Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Yaani bado nacheka,
Niko kwenye foleni barabarani, amenifuata muuza icecreem (na baiskeli yake ya Azam, ananifahamu). Akaniuliza, "bro, mjengoni si tarehe 8 mwezi wa pili eh?"
nikamwabia ndiyo, akasema "hapo ccm walipo nakuambia bro, ugali wa moto mboga ya moto na pilipili kali. Yaani wanakula ndiyo lakini machozi machozi yanawamiminika blublublublu na makamasi juu. Wanatamani February isifife. Mi nasubiria tu bro, labda wazuie wabunge wa Chadema wasiingie bungeni."
nimefurahi jinsi huyu kijana alivyoweza kuwasilisha kwa upana kiasi hicho hali halisi ya siasa na uchumi wa nchi yetu kwa kutumia maneno machache hivyo. Huyu kijana hana uwezo wa kutumia internet wala kununua gazeti.
Lakini ana ufahamu kamili wa nini kinaendelea na matarajio yake kwa bunge na wabunge wa upinzani ni thabiti
je, wabunge wa Chadema watamfurahisha au kumkatisha matumaini huyu kijana? Matarajio makubwa namna hii na thabiti ni makubwa mno kwa wabunge wa Chadema kutekeleza?
Niko kwenye foleni barabarani, amenifuata muuza icecreem (na baiskeli yake ya Azam, ananifahamu). Akaniuliza, "bro, mjengoni si tarehe 8 mwezi wa pili eh?"
nikamwabia ndiyo, akasema "hapo ccm walipo nakuambia bro, ugali wa moto mboga ya moto na pilipili kali. Yaani wanakula ndiyo lakini machozi machozi yanawamiminika blublublublu na makamasi juu. Wanatamani February isifife. Mi nasubiria tu bro, labda wazuie wabunge wa Chadema wasiingie bungeni."
nimefurahi jinsi huyu kijana alivyoweza kuwasilisha kwa upana kiasi hicho hali halisi ya siasa na uchumi wa nchi yetu kwa kutumia maneno machache hivyo. Huyu kijana hana uwezo wa kutumia internet wala kununua gazeti.
Lakini ana ufahamu kamili wa nini kinaendelea na matarajio yake kwa bunge na wabunge wa upinzani ni thabiti
je, wabunge wa Chadema watamfurahisha au kumkatisha matumaini huyu kijana? Matarajio makubwa namna hii na thabiti ni makubwa mno kwa wabunge wa Chadema kutekeleza?