Uchumba wangu umevunjwa

Sms zilipoingia simu ilikuwa wapi? Umeshika wewe au mchumba au ipo pekee yake? Kama pekee yake nani alianza kuishika mliposikia msg zimeingia? Kama ni wewe uliposhangaa hiyo msg ndiyo mchumba kaanza kuondoka? Na kama ni mchumba ni kawaida yake kupokea simu/sms zako Mara tu zikiingia? Kwa hayo maswali ukipata majibu unaweza kuelewa mchezo ulipoanzia?
Simu nilikuwa nmeshika mimi ....nilikuwa na-set alarm tulale,kwa sababu kesho yake nilikuwa na safari ya mbali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
You have a point. Kila mtu ana react kivyake. Ushauri wangu ni kuwa asijarib kumlazimisha bibie amwelewe bali aendelee kimya kimya kumtafuta mbaya wake. Atakapomjua basi amalizie kesi

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo nahisi ataharibu huyu mtoa mada,amfuate akaongee nae,dada kaondoka huenda ni hasira na usikute wote wanachezewa. Mtoa mada akikaa kimya na mdada atakata tamaa. Mtoa mada hana kosa ila hiyo msg imeshamtia doa hana budi kubembeleza
 
Wadau, Mimi ni mwanaume....kuna tatizo limenikumba na kuharibu uchumba wangu. Nilikuwa na mchumba wangu nyumbani kwangu,mida ya saa 5 usiku. Kabla hatujalala tukiwa wote,wakati huo nilikuwa niki-set alarm huku mchumba wangu akiiangalia simu yangu,ghafla iliingia sms ya mahaba mazito kutoka kwa mtu nisiyemfahamu.....kulingana na sms hiyo alidai kuwa amemisi penzi langu sana na angetamani tuonane,hivyo nimfuate au kama nipo bize aje yeye..Kiukweli nilichanganyikiwa na mwanamke wangu alishindwa kunielewa. Nkampigia simu hakupokea, akadai yupo kwenye makelele akitoka atanipigia. Nkamuuliza wewe ni nani ....akadai yeye ni Vero mpenzi wangu. Wakati mimi sijawahi kuwa na mpenzi wala mtu wa karibu au ambae nina mazoea nae tu,anaeitwa Vero. Nilipoendelea kupiga simu yake hakupokea akadai atanipigia soon..... Mwanamke wangu alishindwa kunielewa na akaondoka usiku ule. Alipoondoka nilimtafuta huyo muhuni lakin hakupokea simu,akidai yupo kwenye sherehe ....akitoka atanitafuta,lakini mpaka napaandika uzi huu sijapokea simu yake na mara nyingi hapatikani.

Wadau naomba mnisaidie nitamfahamu vipi huyu mtu ambae lengo lake ni kuniharibia mambo yangu.
Naambatisha na "conversation" tulofanya na huyo muhuni.View attachment 1002396

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona inaonesha kama number yake tayari umeshaisavu na jina linaloanzia na M.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo gf wako anaujua huo mchezo vizuri tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ni kweli, hajafanya vizuri. Angemwambia tu ukweli kuwa hawezi kuendelea naye tena ili waachane

Japo pia inawezekana kabisa ni sms ya bahati mbaya na bibie kapanic bure. Nakumbuka iliwahi kunikuta hii, kuna mtu alinipigia kimakosa badala ya kumpigia boss wake nikamwambia kakosea namba ila akawa ananing'ang'aniza kuwa nimpe simu boss wake aongee naye maana amepata ajali nikamwambia kakosea namba ila akawa mkali na kunitolea maneno makali. Baadae kwenye saa 3 usiku akanipigia kuniomba msamaha, haikutosha akanitumia na sms.

Sasa sijui ilikuwaje mkewe akaona zile calls na sms, akauwasha moto. Akanipigia simu kunitukana na kuniambia ananiachia huyo mume ila nitakiona cha moto nilimwelezea situation ilivyokuwa lakini hakunielewa mpaka nikamwambia basi afanye analolitaka.
 
Kwa mimi mwenye uzowefu kwenye hii sekta ya mahusiano, naomba nihitimishe kwa kusema kwamba.....Huyo mwanamke alikua hakupendi, na alikua ana target umkosee ili apate strong reason ya kukuacha.
Kimsingi ipo hivi...... Mwanamke kama anakupenda, hata ikitokea amekufumania ukiwa kifuani mwa mwanamke mwingine huyo hawezi akakuacha ama lahh, atakupa nafasi ya kukusikiliza basi hata umdanganye na kisha maisha yaendelee.

