Megawatt B
JF-Expert Member
- Aug 23, 2011
- 259
- 69
UDA ikiwa na mwekezaji mpya Simon Group, hivi karibuni imeingiza magari mapya 15 aina ya TATA na pembeni kuna nembo ya Marcopolo. sina tatizo na aina ya gari wala nembo, tatizo langu ni muundo wa magari yenyewe, hivi kweli kwa karne hii Town buses zinaagizwa za mlango mmoja kama vipanya? watu waendelee kusukumana wakati wa kuingia na kuteremka kwenye basi? nilidhani mwekezaji Simon group atakuja kisasa zaidi na kuwa na magari yenye hadhi ya Town au City Bus yenye milango miwili, yaani wakuingia na wakutokea. sijui wadau mna maoni gani juu ya hili na ikiwezekana yulijadili maana nilimsikia Kasena (MD wa Simon Group) anajigamba wataleta mabsi mengine 200 kufikia mwezi Machi 2013.