UDSM yaongozwa na Mstaafu

UDSM yaongozwa na Mstaafu

Hakuna hoja ya maana hapa. Nchi bado inamuhitaji profesa mukandara. Kumbuka huyu gwiji amesoma University of Carlifornia berkeley, one of the very few word class universities. Wamerekani wanaita ivy league. Halafu waraka wa serikali unamruhusu professa kufundisha mpaka akiwa na umri wa miaka 70. Kwa hiyo mukandara bado ana miaka 10 ya kufundisha hapo mlimani.

wewe unaongelea kufundisha wakati mleta mada anaongelea kuongoza.
Mleta mada anaongelea sheria na taratibu wewe unaongelea habari za 'eti' kasoma california university of Bakari sijui, mradi umeamua kuchanganya tu.
Haya mkuu, only if thats what makes you happy, then keep your head up.
 
Jibu hoja. Slaa anaingiaje hapa? Kama huna cha kuchangia nyamaza kimya. Hatupendi kusoma upuuzi wenu hapa.

hahahahahahahahahahahahahah! unachowaza wewe na huyo jamaa ni tofauti kabisa alijua mko pamoja!!!!!!!!! mhe. utaifakwanza umesoma hii kitu lakini?
 
Last edited by a moderator:
Sio issue ya kujua-ukifikia retirement age unaachia ngazi ya madaraka kama kiongozi. Professor kuendelea kama professor kwa mkataba ni issue tofauti kabisa. Sasa tuseme "imempendeza" mkulu huyu bwana aendelee au apewe mkataba wa aina hiyo.
Na wewe chemsha bongo kidogo! Compulsory age of retirement for professors is 70 years! Mkandara hajafikisha miaka 70 na wala hayuko katika mkataba!

Serikalini compulsory age of retirement is 60 years! Kwa maana hiyo kama mfanyakazi wa serikali wakiwemo makatibu wakuu wanaendelea na kazi, basi hao wanaendelea kwa mkataba!
 
Na wewe chemsha bongo kidogo! Compulsory age of retirement for professors is 70 years! Mkandara hajafikisha miaka 70 na wala hayuko katika mkataba!

Serikalini compulsory age of retirement is 60 years! Kwa maana hiyo kama mfanyakazi wa serikali wakiwemo makatibu wakuu wanaendelea na kazi, basi hao wanaendelea kwa mkataba!

Hakuna circular ya maprofessor kuritire at 70. Retirement bado ni at 60 kwa vyuo vyote va uma na baada ya hapo kunauwezekano wa kupewa contract kama professor pale idara yako na chuo watakopohitaji services zako na utumishi ikiridhia otherwise hakuna mkataba.
 
slaa ana miaka mingapi? mbona hastaafu au kwa kuwa ile anayoiongoza ni NGO


Na wewe kama sio mende Mangula na Kinana wa Tembo wana umri wa miaka mingapi? Si wote ni Wana Nyadhifa za Juu CCM na hasa huko wa Tembo ni Katinu Mkuu??? Tusaidie kidogo hapa kwa kuwa tunapata shiida kuelewa. By the way Uchaguzi wa Chadema ni mwaka huu usipate shida kuumiza akili.
 
kilaza ni kilaza forever, Chuo kuu cha DSm na chama cha siasa ni vitu viwili tofauti.
Dr Slaa sio mtumishi wa umma ni mtumishi wa chama cha siasa
wale hawako binded na kanuni za utumishi wa umma
Mukandala ni mtumishi wa Umma anapaswa kujiuzulu mapema ameshafika 60 yrs
hata jambo dogo kuelewa ni shida sasa kwanini nisiseme watanzania kama wewe wamelaaniwa?

sidhani au sina hakika kama wanaongezewa mikataba wanaruhusiwa kuwa na vyeo
na pia niseme wazi kile chuo 70% ya viongozi pale ni wahaya, same to Mandela University
ubaguzi wao umewafanya madr na maprof wengi kuvukimbia hivi vyuo...kubali usikubali ukweli ndio huo

Umeeleza vizuri mwisho ukaharibu kwa kuwatuhumu Wahaya kwamba wamejaa ktk menejimenti za vyuo vya UDSM na Mandela. Ni tuhuma muflisi!

