Uchu wa Viongozi Wetu

Companero

Platinum Member
Jul 12, 2008
5,604
1,704
Wajuvi wa mambo wanasisitiza kuwa riwaya makini hasa zile zilizoandikwa na watu walio karibu na Serikali huwa zinakuwa na taarifa nyeti zilizofichwa kisanii ili kuwafikishia ujumbe wasomaji, yaani wananchi, bila Serikali kushtuka kirahisi. Sasa kuna hii riwaya ya A. E. Musiba inayoitwa 'Uchu' iliyotoka mwaka 2000. Riwaya hii inamuongelea kiongozi mmoja kwa jina JKS na jinsi alivyopatwa na mshtuko huko Ughaibuni baada ya kukuta akaunti yake ya fedha katika benki ya huko imefungwa bila yeye kujua. Kuna mtu yoyote anaelewa nini hasa Musiba ambaye kwa sasa yuko karibu sana na JK katika masuala ya kuinadi Tanzania kwa wawekezaji anajaribu kutueleza hapa? Yafuatayo ni maelezo ya awali katika kitabu hicho ambacho yanaonesha kuwa hii haikuwa riwaya ya kawaida tu bali, kama ilivyo riwaya ya 'Makuwadi wa Soko Huria' au 'Miradi Bubu ya Wazalendo', ilikuwa ni utafiti mpana wa kile kinachoendelea nyuma ya mapazia ya viongozi wetu na wawekezaji wao:

"Kitabu hiki kimeandikwa kwa heshima ya marehemu Abdool Karrim Essack, mwanamapinduzi wa Afrika. Karrim Essack ndiye aliyenichochea kufanya utafiti wa kukiandika kitabu hiki. Siku chache kabla ya kifo chake alipitia ofisini kwangu na kumwuliza katibu shaksia wangu kama nimemaliza kukiandika kitabu hiki. Alipojibiwa bado aliniandikia maneno yafuatayo, ambayo namnukuu kwa kutafsiri: 'Bwana Musiba, Afrika inaingia katika kipindi kipya, kipindi cha ukombozi wa pili. Ukombozi huu ni ukombozi wa fikra na upiganaji wake utakuwa wa kuwaelimisha Waafrika watambue kuwa wao ni taifa lililo kamili na ambalo litakuwa na nguvu kubwa ya kuiongoza dunia katika karne ijayo. Hivyo, kuanzia sasa lazima Afrika iwe na uwezo wa kujiamulia mambo yake yenyewe, ijenge uchumi wake imara ili iondokane na dhana ya misaada. Mwandishi kama wewe una wajibu mkubwa wa kupigana vita hii kwa kalamu. Bwana Musiba andika, na sasa andika zaidi. Punguza shughuli zingine. Afrika inakuhitaji kwani kalamu sasa itakuwa na nguvu kuliko mtutu wa bunduki.'"

Hivi riwaya za huyu 'Willy Gamba' vinapatikana wapi hasa ile ya 'Hujuma'?
 
Wajuvi wa mambo wanasisitiza kuwa riwaya makini hasa zile zilizoandikwa na watu walio karibu na Serikali huwa zinakuwa na taarifa nyeti zilizofichwa kisanii ili kuwafikishia ujumbe wasomaji, yaani wananchi, bila Serikali kushtuka kirahisi. Sasa kuna hii riwaya ya A. E. Musiba inayoitwa 'Uchu' iliyotoka mwaka 2000. Riwaya hii inamuongelea kiongozi mmoja kwa jina JKS na jinsi alivyopatwa na mshtuko huko Ughaibuni baada ya kukuta akaunti yake ya fedha katika benki ya huko imefungwa bila yeye kujua. Kuna mtu yoyote anaelewa nini hasa Musiba ambaye kwa sasa yuko karibu sana na JK katika masuala ya kuinadi Tanzania kwa wawekezaji anajaribu kutueleza hapa? Yafuatayo ni maelezo ya awali katika kitabu hicho ambacho yanaonesha kuwa hii haikuwa riwaya ya kawaida tu bali, kama ilivyo riwaya ya 'Makuwadi wa Soko Huria' au 'Miradi Bubu ya Wazalendo', ilikuwa ni utafiti mpana wa kile kinachoendelea nyuma ya mapazia ya viongozi wetu na wawekezaji wao:

