Jannatul Firdaus
JF-Expert Member
- Aug 4, 2026
- 353
- 789
Timu ya taifa ya Uganda ya vijana chini ya umri wa miaka 23 ‘Kobs’, imejitoa kwenye mashindano ya kuwania kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika kwa Vijana weny umri chini ya miaka 23 (AFCON U23) 2027.
Uamuzi huo umekuja baada ya Shirikisho la Soka Uganda (FUFA) kushindwa kupata fedha za kutosha kumudu gharama za mashindano hayo.
Uganda ilikuwa imepangwa kucheza dhidi ya Ethiopia katika raundi ya kwanza ya kufuzu.
Mchezo wa kwanza ulitarajiwa kuchezwa Ethiopia Septemba 28, huku mchezo wa marudiano ukipangwa kupigwa Uganda, Oktoba 6, mwaka huu.
Hata hivyo, FUFA imesema imeamua kuiondoa Uganda kwenye mashindano hayo kwa sababu hakukuwa na fedha za kutosha kuiwezesha timu kushiriki kikamilifu.
Uamuzi huo umekuja baada ya Shirikisho la Soka Uganda (FUFA) kushindwa kupata fedha za kutosha kumudu gharama za mashindano hayo.
Uganda ilikuwa imepangwa kucheza dhidi ya Ethiopia katika raundi ya kwanza ya kufuzu.
Mchezo wa kwanza ulitarajiwa kuchezwa Ethiopia Septemba 28, huku mchezo wa marudiano ukipangwa kupigwa Uganda, Oktoba 6, mwaka huu.
Hata hivyo, FUFA imesema imeamua kuiondoa Uganda kwenye mashindano hayo kwa sababu hakukuwa na fedha za kutosha kuiwezesha timu kushiriki kikamilifu.