Mzee Tupa tupa anayo hoja ya msingi sana kwasababu Mukandala ni mtumishi wa umma,lazima sheria na kanuni zifuatwe kwa yeye kustaafu baada ya kufikisha umri wa miaka 60. Kuendelea kushikilia nafasi ya VC ni makosa,pengine kama ataongezewa muda wa kuendelea kufundisha kama baadhi ya Wahadhiri walivyo ongezewa!

Mimi huwa naamini kwamba mtu mchapa kazi wa kweli akifikisha umri wa kustaafu anajiondokea,anakwenda kupumzika,anaachana na pressure za kila siku za maofisini. Lakini ni kinyume huku Afrika,wengi hawataki kustaafu,na utendaji wao sifuri!
 
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam almaarufu kama UDSM kwasasa kinaongozwa na Mstaafu.Hii ni kwakuwa Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof. Rwekaza Sympho Mukandala ameshafikisha umri wa kustaafu ingawa bado yuko madarakani. Nyaraka rasmi zinazopatikana katika www.udsm.ac.tz zinaonesha kuwa Prof. Mukandala amezaliwa Septemba 30, mwaka 1953.

Tarehe husika inamaanisha kuwa Prof.Mukandala alistaafu rasmi tarehe 30/9/2013. Hatahivyo, Prof. Mukandala ameendelea kuwa madarakani chuoni hapo kama Makamu Mkuu wa UDSM. Kwa mujibu wa mkataba wake wa uteuzi katika cheo alichopo, anapaswa kumaliza mwaka 2015. Lakini, tayari ni mstaafu.

Kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma, mstaafu hapaswi kuendelea na madaraka au nafasi aliyonayo. Hakuna Wanazuoni wengine wa kuteuliwa katika nafasi hiyo hadi mstaafu aendelee kuwa ofisini?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
si ukaichukue hiyo nafasi kama unaipenda? wivu wa kijinga haujengi
 
Na wewe chemsha bongo kidogo! Compulsory age of retirement for professors is 70 years! Mkandara hajafikisha miaka 70 na wala hayuko katika mkataba!

Serikalini compulsory age of retirement is 60 years! Kwa maana hiyo kama mfanyakazi wa serikali wakiwemo makatibu wakuu wanaendelea na kazi, basi hao wanaendelea kwa mkataba!
mwaghona sewo
 

Kama hujui ni vyema ukauliza. VC wa mlimani na hata vyuo vingine vya umma ni lazima awe na rank ya uprofesa. Sasa hata ukimuondoa mukandara kwenye nafasi ya VC, ni lazima utafutue profesa mwingine ili aweze kujaza nafasi ya VC. Lakini kumbuka serikali imeruhusu maprofesa kufanya kazi hadi umri wa miaka 70.Kwa kigezo hicho, Mukandara ni VC halali kwa mujibu wa taratibu za serikali.
Hivi kila Profesa lazima awe VC? Hoja hapa sio cheti cha Mukandara, issue ya mleta uzi ni hicho cheo cha u-VC na sio u-profesa au u-recturer!
 
Muda wa kustaafu kwa lazima ni miaka 60, baada ya hapo mtu anaweza kupema mkataba akafanya kazi ya taaluma yake, in this case, ukufunzi, na sio utawala, siku hizi imekuwa kawaida sheria kupindishwa na wakuu kwa manufaa yao na watu wao wa karibu!!
 
Hakuna hoja ya maana hapa. Nchi bado inamuhitaji profesa mukandara. Kumbuka huyu gwiji amesoma University of Carlifornia berkeley, one of the very few word class universities. Wamerekani wanaita ivy league. Halafu waraka wa serikali unamruhusu professa kufundisha mpaka akiwa na umri wa miaka 70. Kwa hiyo mukandara bado ana miaka 10 ya kufundisha hapo mlimani.

