Ufafanuzi wa maswali mbalimbali ya wadau wa elimu kuhusu matokeo ya mtihani wa kidato cha nne-2013

Kwamba ufafanuz wa wapi watachaguliwa kuendeleana ngaz za juu utatolewa,hii inanipa wasiwas kwamba inawezekan hakuna mipango iliyo kamili mpaka watakapo kaa na kujadi n wap watawapeleka,kama upo kwann bas usitolewe mapema ili watu wajue mbiv na mbich my take balaza wafanye kaz zao kwa weledi kwa kuzingatia maslah ya nchi na sio matakwa binafsi au makundi flan hasa ya kisiasa
 
Kitu ambacho sijaelewa hapa inakuwaje E na F zote zina hadhi sawa yaani Fail. Kama E ina hadhi sawa na F, kulikuwa na sababu gani ya kuianzisha mpaka imesababisha mkanganyiko wa madaraja watu wanaopata pointi sawa kuanzia 41-45. Hii inachanganya watu bila sababu ya msingi. Yaani NECTA wameifa tu kuwa nchi nyingine zina makundi mengi bila kutueleza ndani ya hayo makundi kuna nini. Tusifanye kazi kwa mazoea na kuiga tuangalie inaongeza thamani gani katika elimu ya taifa letu


Inasemekana wamebadilisha mawazo wakafanya tofauti na ilivyopangwa awali:
"Kwa mfumo huu, alama ya ufaulu ilikuwa iwe E na CA zilitakiwa kuchangia asilimia 40. Hata hivyo mfumo huo haukutumika kama ilivyotangazwa na badala yake alama ya ufaulu imekuwa D na CA zimechangia 30, jambo ambalo bado halijawafurahisha wadau."
(SOURCE: Mwananachi)
 
Mkuu nashukuru kwa ufafanuzi. Ika nimezidi kuchanganyikiwa, unaposema wamebadilisha mawazo hao ni akina nani? Kumbuka kuwa Prof Mchome alipokuwa anatangaza viwango vya ufaulu alisema kuwa vimetokana na mawazo ya wadau. Sasa inawezekana kweli jambo ambalo lilitokana na mawazo ya wengi kupitia madodoso libadilishwe tu eti kwa sababu WAMEAMUA KUBADILISHA MAWAZO? HAO NI AKINA NANI TUWAJUE? NCHI INAONGOZWAJE NDUGU ZANGU YAANI MTU ANAWEZA AKAAMKA AKAJIAMULIA TU JAMBO LINALOATHIRI WATANZANIA KADRI ANAVYOTAKA YEYE?



Inasemekana wamebadilisha mawazo wakafanya tofauti na ilivyopangwa awali:
"Kwa mfumo huu, alama ya ufaulu ilikuwa iwe E na CA zilitakiwa kuchangia asilimia 40. Hata hivyo mfumo huo haukutumika kama ilivyotangazwa na badala yake alama ya ufaulu imekuwa D na CA zimechangia 30, jambo ambalo bado halijawafurahisha wadau."
(SOURCE: Mwananachi)
 
Mkuu Cambri,
Uchaguzi wangu wa maneno ("kubadili mawazo") haukuwa mzuri.
Kinachoonekana ni kwamba mipango ya awali imebadilishwa kama inavyosomeka kwenye quote niliyoweka hapo toka Mwananchi.
 
Back
Top Bottom