UDOM-COED! Kilio ni maji maji maji

UDOM-COED! Kilio ni maji maji maji

tisa desemba

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2011
Posts
434
Reaction score
115
Wakuu suala la ukosefu wa maji hapa udom college of education limezidi kushika kasi hasa kwa wiki hii, maji yamekuwa yakitoka kwa nadra sana tena katika block chache sana (si zaidi ya 4 kati ya 20 zilizopo) nyakati za asubuhi na jioni wanachuo wengi wamekuwa wakizunguka huku na huku kutafuta maji bila mafanikio! Vyooni hali si nzuri! Nyuma ya block R, M, J na D nimeshudia vinyesi vya binadamu vikiwa vichakani! Tunakolekea si kuzuri! Serikali ya wanafunzi wako kimya! Naomba wakuu wa Udom mnaopitia hapa msaidie kutatua tatizo hili kwani ikiendelea hivi wikiendi hali itakuwa mbaya zaidi! Naomba kutoa hoja!
 
Hilo tatizo la maji lipo tangu chuo kinaanza na hasa huko Ng'ong'ona ndo limezidi na ni ngumu kuisha ukiangalia lication ya chuo na huo mkoa maji ni shida hata town kwenyewe.
 
Hapa block H me huwa naoga juu kabisa kwenye paa tena usiku,maana mabafu ni machafu hasa
 
Hilo tatizo la maji lipo tangu chuo kinaanza na hasa huko Ng'ong'ona ndo limezidi na ni ngumu kuisha ukiangalia lication ya chuo na huo mkoa maji ni shida hata town kwenyewe.

Hoja yako inaweza kuwa na mashiko kama hakuna dhamira thabiti ya kuleta maji Coed na ni kwa ajili ya kujijitea tu! Ila kwa wa watu wenye nia na dhamira kubwa ya kuleta maji coed! Maji yanaweza kufika tena kwa wingi na wakati wote! Nikukumbushe pia kwa dodoma manispaa maji si tatizo saaana kama ulivyosimuliwa enzi hizo!
 
Acha unafiki umekosa habar mbona mi niko kwenye tank nachota maji mengi tu

Je hilo tank unalochota linatosha kuhudumia college nzima ya education yenye wanafunzi zaidi ya 7000! Usilete utetezi wa kiimla kwa mambo mazito yanayohusu ustawi na afya za watu! Sometime siasa tuwe tunaweka pembeni! Kiukweli kwa wiki hii maji yamekuwa shida sana! Watu wanakwenda kununua na kufua kijijini nje ya chuo!
 
Natumaini Mlacha analitambua tatizo maana si tatizo la jana wala leo ndugu!
 
Hoja yako inaweza kuwa na mashiko kama hakuna dhamira thabiti ya kuleta maji Coed na ni kwa ajili ya kujijitea tu! Ila kwa wa watu wenye nia na dhamira kubwa ya kuleta maji coed! Maji yanaweza kufika tena kwa wingi na wakati wote! Nikukumbushe pia kwa dodoma manispaa maji si tatizo saaana kama ulivyosimuliwa enzi hizo!

Kaka bora ungejibu kistaarabu tu hasa kumquote mtu nakuweka maneno as if unamjua au sure kuwa nimesimuliwa?

Nimeishi Dom. Nimekaa Nkuhungu, Ipagala na Area D ila ukweli ndo huo huo mkoa maji sio kiivyo.

Kuhusu Ng'ong'ona nimekaa hostel hizo first year nimeishi Block L na D semester ya 1 enzi hizo nyingine hazijaisha zilipokamilika nikaishi block K so hali ya huko naijua tu vizuri maji mnaweza kaa hata mwezi yasitoke mpk tunaenda kubembeleza mafundi na wachina watupe na bado wanabania ikafika kipindi mpk mwanachuo mmoja akajitoa mhanga akafungua koki kubwa ya wachina maji yakatoka then akatimuliwa kwa uhalibifu ilikuwa inaumiza maji mnaona wanajengea na kumwagilia maua alafu kwenye tanki hamna mpk tukawa tunakinga maji ya kumwagilia maua na miti yakija tu haijalishi machafu au safi tunachota tu na hali ikiwa tete zaidi tulikuwa tunanunua maji ya Uhai ya lita tano kuogea.
Ila ukweli hiyo ishu ya maji mkoa wa Dom hasa Udom hata wajukuu wenu wanaweza ikuta.

