Udhaifu wa Mwafrika

Udhaifu wa Mwafrika

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,077
Reaction score
136,517
Kuna wakati huwa sielewi kabisa jinsi ambavyo akili zetu sisi Waafrika hufanya kazi. Nasema hivi hususan kurejea ziara ya rais Obama huko Kenya wiki iliyopita na ile ya mwaka juzi alipokuja Tanzania.

Kabla ya ujio wake Tanzania, kulikuwepo na jitihada nyingi za kulisafisha jiji la Dar, ikiwemo kuosha barabara na kufukuza wachuuzi wa biashara ndogondogo kutoka kwenye sehemu ambazo zilisemwa kuwa atapitia.

Huko Kenya nako hii majuzi haikuwa tofauti sana na tulivyofanya sisi. Kuna watu waliondolewa kwenye makazi au maeneo yao ya biashara. Kuna nyasi mpya zilipandwa siku chache tu kabla ya Obama kuwasili mpaka watu wakaanza kumtania Gavana Kidero kwa kuziita hizo nyasi 'Nyasi za Kidero'.

Sina hakika sana na sehemu zingine za Afrika ambazo marais wa Marekani wamewahi kuzitembelea lakini nadhani hakuna tofauti sana.

Sasa mimi huwa najiuliza, kwa nini huwa tunahamisha watu? Ni nini ambacho huwa hatutaki hao marais wakione? Kwani kutokuona kwao ndo kunaondoa ukweli au kunaondoa hali halisi?

Halafu huwa tunamdanganya nani hasa tukifanya hivyo? Hivi kweli tunadhani labda wao hawajui hali jinsi ilivyo? Wao siyo wajinga kiasi hicho.

Na kwani huwa wanapita kwenye hizo sehemu zote ambazo hufagiliwa na kupigwa deki na ambazo watu huhamishwa?

Huko Kenya eti walipanda hadi nyasi kwa lengo la kupendezesha mji. Ndo kusema hilo wazo lilikuja baada ya Obama kutangaza atakwenda Kenya?

Ni kama vile sisi hatupendi vitu vizuri. Kwa sababu, kwa nini isiwe hivyo kila siku? Kwa nini tusipande nyasi pale ambapo tunaona panahitaji kupandwa nyasi? Kwa nini tusiwe na mazoea na utaratibu wa kusafisha mazingira yetu kwa ajili yetu sisi wenyewe na si kwa sababu ya kumvutia mgeni ambaye labda atakaa siku moja au mbili tu?

Tuna udhaifu mbaya sana sisi Waafrika.
 
Ni mambo ya bajeti hayo. kawaida nchi zetu kukiwa na mgeni maarufu anazuru mamlaka husika huandaa bajeti kwa ajili ya ugeni huo. Pia huundwa kamati maalum ya maandalizi. Hapo badi kamatu hutaka kuonesha uhodari wao, watafagia na kudeki barabara, watapanda miti, nk. unakumbuka mwaka flan (nathani 2011) kulikuwa na kikao cha baadhi ya viongozi wa Afrika pale mlimani city. Mitende ilipandwa fasta, niliposikia dhamani ya mtende mmoja nilizimia kwa wivu
 
Hata mimi mkuu nina wasiwasi sana na akili ya mwafrika.
 
Ni mambo ya bajeti hayo. kawaida nchi zetu kukiwa na mgeni maarufu anazuru mamlaka husika huandaa bajeti kwa ajili ya ugeni huo. Pia huundwa kamati maalum ya maandalizi. Hapo badi kamatu hutaka kuonesha uhodari wao, watafagia na kudeki barabara, watapanda miti, nk. unakumbuka mwaka flan (nathani 2011) kulikuwa na kikao cha baadhi ya viongozi wa Afrika pale mlimani city. Mitende ilipandwa fasta, niliposikia dhamani ya mtende mmoja nilizimia kwa wivu

Huo wala siyo ujinga. Ni upumbavu tu.
 
Ukiifikiria akili za mwafrika unaweza kuwa zaidi ya ulivyo hapo.
 
niliwahi kukaa na mzungu mmoja akanisimulia kuhusu utafiti alofanya yeye baada ya kuwa jirani sana na waafrika kutoka Africa akaniambia hivi
1.mwafrika ukimwamba chagua tsh 50,000/ leo na 200,000/ baada ya siku tatu
atachagua 50,000/
2.mwafrika ni mwoga na mnafiki[pretender] akialika watu kwake kama kuna vitu hana ataazima hta kwa jirani ili aonekane anavyo
akamsimulia rafki yake wa kifrika ambaye mara ya kwanza alimdrop kwake na akasema ngoja niingie na ndani akakuta hna kochi,so next alivyoalikwa na mkewe {mzungu } jamaa aliazima kochi
mzuungu akamuuliza kumbe umesha nunua kochi?zile nilizo nunua kwa ajiri yako nitazieleka Good will[Goodwill is charite shop kusaidia wenye uhitaji]
 
