Ufoo Saro Atoka Hospitali, Atoa Shukrani Kwa Mungu na Awashukuru Wote!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,719
114,067
Wanabodi
Mwandishi wa Habari wa ITV, Ufoo Saro, ametoka rasmi hospital na leo amefanya Ibada ya Shukrani katika kanisa la KKKT Kibamba ambapo amemshukuru Mungu kwa yote na kutoa shukrani kwa wote waliosimama na yeye wakati wote wa matatizo wakimfariji na kumsupport kwa hali na mali.

Ibada hii ya shukrani imefuatiwa na chakula cha mchana.

Japo nipo hapa na Ufoo yuko accessible, nina maswali yangu fulani ya dukuduku ningetamani nimuulize, ila nahofia kutonyesha vidonda na kumrudisha kwenye machungu anayojaribu kuyasahau.

Wish afike mahali akiri licha ya kumlilia mama yake aliyeondoshwa na Mushi,anapaswa pia kumlilia Mushi despite all the odds kwa sababu ni mzazi mwenzie na baba wa mtoto wake hivyo amekumbwa na double tragedies!.

Naomba tuungane kwa kumpa Ufoo pole kwa yote ila life has to go on!.

Ufoo, welcome back to the game!.

Pasco.

KITAIFA
Ufoo Saro: Niliokoka kufa kutokana na miujiza ya Mungu, namshukuru

ufoo.jpg

Mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro akisoma somo kwenye biblia wakati wa ibada maalumu ya shukrani kwenye Kanisa la (KKKT ) Usharika wa Kibamba nje kidogo ya Jiji la Dare Salaam jana. Picha na Sanjito Msafiri.

Posted Jumatatu,Novemba18 2013 saa 15:24 PM

KWA UFUPI

  • Ni mara ya kwanza Saro kuzungumza tukio hilo tangu aliporuhusiwa kutoka Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu, MOI ya Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa.

Dar es Salaam. Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa risasi na mzazi mwenzake, Anthery Mushi, amefanya ibada na kusema: "Namshukuru Mungu kwa kumponya."


Ni mara ya kwanza Saro kuzungumza tukio hilo tangu aliporuhusiwa kutoka Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu, MOI ya Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa.

Katika ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la Kilutheli Tanzania (KKKT) Usharika wa Kibamba, Jimbo la Magharibi, Ufoo huku akitokwa na machozi na wakati mwingine kushindwa kuzungumza alisema: "Ni miujiza tu ya Mungu yeye kunifanya mimi kuwa hai leo."

Mtangazaji huyo ambaye alilazwa kwa zaidi ya wiki mbili, aliwashukuru watu wote waliomtia moyo, kumsaidia kipindi chote alichokuwa mgonjwa.

"Sina cha kuwalipa, ninawashukuru sana kwa wema wenu, pia kwa kuniombea. Mungu ni mkubwa na amenipigania, naendelea vizuri kwa sasa," alisema na kuongeza:

"Mungu alinisimamia na nyinyi pia mliniombea, hakika sina budi kushukuru kwa kila jambo. Nitasoma zaburi ya 146 katika Biblia Takatifu ili kumshukuru Mungu kwa kunisaidia."

Ufoo alisema kuwa ameamua kumshukuru Mungu kwa sababu siyo watu wote wanaopata matatizo kama yake wanapona.

Mchungaji aliyeongoza misa hiyo iliyoanza saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana, Joseph Maseghe alisema Mungu hakupanga Ufoo afariki dunia kwa kupigwa risasi.

"Mungu bado anakuhitaji, hakupanga ndiyo maana upo nasi leo. Hautakiwi kulia huu ni mwanzo wa maisha yako mengine, usilie unachotakiwa ni kumshukuru Mungu kwa kila jambo," alisema.

Misa hiyo ilihudhuliwa na watu mbalimbali wakiwamo wafanyakazi wa ITV pamoja na Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Grace Kihwelu, Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), John Heche.

Baada ya kumalizika kwa misa hiyo, ndugu na marafiki wa karibu wa Ufoo walialikwa na mtangazaji huyo katika hafla fupi ya chakula cha mchana.

