#COVID19 Uganda bado Covid19 ni tatizo, lockdown ipo palepale

RAKI BIG

JF-Expert Member
Apr 26, 2020
394
456
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kuwa Shule, makanisa, misikiti, vilabu, vilabu vya usiku, maeneo ya kufanyia mazoezi na saluni za urembo zitaendelea kufungwa ili kuepuka maambukizi ya virusi vya corona.

Museveni amesema kuwa si rahisi kwa maeneo hayo kufuata masharti ya kutochangamana. Rais Museveni pia amesema muda wa kuwa ndani ya nyumba utaendelea kuwa kuanzia saa moja usiku mpaka saa kumi na mbili kamili asubuhi kwa siku 21 zaidi.

Makanisa, vilabu vya pombe, vilabu vya usiku , maeneo ya kufanya mazoezi na sauna yataendelea kufungwa kwa siku 21, huku kufungua shule kwa wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mitihani kukiwa kumeahirishwa wakisubiri kwa mwezi mmoja.

''Tumeamua kuahirisha kufunguliwa kwa shule kwa wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mitihani kwa mwezi mmoja zaidi tukijiandaa zaidi na kutazama hali ilivyo''.Alisema

Usafiri wa umma unatarajiwa kurejeshwa Alhamisi ya wiki hii kwa masharti maalum.

BBC Swahili
 
Hahah daah 21 days more

Waganda wanajiuliza hivi Covid iliyopo Uganda ndio iliyoko Bongo?Mbona huko watu wanapiga bata,shule zinafunguliwa,Parte after parte kama kawa,Ligi kuu inaanza fresh kabisaa.

Kwa E/Africa atakaesanda huu mziki wa Lockdown ni Kenya maana sasa hivi wako hoi bin taaban.
 
Hahah daah 21 days more

Waganda wanajiuliza hivi Covid iliyopo Uganda ndio iliyoko Bongo?Mbona huko watu wanapiga bata,shule zinafunguliwa,Parte after parte kama kawa,Ligi kuu inaanza fresh kabisaa.

Kwa E/Africa atakaesanda huu mziki wa Lockdown ni Kenya maana sasa hivi wako hoi bin taaban.
haha huku bongo koona😂 hakuna nadhani ni mwendo wa bata tu..ila namuonea sana huruma trump ana koona 😂 ana maandamano kazi anayo mwaka huu
 
haha huku bongo koona😂 hakuna nadhani ni mwendo wa bata tu..ila namuonea sana huruma trump ana koona 😂 ana maandamano kazi anayo mwaka huu
Hahah Trump jamaa wamemchanganya kabisa aisee mpaka jana ikabidi ashike biblia aende pale mbele ya jengo la kanisa kupiga nayo picha hahah,mara police wake nao wanawapigia magoti waandamanaji hapo Mroto anawacheki tu anasema hiiiiiiiiii i wish i could be IGP.
 
Back
Top Bottom