Uhai wa chadema 2014

Uhai wa chadema 2014

JGG

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
323
Reaction score
136
Nimejaribu kusikiliza maelezo ya zito ktk video ya tuhuma dhidi yake na ambayo ipo hapa jamvini, nimegundua yafuatayo:

  1. [*=1]CHADEMA kuna tatizo la mifumo sawa na matatizo ya mifumo tuliyonayo ktk taifa letu
    [*=1]Zitto anautumia vizuri udhaifu huo wa mifumo kwa sababu zake binafsi ambazo nadhani anazielewa mwenyewe kwa maana mtu ambaye ni NAIBU KATIBU WA CHAMA ansema:

  • Yeye amekuja kwenye siasa za kitaifa akiwa na umri mdogo sana, jiulize kuna mahusiano gani kati ya umri na IQ
  • Chadema hakuna migogoro lakin anapigwa mishale ndani ya chama kwa kuwa uchaguzi umekaribia na kuna nongwa kwa sababu yeye aliwahi kugombea nafasi ya mwenyekiti
  • Yanayotokea chadema yalishawahi kutokea vyama vingine na kimsingi hakuna jipya maana waliowahi kuitwa WASALITI leo ni makamanda wa chadema eg marando
  • Anapambana uswisi kutetea pesa za watz an Africa na anahitaji kupewa moyo lakin anakwamishwa na baadhi ya CDM, jiulize ‘ANAPAMBANA’ na siyo km chama au timu TUNAPAMBANA

Ushauri kwa CHADEMA:
  • Zito anatumia udhaifu huo wa mfumo kufanikisha kazi aliyotumwa na ccm. Kwa hiyo ikiwa kweli atapambana kuwa mwenyekiti wa chama na ukweli ni kuwa hawezi kupata lakini atatumia yanayotokea sasa ku justfy kuwa aliundiwa mgogoro ili mbowe mtu wa kaskazini aendelee kuwa mwenyekiti


  • Mbowe umeshafanya kazi kubwa sana na huhitaji sana kuwa mwenyekiti ili uweze kuendelea kutoa mchango wako ktk harakati za kuwakomboa watz maana CHADEMA ni timu na siyo individuals. Kwa hiyo ikiwa zito atafanya kweli epuka kupambana na zito katika nafasi ya mwenyekiti kwa kuwa lengo lake siyo kushinda bali kushindwa ili kushindwa huko kuwe mtaji wa kufanikisha mradi maalum wa kuibomoa CHADEMA. Chama kina watu wengi sana makini ambao misimamo yao wameshaonesha kwa vitendo, Lissu, Mnyika, Msigwa, Prof Safari, etc etc.

Wewe unayehitaji mabadiliko katika Tanzania unaishauri nini CHADEMA?
 
Zitto kanyanyasaswa sana,kasemwa sana,kawindwa sana,amekwepa sana maovu sasa naona ameamua liwalo na liwe.
 
Ushauri mzuri sna,ila tatzo sasa mbowe kile kiti hawez achia,nilishaonya tena!!kile kiti ni special kwa watu wa kanda maalumu tu!!hao wengne cijui kina lisu cijui safari watasikia nafs hyo tu kwenye radio
 
Zitto kanyanyasaswa sana,kasemwa sana,kawindwa sana,amekwepa sana maovu sasa naona ameamua liwalo na liwe.

vizabizabina na viherehere kama nyie hamfanyi kazi zenu, kazi kubwa mlonayo ni kufuatilia post zinazohusu CDM mtie umbea wenu.
CDM haina mgogoro, nyie msiojitambua ndio mnatangaza mgogoro ndani ya CDM wakati nyie na ccm lenu mnataabika kwa rushwa na wizi wa fedha za umma. cdm hakuna mgogoro bali kuna tofauti za kimtazamo tu ambazo zitaisha kwani zinashughuliiwa kichama kama taasisi na sio kwa kelele zenu za hapa jf.
 