Akizungumza wakati akiwakaribisha wageni katika chakula cha mchana, alisema: "Nimepata pigo kubwa katika maisha yangu, familia yetu sasa haina baba wala mama, kweli namshukuru Mungu na nawaombea kwa Mungu wote walioniombea na kunitakia mema, sijui nimpe nini Mungu, sijui kwa kweli."
Source: Mwananchi.
 
Dah...! Pole yake hadi nilianza kusahau sababu ya katiba,msiba wa Dk.wetu,makontena ya meno ya tembo,Zitto vs Lema,Lema vs Sadiffa na mzee wa vidosho a.k.a Berluscony wa bongo Prof.Kapuyanga.
 
Wanabodi
Mwandishi wa Habari wa ITV, Ufoo Saro, ametoka rasmi hospital na leo amefanya Ibada ya Shukrani katika kanisa la KKKT Kibamba ambapo amemshukuru Mungu kwa yote na kutoa shukrani kwa wote waliosimama na yeye wakati wote wa matatizo wakimfariji na kumsupport kwa hali na mali.

Ibada hii ya shukrani imefuatiwa na chakula cha mchana.

Japo nipo hapa na Ufoo yuko accessible, nina maswali yangu fulani ya dukuduku ningetamani nimuulize, ila nahofia kutonyesha vidonda na kumrudisha kwenye machungu anayojaribu kuyasahau.

Wish afike mahali akiri licha ya kumlilia mama yake aliyeondoshwa na Mushi,anapaswa pia kumlilia Mushi despite all the odds kwa sababu ni mzazi mwenzie na baba wa mtoto wake hivyo amekumbwa na double tragedies!.

Naomba tuungane kwa kumpa Ufoo pole kwa yote ila life has to go on!.

Ufoo, welcome back to the game!.

Pasco.

Paso, tunampa pole sana.Mungu amjalie afya njema na moyo wa uvumilivu kwa double tragedy! LAKINI kama (na nasema kama maana hatuna uhakika) yaliyosemwa ni kweli kuhusu marehemu mzazi mwenzake-dhuluma dhuluma????????, then ajitafakari mara mbili.
 
Paso, tunampa pole sana.Mungu amjalie afya njema na moyo wa uvumilivu kwa double tragedy! LAKINI kama (na nasema kama maana hatuna uhakika) yaliyosemwa ni kweli kuhusu marehemu mzazi mwenzake-dhuluma dhuluma????????, then ajitafakari mara mbili.
Hili pia nilitamani kumuuliza, ila kumuuliza mhanga swali kama hili ni kukosa utu, infact nilitamani hata kuuliza suicide ya risasi mbili!.
Vitu vingine inakubidi unapotezea tuu!.
Pasco
 
Ufoo,hayo ndo maisha kuna raha,huzuni,furaha,chareko nk.na kamwe hujafavhujaumbika pole na karibbu tena ulingoni.
 
Wanabodi
Mwandishi wa Habari wa ITV, Ufoo Saro, ametoka rasmi hospital na leo amefanya Ibada ya Shukrani katika kanisa la KKKT Kibamba ambapo amemshukuru Mungu kwa yote na kutoa shukrani kwa wote waliosimama na yeye wakati wote wa matatizo wakimfariji na kumsupport kwa hali na mali.

Ibada hii ya shukrani imefuatiwa na chakula cha mchana.

Japo nipo hapa na Ufoo yuko accessible, nina maswali yangu fulani ya dukuduku ningetamani nimuulize, ila nahofia kutonyesha vidonda na kumrudisha kwenye machungu anayojaribu kuyasahau.

Wish afike mahali akiri licha ya kumlilia mama yake aliyeondoshwa na Mushi,anapaswa pia kumlilia Mushi despite all the odds kwa sababu ni mzazi mwenzie na baba wa mtoto wake hivyo amekumbwa na double tragedies!.

Naomba tuungane kwa kumpa Ufoo pole kwa yote ila life has to go on!.

Ufoo, welcome back to the game!.

