George Smiley
JF-Expert Member
- Oct 24, 2011
- 471
- 266
"Katika ziara hii Zitto atakutana na Mawaziri Wakuu wa majimbo ya Nord Rhein Westphalen jimbo ambalo limefanikiwa sana katika vita dhidi ya ukwepaji kodi unaotokana na raia wa Ujerumani kuficha fedha kwenye mabenki ya Uswiss na wa jimbo la Lower Saxony kwa ajili ya mazungumzo kuhusu ukarabati wa Meli ya Liemba na kujenga mahusiano kati ya Mkoa huu na Mkoa wa Kigoma pia kati ya mji wa PapenBurg na Manispaa ya Kigoma" - https://zittokabwe.wordpress.com/2012/12/08/press-release-ndugu-zitto-ziarani-ulaya/
Kuna problem kidogo:
1. Pesa zilishaletwa Dar kwa ajili ya mchakato mzima wa ukarabati wa hiyo meli na mengineyo
2. Tatizo liko kwenye wizara ya mwakyembe ambako kuna watu wameamua kwa kusudi na kuleta dilidali na imeleta harufu ya rushwa
3. Zitto huko alikokwenda watamrudisha Dar kwani tatizo haliko Ujerumani taizo liko Dar unless na yeye kuna jambo analificha
4. Ushajiuliza kwa nini kuhusu hili yeye Zitto Kanyamaza? katika hali ya kawaida angekuwa kashaita press conference na kulalama vilivyo Zitto style na asingeishia maelezo tuu bali angetemebelea radio stations, tv stations , makala zake angekuwa kashazimwaga humu JF na kwenye mtandao wake, bila kusahau kule Facebook na Twitter.
5. Kuhusu pesa zilizofichwa ujerumani sote tunajua pesa za zikishaenda kwa wazungu huwa hazirudi (lakini hii sio thread yake)
6. Kingine cha kujiuliza ni kuwa wan KIGOMA mko wapi? hivi huko Kigoma hakuna pressure groups zaidi ya huyu mbunge wenu?
George Smiley,Mwakyembe alikukosea nini? unamuandama sana! Kibaya zaidi tuhuma zako zote zinakosa ushahidi.
Sitoandika mengi leo lakini kuna harufu ya ufisadi wa kutisha kuhusu hii meli ya MV LIEMBA ambayo serikali ya Ujerumani walikuwa tayari kutoa pesa ili itengenezwe ili iendelee kutoa huduma kwa wananchi kwenye ziwa Tanganyika.
Meli hii ambayo historia yake mnaweza kuipata hapa:
MV Liemba - Wikipedia, the free encyclopedia
cha ajabu mbunge wa Kigoma bwana Zitto Kabwe ambaye sasa yuko huko Ujerumani naye amekuwa kimya kuhusu hatma ya hii meli ambayo ni kiungo maalim kwenye jimbo lake na pia tusisahau kuwa ofisi ya waziri Mwakyembe nayo imekataa huu msaada wa BURE toka serikali ya Ujerumani.
Habari za uhakika ni kuwa Ofisi ya waziri Mwakyembe wanataka wapewe chochote ili kupata huu msaada toka kwa serikali ya Ujerumani, na kimya cha Zitto nacho kinaonyesha kuwa haoni kama huuu usafiri una manufaa kwa nanachi wa Jimbo lake.
Lakini pia inaelekea kuwa huku kununa kwa serikali yetu kuna weza kukawa kuko linked kwa namna moja au nyingine na ile issue ya Serengeti (lakini hili hapa si mahala pake) ila ukweli usiopingika kuwa kuna hata TTB wako bize ku promote maeneo ya ziwa Tanganyika na hasa ukizingatia tayari upo usafiri wa anga kati ya Kigoma na Sumbawanga, na hii meli ingetengenezwa ingekuza uchumi wa visiwa na maeneo mengine yaliopo kwenye hili ziwa.
Taarifa zinasema kuwa tayari serikali ya Kenya na Kenya Tourist Board tayari washa lobby kuwa hizo pesa zipelekwe kwao kama Tanzania hatuzitaki ili ziwasaidie kwenye maeneo mengine ya utalii.
.........
Neno ufisadi linanajisika kweli kweli.......
Sio kila jambo linafuatiliwa kwa kupigiwa kelele.Waziri Mwakyembe na mie tunafuatilia kwa karibu suala hili muhimu sana kwa historia ya Tanzania na Ujerumani. Hili sio suala la msaada wa kifedha. Hili ni suala la historia yetu na waliokuwa wakoloni wetu. Lina faida kotekote, wao kuweka historia yao na sisi kupata huduma ya usafiri wa uhakika.
neno ufisadi linanajisika kweli kweli.......
Dr. Mwakyembe wala wizara yake hawahusiki kabisa na kuchelewa kwa mradi huu wa mv liemba. Ikumbukwe kwamba masuala ya ushirikiano wa kimaendeleo yapo chini ya wizara ya fedha. Mwalimu wangu mwakyembe mapema mwaka huu alifanya ziara nchini ujerumani na suala hili kuzungumzwa kwa kina sana.
Mradi huu wa mv liemba tumeanza kuufuatilia haswa haswa mwaka 2009 nikiwa mwanafunzi ujerumani, balozi ngemera na aliyekuwa waziri mkuu wa jimbo la lower saxony mr. Wulf ambaye baadaye alikuwa rais wa ujerumani.hapa kati kati kuna tatizo limetokea.
Nimekutana na uongozi wa lower saxony na tumeona changamoto ipo wapi. Wajerumani hawajatoa hata senti tano kuhusu mradi huu.
Sio kila jambo linafuatiliwa kwa kupigiwa kelele.waziri mwakyembe na mie tunafuatilia kwa karibu suala hili muhimu sana kwa historia ya tanzania na ujerumani. Hili sio suala la msaada wa kifedha. Hili ni suala la historia yetu na waliokuwa wakoloni wetu. Lina faida kotekote, wao kuweka historia yao na sisi kupata huduma ya usafiri wa uhakika.
halafu hapohapo na ufisadi wa zitto upo wapi?George Smiley,Mwakyembe alikukosea nini? unamuandama sana! Kibaya zaidi tuhuma zako zote zinakosa ushahidi.