vizabizabina na viherehere kama nyie hamfanyi kazi zenu, kazi kubwa mlonayo ni kufuatilia post zinazohusu CDM mtie umbea wenu.
CDM haina mgogoro, nyie msiojitambua ndio mnatangaza mgogoro ndani ya CDM wakati nyie na ccm lenu mnataabika kwa rushwa na wizi wa fedha za umma. cdm hakuna mgogoro bali kuna tofauti za kimtazamo tu ambazo zitaisha kwani zinashughuliiwa kichama kama taasisi na sio kwa kelele zenu za hapa jf.

mbna hasira sna?tunataka tuwajue hao vifaranga na mama yao ni akina nani
 
vizabizabina na viherehere kama nyie hamfanyi kazi zenu, kazi kubwa mlonayo ni kufuatilia post zinazohusu CDM mtie umbea wenu.
CDM haina mgogoro, nyie msiojitambua ndio mnatangaza mgogoro ndani ya CDM wakati nyie na ccm lenu mnataabika kwa rushwa na wizi wa fedha za umma. cdm hakuna mgogoro bali kuna tofauti za kimtazamo tu ambazo zitaisha kwani zinashughuliiwa kichama kama taasisi na sio kwa kelele zenu za hapa jf.
Pengine nikuombe unikome make jf siyo jukwaa la mjomba wako wala sijakulazimisha kusoma post zangu matatizo yako ya kifamilia usitake nikusaidie bora uza mandazi wenzako wauze karanga kila mja anaouhuru wa kutoa mawazo yake chadema kilianza na sheatani lazima kife na shetani.
 
mbna hasira sna?tunataka tuwajue hao vifaranga na mama yao ni akina nani
Mkuu hilo ndiyo la msingi lakini kwa kiasi fulani vifaranga wanajulikana kilichobaki ni kujua hao mama zao ni wepi ambao wapo chini ya chungu.
 
Nimejaribu kusikiliza maelezo ya zito ktk video ya tuhuma dhidi yake na ambayo ipo hapa jamvini, nimegundua yafuatayo:

  1. [*=1]CHADEMA kuna tatizo la mifumo sawa na matatizo ya mifumo tuliyonayo ktk taifa letu
    [*=1]Zitto anautumia vizuri udhaifu huo wa mifumo kwa sababu zake binafsi ambazo nadhani anazielewa mwenyewe kwa maana mtu ambaye ni NAIBU KATIBU WA CHAMA ansema:

  • Yeye amekuja kwenye siasa za kitaifa akiwa na umri mdogo sana, jiulize kuna mahusiano gani kati ya umri na IQ
  • Chadema hakuna migogoro lakin anapigwa mishale ndani ya chama kwa kuwa uchaguzi umekaribia na kuna nongwa kwa sababu yeye aliwahi kugombea nafasi ya mwenyekiti
  • Yanayotokea chadema yalishawahi kutokea vyama vingine na kimsingi hakuna jipya maana waliowahi kuitwa WASALITI leo ni makamanda wa chadema eg marando
  • Anapambana uswisi kutetea pesa za watz an Africa na anahitaji kupewa moyo lakin anakwamishwa na baadhi ya CDM, jiulize ‘ANAPAMBANA’ na siyo km chama au timu TUNAPAMBANA

Ushauri kwa CHADEMA:
  • Zito anatumia udhaifu huo wa mfumo kufanikisha kazi aliyotumwa na ccm. Kwa hiyo ikiwa kweli atapambana kuwa mwenyekiti wa chama na ukweli ni kuwa hawezi kupata lakini atatumia yanayotokea sasa ku justfy kuwa aliundiwa mgogoro ili mbowe mtu wa kaskazini aendelee kuwa mwenyekiti


  • Mbowe umeshafanya kazi kubwa sana na huhitaji sana kuwa mwenyekiti ili uweze kuendelea kutoa mchango wako ktk harakati za kuwakomboa watz maana CHADEMA ni timu na siyo individuals. Kwa hiyo ikiwa zito atafanya kweli epuka kupambana na zito katika nafasi ya mwenyekiti kwa kuwa lengo lake siyo kushinda bali kushindwa ili kushindwa huko kuwe mtaji wa kufanikisha mradi maalum wa kuibomoa CHADEMA. Chama kina watu wengi sana makini ambao misimamo yao wameshaonesha kwa vitendo, Lissu, Mnyika, Msigwa, Prof Safari, etc etc.

