UDA: Hatujafilisika na hatuna dalili za kufilisika

UDA: Hatujafilisika na hatuna dalili za kufilisika

TAARIFA KWA UMMA


Kumekuwepo na taarifa za uwongo kwenye vyombo vya habari, hasa kijarida cha Dira ya Mtanzania, na mitandao ya kijamii kuhusu uongo kuwa kufilisika kwa Shirika la Usafiri Dar Es Salaam (UDA) Limited.

Menejimenti ya Shirika la Usafiri Dar Es Salaam inakanusha uwongo huo kuwa UDA haijafilisika na haina dalili zozote za kufilisika isipokuwa ni Shirika la namba moja nchini na Afrika Mashariki na Kati linalokuwa kwa kasi ya ajabu kimaendeleo na kibiashara.

Zifuatazo ni takwimu zinazodhihirisha ukweli huu:

  1. UDA imeongeza idadi ya mabasi kutoka mabasi 7 makukuu na mabovu Mwaka 2012 na kufikia takribani mabasi 400 mwaka 2015 yakiwemo mabasi 255 ya kawaida na mabasi makubwa - Hercalus, mapya na ya kisasa kabisa duniani (ya BRT) 140.
  2. Ndani ya miaka 3, kampuni ya UDA imekuwa kwa zaidi ya asilimia 5,000
  3. Kampuni hii imeweza kufanya maandalizi yote ya kuwezesha kuendesha mradi wa mabasi yaendayo haraka (DART Project) kwa ufanisi mkubwa. Mbali na kununua mabasi, kampuni imeweze kununua mtambo bora na wa kisasa kabisa duniani wa kukusanya nauli na kuongezea mabasi (Intelligent Transportation System – ITS) wenye thamani kubwa kutoka Ubelgiji na Ujerumani. Vile vile kampuni imeweza kusaili na kufundisha madereva wa Kitanzania zaidi ya 300 na kuwaajiri kwa ajiri ya kuendesha mradi wa mabasi yaendayo haraka (DART Project)
  4. Kampuni imejenga karakana bora na imara na kununua vitendea kazi vya kisasa kwa ajiri ya mabasi yake ya kawaida na mwendo haraka.
  5. Kampuni imepeleka watendaji wake kwenye miradi mbalimbali ya BRT duniani ili kupata uzoefu wa kuwawezesha kuendesha mradi wa mabasi yaendayo haraka (DART Project) kwa ufanisi. Vile vile Kampuni imeweza kuajiri wataalam kutoka nje (expatriates) kwa ajiri kuongezea nguvu wataalam wake wa ndani.
Kwa takwimu chache hizo hapo juu, Kampuni ya UDA ni namba moja Afrika kwenye sekta ya usafirishaji wa abiria barabarani kwa idadi ya watu inaosafirisha, idadi ya mabasi na ubora wa menejimenti.

Mafanikio haya ya Kampuni ya UDA yanatokana na umahiri wa uendeshaji kutoka Simon Group chini Uongozi thabiti wa Mwenyekiti wake Ndugu Robert Simon Kisena na si vinginevyo, kama washindani wetu wavyojaribu kutuchafua kwamba kuna wanasiasa nyuma yake.

Tunawataka washindani wetu waache tabia ya fisi ya kumfuata mtu anayetembea kwa haraka wakidhani atandondosha mkono wapate kitoweo vinginevyo watakufa njaa.

Imetolewa na Uongozi wa SHIRIKA LA USAFIRI DAR ES SALAAM (UDA) LIMITED

Fiction; James Hardley Chase@his best!! Hakuna uwekezaji hapo; bali Uporaji na upotoshaji uliodhaminiwa na kufadhiliwa
na Msoga Plc
 
Kuweweseka.
Jipu kwa mtazamo lakini ni cancer tumor hii. Magu anaivutia pumzi kwanza.
 
mmh! Wajiweke tayar kukamuliwa jipu maana inaonekana limeiva haswa, haliitaji ata wembe kulichana
 
Taarifa haina thamani ya mtaji wa kampuni kabla na baada,madeni wala gharama za manunuzi za mitambo,tunaaminishwa tu kwa kutajiwa imekuwa kwa 5,000%.Ni kama mipasho fulani hivi..
ndio utendaji wetu "uliotukuka" wa utoaji habari. tena usishangae, huwenda hiyo imeandaliwa na msomi.
yaani angalau basi angetuaminisha haifilisiki kwa kutuwekea japo kiambatanisha cha financial statement kwa mwaka uliokwisha (dec 2015).
 
