Ugomvi wangu na Membe ni Yeye kuwa Rais wa JMT tu, ila kwa hili naungana nae mkono tena kwa 100% kabisa

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,571
108,925
Matukio ya Utekaji nchini Tanzania ni Utamaduni mpya usiokubalika, Wastaafu tusijione Shughuli ziliisha( Chanzo Taarifa: MillardAyo.com )

" Suala la utekaji au Watu kupotea linaweza kuiharibia Nchi yetu heshima Duniani, linaweza kuiondolea Nchi yetu hali ya usalama ambayo tulikuwa nayo tangu tupate uhuru lakini pia hali inaweza kujenga chuki kubwa sana ya Wananchi dhidi ya Serikali popote Duniani " ( Chanzo Taarifa: MillardAyo.com )

" Hili Suala la Utekaji lisipokemewa sasa litakuja Kufika hadi katika Uchaguzi ambapo hapo linaweza kusababisha taswira ya nchi Kuharibiwa kwani wapo ambao hawatakubaliana nalo na watakuwa tayari kwa lolote lile " ( Chanzo Taarifa: MillardAyo.com )


Tukumbuke kuwa huyu Membe aliwashawahi kuwa Ofisa Usalama ( Jasusi Mwandamizi ) kabisa ndani ya Taasisi Nyeti ya Usalama wa Taifa nchini ( TISS ) hivyo kama na Yeye leo hii amefikia Kutovumilia na Kuyasema haya tena hadharani na bila Kificho wala Unafiki basi Wahusika wote au wale Maduduna ( Wapumbavu ) wachache wanaoratibu huu Upuuzi wajitathmini na wakiweza waende haraka katika Nyumba zao za Ibada Wakatubu Ukatili wao walioufanya kwa Watanzania wenzao au hata Wageni kabla Kofi la Kiama la Mwenyezi Mungu halijawashukia.

Sina tatizo na IQ yake Mzee Membe na najua ya kwamba ni Mmoja wa Watu walioshiba kama siyo Kukomaa kabisa na Udiplomasia na bahati nzuri hata huo Udiplomasia wenyewe anauweza na unampenda vile vile kuliko wengine ambao huu ni mwaka wa Tatu unaenda wa Nne hawana hata Robo Tatu ya Udiplomasia japo wanaulazimisha, ila katika Suala ya Yeye kutaka kuwa Rais wa JMT hapo ndipo nitamkatalia kutokana na sababu zangu kadhaa ila kwa leo siyo mahala pake kwa Mimi kuzitaja hapa.

Nami namalizia pia kwa kusema Wastaafu nchini Tanzania hasa wale Viongozi na waliowahi Kuongoza Taasisi na Idara Nyeti nchini Tanzania tambueni kuwa kwa kuwa bado mpo Hai basi nyie bado mnatakiwa Kupaza Sauti zenu na ikibidi hata Kuwakemea hawa Maduduna ( Wapumbavu ) wachache wanaochafua Taasisi zenu ambazo mliziongoza vyema na hazikuchafuka kama ilivyo sasa.
 
Unapoona mtu mwenye IQ kubwa anatoa neno ni lazima utafakari kabla hujakurupuka kujibu!!

Hapo kwenye red alikua ana maanisha nini huyu mwanadiplomasia/Jasusi wa kitanzania?
 
Kujionyesha kwamba unampinga kwa hoja ya yeye kuwa Rais ni hoja fungati tu ya kuonekana kwamba humtaki ili ufikishe ujumbe lengwa!
Eti mwanadiplomasia na diplomacy inamhitaji! Hivi huwa mnatumia akili gani kuleta hoja zilizoathirika humu jamvin? Yeye alifanya nini kipindi diplomacy alikuwa anainyonya kama pipi ? Hivi kumpenda kwake huko unasahau mgogoro wa Malawi? Rwanda je????acha unafiki mjomba!
 
Safi sana Membe, Wewe umewahi kuwa Jasusi mbobezi, enzi zenu watu walikuwa wanashughulikiwa lakini hakukuwa na utekajitekaji wa kishamba!

Kiongozi hii Comment yako nimeipenda mno kwani imesimama / imetakata vyema kabisa. Ningekuwa Jirani nawe angalau ningejipigapiga nikununulie hapa Pepsi Bigi au Mirinda Nyeusi Bigi na hata Mirinda Orange Bigi ili ujipongeze. Umemaliza kila Kitu!
 
Kujionyesha kwamba unampinga kwa hoja ya yeye kuwa Rais ni hoja fungati tu ya kuonekana kwamba humtaki ili ufikishe ujumbe lengwa!
Eti mwanadiplomasia na diplomacy inamhitaji! Hivi huwa mnatumia akili gani kuleta hoja zilizoathirika humu jamvin? Yeye alifanya nini kipindi diplomacy alikuwa anainyonya kama pipi ? Hivi kumpenda kwake huko unasahau mgogoro wa Malawi? Rwanda je????acha unafiki mjomba!