Wewe unayehitaji mabadiliko katika Tanzania unaishauri nini CHADEMA?

Mi nashaur zito akigombea mbowe amwachie tundulisu
 
Nashauri Chadema wamuachie Zitto kabwe awe Mwenyekiti kwasababu ndie mwenye uwezo kuliko Mbowe.
 
Mkuu hilo ndiyo la msingi lakini kwa kiasi fulani vifaranga wanajulikana kilichobaki ni kujua hao mama zao ni wepi ambao wapo chini ya chungu.

ben mtembea na sumu mnamuweka kweny kundi la vifaranga au mama wa vifaranga?
 
Cdm mgogolo UPo Zito kavumilia sana dr slaa anaposafiri Mtu wa kukaimu ni Zito lakini chadema wanampa mnyika Zito Hana ofisi cdm yupoyupo msemaji wa Chama wanamjenga mnyika hamuwezi Zito hats iweje Kule kuteuliwa na jopo la dunia kufuatilia mabilioni uswisi ni sifakubwa mbona hakuteuliwa mnyika?
 
ZITTO HATARINI
Tangu November 11, 2013,





*Atumiwa ujumbe wa kumtishia kumuondoa duniani


*Sasa aamua kumvaa Dk Slaa, ampa masharti mazito


*Asema yeye ni binadamu, ana nyama, damu sasa amechoka


Na Mwandishi Wetu


NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), amesema amepokea ujumbe wa kumtishia maisha iwapo ataendelea na jitihada zake za kupambana na ufisadi.


Hata hivyo, amesema akiwa katika ziara ya Bara la Ulaya kati ya Oktoba 21 hadi Novemba 2 mwaka huu amepokea kwa njia ya barua pepe ripoti inayoitwa "Taarifa ya Siri ya Chadema" ambayo pia ilikuwa imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.


Kwa mujibu wa taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa Dar es Salaam jana Zitto "taarifa ya Chadema inasema chama hicho (chama changu), kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini mimi napokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema".


Zitto alisema ripoti hiyo ilimhusisha pia na mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi kiasi cha dola za Marekani 250,000 kupitia kwenye akaunti yake binafsi.


Alisema taarifa hiyo ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imemfedhehesha , kumsikitisha na kumkasirisha.


"Taarifa hii iliibuliwa katika kipindi ambacho nilikuwa safarini kutetea haki za Watanzania na Waafrika ambao utajiri wao wa rasilimali unafaidiwa na watu wachache waliohifadhi mali katika nchi za nje na pia kupigania kampuni za mataifa tajiri yalipe kodi stahiki katika nchi zetu.


"Pengine lengo la ripoti hiyo lilikuwa ni kutaka kunipoteza kutoka katika nia na dhamira yangu ya dhati ya kutaka Watanzania wafaidike na utajiri wao. Muda ambao watunzi wa ripoti hiyo waliamua kutoa taarifa yao unazua maswali mengi kuliko majibu,"alisema Zitto.


Aliongeza kuwa anafahamu kuwa yeye ni mwanasiasa ambaye amekuwa mlengwa wa mashambulizi kutoka kwa makundi mbalimbali ya wanasiasa na vikundi vyao. "Kama mwanasiasa, niko tayari kupokea changamoto zozote zinazokuja na uanasiasa wangu".


Hata hivyo, kitu ambacho hawezi kukubali Zitto ni kwa watu kutumia jina lake na uanasiasa wake kumchafua yeye binafsi na watu wengine wasiohusika kwa sababu ya kutaka kutimiza malengo yao ya kidhalimu.


Alifafanua kuwa raia huyo wa Kijerumani tayari amekana kuhifadhi fedha zake. Kwa maelezo yake kwa baadhi ya viongozi wa Chadema amekana kuwa na akaunti inayotajwa na amekana pia kuwepo nchini Ujerumani katika siku na wakati uliotajwa kwenye ripoti hiyo.


"Ripoti hiyo imemtaja pia mtu kama Dk.Charles Kimei, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB ikidai nilikutana naye na alishiriki kwenye igizo hilo la kunipa fedha.


