Uchungu wa uongo hii ndio tofauti ya leba ya uongo na leba ya kweli

OCC Doctors

Senior Member
Jul 20, 2018
104
151
Maumivu ya uongo, uchungu wa Leba ya uongo (false labor, spurious labor). Leba ya uwongo inapatikana zaidi kwenye mimba ya kwanza kuliko kwa wanawake walio wahi kuzaa awali. Kawaida huonekana kabla ya kuanza kwa uchungu wa kweli wa leba, kwa wiki 1 au 2 kwa mimba ya kwanza na kwa siku chache kwa walio wahi kuzaa awali. Sababu ya maumivu haya ni kunyooka kwa mlango wa uzazi na sehemu ya chini ya mji wa uzazi.

Maumivu ya uzazi ya uwongo huwa ni dhaifu, huzuiliwa kwenye sehemu ya chini ya fumbatio na kinena, hayahusiani na ugumu wa mji wa uzazi, hayana sifa nyingine za uchungu wa kweli wa kuzaa na huondoka kwa dawa za maumivu.
............
Ifahamu leba ya ukweli:
Miezi 9 ya ujauzito huisha kwa kuzaliwa mtoto, tukio la leba hufanya wanawake wengi kuogopa kwa sababu mchakato unaweza kuwa na machungu makali.

Wanawake wengine huwa na wasiwasi juu ya uwezo wao wa kukabiliana na maumivu.
Maumivu ni makali na magumu, na yana mambo mengi ikiwemo kuathirika kisaikolojia. Maumivu kawaida huhusishwa na kuumia na uharibifu wa tishu za kizazi.
Kuongezeka kwa maumivu mwishoni mwa ujauzito mara nyingi ni ishara ya kwanza kwamba leba imeanza.

Wakati wa leba halisi, mikazo ya mji wa mimba huanza taratibu, inayofuata mtindo maalum na yenye nguvu. Mikazo hii huongezeka na haiwezi kupunguzwa kwa dawa za kutuliza maumivu. Ikiwa mwanamke atatumia dawa za kutuliza maumivu, dalili za uchungu zinaweza kutulia kidogo, lakini leba halisi bado huendelea.

Mara nyingi, leba hutokea wakati mtoto ameumbika kikamilifu, kufikia hatima ya wakati anaofaa kukaa mwilini mwa mama, yaani kati ya wiki 37-40 za ujauzito. Leba huashiria mwisho wa kipindi cha mtoto kukaa kwenye mji wa mimba na mwanzo wa maisha nje ya mwili wa mama.

255377154_608202776969704_9120427995659511144_n.jpg
 
kuna hio kugeuka kwa mtoto ilinitokea mimba yangu ya kwanza ikiwa na miezi saba nilijua ndio uchungu nilikimbizwa mbio mbio hospital kupigwa ultra sound nikaambiwa mtoto alikua anageuka inakuaje hio au ndio hiohio false labour??
 
Kipindi nafanya kazi huko interior ambako hata vifaa ni haba, nilikua nikiona dalili nsizoelewa kwenye labor, only way to knw kama n true labor nampa paracetamol hata 1 G af nangojea 45 minutes. Kama uchungu huo ukisepa in 45minutes namwambia aende home akangoje true labor.
Hyo ikifika, hainaga stori, kila rangi utaiona
 
Kipindi nafanya kazi huko interior ambako hata vifaa ni haba, nilikua nikiona dalili nsizoelewa kwenye labor, only way to knw kama n true labor nampa paracetamol hata 1 G af nangojea 45 minutes. Kama uchungu huo ukisepa in 45minutes namwambia aende home akangoje true labor.
Hyo ikifika, hainaga stori, kila rangi utaiona
Kumbe pcm ukinywa unapoa? Je kuoga maji yq baridi je?? Nayo inapoza?
 
Maumivu ya uongo, uchungu wa Leba ya uongo (false labor, spurious labor). Leba ya uwongo inapatikana zaidi kwenye mimba ya kwanza kuliko kwa wanawake walio wahi kuzaa awali. Kawaida huonekana kabla ya kuanza kwa uchungu wa kweli wa leba, kwa wiki 1 au 2 kwa mimba ya kwanza na kwa siku chache kwa walio wahi kuzaa awali. Sababu ya maumivu haya ni kunyooka kwa mlango wa uzazi na sehemu ya chini ya mji wa uzazi.

Maumivu ya uzazi ya uwongo huwa ni dhaifu, huzuiliwa kwenye sehemu ya chini ya fumbatio na kinena, hayahusiani na ugumu wa mji wa uzazi, hayana sifa nyingine za uchungu wa kweli wa kuzaa na huondoka kwa dawa za maumivu.
............
Ifahamu leba ya ukweli:
Miezi 9 ya ujauzito huisha kwa kuzaliwa mtoto, tukio la leba hufanya wanawake wengi kuogopa kwa sababu mchakato unaweza kuwa na machungu makali.

Wanawake wengine huwa na wasiwasi juu ya uwezo wao wa kukabiliana na maumivu.
Maumivu ni makali na magumu, na yana mambo mengi ikiwemo kuathirika kisaikolojia. Maumivu kawaida huhusishwa na kuumia na uharibifu wa tishu za kizazi.
Kuongezeka kwa maumivu mwishoni mwa ujauzito mara nyingi ni ishara ya kwanza kwamba leba imeanza.

Wakati wa leba halisi, mikazo ya mji wa mimba huanza taratibu, inayofuata mtindo maalum na yenye nguvu. Mikazo hii huongezeka na haiwezi kupunguzwa kwa dawa za kutuliza maumivu. Ikiwa mwanamke atatumia dawa za kutuliza maumivu, dalili za uchungu zinaweza kutulia kidogo, lakini leba halisi bado huendelea.

Mara nyingi, leba hutokea wakati mtoto ameumbika kikamilifu, kufikia hatima ya wakati anaofaa kukaa mwilini mwa mama, yaani kati ya wiki 37-40 za ujauzito. Leba huashiria mwisho wa kipindi cha mtoto kukaa kwenye mji wa mimba na mwanzo wa maisha nje ya mwili wa mama.

255377154_608202776969704_9120427995659511144_n.jpg
Wanawake ni waongo sanaaa unaweza ukakuta ata kuzaa sio uchungu kiivyo sema Kwa sababu ya uongo wao wanakuza mambo
😁😁😁😁
 
kuna hio kugeuka kwa mtoto ilinitokea mimba yangu ya kwanza ikiwa na miezi saba nilijua ndio uchungu nilikimbizwa mbio mbio hospital kupigwa ultra sound nikaambiwa mtoto alikua anageuka inakuaje hio au ndio hiohio false labour??
Huwa ni dalili za Mtoto kugeuka (Cephalic Presentation). Mtoto kugeuka ni vile Mtoto anapokuwa amegeuza kichwa chini kwenye Nyonga ya Mjamzito na pia Sura ya Mtoto kuangalia nyuma na chogo cha kichwa kuwa sehemu ya mbele au kwenye kinena cha Mwanamke Mjamzito. Miongoni mwa Dalili zake ni Kuhisi mtikisiko au Mtoto kucheza zaidi sehemu ya juu ya kitovu au Maeneo ya Mbavu. Kuhisi mtikisiko au Mtoto kucheza zaidi sehemu ya kitovu au sehemu ya kati na mbele ya Tumbo la Mjamzito, Kuhisi Mgandamizo au Presha zaidi kwenye Nyonga, Kuhisi mvutiko au kuvuta kwenye Nyonga.
 
Back
Top Bottom