Udom wakigoma nani alaumiwe

Kaka mwisho

JF-Expert Member
Dec 19, 2011
402
165
Chanzo cha migomo vyuo vikuu kwasasa ni kuchelewashwa kwa pesa ambazo kwa sasa hutolewa na chuo husika. Mpaka sasa udom kuna wanafunzi hawajapata hata la kwanza na la hawamu ya pili muda umefika lakini bado hawajapewa. Je yakitokea kama ya udsm na st john dom nani alaumiwe?
 
ushauri wangu wewe kuwa mpole kwani ukilianzisha tu utapoteza masomo si umeona yaliyo wakuta udsm,je wale wenzenu walio timuliwa wameludishwa hadi leo? hii nchi ni watu wachache na familia zao
 
Chanzo cha migomo vyuo vikuu kwasasa ni kuchelewashwa kwa pesa ambazo kwa sasa hutolewa na chuo husika. Mpaka sasa udom kuna wanafunzi hawajapata hata la kwanza na la hawamu ya pili muda umefika lakini bado hawajapewa. Je yakitokea kama ya udsm na st john dom nani alaumiwe?
Endeleeni kuwa wapole na wavumilivu kwani Tanzania ni kisiwa cha amani na uvumilivu bila kusahau upole
 
Ushauri wangu ni huu: Fanyeni juu chini mtume VIONGOZI wenu (wanotambulika kisheria siyo wanaharakaharaka isiyokua na barak) waende Bodi ya mikopo Dar es Salaam wamuone Lubambura na wasikubali kuondoka eneo hilo bila cheki au nyaraka zinazoonesha kuwa hela imeshatumwa chuoni lasivyo mtagomea chuo mtagombana na mheshimiwa Kikula wakati huenda hausiki kabisa. Cha msingi tujue fedha hazitolewi na vyuo bali bodi ya mikopo na ndipo tatizo lilipo. Nilishashauri mara nyingi humu na kwa barua rasmi kwenda loarns bodi kuhusu wao kuwa wabunifu wasihusike kabisa na kuhakiki wakopaji na disbursement ya mikopo direct to students bali waziachie taasisi za fedha tena hukohuko mwanafunzi anakotoka wao wahusike na uratibu tu maana kazi hiyo hawaiwezi kabisa.

Kazi ya ada katika ulimwengu huu wa uchangiaji wa maendeleo ulioletwa na IMF na WB na tusioweza kuukwepa kwa hali yetu ya sasa ni kazi ya mzazi. Hivyo kama fedha zitapelekwa katika mabenki ndipo wazazi na wanafunzi tutajua kuwa ni mkopo na wale wenye uwezo hawatakopa ila watawaachia watoto wa masikini kukopa badala ya hii means testing isiyo na macho wala miguu na priorities isiyoeleweka. Wenzetu hapo Uganda tu mzazi ndiyo mwenye jukumu la kulipa ada chuo kinachojua ni umelipa ada unasoma la nenda home. Wanaopewa udhamini wa serikali ni wachache sana na hao ni wale ama wamefaulu sana au wanaosoma masomo ya huduma kama waalimu wa sayansi na udaktari.

Mwisho nirudie wana UDOM na vyuo vingine nchini Tanzania tusipende kufanya migomo kimhemuko bali tufanye migomo stahiki na yenye mantiki hata raia wa kawaida wakisikia wanawaunga mkono. Kugomea chuo bila kuwa na uhakika hela iko wapi ni mhemuko na ni ujinga. Fanyeni utafiti hela kama imekuja chuo na lini imekuja kama la bodi wanazubaa nini au wamezubaishwa na nani (hapa namaanisha chuo kutopeleka majina kwa wakati au wanafunzi kutoweka sahihi za kupokea fedha kwa wakati au)?

Nawatakia wanajamii wote HERI YA SIKUKUU YA NOELI NA MWAKA MPYA WENYE BARAKA
 
Back
Top Bottom