Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Wajuvi wa mambo wanasisitiza kuwa riwaya makini hasa zile zilizoandikwa na watu walio karibu na Serikali huwa zinakuwa na taarifa nyeti zilizofichwa kisanii ili kuwafikishia ujumbe wasomaji, yaani wananchi, bila Serikali kushtuka kirahisi. Sasa kuna hii riwaya ya A. E. Musiba inayoitwa 'Uchu' iliyotoka mwaka 2000. Riwaya hii inamuongelea kiongozi mmoja kwa jina JKS na jinsi alivyopatwa na mshtuko huko Ughaibuni baada ya kukuta akaunti yake ya fedha katika benki ya huko imefungwa bila yeye kujua. Kuna mtu yoyote anaelewa nini hasa Musiba ambaye kwa sasa yuko karibu sana na JK katika masuala ya kuinadi Tanzania kwa wawekezaji anajaribu kutueleza hapa? Yafuatayo ni maelezo ya awali katika kitabu hicho ambacho yanaonesha kuwa hii haikuwa riwaya ya kawaida tu bali, kama ilivyo riwaya ya 'Makuwadi wa Soko Huria' au 'Miradi Bubu ya Wazalendo', ilikuwa ni utafiti mpana wa kile kinachoendelea nyuma ya mapazia ya viongozi wetu na wawekezaji wao:
"Kitabu hiki kimeandikwa kwa heshima ya marehemu Abdool Karrim Essack, mwanamapinduzi wa Afrika. Karrim Essack ndiye aliyenichochea kufanya utafiti wa kukiandika kitabu hiki. Siku chache kabla ya kifo chake alipitia ofisini kwangu na kumwuliza katibu shaksia wangu kama nimemaliza kukiandika kitabu hiki. Alipojibiwa bado aliniandikia maneno yafuatayo, ambayo namnukuu kwa kutafsiri: 'Bwana Musiba, Afrika inaingia katika kipindi kipya, kipindi cha ukombozi wa pili. Ukombozi huu ni ukombozi wa fikra na upiganaji wake utakuwa wa kuwaelimisha Waafrika watambue kuwa wao ni taifa lililo kamili na ambalo litakuwa na nguvu kubwa ya kuiongoza dunia katika karne ijayo. Hivyo, kuanzia sasa lazima Afrika iwe na uwezo wa kujiamulia mambo yake yenyewe, ijenge uchumi wake imara ili iondokane na dhana ya misaada. Mwandishi kama wewe una wajibu mkubwa wa kupigana vita hii kwa kalamu. Bwana Musiba andika, na sasa andika zaidi. Punguza shughuli zingine. Afrika inakuhitaji kwani kalamu sasa itakuwa na nguvu kuliko mtutu wa bunduki.'"
Hivi riwaya za huyu 'Willy Gamba' vinapatikana wapi hasa ile ya 'Hujuma'?
"Kitabu hiki kimeandikwa kwa heshima ya marehemu Abdool Karrim Essack, mwanamapinduzi wa Afrika. Karrim Essack ndiye aliyenichochea kufanya utafiti wa kukiandika kitabu hiki. Siku chache kabla ya kifo chake alipitia ofisini kwangu na kumwuliza katibu shaksia wangu kama nimemaliza kukiandika kitabu hiki. Alipojibiwa bado aliniandikia maneno yafuatayo, ambayo namnukuu kwa kutafsiri: 'Bwana Musiba, Afrika inaingia katika kipindi kipya, kipindi cha ukombozi wa pili. Ukombozi huu ni ukombozi wa fikra na upiganaji wake utakuwa wa kuwaelimisha Waafrika watambue kuwa wao ni taifa lililo kamili na ambalo litakuwa na nguvu kubwa ya kuiongoza dunia katika karne ijayo. Hivyo, kuanzia sasa lazima Afrika iwe na uwezo wa kujiamulia mambo yake yenyewe, ijenge uchumi wake imara ili iondokane na dhana ya misaada. Mwandishi kama wewe una wajibu mkubwa wa kupigana vita hii kwa kalamu. Bwana Musiba andika, na sasa andika zaidi. Punguza shughuli zingine. Afrika inakuhitaji kwani kalamu sasa itakuwa na nguvu kuliko mtutu wa bunduki.'"
Hivi riwaya za huyu 'Willy Gamba' vinapatikana wapi hasa ile ya 'Hujuma'?