Masuala ya Malawi na Rwanda yana Uhusiano gani na Hoja yake ya Utekwaji Watu Kulikokithiri nchini Tanzania? Kuna Watu hapa JamiiForums ni Maduduna ( Wapumbavu ) hadi mnakera.
 
Masuala ya Malawi na Rwanda yana Uhusiano gani na Hoja yake ya Utekwaji Watu Kulikokithiri nchini Tanzania? Kuna Watu hapa JamiiForums ni Maduduna ( Wapumbavu ) hadi mnakera.
Wewe ndo mpumbavu ! Masuala ya kutekwa watu yameanza leo??? Mbona unakuwa popoma kiasi hicho??? Soma historia acha upumbavu wako!!


Mwanajf unaamini maneno ya mwanasiasa mfu kwamba eti kutekwa watu ni utamaduni mpya !! Stupid and shame on you!!

Watu wanstekwa Hata nchi zilizoendelea sembuse nyinyi waswahili
 
Wewe ndo mpumbavu ! Masuala ya kutekwa watu yameanza leo??? Mbona unakuwa popoma kiasi hicho??? Soma historia acha upumbavu wako!!


Mwanajf unaamini maneno ya mwanasiasa mfu kwamba eti kutekwa watu ni utamaduni mpya !! Stupid and shame on you!!

Watu wanstekwa Hata nchi zilizoendelea sembuse nyinyi waswahili

Kwa maelezo yako tu haya yaliyojaa Ududuna ( Upumbavu ) mtupu inaonyesha Wewe ni Miongoni mwa Watekaji Watu na Usiyejulikana Mwandamizi kabisa ndani ya Tanzania yetu hii. Nashukuru kwa Kujipambanua na Kujiweka pia wazi mwenyewe japo kwa njia ya Kificho. Sasa mnaanza Kuumbuka taratibu kwani Laana za Mliowatesa na hata kuwapa Tiketi za Lazima pasipo ridhaa zao kwenda Udongoni ( Mavumbini ) sasa zinaanza Kuwateseni na zitawatesa sana tu.
 
Kujionyesha kwamba unampinga kwa hoja ya yeye kuwa Rais ni hoja fungati tu ya kuonekana kwamba humtaki ili ufikishe ujumbe lengwa!
Eti mwanadiplomasia na diplomacy inamhitaji! Hivi huwa mnatumia akili gani kuleta hoja zilizoathirika humu jamvin? Yeye alifanya nini kipindi diplomacy alikuwa anainyonya kama pipi ? Hivi kumpenda kwake huko unasahau mgogoro wa Malawi? Rwanda je????acha unafiki mjomba!
Huo mgogoro wa Malawi aliuleta Membe? Na huo wa Rwanda aliuleta Membe?Mgogoro wa Malawi ulianzishwa na uongozi wa Malawi wenyewe, na Membe akiwa kama foreign minister akatamka hadharani hatambui madai ya Malawi, na kwamba Tanzania itakuwa tayari kwa lolote kuhakikisha mipaka yake inalindwa. Na ni kutokana na msimamo wake huo ndio maana mgogoro ukafikishwa hadi kwa viongozi wenye heshima zao Afrika ili kuutatua! Kumbe ulitarajia kifanyike nini zaidi ya hapo?

Tuje Rwanda! Hivi kuna mwenye macho na masikio asiyefahamu kwamba mgogoro wa Rwanda ulianzishwa na Kagame, kisa tu alishauriwa na JK akae meza moja na waasi wa Rwanda ili kutatua migogoro isiyoisha! At the end mgogoro ukaisha na ndio maana PK alikuja Dar es salaam somewhere in May 2015! Hapo napo ulitarajia Membe afanye nini tofauti?!

Hivi unafahamu lolote wewe kuhusu Tanzania na international diplomacy?
 
Unapoona mtu mwenye IQ kubwa anatoa neno ni lazima utafakari kabla hujakurupuka kujibu!!

Hapo kwenye red alikua ana maanisha nini huyu mwanadiplomasia/Jasusi wa kitanzania?
Heee, vipi tena. Mbona leo mambo mengi yananipita pembeni hata nisielewe ninachosoma?

Red, naziona katika maandishi ambayo ni maneno yalisemwa na mtu mwenye IQ kubwa nyingine, lakini yeye sio 'Mwanadiplomasia Nguli! au? In fact huyu wa pili , hilo neno diplomasia halimo kabisa katika kamusi yake.

Sasa sielewi, sijui, labda nahitaji mawani ya kusomea.
 
