Uganda yakana kutomuunga mkono mgombea wa Kenya

comrade igwe

JF-Expert Member
Jan 12, 2015
7,295
3,939
_93901970_yoweri_museveni_bbc_interview_640x360_bbc_nocredit.jpg

Rais Yoweri Museveni wa Uganda

Taifa la Uganda limekana madai kwamba halikumuunga mkono waziri wa maswala ya kigeni kutoka Kenya Amina Mohammed kugombea wadhfa wa mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika

Bi Mohammed ambaye alikuwa anapigiwa upatu kushinda wadhfa huo aliyalaumu mataifa ya Afrika mashariki kwa kuihadaa Kenya na kutaka uchunguzi ufanywe.

Vyombo vya habari nchini Kenya vimesema kuwa mataifa ya Uganda, Burundi na Djibout hayakumpigia kura Amina Mohammed katika raundi ya mwisho na hivyobasi kumsaidia mgombea wa Chad Moussa Faki Mahamat kushindwa kiti hicho.

Bw Mahamat alipata thuluthi mbili ,ama kura 36 na kutangazwa mshindi.
 
Basi kama sisi na uganda tumemuunga mkono huyo mama basi na kwa kuwa Chad ni Francophone basi kuna francophone hapa Afrika mashariki alimuunga mkono chad labda watakua akina Urakoze wote wawili
 
Sasa huyo bi mkubwa anasema uchunguzi ufanyike ili nini na iweje? kwani nn bana kama kakosa kakosa tu waende Kurasini wakamuone Deus Kibamba awape somo
 
Tulimpigia mara mbili round zote wale je parle's france waliwafuata ndugu zao mpaka
N'Djamena
Kama tulimpigia Balozi Amina wa Kenya basi vyombo vya habari Kenya havisemi wazi. Havitamki ya kuwa "Tunashukuru ndugu zetu wa Tanzania walitukumbuka na kutuunga mkono". Kauli hiyohaisikiki kabisa. Daah!
 
Back
Top Bottom