Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,513
- 9,309
Ripoti za vyombo vya habari Uganda vinakariri mashahidi wakisema kwamba Francis Kalibala, aligongwa na gari la jeshi la Uganda UPDF wakati msafara wa Bobi Wine ulikuwa unarudi Kampala kutoka Masaka katika kampeni.
Katika taarifa kupitia mitandao ya kijamii Bobi Wine amesema “nasikitika kutangaza kifo cha mmoja wa walinzi wangu Francis Kalibala aliyegongwa na gari la jeshi namba H4DF 2382 ambalo liliziba njia karibu na Busega na kutuzuia kupita.” Ameandika Bobi Wine na kuongeza kusema“Francis amefariki mda mfupi baada ya kufika katika hospitali ya Rubaga.”
Lakini msemaji wa jeshi la Uganda Brig. Flavia Byekwaso amesema katika taarifa kwa vyombo vya habari kwamba Francis alianguka kutoka kwa gari lililokuwa linaendeshwa kwa mwendo wa kasi.
“Francis hakugongwa na gari la jeshi la UPDF. Alianguka kutoka kwa gari namba UBF 850Z .” amesema Byekwaso katika ujumbe wa twitter.
Waandishi wa habari wajeruhiwa vibaya
Kabla ya tukio hilo, waandishi kadhaa wa habari walishambuliwa na polisi na kujeruhiwa vibaya.
Waandishi hao walikuwa wanafuatilia tukio ambalo polisi walimzuia Bobi Wine kufanya kampeni na kuzua makabiliano kati ya polisi na wafuasi wa Bobi wine katika mji wa Masakaa.
Waandishi walipigwa na kujeruhiwa na mabomu ya kutoa machozi.
Wamelazwa hospitalini mjini Masaka.
Miongoni mwao ni mpiga picha wa televisheni ya Bobi Wine ya Ghetto TV, Ashraf Kasirye, mwandishi wa shirika la habari la Nation Media Group – NTV Ali Mivule.
“Gesi ya kutoa machozi ilitumika kutawanya wafuasi wa Bobi Wine na kwa bahati mbaya waandishi wa habari walijeruhiwa,” amesema msemaji wa polisi Fred Enanga.
Katika taarifa kupitia mitandao ya kijamii Bobi Wine amesema “nasikitika kutangaza kifo cha mmoja wa walinzi wangu Francis Kalibala aliyegongwa na gari la jeshi namba H4DF 2382 ambalo liliziba njia karibu na Busega na kutuzuia kupita.” Ameandika Bobi Wine na kuongeza kusema“Francis amefariki mda mfupi baada ya kufika katika hospitali ya Rubaga.”
Lakini msemaji wa jeshi la Uganda Brig. Flavia Byekwaso amesema katika taarifa kwa vyombo vya habari kwamba Francis alianguka kutoka kwa gari lililokuwa linaendeshwa kwa mwendo wa kasi.
“Francis hakugongwa na gari la jeshi la UPDF. Alianguka kutoka kwa gari namba UBF 850Z .” amesema Byekwaso katika ujumbe wa twitter.
Waandishi wa habari wajeruhiwa vibaya
Kabla ya tukio hilo, waandishi kadhaa wa habari walishambuliwa na polisi na kujeruhiwa vibaya.
Waandishi hao walikuwa wanafuatilia tukio ambalo polisi walimzuia Bobi Wine kufanya kampeni na kuzua makabiliano kati ya polisi na wafuasi wa Bobi wine katika mji wa Masakaa.
Waandishi walipigwa na kujeruhiwa na mabomu ya kutoa machozi.
Wamelazwa hospitalini mjini Masaka.
Miongoni mwao ni mpiga picha wa televisheni ya Bobi Wine ya Ghetto TV, Ashraf Kasirye, mwandishi wa shirika la habari la Nation Media Group – NTV Ali Mivule.
“Gesi ya kutoa machozi ilitumika kutawanya wafuasi wa Bobi Wine na kwa bahati mbaya waandishi wa habari walijeruhiwa,” amesema msemaji wa polisi Fred Enanga.