Bahati mbaya mfumo huu umeanzia ngazi ya familia. Ukisikia mgeni anakuja ndipo unaanza kutengeneza mazingira ya nyumba yako...
Hivyo, tatizo la kukurupuka, kutokuwa na mipango ya mda mrefu ni udhaifu mkubwa wa mwafrika.
Nachukulia mfano mdogo wa uandikishaji katika daftari la kudumu la wapiga kura. Serikali imekueupuka kujifunika shuka asubuhi, tangu 2010 baada ya uchaguzi walitakiwa kujiandaa na kufanya mchakato huo mapema, ili mfumo ufanyiwe majaribio kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na kura za maoni, yale matatizo yafanyiwe kazi ili 2015 kwenye uchaguzi mkuu kusiwe na shida. Angalia sasa, hizo foleni, watu wamekosa kujiandisha, matatizo mengi...na hatuwezi kujua kama haitaleta shida kwenye uchaguzi..
Kukurupuka kumeanzia ngazi ya familia hadi serikali inayotuongoza..