niliwahi kukaa na mzungu mmoja akanisimulia kuhusu utafiti alofanya yeye baada ya kuwa jirani sana na waafrika kutoka Africa akaniambia hivi
1.mwafrika ukimwamba chagua tsh 50,000/ leo na 200,000/ baada ya siku tatu
atachagua 50,000/
2.mwafrika ni mwoga na mnafiki[pretender] akialika watu kwake kama kuna vitu hana ataazima hta kwa jirani ili aonekane anavyo
akamsimulia rafki yake wa kifrika ambaye mara ya kwanza alimdrop kwake na akasema ngoja niingie na ndani akakuta hna kochi,so next alivyoalikwa na mkewe {mzungu } jamaa aliazima kochi
mzuungu akamuuliza kumbe umesha nunua kochi?zile nilizo nunua kwa ajiri yako nitazieleka Good will[Goodwill is charite shop kusaidia wenye uhitaji]

Tuna safari ndefu sana.
 
Mkuu haya mambo tumejizoesha kuanzia ngazi za chini... mfano mtu ukiskia mgeni anakuja kwako ndo unaanza kusafisha ghetto na kama ukimshtukiza utaskia oooh ndo nilikua nataka nifanye usafi... hata mdada ukiongozana nae kwake baada ya kutoka kazini mkifika utaskia ooh leo sikutandika kitanda nilichelewa kuamka....sasa hii imeenda hadi kwenye ngazi za kiutawala siku mkipata mgeni ndio mnahangaika kumwaga vifusi barabarani kisa waziri anakuja.. hii niliionaga pale SUA mwaka 2004 alipokuja waziri wa elimu ya juu aisee barabara zilimwagwa vifusi utadhani nani anakuja sijui...sasa kama wasomi tu wanafanya hivu si ndio mfumo mzima uko hivi? Kwa kweli sisi waafrika kuna kitu bado tunakikosa kwenye akili zetu na tabia hizi kwa mtu mmoja mmoja ndio zinajengeka kuwa tabia za jamii nzima... ila cha kushangaza utakuta tabia zetu zinafanana across Africa hata kama mataifa yetu ni tofauti.
 
Mkuu haya mambo tumejizoesha kuanzia ngazi za chini... mfano mtu ukiskia mgeni anakuja kwako ndo unaanza kusafisha ghetto na kama ukimshtukiza utaskia oooh ndo nilikua nataka nifanye usafi... hata mdada ukiongozana nae kwake baada ya kutoka kazini mkifika utaskia ooh leo sikutandika kitanda nilichelewa kuamka....sasa hii imeenda hadi kwenye ngazi za kiutawala siku mkipata mgeni ndio mnahangaika kumwaga vifusi barabarani kisa waziri anakuja.. hii niliionaga pale SUA mwaka 2004 alipokuja waziri wa elimu ya juu aisee barabara zilimwagwa vifusi utadhani nani anakuja sijui...sasa kama wasomi tu wanafanya hivu si ndio mfumo mzima uko hivi? Kwa kweli sisi waafrika kuna kitu bado tunakikosa kwenye akili zetu na tabia hizi kwa mtu mmoja mmoja ndio zinajengeka kuwa tabia za jamii nzima... ila cha kushangaza utakuta tabia zetu zinafanana across Africa hata kama mataifa yetu ni tofauti.

Umemaliza kabisa haina haja ya kuongezea.
 
Nyani Ngabu

Ukichunguza sana waweza kukuta hata katika ngazi ya institutions na households ufanya hivyo hivyo pale wanapofikiwa na ugeni. Kwa nini isiwe kila siku kunafanyika usafi katika ngazi hizo za chini bila kufikiwa na ugeni?
 
Last edited by a moderator:
Waafrika hatuna mfumo maalumu wa kuendesha maisha yetu.
Waafrika hatuna maisha ya kujipanga.
Waafrika tunakurupuka kwenye maamuzi hata kama ni kwaajili ya maisha yetu.
Waafrika ni waoga wa kufanya maamuzi magumu. (Hii nimeiona sana kwa wazungu na race nyingine).
Waafrika tunapoteza muda mwingi sana kwa mambo yasio na maana.
Waafrika tuna mawazo mgando, hatupo tayari kuchukua mawazo mapya.
Utandawazi umetuvua nguo waafrika, tunaonekana kama vinyago.
Waafrika hatuna identity yetu ya kujivunia.
Waafrika tunasindikiza wengine wanaoishi.
 
hii inaonyesha jinsi waliowengi kushindwa kujithamini na kujidharau, lakini kwa yule anayejitambua hanabudi kuonyesha mfano kwa jamii inayomzunguka kwa kuweka mazingira yake safi (yanayoonekana na yasiyoonekana). kuongea ni jambo jema kwa kuwa ujumbe unawafikia watu wengi na kutenda huonyesha ni jinsi gani kutakavyopendeza ikiwa kila mmoja atatimiza wajibu wake.
 
Back
Top Bottom