Hapo kwenye RED: Waraka unamruhusu Profesa kufundisha lakini sio kushika wadhifa wa uongozi. Hapo hoja ya Tupatupa inabaki kuwa valid.
cc: utaifakwanza

 
Last edited by a moderator:

Kama hujui ni vyema ukauliza. VC wa mlimani na hata vyuo vingine vya umma ni lazima awe na rank ya uprofesa. Sasa hata ukimuondoa mukandara kwenye nafasi ya VC, ni lazima utafutue profesa mwingine ili aweze kujaza nafasi ya VC. Lakini kumbuka serikali imeruhusu maprofesa kufanya kazi hadi umri wa miaka 70.Kwa kigezo hicho, Mukandara ni VC halali kwa mujibu wa taratibu za serikali.
sio lazima awe prof. Hata dk anaweza kuongoza chu
 
ni nani kakudanganya ni maprof tu wanatakiwa kuongoza chuo au kukaimu ukuu wa chuo. Acha kudanganya chali.
 
nlimaanisha uongozi wake umekifanya chuo kuwa katika hali mbaya
walimu wanakosa hata chaki, vyoo havina hata dawa na toilet paper
usalama wa chuo kwa wanafunzi na walimu ni wa mashaka
ameshindwa kutatua matatizo yote hayo chuoni
pia anatuhumiwa kutoa upendeleo sana kwa wahaya wenzake kuwapatia nafasi hapo chuo na ajira
sina haja kuwaorodhesha hapa wanajijua...
watu wa UDSM=UDASA wanajua hili wala sio hoja mufilisi....so its time for him to go
wapo wenye uzoefu zaidi yake.

Umeeleza vizuri mwisho ukaharibu kwa kuwatuhumu Wahaya kwamba wamejaa ktk menejimenti za vyuo vya UDSM na Mandela. Ni tuhuma muflisi!

Mzee Tupa tupa anayo hoja ya msingi sana kwasababu Mukandala ni mtumishi wa umma,lazima sheria na kanuni zifuatwe kwa yeye kustaafu baada ya kufikisha umri wa miaka 60. Kuendelea kushikilia nafasi ya VC ni makosa,pengine kama ataongezewa muda wa kuendelea kufundisha kama baadhi ya Wahadhiri walivyo ongezewa!

Mimi huwa naamini kwamba mtu mchapa kazi wa kweli akifikisha umri wa kustaafu anajiondokea,anakwenda kupumzika,anaachana na pressure za kila siku za maofisini. Lakini ni kinyume huku Afrika,wengi hawataki kustaafu,na utendaji wao sifuri!
 
Ndugu zangu wanajamii, nimekua nikipata taabu sana kutambua uwezo wetu wa kutafiti, kuchambua na kubainisha mada zenye mashiko humu. Mara nyingine tunaleta mada kiushabiki au kwa kupata dokezo tu. Hii ni sawa na mwandishi wa habari anapopata tip kuhusu habari fulani badala ya kuifanyia kazi kujua undani wake yeye anaenda newsroom anaandika anayoyajua kisha story inatoka vivyo sivyo.

Nimeanza na utangulizi huo hasa kwasababu ya hoja aliyoilete vuta-nkuvute kuhusu Mukandala kuendelea kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilihali ameshastaafu. Nadhani huyu ndugu yangu anahoja nyingine ya sirini zaidi ya hiyo ya kustaafu maana ameleza mwanzo vyema kisha anamalizia "hakuna maprofesa wengine wa kushika wadhifa huo mpaka wastaafu waendelee kuongoza?" Baada ya utafiti na uchambuzi na kuongea na baadhi ya maprofesa wakongwe pale UDSM nimeona niwashirikishe haya yafuatayo:-

Prof. Mpangala ameniambia si kila profesa anaweza kuwa VC, wapo maprofesa wengi ambao tangu wameanza kufundisha chuo wakiwa adogo hadi wamekua maprofesa hawajawahi kushika hata wadhifa wa Ukuu wa Idara (Head of Department), pili kiongozi wa chuo anaajiriwa kama mwalimu tu na sii kama vc au kiongozi mwingine na ndiyo maana hata vc analipwa mshahara wake kama profesa pamoja na leadership allowances and benefits.