"Niseme mapema tangu kuzaliwa kwangu sijawahi hata mara moja kukutana na Dk. Kimei popote pale ndani au nje ya nchi. Kumuingiza mtu aliyejenga jina lake kwenye taaluma ya kibenki kwa sababu tu ya lengo ovu la kumchafua Zitto Zuberi Kabwe si uungwana bali ni unyama,"alisisitiza.


Aliongeza kutokana na uchafuzi huu wa wazi dhidi ya taswira yake binafsi na watu wengine walioingizwa kwenye mkumbo huu, ameamua kuandika barua rasmi kwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Wilbrod Slaa kumwomba athibitishe kinachoitwa Taarifa ya Siri ya Chadema ni kweli ni taarifa ya chama au aikanushe ili aweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa hekaya hiyo.


"Cha ajabu, nimepokea ujumbe wa kutishiwa maisha kutoka kwa mtu(jina tunalo) na kuahidiwa kunipoteza iwapo nitaendelea na jitihada zangu za kupambana na ufisadi na kutafuta haki kwa Watanzania wote pasipo kujali tofauti zao za kiitikadi, kikanda, kikabilia na kidini,"alisema Zitto katika taarifa hiyo


Alisisitiza anatarajia kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wote ambao wamehusika na utungaji na uenezi wa taarifa hiyo.


"Nitahakikisha wahusika wanatafutwa na kufunguliwa mashtaka stahiki ya upotoshaji na kuchafuana.Ni matarajio yangu wale wenye mapenzi mema na Tanzania, mimi binafsi na utawala wa sheria, wataelewa nia yangu ya kutafuta haki katika suala hili,"alisema Zitto.


Hata hivyo, Zitto alisema ameamua kujitolea maisha yake kwa ajili ya Watanzania na kama alivyowahi kusema Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela;"Struggle Is My Life."


Migogoro Chadema


Wakati huo huo Zitto amesema Chadema hakuna migogoro na kinachoonekana kuna watu wachache wasio na shughuli kuamua kuwagombanisha viongozi ndani ya chama hicho.


Zitto alitoa kauli hiyo juzi wilayani Kaliua mkoani Tabora wakati akihutubia wananachi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Kolimba ambapo alitumia nafasi hiyo kueleza kinachoendelea Chadema.


Alisema kuna watu wachache hawana kazi ya kufanya na wanachokifanya sasa ni kutengeneza mazingira viongozi kugomabana na ikitokea hivyo, ndio furaha kwao.


Alifafanua kuwa mwaka 1995 kabla ya chama kuamua kukiunga mkono Chama cha NCCR Mageuzi, Edwin Mtei na Bob Makani waligombea nafasi ya kutaka kuwania uraisi ndani ya chama hicho na hakukuwa na misigano yoyote kwa kuwa walijua malengo yao ni kuwatumikia watanzania


"Hali ya watu kuwania nafasi moja ndani ya Chadema ilijirudia mwaka 1998 kwa nafasi ya uenyekiti kuwaniwa na watu wawili tofauti na hakukuwa na mgogoro,"alisema.


Aliongeza uchaguzi ndani ya chama hicho ulifanyika mwaka 2009 wakapata viongozi na kisha wakaingia kazini na kilichotokea ni kuvuna wabunge, madiwani na wenyeviti wengi.


"Sasa hali inaanza kuwa ya ajabu ajabu utafikiri kuna mtu aliyetangaza kugombea.Hatua yangu ya mwaka 2009 ilitokana na kile alichokuwa amekiona kuwa kutekeleza demokrasia ndani ya chama changu kutokana na waliomtangulia kujitokeza kuwania nafasi walizoona zinawafaa.


"Mimi ni binadamu nina damu na nyama katika umri huu mdogo nimepigwa mishale mingi sana ya kisiasa ninaumia na damu inanitoka sasa nimechoka kupigwa mishale ni lazima viongozi tuambiane ukweli na tukemee hali hii,"alisema Zitto


Hata hivyo, alisema mwanzoni hapakuwa na chama chenye nguvu kama NCCR mageuzi, lakini walipoanza kupigana kile alichokiita mishale, chama hicho kilisambaratika.


Alisema walimchafua sana Mabere kuwa yeye ni msaliti, lakini hivi sasa Marando ndio wao ndani ya Chadema na ndio mwanasheria wao , hivyo lazima waambiane ukweli.