"Kitabu hiki kimeandikwa kwa heshima ya marehemu Abdool Karrim Essack, mwanamapinduzi wa Afrika. Karrim Essack ndiye aliyenichochea kufanya utafiti wa kukiandika kitabu hiki. Siku chache kabla ya kifo chake alipitia ofisini kwangu na kumwuliza katibu shaksia wangu kama nimemaliza kukiandika kitabu hiki. Alipojibiwa bado aliniandikia maneno yafuatayo, ambayo namnukuu kwa kutafsiri: 'Bwana Musiba, Afrika inaingia katika kipindi kipya, kipindi cha ukombozi wa pili. Ukombozi huu ni ukombozi wa fikra na upiganaji wake utakuwa wa kuwaelimisha Waafrika watambue kuwa wao ni taifa lililo kamili na ambalo litakuwa na nguvu kubwa ya kuiongoza dunia katika karne ijayo. Hivyo, kuanzia sasa lazima Afrika iwe na uwezo wa kujiamulia mambo yake yenyewe, ijenge uchumi wake imara ili iondokane na dhana ya misaada. Mwandishi kama wewe una wajibu mkubwa wa kupigana vita hii kwa kalamu. Bwana Musiba andika, na sasa andika zaidi. Punguza shughuli zingine. Afrika inakuhitaji kwani kalamu sasa itakuwa na nguvu kuliko mtutu wa bunduki.'"

Hivi riwaya za huyu 'Willy Gamba' vinapatikana wapi hasa ile ya 'Hujuma'?

Point ni nini hapa?
 
Hawa mabwana mbona walikuwa na wazo jema sana ,tumuunge mkona ambayo bado yu hai.
 
Elvis Musiba na Joram Kiango walikuwa ndio the best...yani nilipokuwa bwana mdogo kuanzia miaka 9 hivi...Nilikuwa sizikosi hizo riwaya hata iweje.

Kuanzia riwaya zenye maudhui ya ukombozi wa Afrika...Na mpambano na Kaburu...Hawa watu ni wa kuwa enzi...Na vitabu vyao vichapishwe upya vina ujumbe mkubwa sana na muhimu.

Namkumbuka sana jamaa yangu mmoja anaitwa Immanuel Shuma...Huyu alikuwa akiniletea karibu kopi zote mara baada ya yeye kuzisoma.
 
Point ni nini hapa?

Pointi ni: Kama ni kweli ukitaka kumficha Mwafrika/Mtanzania kama wewe na mimi kitu kiweke katika Maandishi/Kitabu, je, sisi tunawezaje kuelewa haya wanayojaribu kutufunulia kina Musiba, kuhusu Uchu wa kina JKS, kwa kutumia sanaa ya uandishi/utunzi?
 
Kiongozi ninayemjua ambaye alikuwa account yake tupu ni Marhemu Kigoma Malima. Kama kuna mwingine sina habari zake. Tuendelee na mjadala.
 
Kiongozi ninayemjua ambaye alikuwa account yake tupu ni Marhemu Kigoma Malima. Kama kuna mwingine sina habari zake. Tuendelee na mjadala.

Kweli inawezekana kuzifrizi hizi akaunti za viongozi? Sasa wameshavifungia vijisenti kule Jezi? Au ndio yale ya hotuba ya Kikastro iliyodai kule Idodomya kuwa ni vigumu sana kufuatilia hizo akaunti kama suala haliwahusu na kuwagusa moja kwa moja wenzetu wa huko Ughaibuni?
 
It because waliku brain washed na vyakula vya misaada kutoka NJE miaka ya sitini na mwanzoni mwa sabini. Akili zao sasa zimekuwa manipulated kuwa na ubinafsi na umimi. Bado naendelea kutafiti na nimalizapo hili nitamwaga jamvini data
 
Jasusi,

Si unakumbuka ni nani aliyefunga akaunti ya Kighoma Malima ndiye anayetoa misamaha kwa wakwapuaji wa EPA?
 
Back
Top Bottom