Profesa mwingine ambaye hakupenda nitaje jina lake ila inasemekana ndiye mwenye umri mkubwa na amekitumika chuo kwa zaidi ya miaka 45 ikiwa ni kama profesa na nyadhifa nyingine za juu, anasema, hapo kale Mtendaji mkuu wa chuo aliletwa na Waziri Mkuu Nyerere ambaye aliitwa Prof. Cranford Pratt mwaka 1961, baada ya kuweka mazingira ya chuo vyema, baada ya hapo alikuja mswahili lakini ikaamuliwa kiongozi wa chuo atoke kwenye chama na serikali ndipo Ndugu Pius Msekwa akachuka uongozi miaka ya 1970 ambapo ndipo kilikuwa chuo kamili. Ikumbuke mwanzo kilikua sehemu ya chuo cha East Africa. Baada ya msekwa wakaja wengine kina Dr. Chagula, Balozi Kuhanga, Prof. Mmari na kisha Prof. Luhanga. hao wote walichaguliwa kwa kuteuliwa na rais lakini utaratibu wa chuo ulifuatwa kiukamilifu. Prof. Chachage na timu yake walipigana kufa na kupona kuhakisha chuo kinapata Hati Idhini (Charter) ambayo pamoja na mambo mengine waliyokua wanapigania ni viongozi kuchaguliwa na wanachuo yaani waalimu, wanafunzi na wafanyakazi waendeshaji kupitia tume u kamati maalumu (credible search team) kisha baada ya kupata watu watatu wenye weledi basi hupekwa kwenye mamlaka za uteuzi. Ndiyo maana hata wakati wa kutafuta VC baada ya Prof. Luhanga kumaliza muda wake kulikua na purukushani sana zikiongozwa na Chachage na mwisho alifanikiwa maana Raisi Mkapa alibariki chuo kiwe na Charter yake kwa mujibu wa sheria na viongozi watafutwe kupitia search teams na siyo Makampuni, agents au kutoka serikalini moja kwa moja. Prof. Mukandala alipitia mchakato huo ambao uliungwa mkono na UDASA chini ya mwenyekiti Chahchage na Baraza la wafanyakazi.

Profesa mwingine wa SUA ameniambia kuwa kamati ya viongozi wa vyuo vya umma (CPCVT) ikishirikiana na vyama vya wafanyakazi wa vyuo vikuu walikutana na Rais na Watendaji wa Wizara ya Utumishi na Hazina wakatoa mapendekezo yao ikiwa ni pamoja na ombi la kubadili umri wa kustaafu kwa waalimu wa vyuo vikuu na baada ya mchakato mrefu ikakubaliwa kuwa Senior Lecturers watastaafu wakiwa na miaka 65 na Maprofesa ni miaka 70 ila akipenda anaweza kustaafu akiwa na umri wa chini ya hapo.

Baada ya hayo naomba msaada katika haya:-

Kwa maelezo hayo je mleta mada ni kwamba hajui vc anapatikanaje? Kuhusu sheria kuwa haimruhusu Prof. Mukandala kuwa VC kwanini hatuendi mahakamani? kwanini tunasemea chinichini? Tuache majungu yasiyo na tija.

Ndugu Lokisa amesema uongozi wa UDSM umejaa wahaya. Sijamuelewa labda atuweke wazi kwa kutoa majina ya viongozi hao na kutueleza yupi mhaya na yupi ni kabila gani. Nasema hivi kwasababu nimeona kwenye website ya UDSM list ya viongozi kama kuna wahaya ni aslimia 1 tu ambaye nimeweza kumuona ni dean wa Sheria na wengine wawili ni heads of departments. Labda ndugu yetu anawafanhamu vyema atuletee hapa otherwise atakua ni mbaywayu.