Bora tu mwaka wapili tulirudi college yetu social science tukidhani shida hakuna maana watu wengi wa coed walikuwa wakuamini hivyo kumbe shida ipo vilevile tho ile ilikuwa college ya kwanza kujengwa nashukuru tu nilimaliza ila iyo ishu hata mkienda bungeni kwa Udom maji hata ukiangalia kule Ng'ox vijijini ni shida kukame sana.
 
Natumaini Mlacha analitambua tatizo maana si tatizo la jana wala leo ndugu!

Wanalijua sana ila hapo kelele utapiga mwisho wasiku utavaa joho na utarudi kufundisha hapohapo ila hakuna hatua yoyote inayochukuliwa.
 
Wanalijua sana ila hapo kelele utapiga mwisho wasiku utavaa joho na utarudi kufundisha hapohapo ila hakuna hatua yoyote inayochukuliwa.

Ni kweli mkuu, ila hatuwezi kuacha kupiga kelele kwa sababu tu wameziba masikio! Tutaendelea kuwaambia kuwa tatizo la maji udom ni kubwa na linahitaji utatuzi wa program za haraka na za mda mrefu!
 
Kwa nini msiandamane kibavicha fimbo ya mbali haiui tisa disemba mayuni mpo

Mkuu, masuala mengine hayahitaji itikadi za vyama! Tatizo la maji udom haliwaathiri CHADEMA, CUF WALA NCCR! ni tatizo linalowaathiri watanzania woote wanajumuiya wa udom kuanzia waalimu, wanafunzi, wawekezaji ndani ya chuo ie cafeteria, kampuni za usafi, kampuni za ulinzi nk nk! Sasa sidhani kama woote hawa ni wanabavicha! TUJENGE MOYO WA UZALENDO TUACHE ITIKADI!
 
Mijitu mingine kwa uongo, maji yapo full kasoro siku mbili tatu wakati bomba lililopasuka likofanyiwa marekebisho. Vipi unalalamika maji sasa hivi na miaka ya kuanzia 2010/2011 ungesemaje?
 
Wakuu suala la ukosefu wa maji hapa udom college of education limezidi kushika kasi hasa kwa wiki hii, maji yamekuwa yakitoka kwa nadra sana tena katika block chache sana (si zaidi ya 4 kati ya 20 zilizopo) nyakati za asubuhi na jioni wanachuo wengi wamekuwa wakizunguka huku na huku kutafuta maji bila mafanikio! Vyooni hali si nzuri! Nyuma ya block R, M, J na D nimeshudia vinyesi vya binadamu vikiwa vichakani! Tunakolekea si kuzuri! Serikali ya wanafunzi wako kimya! Naomba wakuu wa Udom mnaopitia hapa msaidie kutatua tatizo hili kwani ikiendelea hivi wikiendi hali itakuwa mbaya zaidi! Naomba kutoa hoja!
sasa wewe badala uende ukaripoti sehemu husika unakuja kulialia huku ili sisi tukusaidie nini think big guy
 
Wakuu suala la ukosefu wa maji hapa udom college of education limezidi kushika kasi hasa kwa wiki hii, maji yamekuwa yakitoka kwa nadra sana tena katika block chache sana (si zaidi ya 4 kati ya 20 zilizopo) nyakati za asubuhi na jioni wanachuo wengi wamekuwa wakizunguka huku na huku kutafuta maji bila mafanikio! Vyooni hali si nzuri! Nyuma ya block R, M, J na D nimeshudia vinyesi vya binadamu vikiwa vichakani! Tunakolekea si kuzuri! Serikali ya wanafunzi wako kimya! Naomba wakuu wa Udom mnaopitia hapa msaidie kutatua tatizo hili kwani ikiendelea hivi wikiendi hali itakuwa mbaya zaidi! Naomba kutoa hoja!

Hebu wakati mwngne uwe unajarb kutumia akili,japo hyo kidogo uliyonayo. Hao wakuu wa udom wanaopitia humu unaotaka watatue tatzo lako kwani wapo chuo gan wao? si ni udom hapohapo? kwan hawajaona hlo tatzo? je,kama wameshndwa kulisolve unafkr ukilalamika humu ndo watalisolve?
wewe c ajabu hata mambo ya familia yenu unaweza kuyaleta humu jf.Next time uwe unafkiria kwanza kabla hujaandika kitu!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom