Uganda: Chama tawala NRM wataka Museven aongoze hadi kifo

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,193
25,504
Chama tawala cha nchini Uganda-NRM wamemtaka Rais Yoweri Kaguta Museveni aongoze hadi kifo. Wamedai kuwa Uganda nzima hakuna anayeweza kuwa Rais isipokuwa Rais Museveni.

Tayari NRM wameanza mchakato wa kutaka marekebisho ya katiba yatakayomuwezesha Rais Museveni kugombea Urais mwaka 2021 ingawa atakuwa amevuka umri unaoruhusiwa kikatiba. Katiba ya Uganda kama ilivyo sasa inataka mgombea asiwe na umri unaozidi miaka 75.

Mwaka 2021,Rais Museveni atakuwa na miaka 76. NRM wamesema umri hauwezi kuwa kikwazo kwakuwa ibara ya katiba itabadilishwa. Wametaka wote wanaopinga jambo hilo wachunguzwe. Hadi sasa,Rais Museveni hakusema chochote kuhusu jambo hilo. Amekuwa madarakani tangu mwaka 1986.

Chanzo: ITV Habari
 
Harafu huyo ni lafiki wa Magufuri,,na hao NRM ni malafiki wa CCM?? Hivi kwa nini vyama tawala vya africa vinafanana sana akili na mawazo??,yaani hawajui kupinga wanachoambiwa na viongozi wao hata kama ni ujinga,,anyway sisi ya Uganda hayatuhusu watajijua
 
....Hiki kipande cha hii paragraph chenye haya maneno kuntu ya the late Mwl Nyerere nimekichota kutoka kwenye uzi wa member mmoja humu ndani........

.....''Plato, Myunani wa kale, alipendekeza kuwa wanafalsafa ndio wanafaa kuwa watawala wa nchi, maana wanasifa mbili muhimu: kwanza, wana uwezo wa kutawala na pili hawapendi kutawala. Kwahiyo, Jamhuri ya Plato ilikuwa na sheria ya kuwalazimisha wanafalsafa kutawala kwa zamu; na mtu zamu yake ya kutawala ikiisha, atafurahi sana kurudia kazi zake za falsafa ambazo ndizo hasa anazipenda. Lakini nchi zetu hazitawaliwi na wanafalsafa wa Plato; watawala wetu ni wanasiasa wa kawaida ambao wanapenda sana kutawala hata kama hawana uwezo wa kutawala, na wakisha chaguliwa hawatoki kabisa bila kulazimishwa. Si busara kuwaachia wao wenyewe ndio wawe waamuzi wa lini waache kuwa watawala''....
 
Nawasikitikia waganda, Mseveni ndo kisha chukua hivyo term nyingine. Ni umugabe mpaka anakufa. Kuna la kujifunza pia. wanachama wa chama cha NRM wanataka kubadilisha katiba ili Mseveni agombee urais mpaka kufa, mhusika mkuu ambaye ni Mseveni yuko kimya.

Habari za rais wetu kuongezewa muda zimeshaanza na hata hata miaka 2 haijafika, kelele hizi zitazidi kuongezeka hasa awamu ya pili, ungetarajia rais muungwana awakemee watu hawa ili hili jambo lisiwakae akilin. Kama Kagame, mwanzoni wanakuwa kimya, mwishoni wanasema wao wanafuata matakwa ya wananchi.
 
Yule wa Kenya kanunua magari washawasha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka huu.

Huyu wa Uganda ni rais wa maisha tayari.

Kule Rwanda kila mtu anajua kinachoendelea.

Pale Jamhuri ya Demokrasia ya Congo, kiranja wao amehairisha uchaguzi mwaka huu kwakuwa serikali haina pesa.

Burundi ndio aibu...

Nitakuja kumalizia kuhusu hapa kwetu...
 
Madikteta ndivyo walivyo! Na hapa nyumbani napo wale ZERO BRAINS nao wameshaanza kumpigia debe fisadi, mwizi na dikteta uchwara eti atawale milele! Sijui kwa lipi hasa! Kweli mtaji wa wahuni na mafisadi ni wale waliopitia shule za kata na wenye uwezo finyu wa kuchanganua mambo kwa kina.

Chama tawala cha nchini Uganda-NRM wamemtaka Rais Yoweri Kaguta Museveni aongoze hadi kifo. Wamedai kuwa Uganda nzima hakuna anayeweza kuwa Rais isipokuwa Rais Museveni.

Tayari NRM wameanza mchakato wa kutaka marekebisho ya katiba yatakayomuwezesha Rais Museveni kugombea Urais mwaka 2021 ingawa atakuwa amevuka umri unaoruhusiwa kikatiba. Katiba ya Uganda kama ilivyo sasa inataka mgombea asiwe na umri unaozidi miaka 75.

Mwaka 2021,Rais Museveni atakuwa na miaka 76. NRM wamesema umri hauwezi kuwa kikwazo kwakuwa ibara ya katiba itabadilishwa. Wametaka wote wanaopinga jambo hilo wachunguzwe. Hadi sasa,Rais Museveni hakusema chochote kuhusu jambo hilo. Amekuwa madarakani tangu mwaka 1986.

Chanzo: ITV Habari
 
Chama tawala cha nchini Uganda-NRM wamemtaka Rais Yoweri Kaguta Museveni aongoze hadi kifo. Wamedai kuwa Uganda nzima hakuna anayeweza kuwa Rais isipokuwa Rais Museveni.

Tayari NRM wameanza mchakato wa kutaka marekebisho ya katiba yatakayomuwezesha Rais Museveni kugombea Urais mwaka 2021 ingawa atakuwa amevuka umri unaoruhusiwa kikatiba. Katiba ya Uganda kama ilivyo sasa inataka mgombea asiwe na umri unaozidi miaka 75.

Mwaka 2021,Rais Museveni atakuwa na miaka 76. NRM wamesema umri hauwezi kuwa kikwazo kwakuwa ibara ya katiba itabadilishwa. Wametaka wote wanaopinga jambo hilo wachunguzwe. Hadi sasa,Rais Museveni hakusema chochote kuhusu jambo hilo. Amekuwa madarakani tangu mwaka 1986.

Chanzo: ITV Habari
Jinga kabisa madarakani kabla hata sijazaliwa?
 
Back
Top Bottom