Ndugu Mnyamahodzo, nadhani tunahitaji kujua kikomo cha utendaji kazi ni kipi kati uprofesa na uongozi. Ila umesema napaswa kuondoka kama Luhanga alivyoondoka. Nimejaribu kumpata Prof. Luhanga akasema kuwa yeye ndiye VC aliyedumu kwenye uongozi kwa muda mrefu sana tangu 1991 hadi 2005 na hadhani kama itakujatokea mtu atakayefikia record yake maana siku hizi utaratibu umebadilika. sasa sijui ndugu mnyamahodzo alitaka kumaanisha luhanga aliondoka kabla ya umri wake wa kustaafu au vipi ila anaweza kutuweka wazi tu kuwa Luhanga aliondoka madakani akiwa na umri gani?

Kkarumekenge, umeuliza kama mukandala anamaandiko aliyoyachapisha hahaaaaaaa nashangaa maana mukandala ameanza kuchapisha vitabu tangu akiwa Berkely na pia atakuwaje Profesa kama haja publish? Nadhani hapa uelewa wako ni mdogo sana kuhusu taratibu za mtu kuwa Prof. Uprofesa siyo cheo ni Degree kwa maneno mengine ambapo mwisho kabisa kama ngazi ya kuhitimu Prof. anatoa kitu kinaitwa Professorial Lectuer sijui kama unakifahamu. Swala la Redet kumpa Mukandala utajiri sijui kama ni kweli labda utuwekee hadharani utaji wake na namna hiyo redet ilivyouleta maana katika matajiri sijui kama mukandala anathubutu hata kutia kidole achila mbali mguu!!!!!!!!!!!!!! Kwa mimi ninavyofahamu na kwa kazi ambayo nimeshapewa na baraza moja la redet huko Zanzibar miaka ya 2005 sijui kama kuna tamko lilishatolewa bila kuwa na data yakinifu. Nakushauri uende pale UDSM umuone Dr. mmoja anaitwa Dr. Makulilo wa Political Science ambaye alifanya utafiti yakinifu kuhusu tafiti za siasa na hayo matamko akupe nini alichogundua. Ukweli ni kwamba REDET inafanya kazi kimataifa syo kama agents wa mifukoni mmmh. Kuhusu Tido Mhando nadhani nilishawahi andika humu kuwa Tido ndiye aliyoifikisha TBC ilipo ndiyo alitaka TBC ifanye kazi kama BBC bila kujua TBC ni ya Tanzania na BBC ni ya UK na hivyo kila moja ina maslahi tofauti. Sikatai kuwa aliiweka TBC katika hali ya sasa, hali ya hadhi ya juu lakini pia hakua mzalendo mshahara wake tunaujua? alikua analipwa kiasi gani na kwa Pound au kwa Shilingi?

Nadhani humu kuna mipasho mingi au kuna watu wanahitaji u VC, nawashauri msubiri ikifika wakati mjaze majina ili michakato ifanyike. Mambo ya vyuo vikuu tuwaachie wao huko si kwenye siasa hasa zetu za majitaka zenye tamaa na ulafi wa madaraka badala ya kujenga nchi. Kuna watu wanakaa chini kazi yao ni kuangalia Mukandala kakosea wapi, kikwete ameenda wapi kombo ili apate pa kuanzia. Mbana nasi hatuanzishi ya kwetu ili tuonekane tuwe viongozi au matajiri. Swala la imempendeza mkuu yanatoka wapi katika u VC? Tena kwa ufahamu wangu Mukandala amefanya kazi karibu na Mkapa zaidi kuliko JK kama mshauri wake wa siasa.

Mwisho tufanye kazi tuchambue mambo tuache kutemewa na kupelekwa kilisulisu, lemalema, lusindelusinde au nchembanchemba humu
 
Back
Top Bottom