Kuna Dr mmoja aliwahi kuniambia Hawafaidi mshahara Bali in madenti tu ndo wanachofaidi
Nasami. Pole sana kwa kuwa dhaifu katika kila kitu kuhusiana na elimu ya juu. Sheria zote za vyuo vikuu zinampa mwanafunzi nguvu za kisheria kukata rufaa katika maamuzi yotr yanayofanywa na wahadhiri, bodi za matokeo na hata seneti. Lengo likiwa kama kweli umenyimwa alama zako kwenye majaribio na mitihani, vyombo vya rufaa vitakupatia haki yako na mhadhiri ataadhibiwa, ikithibitika amefanya makosa kwa kukusudia.
Tatizo la wewe na wenzako msiokuwa na uelewa ni kutokusoma sheria za chuo na za mitihani. Pia wewe ni katika wale wanafunzi wasiokuwa na uwezo na kujiamini, hivyo kubaki kupiga kelele na kutafuta huruma za wahadhiri, ambalo nalo ni kosa. Hapa jamii forum umeeleiezwa mengi. Na mimi nasisitiza kuwa mbinu sahihi ya kufaulu masomo ya chuoni ni kusoma kwa bidii, hasa kwa wewe ambaye ni dhaifu kichwani, soma sana tena sana, fanya majaribio yote, jibu mitihani kwa kujiamini. Hapo mhafhiri hawezi kuwa na fursa ya kukuonea, kukupendelea au kukutumia.
Hili ni tatizo linalotokana na pande zote mbili...! Mwanafunzi na Mwalimu. Mwanafunzi kama unajiweza katika somo husika la mwalimu mpuuzi, ukifanya mtihani wake ukafauru lakini mwalimu akakukosesha kwa makusudi na ukiwa na uhakika kuna taratibu za kukata rufaa, hiyo rufaa ikishindikana unaenda mahakamani. Hautakuwa wa kwanza kupata degree ya mahakamani. Tatizo wanafunzi wanaoshindwa kujiamini na kuwa shughulikia walimu wapuuzi kwa kujilegeza hata pale wanapokuwa na haki. Pia vitendo vya kuvaa nguo za ajabu zinazo oonyesha baadhi ya sehemu nyeti karibu wazi na kujipeleka kwa mwalimu mpuuzi akuongezee maksi ni upuuzi mwingine. Tatizo kwa mwalimu ni mwalimu kushidwa kudhibiti upuuzi wake. Ukijijua wewe ni mpuuzi usikubali kuhusu mwanafunzi aje ofisi kwako amevaa kipuuzi, muda ambao si rafiki kwa usalama wa kudhibiti upuuzi wako, iweke ofisi yako katika mazingira yasiyo ya falagha unapotembelewa na mwanafunzi mwenye nia ya kipuuzi...! Ni hayo kwa leo.
Bwana Nasami. Waambie hao wanawake unaosema wanaonewa na kunyanyaswa na wahadhiri, wajitokeze, watetee haki zao. Kwani sheria ipo upande wao. Kama kweli wamenyimwa alama katika mitihani na majaribio kwa sababu za kingono, wana uhakika kuwa walifanya vizuri mitihani yao, walihudhuria madarasa bila tatizo, hawajaruka kufanya majaribio hata mara moja, waelekeze sasa waende kwa dean of students, wakitoka hapo wakajaze fomu za kukata rufaa na nakuhakikishia watafaulu, na wahadhiri wataumbuja na kuchkuliwa hatua. Lakini kama hao mabinti ni wale wale, wategemea huruma na miili yao, wasijaribu hilo, kwani wataonekana hawafai hata kuwepo chuoni. Kwa uzoefu wangu, hakuna mwanamke mwenye akili za kutosha darasani aliyeiosa alama zake za masomo kwa sababu za mizengwe ya wahadhiri.
Wengi wanajilengesha.