Jamani Kisena hata wewe unafikiri utawadanyanya Watanzania milele? hizo hadithi mwambie Masaburi, Riziwani na JK Msoga band wezi wenzako, Masaburi alliitwa kwenye mdahalo akasema yuko ikulu anafuturu, jasho la wananchi wa Dar Es Salaam wengine leo marehemu mmelipoka wewe na familia yako kwa faida ya aliyekuwa Rais, Kampuni iliyokua inaenda vizuri mkaipapura maana uongozi wa biashara hauujui ni wizi tu, mkaenda mkapewa na godown iliyokuwa na mabasi ya Scandinavia mkaigeuza ofisi ya wanyantuzu watano mamia ya watu wakapoteza kazi, mabasi yamechoka mkapewa njia za upendeleo za daladala wengine wakafukuzwa, bado hamjashiba na huyo mpumbavu aliyewaingiza kwenye mwendo kasi akae chonjo, time has come uongo wa asiyesoma na ukweli wa wasomi hauwezi kukaa chungu kimoja, unajifanya mbabe kwa kuwa wakati wa JK ulimzaba vibao mkuu wa kituo huko kwenu, tulikuangalia sasa wakati wako umefika, andaa pamba na taulo la kufuta usaha, hivi tutaendeleje kuwa na nchi ya amani kama watu kama nyie mnaendelea kutupora mali zetu? kama wewe mfanyabiashra kwa nini huendi kuanzisha chako, JPM tunataka huyu mtu atolewa na kuwekwa mbali kabisa na mradi wa BRT ili tuvuke hapa salama
 
TAARIFA KWA UMMA


Kumekuwepo na taarifa za uwongo kwenye vyombo vya habari, hasa kijarida cha Dira ya Mtanzania, na mitandao ya kijamii kuhusu uongo kuwa kufilisika kwa Shirika la Usafiri Dar Es Salaam (UDA) Limited.

Menejimenti ya Shirika la Usafiri Dar Es Salaam inakanusha uwongo huo kuwa UDA haijafilisika na haina dalili zozote za kufilisika isipokuwa ni Shirika la namba moja nchini na Afrika Mashariki na Kati linalokuwa kwa kasi ya ajabu kimaendeleo na kibiashara.

Zifuatazo ni takwimu zinazodhihirisha ukweli huu:

  1. UDA imeongeza idadi ya mabasi kutoka mabasi 7 makukuu na mabovu Mwaka 2012 na kufikia takribani mabasi 400 mwaka 2015 yakiwemo mabasi 255 ya kawaida na mabasi makubwa - Hercalus, mapya na ya kisasa kabisa duniani (ya BRT) 140.
  2. Ndani ya miaka 3, kampuni ya UDA imekuwa kwa zaidi ya asilimia 5,000
  3. Kampuni hii imeweza kufanya maandalizi yote ya kuwezesha kuendesha mradi wa mabasi yaendayo haraka (DART Project) kwa ufanisi mkubwa. Mbali na kununua mabasi, kampuni imeweze kununua mtambo bora na wa kisasa kabisa duniani wa kukusanya nauli na kuongezea mabasi (Intelligent Transportation System – ITS) wenye thamani kubwa kutoka Ubelgiji na Ujerumani. Vile vile kampuni imeweza kusaili na kufundisha madereva wa Kitanzania zaidi ya 300 na kuwaajiri kwa ajiri ya kuendesha mradi wa mabasi yaendayo haraka (DART Project)
  4. Kampuni imejenga karakana bora na imara na kununua vitendea kazi vya kisasa kwa ajiri ya mabasi yake ya kawaida na mwendo haraka.
  5. Kampuni imepeleka watendaji wake kwenye miradi mbalimbali ya BRT duniani ili kupata uzoefu wa kuwawezesha kuendesha mradi wa mabasi yaendayo haraka (DART Project) kwa ufanisi. Vile vile Kampuni imeweza kuajiri wataalam kutoka nje (expatriates) kwa ajiri kuongezea nguvu wataalam wake wa ndani.
Kwa takwimu chache hizo hapo juu, Kampuni ya UDA ni namba moja Afrika kwenye sekta ya usafirishaji wa abiria barabarani kwa idadi ya watu inaosafirisha, idadi ya mabasi na ubora wa menejimenti.