"Viongozi tuonye haya mambo, tusipoonya tutaonekana tunashiriki na sisi, Waha tunamsemo, kwamba ‘ukiona kifaranga yupo juu ya chungu, jua mama yake yupo chini,"alisema Zitto na kushuka jukwaani.






Akizungumza Dar es Salaam jana kuhusu taarifa hiyo ya Zitto, Mkurugenzi wa Mawasiliano Chadema, John Mnyika alisema Zitto anaomba kitu ambacho anajua kabisa kwamba chama hicho kimefanya.


"Anajua Andrea Cordes aliniandikia email na nakala kwake na nikajibu kuwa ripoti hiyo haijaandikwa na Chadema makao makuu .


"Kikipokea malalamiko rasmi chama kitachunguza ukweli au uongo wa madai yaliyotolewa kwenye ripoti hiyo kwa sasa chama kinachukulia tu kama ripoti na habari nyingine nyingi zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii mara kwa mara kuhusu Chadema na viongozi wake mbalimbali,"alisema Mnyika.


Aliongeza hata Mshauri wa masuala ya Ufundi Chadema Dk. Kitila Mkumbo anafahamu kuwa mara baada ya ripoti hiyo kuwekwa kwenye mitandao ,Naibu Katibu Mkuu Zitto alitoa kauli.


Alisema kama hakuridhika na majibu ya Zitto na kuona kulikuwa na mahitaji ya ziada anaamini Dk. Kitila anaelewa taratibu za chama angeweza tu kuwasiliana na vijana wa idara ya uenezi aliowataja kwenye andiko lake kwenye mitandao ya kijamii na idara ingetoa ufafanuzi zaidi.


"Mjadala huu usikuzwe bila sababu za msingi na kufunika masuala mengine muhimu ya kitaifa yanayoikabili nchi yetu kwa sasa.Kama kuna malalamiko yoyote yaletwe kiofisi na kwenye vikao vya chama yatashughulikiwa,"alisema Mnyika.
 
Ushauri mzuri sna,ila tatzo sasa mbowe kile kiti hawez achia,nilishaonya tena!!kile kiti ni special kwa watu wa kanda maalumu tu!!hao wengne cijui kina lisu cijui safari watasikia nafs hyo tu kwenye radio
Mchukueni ZITTO mkampe uenyekiti huko ccm,mbona uenyekiti dhaifu wa KIKWETE,MREMA,LIPUMBA NA CHEYO hamhoji? Kama mnakerwa na mbowe hamieni CHAUSTA.
 
Zitto Hatarini Kuuawa CHADEMA!

