anti-terrorism act ya mmarekani,we had better spent time kutafta detail za watanzania waliofungua account za mabilioni ya walipa kodi nchi za nje na si kushughulika na walalahoi kwamba wakapange foleni tena bank kuupdate account zao
 
Kabla ya kufikiria kufanya jambo lazima inambidi mtu atafakari. Benki Kuu sidhani kama walitafakari endapo shughuli hii itafanikiwa. Na je, ni kwa kipindi gani.

Serikali ilikuja na zoezi la kubadilisha Leseni za Madereva wa magari, ni zoezi ambalo waliliona ni jepesi sana hapo awali lakini baadaye waligundua kuwa ni gumu. Muda uliopangwa ulipita pasipo kufanikiwa na ikawa ni usumbufu kwa wananchi. Mwishowe wakabadilisha utaratibu.

Serikali itangaza kuwa namba zote za Simu za Mkononi zisajiliwe, na wakatoa muda wa mwisho kusajili na mtu asiposajili namba inafungwa. Waliona ni zoezi rahisi sana kutekelezeka lakini baadaye wenyewe waligundua kuwa ni NGUMU.

je, hadi leo kuna namba ambayo ilifungwa kwa kutokusajiliwa??

Je, nini ilikuwa lengo la kusajili namba za simu za mkononi?

Je, uhalifu wa kutumia Simu umemalizika?

Je, ni gharama kiasi gani zilitumika?

Sasa Benki Kuu lazima wafikirie kuwa Mabenki nchini yana wateja wangapi, na hili zoezi litachukua muda gani kuwapitia wateja wote.

Vinginevyo yatakuwa ni yaleyale ya Bwana PINDA "MADAKITARI WOTE WARUDI KAZINI HADI KESHO ASUBUHI" kusema pasipo kutafakari jambo.

KUSEMA NI RAHISI SANA AKINI KUTEKELEZA NI NGUMU KULIKO KUMEZA LITA YA POMBE YA GONGO.

TAFAKARIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Watendaji wa serikali yetu huwa wanakurupuka tu bila kufanya study yoyote. Sasa huu utakuwa ni usumbufu
 
Muda wa kuhakiki taharifa za wateja, ulitolewa tangu mwezi wa 9, mwaka jana hadi 31 march 2012, ni uzembe tu wa mabenk walizembea , wengi wameanza kuakiki kuanzia jan 2012.
 
Huu ni usumbufu kwa wateja, kwani wakati wanawasajili hawakuchukuwa details zao pamoja na wadhamini?
 
mabenki yanatakiwa kuhakiki data za wateja ambazo tayari wanazo au wateja wanatakiwa ku-update data zao zilizopo kwenye benki zao? kama issue ni hii ya pili, i can't imagine muda na resources nyingine tutakazopoteza kwa ajili ya kukurupuka kujifanyia mambo bila kutafakari implications zake
 
Benki Kuu ya Tanzania imezitaka benki zote nchini kuhakiki taarifa za wateja wao, sote tunajua jinsi ilivyo rahisi kwa mtu kuchonga muhuri feki mtaani na jinsi watendaji wa kata na mitaa wasivyo makini katika kuwathibitisha watu wanaokwenda kwao kuomba utambulisho.
Naamini Benki Kuu (kupitia UWT) wanayajua yote haya na kama ningekuwa Gavana nisingepoteza muda kuziomba benki zihakiki wateja wao badala yake ningeiomba serikali iharakishe mchakato wa kuleta vitambulisho vya uraia, pamoja na zoezi la kuhakiki anwani za makazi ya watu.

Naamini zoezi hili litafanyika na pesa haramu zitaendelea kuingia kwenye mfumo wa benki zetu bila wahusika kugundulika, kama kweli lengo ni kudhibiti fedha haramu serikali ianze kwanza na uhakiki wa vyanzo vya mapato vya wamiliki wa magorofa yanayoota kila uchao mitaani.

Mkuu umeweka hili suala vizuri sana, lakini tatizo la nchi hii hata viongozi hawajui vipaumbele vyetu ni vipi/ au viwe vipi? Na ushauri kama huu hawautaki. Zaidi ya kusababisha usumbufu (hebu fikiria wale ambao akaunti ilifunguliwa Kigoma na nu muhusika alisha hamia Dar es Salaam),
HAta hivyo mengi yatatakuwa marudio ya information zile zile kwani details zilizopo wakati mtu anafungua akaunti na hizo hizo watakazoambulia. Tatizo huna mfumo ambao utalink taasisi zote muhimu ili kuverify data zitakazotolewa na muhusika kama ambavyo National ID ingefanya
 
Ina maana kila baad ay amuda watakuwa wanfanya hivyo? maana status zinabadilika, location, occupation n.K Inabidi wajipange wajue vitu muhimu wanavyohitaji ni nini?
 
Issue ya kuhakiki isingekuwa tatizo,shida ni implication ya zoezi lenyewe pia hakuna uhakika kama taarifa tunazo update sasa hazitakuwa out of date baada ya muda fulani .Haya mambo tutakurupuka hadi lini kuna haja ya kuwa na mifumo mizuri ya ku link taarifa za wananchi popote walipo pia kuwepo projection ya mambo jamani...kila siku mifumo tunabadili as if hii nchi imezaliwa jana duh,zoezi la vitambulisho vya taifa linaweza kusaidia matatizo kama haya ila shida ni kuwa zoezi lenyewe limeshakuwa la kisiasa tayari,na hapa ndipo tunapopotea njia always..too much politics over professionalism.TAIFA LISILO HESHIMU WATAALAMU NA WASOMI WAKE LINA NJIA NDEFU KUPATA MAFANIKIO KTK ASPECTS MBALIMBALI!!
 
Back
Top Bottom