Mafanikio haya ya Kampuni ya UDA yanatokana na umahiri wa uendeshaji kutoka Simon Group chini Uongozi thabiti wa Mwenyekiti wake Ndugu Robert Simon Kisena na si vinginevyo, kama washindani wetu wavyojaribu kutuchafua kwamba kuna wanasiasa nyuma yake.

Tunawataka washindani wetu waache tabia ya fisi ya kumfuata mtu anayetembea kwa haraka wakidhani atandondosha mkono wapate kitoweo vinginevyo watakufa njaa.

Imetolewa na Uongozi wa SHIRIKA LA USAFIRI DAR ES SALAAM (UDA) LIMITED
Hii taarifa inaonesha kweli shirika linafilisika. Haijagusia chochote kukanusha kilichoandikwa na gazeti. Hoja ni kwamba UDA imefilisika kutokana na madeni yatokanayo na kukopa fedha, Deni la TRA (PAYE) na deni la NSSF (michango ya watumishi). Nyie mnajitete kwa kutaja idadi ya mabasi tena ya mkopo. Bye UDA
 
Ni kampuni ya kwanza Africa kwa usafirishaji wa Abiria ? SAA wametangaza wamefilisika maana madeni ni mengi kuriko mtaji na Dec tuu waliongeza ndege mpya kadhaa..hayo sio majibu ya kufilisika kwa kampuni ni majibu ya kufirisika kwa wanamuziki au wacheza soka au msanii yoyote..Repoti ya Fedha ipo kienyeji sana Mkuu soma magazeti yale wanayotoa Ripoti za Fedha za benk fulani au Halmashauri na si utanii huu hapo juu..
 
TAARIFA KWA UMMA


Kumekuwepo na taarifa za uwongo kwenye vyombo vya habari, hasa kijarida cha Dira ya Mtanzania, na mitandao ya kijamii kuhusu uongo kuwa kufilisika kwa Shirika la Usafiri Dar Es Salaam (UDA) Limited.

Menejimenti ya Shirika la Usafiri Dar Es Salaam inakanusha uwongo huo kuwa UDA haijafilisika na haina dalili zozote za kufilisika isipokuwa ni Shirika la namba moja nchini na Afrika Mashariki na Kati linalokuwa kwa kasi ya ajabu kimaendeleo na kibiashara.

Zifuatazo ni takwimu zinazodhihirisha ukweli huu:

