Huku kukiwa na takribani miezi miwili tuuu tokea Rais J.Kikwete kukizindua Rasmi Chuo cha Nelson Mandela maarufu kama Nelson Mandela African Institute of Science and Technology, kashfa nzito, na ufisadi wa kutisha umebainika kufanywa na Naibu wa Makamu mkuu wa chuo hicho (Deputy Vice Chancellor Planning, Finance and Administration).
Ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka umebainika katika zoezi la ukaguzi audit ambalo bado linaendelea kufanyika chuoni hapo, imebainika kuwa mengi ya matatizo hayo yamekuwa yakilalamikiwa na wafanyakazi bila kufanyiwa kazi na uongozi wa chuo hicho kwa mda mrefu
Haya ni baadhi tuu ya mambo machafu yaliyobainika na yanayosemekana kufanywa na Profesa huyo bila aibu yeyote.
1. Kwa mwaka wa fedha 2011/12 Ametumia takribani Tsh 50m (Milioni Hamsini) kwa safari za ndani tuu, ambazo nyingi ni zake binafsi kwenda Dsm ilipo familia yake. Siku za safari zikiwa ni kuondoka Alhamisi na kurudi J3 takriban kila wiki. (Inasemekana anajenga ghorofa mjini DSM kwa hyo anakwenda kusimamia nk).Gharama zote za safari zimelipwa na Chuo yeye akiwa ndio muhidhinishaji wa malipo yote.
2. Imebainika kwamba Safari zote wanazotakiwa kwenda wafanyakazi waliopo chini yake anakwenda yeye. Mf. masuala yote ya Budget, Mipango, Mishahara na watumishi, yanayotakiwa kufuatiliwa na wataalamu wa kada hizo amekuwa akienda yeye bila kushirikisha wataalam hao. Pia amekuwa akijilipa safari zake zote anazosafiri huku wafanyakazi wengine wakishindwa kusafiri safari za kikazi au wakisafiri bila kulipwa kwa kisingizio cha kutokuwepo kwa fedha.
3. Imebainika kwamba Manunuzi yote ya Taasisi amekuwa akifanya yeye kwa kusaidiana na rafiki yake wa Karibu ambaye ni ESTATE Manager, bila kuhusisha kitengo cha manunuzi ambacho kipo, hivyo kikiuka taratibu zote za manunuzi, na pia kununua vifaa vingi visivyohitajika ama vyenye ubora hafifu sana na kwa bei ghali sanaaa! Mf. Huku Taasisi ikihitaji kununua printers 6 zenye kutumia smart cards bila kuhusisha wataalam yeye na mwenzake wakajikuta wamenunua printers 6 za kuprint Identity cards ambazo zimelipiwa na hazifanyi kazi kabisa wala haziwezi kutumika Vile vile amebainika kununua magenerator mawili tokea Zanzibar alipokuwa akifanya kazi na yote mawili hayafanyi kazi, pamoja na kununuliwa kwa gharama kubwa tuuu.
4. Imebainika kwamba Huku akilimbikiza madeni ya wafanyakazi (wafanyakazi wapya wamekuwa wakichukua hadi miezi 6 kulipwa malipo yao ya kuamisha familia nk) amekuwa akiwalipa watoa huduma mbalimbali bila kufuata taratibu zozote na kwa muda muafaka.
5. Matumizi mabaya ya rasilimali, imebainika kwamba hata gari la taasisi analotumia yeye hataki litumiwe na afisa mwingine yeyote Yule na anaposafiri huwa linapaki nyumbani kwake hadi arudi.
6. Kuna tuhuma ambazo zimekwisha fika kwa Mkuu wa Mkoa na Makamu mkuu wa chuo, huku kukiwa na ushaidi kuwa amekuwa akitoa ajira kwa akina dada na hasa masekretari wake kwa rushwa ya Ngono! Hili limefika TAKUKURU na linafanyiwa kazi kwa kuwahusisha baadhi ya masekretari aliowafukuza ama walioamua kuacha kazi kwa sababu yake.