Zitto Hatarini Kuuawa CHADEMA!
YADAIWA ILIPANGWA ANYWESHWE SUMU HOTELINI, DK SLAA ATAJWA KUMTUMA SAANANE KUMMALIZA, MWENYEWE AKANUSHA, ASEMA NI SIASA CHAFU TISHIO la kuuawa kwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe,
sasa limechukua sura mpya, baada ya
kuibuika kwa madai mapya kuwa Bosi
wake, Dk. Willbrod Slaa, alipanga njama
za kumuangamiza, MTANZANIA Jumatano linaripoti. Duru za habari zinaeleza kuwa Zitto,
ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma
Kaskazini na Naibu Kiongozi wa
Upinzani bungeni, anadaiwa alitaka
kuuawa kwa sumu na Katibu Mkuu wa
chama hicho, Dk. Slaa, ambaye alimtumia kada na Mjumbe wa Baraza la
Vijana la Chadema (BAVICHA), Ben
Saanane, kutekeleza mpango huo. Habari zinadai kuwa tukio hilo
lilipangwa kutekelezwa Mei mwaka
jana, katika Hoteli ya Lunch Time, iliyoko
Mabibo External, jijini Dar es Salaam. Kwamba Zitto alilengwa kuuawa kwa
kuwekewa sumu kwenye kinywaji chake
wakati akiwa kwenye mazungumzo na
baadhi ya makada vijana wa chama
hicho katika Hoteli ya Lunch Time. Mmoja wa watu waliokuwa katika tukio
hilo amelieleza MTANZANIA Jumatano
kuwa Zitto alinusurika baada ya
aliyetumwa kumuwekea sumu hiyo
kuidondosha na hivyo kuonekana kwa
watu waliokuwa eneo hilo. Anamtaja mtu aliyetumwa kumuua Zitto
kuwa ni Ben Saanane, ambaye
aliangusha karatasi ya nailoni iliyokuwa
na ungaunga unaosadikiwa kuwa sumu
na kuonekana kwa watu waliokuwa
eneo hilo, akiwemo Zitto mwenyewe pamoja na aliyekuwa Naibu Mwenyekiti
wa Bavicha, Juliana Shonza na Mtela
Mwampamba. Akizungumza na MTANZANIA Jumatano,
Shonza alikiri kutokea kwa tukio hilo
kwa kueleza kuwa yeye na Mwampamba
walihoji kilichokuwa ndani ya nailoni ile,
ambacho kilionekana wazi kuwa ni unga
unga ni nini, ambapo Saanane alikiri kuwa ilikuwa sumu ambayo alipewa na
Dk. Slaa, ili amuwekee Zitto. Shonza alidai kuwa siku ya tukio, yeye
na Zitto walikuwa wamekaa meza moja
na Saanane ambaye mkono wake wa
kushoto ulikuwa umefungwa bandeji
aliyowaeleza kuwa aliifunga kutokana
na maumivu ya mkono. Alisema wakiwa katika maongezi, huku
Saanane akionyesha kuzidiwa na kilevi
alichokuwa amekunywa, alitoa bahasha
ya kaki yenye fedha ili alipie gharama za
vinywaji vya wote ambayo ilidondoka na
ndani yake ikatoka karatasi ndogo ya nailoni ikiwa na unga mwekundu. Kwa mujibu wa Shonza, Saanane
alipobanwa aeleze unga ule ulikuwa
nini, awali alidai ni kilevi aina ya kuberi,
huku akiwataka wasiifungue nailoni
hiyo, jambo ambalo Mwampamba
alilikataa na kulazimisha ifunguliwe pale pale. "Kwa hasira Ben alitaka arudishiwe ile
karatasi, lakini, Mwampamba aliondoka
nayo, usiku huo huo Saanane alimtafuta
Mwampamba hadi nyumbani kwake
akidai apewe mzigo wake. "Mwampamba alimwambia atampa
mzigo wake kwa sharti moja tu la
kusema ukweli kuhusu kilichomo ndani
ya nailoni hiyo na hapo ndipo Ben
alipokiri kuwa alipewa mzigo huo
ambao una unga unga wenye sumu na Dk. Slaa, ili amuwekee Zitto kwa sababu
amekuwa akimsakama ndani ya vikao
vya chama. "Huo ndiyo ukweli ambao nitausema
popote, sasa kama Ben alitudanganya
kwa kumsingizia Dk. Slaa hiyo ni juu yao
wenyewe," alisema Shonza. Shonza alisema hali hiyo iliwaogofya na
kuanza kuwa makini katika mapito yao
na kuongeza kuwa Zitto bado yuko
Chadema kwa sababu ana roho ngumu,
mvumilivu na mkomavu wa kisiasa,
anayeweza kukabiliana na mambo ya hatari. Dk. Slaa alipoulizwa na MTANZANIA
Jumatano kuhusu madai hayo, alisema
hilo ni kosa la jinai, ambalo kama
anatuhumiwa kulifanya anapaswa
kushtakiwa kwenye vyombo vya dola
badala ya tarifa hizo kupelekwa katika vyombo vya habari. "Usipende kutumiwa na watu, lakini
aliyekutuma anajua amekutuma kwa
sababu gani. Sasa nitakujibu, hivi suala
la kuua si ni jinai? Sasa suala la jinai
linapelekwa kwenye vyombo vya dola au
kwenye vyombo vya habari ?. Huyo aliyesema yuko Chadema au yuko
wapi? Aliyesema hakwenda polisi ?. Aliyetaka kuuawa hakwenda pia? Sasa
ninyi media mmekuwa nani? "Wa kumuuliza suala hili ni Saanane
mwenyewe au Shonza, wangekuwa na
nia njema wangekwenda polisi au Zitto
mwenyewe angekwenda polisi kushitaki
kwa kutaka kuuawa," alisema Dk. Slaa. Naye Saanane ambaye amefanya
mahojiano na MTANZANIA Jumatano
kuhusiana na mambo mbalimbali
mabaya ambayo yamekuwa
yakielekezwa kwake, akizungumzia
madai hayo alisema madai hayo hayana ukweli wowote, bali yanaibuliwa sasa na
mahasimu wake kisiasa kwa lengo la
kutaka kumshusha baada ya majaribio
mengi dhidi yake kushindwa. "Kwanza siku ambayo wanasema
tulikuwa wote mimi sikuwa huko,
nashangaa na haiingii akilini kwamba
mimi niende hadi Temeke (kwa
Mwampamba) tena usiku wa manane
kwa ajili ya kufuata sumu ya kuulia panya. "Hizi ndizo siasa halisi za maji taka,
kuliko nipange njama za kuua mtu kwa
malengo ya kisiasa, ni bora niache siasa. Ni mwendawazimu pekee atakayeweza
kuamini tetesi hizi za ovyo kabisa
zinazofanywa na vijana walioshindwa
kujenga hoja za maana kwenye
majukwaa," alisema Saanane. Aliwaonya watu wanaohasimiana naye
kisiasa kuacha kumchafua Dk. Slaa kwa
kutumia jina lake katika mambo
wanayomtuhumu, kwa kile alichoeleza
kuwa ni dhambi kubwa kutunga uongo
na kuusambaza ili kutafuta huruma ya umma wa Watanzania. "Nadhani lengo lao hapa ni kumchafua
Dk. Slaa kwa tuhuma hizi za uongo
zilizotolewa kwa mara ya kwanza na
vijana waliotimuliwa Chadema kwa
kukisaliti chama na baadaye kuhongwa
na makada na viongozi wa CCM ambao wamejiunga nao sasa. "Sasa kwa tuhuma hizo, kwa nini
wasiripoti polisi, inaingiaje akilini mtu
kupanga njama kubwa kiasi hicho halafu
ukae kimya tu," alisema Saanane.