  1. UDA imeongeza idadi ya mabasi kutoka mabasi 7 makukuu na mabovu Mwaka 2012 na kufikia takribani mabasi 400 mwaka 2015 yakiwemo mabasi 255 ya kawaida na mabasi makubwa - Hercalus, mapya na ya kisasa kabisa duniani (ya BRT) 140.
  2. Ndani ya miaka 3, kampuni ya UDA imekuwa kwa zaidi ya asilimia 5,000
  3. Kampuni hii imeweza kufanya maandalizi yote ya kuwezesha kuendesha mradi wa mabasi yaendayo haraka (DART Project) kwa ufanisi mkubwa. Mbali na kununua mabasi, kampuni imeweze kununua mtambo bora na wa kisasa kabisa duniani wa kukusanya nauli na kuongezea mabasi (Intelligent Transportation System – ITS) wenye thamani kubwa kutoka Ubelgiji na Ujerumani. Vile vile kampuni imeweza kusaili na kufundisha madereva wa Kitanzania zaidi ya 300 na kuwaajiri kwa ajiri ya kuendesha mradi wa mabasi yaendayo haraka (DART Project)
  4. Kampuni imejenga karakana bora na imara na kununua vitendea kazi vya kisasa kwa ajiri ya mabasi yake ya kawaida na mwendo haraka.
  5. Kampuni imepeleka watendaji wake kwenye miradi mbalimbali ya BRT duniani ili kupata uzoefu wa kuwawezesha kuendesha mradi wa mabasi yaendayo haraka (DART Project) kwa ufanisi. Vile vile Kampuni imeweza kuajiri wataalam kutoka nje (expatriates) kwa ajiri kuongezea nguvu wataalam wake wa ndani.
Kwa takwimu chache hizo hapo juu, Kampuni ya UDA ni namba moja Afrika kwenye sekta ya usafirishaji wa abiria barabarani kwa idadi ya watu inaosafirisha, idadi ya mabasi na ubora wa menejimenti.

Mafanikio haya ya Kampuni ya UDA yanatokana na umahiri wa uendeshaji kutoka Simon Group chini Uongozi thabiti wa Mwenyekiti wake Ndugu Robert Simon Kisena na si vinginevyo, kama washindani wetu wavyojaribu kutuchafua kwamba kuna wanasiasa nyuma yake.

Tunawataka washindani wetu waache tabia ya fisi ya kumfuata mtu anayetembea kwa haraka wakidhani atandondosha mkono wapate kitoweo vinginevyo watakufa njaa.

Imetolewa na Uongozi wa SHIRIKA LA USAFIRI DAR ES SALAAM (UDA) LIMITED
Nadhani kutakuwa na tatizo kubwa katika mfumo wa kiuongozi hapo UDA mtoa taarifa badala ya kuja na hoja zinazo jibu hoja ya kufilisika kitakwimu kama zilivyoletwa kitakwimu analeta siasa kwenye hoja ambayo haihitaji siasa
 
Statement ya Simon Group inaelezea mambo ambayo Kampuni imefanya. Kwa kiasi fulani ni kweli. Ila swali la msingi ni sources of financing ya shughuli zote walizoeleza in comparison na mapato ya Kampuni. Kampuni inaweza kufilisika hata kama ina ndege nyingi kubwa zinazozunguka duniani kote. Issue siyo kwamba UDA ina mabsi 450 au karakana .... hapana issue ni UDA kwa shughuli wanazofanya wanaweza kurudisha fedha walizotumia kufanya haya yote na wao wakabaki na faida?
 
Wakisema wamefilisika kosa,wakisema hawajafirisika kosa.

Hebu waacheni vijana wakinyantuzu wafanye kazi,mliwauzia shirika nyinyi wenyewe,tena kumbe lilikua na minibus 7 zilizokongoroka
 
Ni jambo la kawaida kwa mfanyabiashara kusaka oppotunity,atatafuta shirika ama kampuni iliyochoka,atatathimini kama inamlipa kuinunua na atainunua na kuiuhisha,haijalishi kama mmemuuzia kwa bei ya hasara ama vipi,makampuni kote duniani yanakua taken over kwa style hiyohiyo
 
am sure taarifa hii itakuwa imeandikwa na mkwere au mtu wa pwani maana imejaa beti za taarabu na mipasho tuu
 
Hata katika biashara zingine mfano Real estate,mfanyabiashara atatafuta jengo lilikongoroka ambalo wenyewe wameshindwa kulimanage,atamuapproach mwenyewe na kuoffer kulinunua,watabargain bei,haijalishi limeuzwa kwa bei ya hasara au vipi,atanunua na kulifanyia matengenezo na kuliuza kwa bei ya juu ama yeye mwenyewe kulifanyia investment,

kama UDA iliuzwa kwa hasara management ya iliyokua uda ndo wanatakiwa kujibu na si aliyeinunua
 
Back
Top Bottom