Naomba kuwasilisha
View attachment 1002401
Hahahahaa kwani kulikuwa na ulazuma wa picha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mawili au zaidi;mchumba wako amecheza mchezo ili akuache, au rafiki wa mchumba wako ameamua kuvuruga uhusiano, au kuna mtu anatamani hiyo nafasi
 
Mhh! Unasema unaamini huyo hawezi kuwa mchumba wako anakuchezea akili?! Mimi namuona kama prime suspect, sababu:
1. Kwanini msg ikaingia muda wa usiku tena yeye ndo akiwa na simu yako? Je, ni kawaida yeye kushika simu yako?
2. Nijuavyo, mwanamke anayekupenda huwa haachi jambo lipite hivyo tu, angetaka kujua kwa undani huyo mtu ni nani, hivyo lazima angetaka kufanya uchunguzi wa kina, sijaelewa kwa kwanini huyo wako aliamua tu kuondoka kimya kimya.
 
If You Prayed For Divine Guidance,this Might Be The Answer, For He Never Faileth , Faith In God And All Things Good. Take It In A Postive Way, ,,. Glory To God,
 
Write your reply...mkuu mbona iyo conversation nimeiona sehemu kwenye group flani Monday
 
Hapo inawezekana ni dili amecheza huyo mchumba wako alitaka akuache akakosa njia sahihi basi akampanga rafiki yake ili atume hiyo meseji ukiwa na mchumba wako

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli tupu uyo demu alitaka tu kumuacha jamaa ndio akapanga hilo dili ,tena alimu esms rafiki yake ,akamwambia nanukuu " NDIO NIMESHIKA SIMU YAKE NOW TUMA HIYO SMS SASA HV" mwisho wa kunukuu, sasa bro jua uyo mpenz wako ndio yupo behind the carpet and stage

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wadau, Mimi ni mwanaume....kuna tatizo limenikumba na kuharibu uchumba wangu. Nilikuwa na mchumba wangu nyumbani kwangu,mida ya saa 5 usiku. Kabla hatujalala tukiwa wote,wakati huo nilikuwa niki-set alarm huku mchumba wangu akiiangalia simu yangu,ghafla iliingia sms ya mahaba mazito kutoka kwa mtu nisiyemfahamu.....kulingana na sms hiyo alidai kuwa amemisi penzi langu sana na angetamani tuonane,hivyo nimfuate au kama nipo bize aje yeye..Kiukweli nilichanganyikiwa na mwanamke wangu alishindwa kunielewa. Nkampigia simu hakupokea, akadai yupo kwenye makelele akitoka atanipigia. Nkamuuliza wewe ni nani ....akadai yeye ni Vero mpenzi wangu. Wakati mimi sijawahi kuwa na mpenzi wala mtu wa karibu au ambae nina mazoea nae tu,anaeitwa Vero. Nilipoendelea kupiga simu yake hakupokea akadai atanipigia soon..... Mwanamke wangu alishindwa kunielewa na akaondoka usiku ule. Alipoondoka nilimtafuta huyo muhuni lakin hakupokea simu,akidai yupo kwenye sherehe ....akitoka atanitafuta,lakini mpaka napaandika uzi huu sijapokea simu yake na mara nyingi hapatikani.

Wadau naomba mnisaidie nitamfahamu vipi huyu mtu ambae lengo lake ni kuniharibia mambo yangu.
Naambatisha na "conversation" tulofanya na huyo muhuni.View attachment 1002396

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahahahahaaaa picha ya kihindi hiyo bro. Pole sana kaka.

Jitathmini, huyo mchumba wako anakupenda kweli maana huenda ni timing ya kukuacha maana baadhi yetu wanaume ni ving'ang'anizi sana na tunasahau kusoma salama za nyakati kabla ya tukio.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maisha ya mahusiano ya siku hizi
1. Jipende , jithamini , jali afya kula vizuri , pendeza.
2. Piga kazi ,, tafuta pesa ,, weka malengo .
3. Katika yote hayo mtangulize Mungu ,,,usisahau sala kila uingiapo na kutoka .

Nawe utakuwa mwenye furaha mengine ni ziada.

PENDA KUJIBEBA HAKUNA WAKUKULETEA FURAHA NDANI YAKO .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom