UFAFANUZI: Waziri Ummy Mwalimu asema hajapiga marufuku vilainishi, NGO'S zapigwa marufuku kusambaza

RUCCI

JF-Expert Member
Oct 6, 2011
1,701
1,714
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kupitia akaunti yake ya Facebook amesema kuwa hajapiga marufuku matumizi ya vilainishi bali amepiga marufuku mashirika yasiyo ya Kiserikali kusambaza vilainishi kwa wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

Kauli yake nimekuwekea hapa chini;

Sijapiga marufuku matumizi ya Vilainishi nchini.

Ukweli: Nimepiga marufuku mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) kununua na kuzambaza vilainishi kwa Wanaume wanaojihusisha na mapenzi na Wanaume Wenzao. Sababu nimeshazieleza.

Hivyo, nafurahi kuwajulisha kuwa tayari baadhi ya Mashirika hayo yameanza kutekeleza agizo hili kwa kuanza kuondoa vilainishi kwenye miradi yao. NAYAPONGEZA SANA. Na niendelee kuyataka mashirika mengine kutii agizo hili ambalo tutalisimamia kikamilifu.

Hatutasita kuchukua hatua ikiwemo kuyafutia usajili mashirika yanayoendelea na miradi ya kusambaza vilainishi kwa wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

Tupambane na UKIMWI kwa kujikita kwenye afua nyingine zinazozingatia sheria za nchi sambamba na mila na desturi zetu watanzania.
 
Kumbe hata mambo ya kiserikali yanatolewa maelezo kwenye kurasa "account" binafsi za Viongozi wake? Kwani wizara haina tovuti? Hiyo account ni verified? Huko anatumia kama mwananchi wa kawaida, hiyo ishu ni ya kiserikali na wala siyo ya waziri Fulani.
 
hahaha!! kwa hiyo vilainishi vitasambazwa na serikali au?
 
Iko haja kwa waandishi wanaopotosha kwa makusudi kauli za viongozi wachukuliwe hatua kali za kisheria ...kuna ongezeko kubwa sana la upotoshaji wa matamko!!

Hata jambo hili lilipotoshwa makusudi na magazeti.
 
Nilishangaa sana kusikia amri hiyo maana vilainishi vinatumika kwa wanandoa pia au wapenzi wa jinsia tofauti
 
Kumbe hata mambo ya kiserikali yanatolewa maelezo kwenye kurasa "account" binafsi za Viongozi wake? Kwani wizara haina tovuti? Hiyo account ni verified? Huko anatumia kama mwananchi wa kawaida, hiyo ishu ni ya kiserikali na wala siyo ya waziri Fulani.
hivi siku hizi ukumbi wa habari MAELEZO haupo?
 
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu hajatafakari vizuri madhara ya maamuzi yake. Ukitaka kuona jambo hilo hebu kila sehemu alipoandika "vilainishi" weka neno "kondomu" halafu uone jinsi anavyoipinga serikali ambayo yeye ni sehemu yake.... Ukifanya hivyo, utakuwa na ujumbe huu:

====================
Sijapiga marufuku matumizi ya Vilainishi nchini--Waziri wa Afya Ummy Mwalimu

Ukweli: Nimepiga marufuku mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) kununua na kuzambaza vilainishi (na kondomu) kwa Wanaume wanaojihusisha na mapenzi na Wanaume Wenzao. Sababu nimeshazieleza. Hivyo, nafurahi kuwajulisha kuwa tayari baadhi ya Mashirika hayo yameanza kutekeleza agizo hili kwa kuanza kuondoa vilainishi (na kondomu) kwenye miradi yao. NAYAPONGEZA SANA. Na niendelee kuyataka mashirika mengine kutii agizo hili ambalo tutalisimamia kikamilifu. Hatutasita kuchukua hatua ikiwemo kuyafutia usajili mashirika yanayoendelea na miradi ya kusambaza vilainishi (na kondomu) kwa wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja. (Mbali ya vilainishi na kondomu) tupambane na UKIMWI kwa kujikita kwenye afua nyingine zinazozingatia sheria za nchi sambamba na mila na desturi zetu watanzania.

====================
Je, mpaka hapo, Ummy Mwalimu bado anayo sifa ya kuendelea kuwa mshauri mkuu wa Rais JPM katika vita ya kimataifa dhidi ya ukimwi? Tafakari!
 
Upotoshaji.....hata bungeni neno hili hutumika saana.
Uchochezi.....hili neno hutumika saana na jeshi la polisi hasa kwa wana siasa pale wanapofunguliwa mashtaka.....Yote ni maneno mazuri na yanawezwa wekwa kwenye group la Kujihami.
 
Kumbe hata mambo ya kiserikali yanatolewa maelezo kwenye kurasa "account" binafsi za Viongozi wake? Kwani wizara haina tovuti? Hiyo account ni verified? Huko anatumia kama mwananchi wa kawaida, hiyo ishu ni ya kiserikali na wala siyo ya waziri Fulani.
Acha kuirudisha nyuma makusudi dunia! Mbona viogozi wengi wanatoa matamko yao kwenye akaunti zao binafsi za fb na twiter?
 
Kumbe hata mambo ya kiserikali yanatolewa maelezo kwenye kurasa "account" binafsi za Viongozi wake? Kwani wizara haina tovuti? Hiyo account ni verified? Huko anatumia kama mwananchi wa kawaida, hiyo ishu ni ya kiserikali na wala siyo ya waziri Fulani.

Ipo katika gazeti la mwananchi!
 
Bado hajui anachokijibu...... Kuna billions kwa ajili hio and she knows it very well
 
AaaaH!!!!! MBAVU ZANGU MIEEE!!?!! Chezea, MCC!! Nilitka kushangaa tAngu lini MHITAJI AKASUSIA MSAADA?!! yaani ukiwa hamnz uctgmee mabadiliko!
 
Vilainishi kwa wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja. Ina maana kuna NGO's zinayatambua hayo makundi na kuamua kuwapelekea vilainishi. Hicho ndicho Ummy Mwalimu anakipinga. La sivyo Serikali iseme inawatambua hao watu.
 
Back
Top Bottom