DALA umenena vyema
Katika hali isiyo ya kawaida imegundulika uwepo wa udhalilishaji mkubwa kwa wanawake wanaosoma katika vyuo mbalimbali nchini, data zinaeleza kuwa vyuo vingi vimekuwa na lecturer ambao hutumia nafasi hyo kuwataka kimapenzi wanafunzi na pindi mwanafunzi huyo akikataa basi matarajio yake katika masomo huwa yanapotea, wakati hilo likifanyika mkuu wa chuo pamoja na idara zake wanalijua hili lakini hakuna hatua zinazochukuliwa, kwa kuumizwa na suala hili nimeona nilete kwa wanajamvi ili ujumbe ufike kwa haraka wanawake wanateseka sana vyuoni mfano ni chuo kikuu kilichopo Tanga, DUCE na kile chenye idad kubwa ya wanafunzi Dodoma
Serikal kupitia vyombo husika chunguzeni haraka sana hali za wamama wetu vyuoni zinatisha
Hivi kama unatimiza coursework, hujasup, huna carryover..... hujipitishi ovyo ofisini kwa watu, ukienda kupeleka kazi unaenda umevaa vizuri na hujichekeshi ovyoo...Huyo lecturer anaanzaje kwanza kukutaka? Haogopi?
Na wao binadamu jamani, wakiona kitonga wanaserereka...muwaachee....
Hili ni tatizo linalotokana na pande zote mbili...! Mwanafunzi na Mwalimu. Mwanafunzi kama unajiweza katika somo husika la mwalimu mpuuzi, ukifanya mtihani wake ukafauru lakini mwalimu akakukosesha kwa makusudi na ukiwa na uhakika kuna taratibu za kukata rufaa, hiyo rufaa ikishindikana unaenda mahakamani. Hautakuwa wa kwanza kupata degree ya mahakamani. Tatizo wanafunzi wanaoshindwa kujiamini na kuwa shughulikia walimu wapuuzi kwa kujilegeza hata pale wanapokuwa na haki. Pia vitendo vya kuvaa nguo za ajabu zinazo oonyesha baadhi ya sehemu nyeti karibu wazi na kujipeleka kwa mwalimu mpuuzi akuongezee maksi ni upuuzi mwingine. Tatizo kwa mwalimu ni mwalimu kushidwa kudhibiti upuuzi wake. Ukijijua wewe ni mpuuzi usikubali kuhusu mwanafunzi aje ofisi kwako amevaa kipuuzi, muda ambao si rafiki kwa usalama wa kudhibiti upuuzi wako, iweke ofisi yako katika mazingira yasiyo ya falagha unapotembelewa na mwanafunzi mwenye nia ya kipuuzi...! Ni hayo kwa leo.
Mnaombishia mleta mada nendeni mkaone yanayofanyika kwny vyuo km CBE, IFM n.k, acha na vyuo vyenye mfumo rasmi wa kiuendeshaji km UDSM, MZUMBE na vinginevyo
Nakubaliana na wewe mimi nikisoma vyuo 2 sikupata shida yoyote nilipokuja kusoma cha 3 among the above nimeishia kupata peptic ulcer watu wanapinga tu ila hbr anayo huyo mwalimu
Mkuu hili limenigusa.
Mimi nilijikuta katika mazingira haya. Kwa umri ni mdogo ukinilinganisha na yule mwalimu ila kwa shughuli zinazoniweka mjini niko level nyingine sasa due to that mwalimu akawa hanipendi coz ana inferiority complex akawa na bifu za kijinga sana dhidi yangu.
Siku moja nikamfuata ofcn nikamuomba asimame kwenye nafasi yake kama mwalimu kutokana na ishara kwamba zile bifu zingetugharimu pia akamind.
Kwenye test alinipiga panga mno, sikuenda kumuona coz nilijiamini kwamba kwnye final ningempiga bao. Aise kwenye final ndo alinipiga zaidi akanipa sup kwa mara ya kwanza na ilikuwa semester yangu ya mwisho. Sikumfuata ila nilienda department nikawaambia kwamba nina contest yale matokeo na la pili nilitishia kumuua yule mwalimu ila kabla ya hapo nitafuatilia utaratibu wa kusahihisha mtihani wangu upya.
Kwenye jopo la walimu wiopendekezwa kusahihisha wakaogopa ila baadae alipatikana kichaa baili wa marks. Huyu jamaa alitoa majibu kwamba mshkaji alinipunja marks 25 kwa makusudi. Siku ya kupokea majibu hayo walimuita mwalimu husika naye kwa woga aliniomba msamaha kama mtoto.
Ukijitambua mbona easy tu!