7. Kutokana na malalamiko mengi ya wafanyakazi, Prof huyu amekuwa akikwepa ziara zote za viongozi mbalimbali wanaotembelea taasisi ya Nelson Mandela, Hakuwepo ktk ziara ya Katibu Mkuu wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Technologia (Chuo kipo chini ya wizara hii), ziara ya waziri wa Mawasiliano, sayasi na technologia, ziara ya waziri Mkuu, na hata ziara ya Mkuu wa Chuo Mh. Makamu wa rais, hii yote inasemekana ni kuogopa kushtakiwa na wafanyakazi
Ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka umebainika katika zoezi la ukaguzi audit ambalo bado linaendelea kufanyika chuoni hapo, imebainika kuwa mengi ya matatizo hayo yamekuwa yakilalamikiwa na wafanyakazi bila kufanyiwa kazi na uongozi wa chuo hicho kwa mda mrefu
Haya ni baadhi tuu ya mambo machafu yaliyobainika na yanayosemekana kufanywa na Profesa huyo bila aibu yeyote.
1. Kwa mwaka wa fedha 2011/12 Ametumia takribani Tsh 50m (Milioni Hamsini) kwa safari za ndani tuu, ambazo nyingi ni zake binafsi kwenda Dsm ilipo familia yake. Siku za safari zikiwa ni kuondoka Alhamisi na kurudi J3 takriban kila wiki. (Inasemekana anajenga ghorofa mjini DSM kwa hyo anakwenda kusimamia nk).Gharama zote za safari zimelipwa na Chuo yeye akiwa ndio muhidhinishaji wa malipo yote.
2. Imebainika kwamba Safari zote wanazotakiwa kwenda wafanyakazi waliopo chini yake anakwenda yeye. Mf. masuala yote ya Budget, Mipango, Mishahara na watumishi, yanayotakiwa kufuatiliwa na wataalamu wa kada hizo amekuwa akienda yeye bila kushirikisha wataalam hao. Pia amekuwa akijilipa safari zake zote anazosafiri huku wafanyakazi wengine wakishindwa kusafiri safari za kikazi au wakisafiri bila kulipwa kwa kisingizio cha kutokuwepo kwa fedha.
3. Imebainika kwamba Manunuzi yote ya Taasisi amekuwa akifanya yeye kwa kusaidiana na rafiki yake wa Karibu ambaye ni ESTATE Manager, bila kuhusisha kitengo cha manunuzi ambacho kipo, hivyo kikiuka taratibu zote za manunuzi, na pia kununua vifaa vingi visivyohitajika ama vyenye ubora hafifu sana na kwa bei ghali sanaaa! Mf. Huku Taasisi ikihitaji kununua printers 6 zenye kutumia smart cards bila kuhusisha wataalam yeye na mwenzake wakajikuta wamenunua printers 6 za kuprint Identity cards ambazo zimelipiwa na hazifanyi kazi kabisa wala haziwezi kutumika Vile vile amebainika kununua magenerator mawili tokea Zanzibar alipokuwa akifanya kazi na yote mawili hayafanyi kazi, pamoja na kununuliwa kwa gharama kubwa tuuu.
4. Imebainika kwamba Huku akilimbikiza madeni ya wafanyakazi (wafanyakazi wapya wamekuwa wakichukua hadi miezi 6 kulipwa malipo yao ya kuamisha familia nk) amekuwa akiwalipa watoa huduma mbalimbali bila kufuata taratibu zozote na kwa muda muafaka.
5. Matumizi mabaya ya rasilimali, imebainika kwamba hata gari la taasisi analotumia yeye hataki litumiwe na afisa mwingine yeyote Yule na anaposafiri huwa linapaki nyumbani kwake hadi arudi.
6. Kuna tuhuma ambazo zimekwisha fika kwa Mkuu wa Mkoa na Makamu mkuu wa chuo, huku kukiwa na ushaidi kuwa amekuwa akitoa ajira kwa akina dada na hasa masekretari wake kwa rushwa ya Ngono! Hili limefika TAKUKURU na linafanyiwa kazi kwa kuwahusisha baadhi ya masekretari aliowafukuza ama walioamua kuacha kazi kwa sababu yake.
7. Kutokana na malalamiko mengi ya wafanyakazi, Prof huyu amekuwa akikwepa ziara zote za viongozi mbalimbali wanaotembelea taasisi ya Nelson Mandela, Hakuwepo ktk ziara ya Katibu Mkuu wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Technologia (Chuo kipo chini ya wizara hii), ziara ya waziri wa Mawasiliano, sayasi na technologia, ziara ya waziri Mkuu, na hata ziara ya Mkuu wa Chuo Mh. Makamu wa rais, hii yote inasemekana ni kuogopa kushtakiwa na wafanyakazi