Pasco.

sasa nafasi yake ITV kipoma joto imekwenda na Devotha Minja tola Moro, sasa atakula wapi za Mushi zikiisha???? pole zake
 
Paso, tunampa pole sana.Mungu amjalie afya njema na moyo wa uvumilivu kwa double tragedy! LAKINI kama (na nasema kama maana hatuna uhakika) yaliyosemwa ni kweli kuhusu marehemu mzazi mwenzake-dhuluma dhuluma????????, then ajitafakari mara mbili.

Nashukuru kwa kunisaidia kuandika niliyotarajia kuandika....kama yaliyosemwa ni kweli kuhusu dhuluma basi ajitafakari mara mbili.
 
Hili pia nilitamani kumuuliza, ila kumuuliza mhanga swali kama hili ni kukosa utu, infact nilitamani hata kuuliza suicide ya risasi mbili!.
Vitu vingine inakubidi unapotezea tuu!.
Pasco
We mvae tu ili tuondoe doubt!! Hata akichukia shauri zake.
 
pamoja sana Pasco wa JF,mpe hi Ufoo saroo ila jaqline selembi naye moto sana,vp unamjua huyo dada jaqline selembi? Kama vp pasco nipe namba yake!!!
 
Last edited by a moderator:
sasa nafasi yake ITV kipoma joto imekwenda na Devotha Minja tola Moro, sasa atakula wapi za Mushi zikiisha???? pole zake

Si nasikia alikiwa na spare tires kibao, nasia hata mh: BWEKA TOZI anahusika!!!!?. Basi mparestina hafi njaa......... Atapata na wengine......kufa kufaana.
 
Anashukuru Wote kwa Upuuzi Mkubwa Alioufanya? Nyie Vipi badala Ya Kumchana Live Mnabaki Kumpa Maneno Ya Moyo ili Iweje? ACHENI UNAFIKI WENU HAYAWANI WAKUBWA! Hivi Unadhani Marehemu hakuwa na Malengo Yake Ya Kimaisha ambayo Yalikatishwa na UMACHAME WA Huyo UFOO Wenu na Mama Yake? Na Dada Zangu Mkiendelea na Tabia Zenu za Kuchuna na Kuwatumia Wanaume Kwa Maslahi Yenu na Kuwasaliti Yatawakuta Sana Haya Ya Akina UFOO Na Kikubwa Tulieni na Ndoa Zenu au na Wapenzi Wenu na Muwe Wavumilivu na Acheni Tamaa za Kijinga na za Kipumbavu na Epukeni Hayo Maisha Ya Maigizo Sisi Wanaume Tuna Hustle kwa Njia Nyingi hapa Mjini hivyo Tukiwapenda Hebu Nanyi basi Rudisheni Upendo, Uaminifu na Heshima Kwetu. Hongera Kwa Kutoka Hospitalini ila Ningefurahi KAMA UNGEANZISHA KITENGO au NGO MAALUM TU KWA KUTOA USHAURI WA BURE KWA WASICHANA, MABINTI, WANAWAKE na AKINA MAMA Wenye Tabia za Kisanii Kama ULIZOKUWA Nazo hadi Ukakoswakoswa Kwenda Kumwona Sir GOD. Ukome na Nyie Wengine MJIFUNZE na REJEENI ULE USEMI USEMAO " UKIMWONA MWENZIO ANANYOLEWA NA WEWE TIA MAJI".
 
Amshukuru mumewake kwanza huko aliko angemwasha kwenyewe sijui kama angetoka
binafsi namshukuru shemeji ingawa ulikuwa na niambaya ila mungu ndie mweza yote na dada amebakia na anaendelea kula mema ya nchi naamini amtamtafuta tena labda mkutane huko mbele y safari after...............
 
Kuna mila ambayo Ufoo ame i ignore. hata siku moja mmachame haolewi na mtu kutoka srhemu fulani uchagani. baba Ufoo alilikemea hili ndio maana hakuiva na Mushi. na Mushi kaanza kufika nyumbani kwa mama Ufoo baada ya mdingi kubuta. Hii mila ni ya siku nyingi na laana hii hsitaisha keenye vizazi vya hivi karibuni.
 
Back
Top Bottom