Ufipa: Heaven on Earth

Ufipa: Heaven on Earth

mama baki huko huko kwa shetani malaika wa watanzania kamwe huwezi mchafuwa ukawa ndiyo habari ya tz bakini na kofuli lenu
 
umehama upinzani umeingia upinzani. una bahati mbaya wewe!
 
Hahaaa mmeshupaza shingo sasa zimevunjika , mnara mlioujenga Mungu kaamua kuuvunja huyu anasema leta tofali anapewa ndoo mwingine anaomba nondo anapewa mchanga hakika ukiujua ukweli nayo kweli itakuweka huru na ukae ukijua Mungu hamfichi mnafiki na kila kitu na na wakati wake , kuna wakati wa kulia ,

Wakati wa kucheka , wakati wa usiku na wakati wa mchana hakuna siri chini ya Mbingu na malipo ni hapa hapa Duniani aliye msafi ndani ya ccm na awe wa kwanza kumpiga jiwe lowassa

Siku zote Mungu huwa hujitenga na unafiki,umbeya, chuki, uzandiki, unyanganyi, dhuluma, rushwa, na mambo mengine yafananayo na hayo msimamizi wa haya ni shetani

Mungu huyu tunaemwamini muumba wa Mbingu na Dunia na vyote vilivyomo anapenda Amani, Upendo, Haki, Furaha na vyote vifananavyo nayo Tulianza na Mungu tutamaliza na Mungu.
 
At last, umekiri kwamba alikotoka Lowassa ni makao ya mashetani, kaondoka mmoja wamebaki wengi. Heri ya nusu-shari
 
Nadhani baada ya kupokea kitu cha Ishirini Bilioni wanaweza kujenga ofisi yao ya kudumu sehemu nyingine yenye hadhi ya kiofisi kidogo.

Wewe mwanamke mwogope Mungu unajua bilioni au umenakilishwa ahonge ili iweje embu acheni unafiki ukweli utajulikana soon Richmond mwasisi wake nani Balali yupo hai au kafa tuoneshwa live misiba yoote ya watu mashuhuri duniani seuse Balali? Hembu acheni masihara na wananchi simamia hii Hakuna siri chini ya Mbingu na hakuna siri ya watu wawili never ever.
 
Mwenyezi Mungu alishaniongoza njia.,sina haja ya kumkufuru kwa kufikiria kujiunga na COALIATION OF HOOLIGANS.

NAENDELEA kumshukuru MUNGU kwa kunionyesha njia na kunitenga na AIBU ya kuwa pamoja na WEZI wapiga dili.
hivi nyie ni serikali gani mnaolea wezi? kwanini mnawajua wezi na hamuwachukulii hatua stahiki?
 
Hahaha maneno ya mkosaji haya. Nyie ni wale watu mnaoomba usiku na mchana kuiombea chadema ife.
Na haifi ng'oo.
 
Juliana Shonza

Hata Musa alizaliwa kwenye himaya ya farao! Nakushangaa we we uliye rudi misri!
 
Last edited by a moderator:
Mwenyezi Mungu alishaniongoza njia.,sina haja ya kumkufuru kwa kufikiria kujiunga na COALIATION OF HOOLIGANS.

NAENDELEA kumshukuru MUNGU kwa kunionyesha njia na kunitenga na AIBU ya kuwa pamoja na WEZI wapiga dili.

WEZI NA WAPIGA DEAL WA MEREMETA, ESCROW,KIWIRA,NYUMBA ZA SERIKALI,EPA N.K. Ushajitenga nao
 
Na wewe si Shetani uliyetoka huko mtaa na ufipa na Kuhamia mtaa wa Lumumba!? Kama wote wanaohama vyama ni Mashetani na wewe umo.
 
Nimepitia hii thread nzima na hapa ndo ninaamini washabiki na wapenzi wa hii ukawa sio watu wazuri, wenye maono, wenye maadili na weredi wa kuishauri na kuipeleka hii nchi mbele. Yaani badala ya kudiscuss mada aliyotoa mtoa mada mnaishia kumtukana na kufanya vijembe.

Mtoa mada umeongea maneno mazito sana, Nchi nyingi za Africa zamekwama kimaendeleo kutokana na wanasiasa kujigeuza kuwa ndo watu wanaofikiri kwa niaba ya wananchi. Nilitegemea wapenzi na wanachama wote wa ukawa kuanza kuwahoji viongozi wao kwa hoja zenye mashiko kuwa nyie mlituambia na mlitulisha hiki juu ya huyu mtu, inakuwa je leo yanatokea haya?

Ni lazima wawahoji kwa nini msitangaze leo mbele ya watanzania wote kuwa tuliwalaghai kwa hoja zote juu ya haya mambo na mtusamee ili watanzania wawahukumu kwenye sanduku la kura kwa unafiki na tamaa zao juu ya pesa?

Kama mmejipanga kuulinda uovu wenu humu kwenye mitandao napenda kusema kuna watu ambao tuko macho, tunafuatilia every step you made na tunafanya uamuzi baada ya kufanya critical analysis. Huu ulaghai manaoufanya hapa haujawai kufanywa marekani na hata ulaya.

Kwa niaba ya watanzania wanaojielewa kamwe hatutakubali kuwapa nchi nyie msiojielewa na ma opportunist wakubwa.
 
Shonza !
Tunajua kwanini umepiga yowe kwa andiko lako hilo Viti Maalumu vitapunguzwa sana na vinaweza visiwepo kutokana na mtakavyopotezwa octoba mwaka huu. Hivyo lazima uanze kulia lia kwani ulichofuata mara kimeyeyuka.acha kupiga mayowe wenye uwezo na kuzichanga karata wamezichanga natumaini umeona upepo umebadilika kabisa .Nisalimie Mtela
 
Pole sana ulikuwa kwa Mwigulu hola, umegombea viti maalum umeshinda lakini viti maalum vinategemea idadi ya kura na kinachokuuma zaidi ni kutokuwa sehemu ya mabadiliko daaah pole sana.Yaani fungu lako ni la kukosa mama!Ndio hivyo hakuna namna tena
 
Nyie Hamjamwelewa huyu dada, Alishinda nafasi ya viti Maalumu huko Songwe sasa ana wasiwasi wa kukosa hata hiyo nafasi kwa kuwa wabunge wa CCM Oct hawatafika asilimia 20%
 
........Huyo unaemuona kuwa ni Shetani ambae mlishindwa kumfukuza, wakati yupo CCM alikuwa Malaika?.
 
Nadhani baada ya kupokea kitu cha Ishirini Bilioni wanaweza kujenga ofisi yao ya kudumu sehemu nyingine yenye hadhi ya kiofisi kidogo.

Umechukia sababu ww unategemea viti maalum na Laigwan atachana wabunge kibao ktk majimbo yanayo shikiliwa na CCM so hata ww hati hati kama utaingia mjengoni!

By the say baba wa siasa za Mbeya Tata Mwandosya umemsikia!!Kasema JK alikwenda Dodoma tayari ana jina lake mfukoni na hakutaki kuacha demokrasia itamalaki!

Kazi mnayo Oktoba 25
 
Back
Top Bottom