Ugomvi kidogo anataka tuachane

Ugomvi kidogo anataka tuachane

Azoge Ze Blind Baga

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2019
Posts
455
Reaction score
1,729
Wakuu salama hapa

Hii ndoa yangu ya mbalimbali ina changamoto sana

Mimi naishi mkoa flani ambako napiga harakati za hapa na pale na mke wangu yupo mkoa wa jirani ameajiriwa huko

Tumefunga ndoa na tuna watoto . Kiukweli naweza sema sijafaidi matunda ya ndoa yani ile kuishi na mke ni mwaka wa 9 huu sikai na mke ni kutembeleana tu na mimi ndo huwa namtembelea zaidi kwa ajili ya kuwaona watoto na kula mbususu

Ila kama mnavyojua binadamu hatujakamilika ingawa tunaishi mbalimbali kwa miaka mingi migogoro ya hapa na pale haiishi.

Na kila tukiwa na ugomvi mdogo tu mke atapiga simu kwa ndugu kunishtakia na ataanza kelele za kutaka kuachana.

Sometimes najiuliza huyu mwanamke ana upendo kweli na mimi au napoteza muda tu maana tunakaa mbalimbali miaka mingi nikimkosea kidogo anakimbilia kusema tuachane bora aishi mwenyewe awe msimbe na mdangaji.

Nimemshauri aombe uhamisho aje tuishi pamoja labda hii migogoro ya hapa na pale itapungua anasema hawezi kuja kukaa pamoja na mimi n

Sasa wadau huyu mwanamke nimkalie kimya tu niendelee na life langu au hata sijui nimfanyaje.

Miaka yote tuliyoishi huyu mwanamke alikopa akajenga nyumba hapa ninapoishi mimi na nimefanya uendelezaji wa haya makazi.

Natamani niimwachie hii nyumba akae na watoto. Maana yeye anasema hawezi kuja kuishi hapa na mimi wakati nyumba ni yake sasa kuna faida gani mi kuendelea kuishi hapa na alishatamka mara kibao hapa hawezi kuja kukaa na mimi hata akihamia mkoa huu hawezi kuishi na mimi. Nipo njia panda na hii ndoa yangu ya mbalimbali.

Ushauri tafadhali.
 
Hili wala halikuhitaki ushauri, hapo hakuna ndoa bali unalea watoto wako tu Bro,

Usiendelee kupoteza muda wako,ugomvi kidogo anageuka mpayukaji wakati mambo yenu ni siri yenu,kukutamkia muachane ina maana hakufeel na hakuhitaji tena,

To be honest huna mke mkuu,

Samahani lakini.
 
Binadamu ni vigumu kuelezea yote lazima kuna mengine au udhaifu wako unauficha

Yeye kajenga nyumba hapo unapoishi na amekataa kuja kuishi hapo na sio sababu ya kazi yake hapana bali hakutaki wewe.

Umemuomba ukaishi nae pamoja na watoto hilo nalo hataki.
Inaonekana labda unampiga sana au una tabia ya ulevi au mengine unayojua wewe na hutaki kuyasema

Kama yote hayo huna pia basi yeye ndio ana mwanaume mwingine na kikwazo ni wewe maana kapata mtu anaemjali zaidi ( huwa wanajidanganya hivyo wengi)

Umekaa nae mbali kwa mda mrefu na maisha kwa kazi ndio yamefanya muwe mbalimbali ila uamininfu na subra imeshindikana kwake

Mkuu oa mwanamke mwingine weka ndani hapo hapo ila jipange pa kwenda akijua anakutimua hapo na hiyo ndio uwezo pekee alionao

Oa baba au una side chick na ameisha zaa
 
Unaishi kwenye nyumba aliyojenga ila anasema hata akihamia hapo ulipo hawezi kuishi na wewe.

Wanawake wanachukulia maisha kama kitu so simple. Kuweza kumudu kuishi mwenyewe siyo vyepesi, utaishia kuwa kahaba tu.

Ongea naye, pengine mtaelewana.
 
Unaishi kwenye nyumba aliyojenga ila anasema hata akihamia hapo ulipo hawezi kuishi na wewe.

Wanawake wanachukulia maisha kama kitu so simple. Kuweza kumudu kuishi mwenyewe siyo vyepesi, utaishia kuwa kahaba tu.

Ongea naye, pengine mtaelewana.
Kasema bora awe msimbe na mdangaji ila anataka aishi mwenyewe na hii kauli yake kila tukiwa na kimgogoro
 
Unaishi kwenye nyumba aliyojenga ila anasema hata akihamia hapo ulipo hawezi kuishi na wewe.

Wanawake wanachukulia maisha kama kitu so simple. Kuweza kumudu kuishi mwenyewe siyo vyepesi, utaishia kuwa kahaba tu.

Ongea naye, pengine mtaelewana.
Amekazana anataka talaka, utakuta kuna mshkaji ndio anamlazimisha achukue talaka amuoe
Haiwezekani ugomvi kidogo anadai talaka
Ana lake jambo
 
Hizi ndoa hizi balaa kweli kweli,vumilianeni tu mkishafikisha miaka 60 mtakuwa marafiki,ila kwa sasa damu bado zinachemka sana...
 
Hakuna ndoa hapo. Anza kufungasha mapema. Cha kwanza hama hapo pangisha bila kumwambia akishajua atakutafuta litazuka bonge la mgogoro usiombe msamaha kaza mpaka kikao cha familia kisha uulize hatima ya ndoa yenu kama ipo ama la. Kama ipo ahamie ulipo
Na huu ndio uamuzi haswa wa kuzingatia
 
Tafuta kiwanja ujenge. Ujenge kwako peke yako.

Ulishafanya makosa ya kujenga nyumba na mwanamke.

Nasema, usirudie tena kujenga nyumba na mwanamke.

Hata wanawake siwashauri wajenge nyumba na wanaume wao.

Ukitaka kuishi kwa raha mwanaume uwe na nyumba yako uliyoijenga peke yako kwa asilimia zote, mwanamke ukitaka uwe na furaha, hakikisha una nyumba pia.

Huyo mwanamke usimbembeleze, hata akijirudi usikubali.

Kuanzia sasa acha kula mbususu yake ili kuepuka magonjwa.

Usirudi nyuma. Jenga kwako, tafuta mwanamke.

Inawezekana unaona ugumu kujenga. Fanya ujenge hata rumu moja tu.
 
Amekazana anataka talaka, utakuta kuna mshkaji ndio anamlazimisha achukue talaka amuoe
Haiwezekani ugomvi kidogo anadai talaka
Ana lake jambo
Na hata akipewa talaka huenda asiolewe na anayemrubuni,au hata akiolewa hawezi kuaminika huko aendako,kama karubuniwa akaomba talaka kwa mumewe aliye zaa naye basi inawezekana kabisa akaja kurubuniwa tena kwa mwingine kama ataolewa huko anapopataka,

Kifupi ukiweza kumrubuni Mwanamke akaomba talaka kwa Mumewe basi huyo hafai tena hata kuaminiwa japo kupewa uchafu ili akautupe jalalani.
 
Hama hapo,jiongeze ndugu,

Na yupo kutafuta sababu muachane,
 
Back
Top Bottom