Huo mgogoro wa Malawi aliuleta Membe? Na huo wa Rwanda aliuleta Membe?Mgogoro wa Malawi ulianzishwa na uongozi wa Malawi wenyewe, na Membe akiwa kama foreign minister akatamka hadharani hatambui madai ya Malawi, na kwamba Tanzania itakuwa tayari kwa lolote kuhakikisha mipaka yake inalindwa. Na ni kutokana na msimamo wake huo ndio maana mgogoro ukafikishwa hadi kwa viongozi wenye heshima zao Afrika ili kuutatua! Kumbe ulitarajia kifanyike nini zaidi ya hapo?

Tuje Rwanda! Hivi kuna macho na masikio asiyefahamu kwamba mgogoro wa Rwanda ulianzishwa na Kagame, kisa tu alishauriwa na JK akae meza moja na waasi wa Rwanda ili kutatua migogoro isiyoisha! At the end mgogoro ukaisha na ndio maana PK alikuja Dar es salaam somewhere in May 2015! Hapo napo ulitarajia Membe afanye nini tofauti?!

Hivi unafahamu lolote wewe kuhusu Tanzania na international diplomacy?

Kiongozi unapoteza sana muda wako Kumuelewesha huyo Duduna ( Pumbavu ) Mkomavu.

Cc: Lucas philipo
 
Wewe ndo mpumbavu ! Masuala ya kutekwa watu yameanza leo??? Mbona unakuwa popoma kiasi hicho??? Soma historia acha upumbavu wako!!


Mwanajf unaamini maneno ya mwanasiasa mfu kwamba eti kutekwa watu ni utamaduni mpya !! Stupid and shame on you!!

Watu wanstekwa Hata nchi zilizoendelea sembuse nyinyi waswahili
Kwa mchango huu hapa unajisikia umetoa bonge la jibu sahihi kabisa kuhusu tatizo la utekaji na maonevu mengine yanayotokea sasa Tanzania!
Taratibu, tutafika tu kama huko ndiko mnakotupeleka.
 
Wewe ndo mpumbavu ! Masuala ya kutekwa watu yameanza leo??? Mbona unakuwa popoma kiasi hicho??? Soma historia acha upumbavu wako!!


Mwanajf unaamini maneno ya mwanasiasa mfu kwamba eti kutekwa watu ni utamaduni mpya !! Stupid and shame on you!!

Watu wanstekwa Hata nchi zilizoendelea sembuse nyinyi waswahili
Ndo una halalisha kutekana kuliko shamiri awamu ya Magufuli?
 
Ahhhhhh maneno mengi, watanzania wenye akili kama zako wako wengi. Hamjui mnakokwenda wala mnalolitaka. Leo hata mjinga kiasi gani akisema kitu mradi anaonekana kutofautiana na utawala huu makini mnambeba na kumpamba. Kuna wakati najiuliza hivi kama CCM ni chama chenye watu makini haiwezi kuwatupia jambo njiani mkalikazania afu mkajikuta mwishoni hamna chenu.CHADEMa nawashauri piganieni sera zenu. Hawa CCM waacheni wenyewe. Mnapotezwa sana kwenye track ma mnaingia kichwa kichwa. Badilikeni kama mnataka kuwa wapinzani.
Huo mgogoro wa Malawi aliuleta Membe? Na huo wa Rwanda aliuleta Membe?Mgogoro wa Malawi ulianzishwa na uongozi wa Malawi wenyewe, na Membe akiwa kama foreign minister akatamka hadharani hatambui madai ya Malawi, na kwamba Tanzania itakuwa tayari kwa lolote kuhakikisha mipaka yake inalindwa. Na ni kutokana na msimamo wake huo ndio maana mgogoro ukafikishwa hadi kwa viongozi wenye heshima zao Afrika ili kuutatua! Kumbe ulitarajia kifanyike nini zaidi ya hapo?

Tuje Rwanda! Hivi kuna macho na masikio asiyefahamu kwamba mgogoro wa Rwanda ulianzishwa na Kagame, kisa tu alishauriwa na JK akae meza moja na waasi wa Rwanda ili kutatua migogoro isiyoisha! At the end mgogoro ukaisha na ndio maana PK alikuja Dar es salaam somewhere in May 2015! Hapo napo ulitarajia Membe afanye nini tofauti?!

Hivi unafahamu lolote wewe kuhusu Tanzania na international diplomacy?
 
Nchi gani zilizoendelea watu kutekwa ni Jambo la kawaida? Kama zipo huwa kuna maelezo yoyote wanapopatikana na polisi? au hugeuka mabubu ghalfla wakiwa huru?
Huwa wanaachiliwa tu na watekaji wao, wanawatoroka au wanapatikana na polisi?
Utekaji wa kishamba.
Wewe ndo mpumbavu ! Masuala ya kutekwa watu yameanza leo??? Mbona unakuwa popoma kiasi hicho??? Soma historia acha upumbavu wako!!


Mwanajf unaamini maneno ya mwanasiasa mfu kwamba eti kutekwa watu ni utamaduni mpya !! Stupid and shame on you!!

Watu wanstekwa Hata nchi zilizoendelea sembuse nyinyi waswahili
 
Back
Top Bottom