CHANZO: Mtanzania
 
usishangae kuambia zitto kapotea ghafla,kashambuliwa na mapanga,kapigwa risasi,kamwagiwa tindkali,kapata ajali!!manake chadema maji yamewazid,wao kumtoa mtu roho kwaajili ya madaraka si ngumu kwao!!watanzania wote tunaomba tuungane kumuombea zitto kwa mwenyez Mungu!!watoa roho chadema wanataka kuona roho yake inakosa uhai
 
Zitto kanyanyasaswa sana,kasemwa sana,kawindwa sana,amekwepa sana maovu sasa naona ameamua liwalo na liwe.

Heheh we jamaa huwa napenda sana kusoma posts zako maana inaonesha ukiwa shule ulikuwa mkorofi sana wewe...
 
usishangae kuambia zitto kapotea ghafla,kashambuliwa na mapanga,kapigwa risasi,kamwagiwa tindkali,kapata ajali!!manake chadema maji yamewazid,wao kumtoa mtu roho kwaajili ya madaraka si ngumu kwao!!watanzania wote tunaomba tuungane kumuombea zitto kwa mwenyez Mungu!!watoa roho chadema wanataka kuona roho yake inakosa uhai
Heri yenu magamba mliowapa ulizi wa uhai Bw Kolimba,kombe,mwaikusa,Mwangosi
 
Nionavyo kwa hakika kabisa Chadema hakuna mgogoro. Hii ni mia ploy ya system kuanzisha mambo ya kuvunja nguvu ya Chama hicho. Kwa taarifa yenu wamefanikiwa kumnunua na kumtumia mmoja wa moderators wa JF kuhakikisha kuwa mtandao huu huandiki tena habari za kuifedhehesha serikali au habari za aina hiyo hazichukui uzito mkubwa. Ni vizuri kuwa waangalifu maana soon nguvu na umaarufu wa JF yenyewe utapotea kabisa. Tutawapa jina la moderator huyo wakati ukifika.
 
Back
Top Bottom