Kilindila Rojas
Member
- Sep 27, 2011
- 19
- 3
Binafsi nashangwaza sana na utendaji kazi wa ofisi ya Admision & DVC- ARC chini ya Prof. Ludovick Kinabo, mana haiji akilini tangu June 2010 tulipo hitimu chuo pale Udom (first intake) hadi sasa hatujapata Academic Transcripts zetu. Si kana kwamba hawajatoa Transcripts kwa wahitimu wote, ila pamoja na kuchelewesha kuzipata hadi June 2011, zaidi ya wahitimu 100 na mimi nikiwemo, transcripts zetu zilikuwa na makosa ya aina mbalimbali, mfano zipo ambazo zilikosewa GPA, Jinsia ya mtu "i.e badala ya Female unawekewa Male", zingine hazikuwekwa picha, & zingine ziliwekwa picha ya watu wengine "tofauti na mwenye transcript". Hivyo basi ilitulazimu kuziacha hizo transcripts kwa ajili ya marekebisho, na tuka ahidiwa kuwa itachukua muda mfupi kufanyiwa hayo marekebisho, chakushangaza toka mwezi wa sita 2011 hadi sasa hakuna hata dalili za kuzipata hizo transcripts, tukifuatilia unapewa ahadi zisizo timia. Nadhani wahusika pale UDOM wana tufanyia haya wakijua kuwa hatuna forum ya kupeleka malalamiko yetu, chakushangaza hadi wanzetu tuliowaacha (waliohitimu mwaka huu) walishapata transcripts zao, hivi hata uki- apply sehemu either kazi au nafasi ya kuendelea na masomo mfano nje ya nchi na ukahitajika kupeleka transcript, mtu utatoa sababu zipi za kujitetea ktk mazingira haya? Jamani tunaomba ushauri wenu njia zipi au nini tufanye ili kulifuatilia suala hili kwa ukaribu!! Nawasilisha.