Uchu wa madaraka tu utaweza kuiua UKAWA... vinginevyyo CCM haina lake 2015

Nna hamu ya kuona wanavoachiana majimbo unguja na pemba. Au watagawana mapande, cuf wataachiwa zanzibar, chadema na nccr bara!
 
Ukawa ni ndoa ya ghalfa u sina hakika kama wanampango wakuendeleza upinzani kwa hali hiyo
 
hawa 3 ni watu wa busara, SLAA, LIPUMBA, na MBATIA je hawa walioko chini yao? Hapa panahitajika mafunzo,semina, za kujipanga na kimkakati pindi ikitokea ukawa kushinda 2015.

kabla yawepo makubaliano ya kuridhiana nai awe Rais, je UKAWA itamaliza baada ya kushinda au kushindwa uchaguzi? je ikishinda mgawanyo wa madaraka utakuwaje?

haya mambo sio ya kuyangalia kijuujuu nchi za kiafrika viongozi wake mara zote ni walafi na wako tayari kulipoteza Taifa lote kwa mtu mmoja.
 
Wana JF
Kwa hali ilivyo sasa kisiasa Tanzania, matumaini makubwa ni kuiombea UKAWA isimame imara... ni kete pekee ya kuiondoa CCM madarakani uchaguzi ujao. Ni kete pekee kwa sababu ni nguvu ya upinzani iliyounganishwa, na ikiwa haitaingiliwa na ibilisi wa tamaa ya madaraka, basi ni wazi CCM hawana lao tena uchaguzi ujao. Ni vema basi nguvu hii ikadumishwa kwa kuanza kupanga mikakati ya kuachiana nafasi ya kugombea kutoka ngazi ya madiwani, ubunge hadi kumweka mgombea moja tu wa Urais.

Hofu ni kuwa CCM sasa matumbo moto wanaweza kupenyeza mapandikizi wa kuchafua hali ya hewa katika UKAWA.
Ila ni imani yangu kuwa kama hawataingiliwa na uchu wa madaraka, na kama mikakati ya kuachiana kata, majimbo, na hata ngazi ya urais. Matumaini ya kuingia kwenye Nchi ijaayo maziwa na asali yapo karibu kuliko ilivyokuwa utitiri wa vyama vya upinzani kuwagawana kura.
Ni maoni yangu tu, msomaji uko huru kukubaliana nami au la.
Mungu ibariki UKAWA.

uko sawa kabisa.
 
kama ndivyo, kwanini basi ccm inakosa usingizi?

Siku zote when u have someone who challenge u lazima ukose amani kwani unawaza wasije wakafanikiwa na wewe ukashindwa,ila my worry kwa UKAWA is ni muungano ambao hauna vision wala target kwa mimi ninavyoona, ukitaka kujua hayo angalia kilichotokea juzi kwani chadema walikua hawajui kwamba kambo pinzania inaundwa na vama vyote pinzani mpaka ilivyokuja ukawa ndio wakabadilisha ndio mana nasema ni ndoa ya ghafla kudumu kwake ni mashaka sana
 
Amini amini nawaambia kwamba UKAWA ni mpango wa Mungu!! 2015 tunaingia kwenye mabadiliko ya uongozi wa nchi hii - Watanzania tuanze kujitayarisha ki-fikra - Ukombozi unakaribia.
 
WANAUKAWA kama wanania ya dhati wataungana kwa ajili ya kuikomboa nchi lakini kama watakua na ulafi wa madaraka kama ...
 
UKAWA wako serious.....Wale pale juu...MBOWE,LIPUMBA na MBATIA ni watu wenye busara zao....Vyama vyao vimepitia magumu mengi...kwa hio wanajua ugumu wa siasa za Bongo unapo fight peke yako....Tulikua tunasali hili suala la Muungano litokee...Sasa limetokea....hatuna Budi kumshukuru Mungu
 
UKAWA muda si mrefu wataanza vita ya wao kwa wao, katika kugombea nyadhifa mbalimbali.

Wasiwasi wangu mimi hauko kwenye kugombea nyadhifa, I'm 100% sure kwa hilo ndugu zangu wa UKAWA wamejipanga nani awe nani kwani ndicho hasa kilichokuwa kinawaangusha siku zote za nyuma. hilo wameligundua na hamtawaweza kwa hilo.

Sasa kuna hili jipya mlilolianzisha Bw. Msalani la kumuita mtu pembeni na kummwagia mahela ambayo hajawahi kuyaona maishani mwake. Hili ndo kila siku naomba Viongozi wetu wasije kuingia majaribuni, pesa ndio ilimfanya hata Yuda amsaliti Yesu. Muwe makini na hili Viongozi wa UKAWA.
 
Back
Top Bottom