Ugali sasa ni chakula cha anasa kuliko wali

Ugali sasa ni chakula cha anasa kuliko wali

SIKUKUU TULIKULA UGALI NA MAMBOGAMBOGA YA KUTOSHA MAANA WALI UNALIWA DAILY
 
ubungo riverside mkuu, kwenye maduka ya mchele......yaani hadi 1600 unapata
Itabidi nipange safari kuja huko, niko kibamba. Wanatuuzia utafikiri ni watalii.
Ila hata maili moja nasikia bei yao ni poa. Asante kwa taarifa.
 
Kufuatia ongezeko kubwa la bei ya unga Jijini Dar es Salaam na labda sehemu zingine za nchi, sasa ni bayana kuwa ni rahisi mtu kumudu kula wali kuliko kula ugali. Kilo ya unga katika baadhi ya mitaa inauzwa hadi Sh. 2,200/= ilhali kilo ya mchele inaweza kupatikana kwa Sh. 2,000/=.

Kufuatia hali hii tujiandae kwa yafuatayo:

-ugali kuwa chakula cha sherehe, harusi na matukio mengine maalumu maana si chakula cha gharama?
-wanafunzi na wafungwa kuanza kutumia wali kama chakula kikuu na ugali kama chakula cha anasa
-nyumba kuu yaani familia kufurahia wali huku michepuko wakigeukia ugali maana si ndio chakula cha anasa?
-wataalamu wa mapishi na lishe watalazimika kubuni pilau ya ugali ili ichukue pahala pa pilau ya wali ambayo sasa si chakula aghali na special tena
-kula ugali kila siku kunaweza kupelekea kuikosa mbingu maana ni kupenda anasa za dunia.
NK

[HASHTAG]#liferealities[/HASHTAG]
Aseee kwel kula ugal ni anasa sahv .hii inatokana na mahindi kugombewa na binadam na mifugo sabb ndo huwa yanatumikaa sanaa kuandaa vyakula vya mifugo kuliko mchele
 
Najaribu kupiga picha nini kitatokea kwa wanafunzi wa shule za bweni watakapotangaziwa "kutokana na kupanda kwa bei ya Sembe chakula cha kila siku kinakuwa wali,ugali inakuwa mara moja kwa wiki siku za weekend au sikukuu "
Wataandamana sababu wali unakinaishaa sanaa
 
Huku kwetu mbona tunanunua kilo mbili za unga shilingi 7,000
 
Usiwasingizie wakulima, wakulima hawapangi bei kutokana na ubepari uliopo nchini mwetu, wanaopanga bei ni walanguzi,madalali na wafanyabiashara, wakulima wanaburuzwa tu.
Dalali hawezi kuuza
debe 1/sh 1200, halafu mkulima auze debe 1/sh 500.

Ni lazma mkulima auze debe 1/sh 1100, na hapo ndipo mlanguzi au dalala naye auze debe 1/sh 1200.

Hivyo mkulima ndiye anayepanga bei.
 
Dalali hawezi kuuza
debe 1/sh 1200, halafu mkulima auze debe 1/sh 500.

Ni lazma mkulima auze debe 1/sh 1100, na hapo ndipo mlanguzi au dalala naye auze debe 1/sh 1200.

Hivyo mkulima ndiye anayepanga bei.
Na vilevile kupanda kwa bei, ukiachana na sababu nyingine; kunategemeana sana na kupatikana kwa bidhaa husika sokoni, aidha kwa mazingira/isiyo bahati, au kwa makusudi/kwa kupanga.(Yaani kuipoteza/kuificha/kuiadimisha kwa makusudi bidhaa fulani sokoni kwa madhumuni ya kuipa thamani zaidi.)

Na hapa si walanguzi/madalali tu, hata wakulima hususani wa kati na wakubwa hufanya haya.

Karibuni tule chapati kwa "mkorofisho" wa samaki wakuu, ugali tumewaachia "vibompa"[emoji119] [emoji119] [emoji119]
 
mkuu umetengua mbavu zangu, pilau ya ugali...hahahahahahhhaa
 
Kufuatia ongezeko kubwa la bei ya unga Jijini Dar es Salaam na labda sehemu zingine za nchi, sasa ni bayana kuwa ni rahisi mtu kumudu kula wali kuliko kula ugali. Kilo ya unga katika baadhi ya mitaa inauzwa hadi Sh. 2,200/= ilhali kilo ya mchele inaweza kupatikana kwa Sh. 2,000/=.

Kufuatia hali hii tujiandae kwa yafuatayo:

-ugali kuwa chakula cha sherehe, harusi na matukio mengine maalumu maana si chakula cha gharama?
-wanafunzi na wafungwa kuanza kutumia wali kama chakula kikuu na ugali kama chakula cha anasa
-nyumba kuu yaani familia kufurahia wali huku michepuko wakigeukia ugali maana si ndio chakula cha anasa?
-wataalamu wa mapishi na lishe watalazimika kubuni pilau ya ugali ili ichukue pahala pa pilau ya wali ambayo sasa si chakula aghali na special tena
-kula ugali kila siku kunaweza kupelekea kuikosa mbingu maana ni kupenda anasa za dunia.
NK

[HASHTAG]#liferealities[/HASHTAG]
Daaa poleni sana jaman
 
Mnalalamika nini? Si ilishasemwa hata ikifika mahali mtu akiuza ng'ombe kupata debe moja ya mahindi ni sawa tu? Sasa ni lazima tuishi kwa mwendo kasi wa standard gauge
 
INASIKITISHA KWA KWELI.... ILA NI FAIDA KWA WALE WALIOKUWA WANAPENDA UBWABWA
 
Jana mwenye nyumba aliisikia harufu ya ugali kutoka kwenye chumba changu.
Leo kanilitea notisi ya kupandisha kodi ya chumba. Teh teh teh
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] father house nae kazidi ana pua za aina gani mpaka akasikia harufu ya ugali
 
Back
Top Bottom