Uchawi ni Janga la ULIMWENGHU

ntamaholo

JF-Expert Member
Aug 30, 2011
12,906
6,909
Uchawi na ushirikina ni suala ambalo lipo kila kona ya dunia hii. Nimetembelea TARIME, wakati naenda kule nilipita DARAJA LA MTO MARA ambalo kabla ya kujengwa kwake, ilikuwepo PANTON=KIVUKO kilichokuwa kinatumika kuvusha watu toka ng'ambo hadi nyingine.

Serikali iliamua kutengeneza daraja la mto huo, ambapo wakazi wa eneo hilo wanabainisha kuwa WACHINA walichukua kandarasi, lakini kila wakijenga, kesho hawakuti hata nguzo moja waliyoisimamisha, hawakuiti hata alama za ujenzi wowote kufanyika. walijaribu mara kadhaa kabla ya kurudisha tenda kwa serikali wakikiri kushindwa kujenga daraja hilo.

baada ya wachina kushindwa, kandarasi ilichukuliwa na WAKOREA, ambao nao kama wachina walishindwa kujenga daraja hilo kwani yaliyowakuta hayakuwa na tofauti ya yale wachina waliyokumbana nao, hivyo nao walirudisha kandarasi.

Ndipo wakaja WARUMI, hawa kama walivyokuwa wenzao, shughuli zote za ujenzi zilifanyika usiku. Lakini tofauti na wenzao, walinunua mbuzi wengi na kondoo na walikuwa hawaliwi, bali wanachinjwa na damu yake inatolewa sadaka hadi ujenzi wa daraja ukakamilika. Darja walilolijenga WARUMI, ni bora sana, na linaswing endapo kitu kizito kimepita juu.

Baada ya warumi kufanikiwa kujenga daraja hilo, eneo hilo hadi leo panaitwa KIRUMI. Baadhi ya picha kuelekea daraja la kirumi ni kama ifuatavyo:-


bonde.jpg

daraja.jpg

daraja mto mara.jpg

mto mara.jpg
watu wengi walipoteza maisha hadi daraja hilo kusimama unavyoliona.
 
maswali ya kujiuliza ni kwamba:-

1. Kwa nini wazungu hupenda kufaya kazi za ujenzi wa madaraja wakati wa usiku na siyo mchana?
2. kuna sababu za kisayansi za wao kufanya hivyo?
 
maswali ya kujiuliza ni kwamba:-

1. Kwa nini wazungu hupenda kufaya kazi za ujenzi wa madaraja wakati wa usiku na siyo mchana?
2. kuna sababu za kisayansi za wao kufanya hivyo?

i once saw in discovery channel na walielezea kuwa madaraja yanajengwa usiku kutokana na mifumo ya upepo..upepo unaovuma usiku nadhan hauna nguvu kubwa kama wa mchana na hii inasaidia katika kulifanya daraja liwe straight,,ni long time sana siwez kuelezea yote waliyosema bt upepo ndio main reason
 
The mainpoint ni kwamba mchana jua ni kali so due to heat expansion inaoccur on iron thats why usiku ndo ryt chois
 
Night-time construction is mainly to avoid traffic congestion and delays that will result from road closures. Heat expansion in metal members is not necessarily the reason since metal will expand regardless be it during construction or operation. Unless if you are dealing with concrete/asphalt where environmental factors (heat,moisture, etc) during placement tend to have an effect on the dry properties(strength,permeability, etc) of the material after placement . A good engineer would take all this into account in their designs (at least that's what my professor says:wink2:). Mchawi mzuri on the other hand will straight up not give a damn and would just roga the p00p out of it.
 
maswali ya kujiuliza ni kwamba:-

1. Kwa nini wazungu hupenda kufaya kazi za ujenzi wa madaraja wakati wa usiku na siyo mchana?
2. kuna sababu za kisayansi za wao kufanya hivyo?
:thinking:
 
Kwa sababu usiku watu na magari mengi yanayopita hivyo kupunguza usumbufu

mkuu lukulo, kabla ya kupost habari hii, niliongea na Engineer mmoja kumwuliza kuna sababu zozote za kisayansi kwa wajenzi wa madaraja kujenga usiku? alinambia hakuna na akaongeza kuwa, kikawaida, mkataba unaposainiwa, zinahesabika saa za kazi kwa maana ya 8hrs only na ikitokea wanaamua kujenga usiku, basi wanaomba kwa serikali wanakubaliwa.

lakini pia, sehemu linapojengwa daraja, siyo rahisi kutumika kusafirishia watu/vitu na kwa daraja hilo kabla ya kujengwa hapakuwahi kuwa na daraja ilikuwepo feery ndiyo iliyokuwa inavusha watu
 
The mainpoint ni kwamba mchana jua ni kali so due to heat expansion inaoccur on iron thats why usiku ndo ryt chois

so you mean kwa mfano ujenzi wa reli ya kati ulifanyika wakati wa usiku kukwepa chuma kuexpand? mbona miradi mingine tofauti na madaraja inajengwa kweupe na inatumia iron ileile? na kama ni daraja la kawaida ambalo halina threat za wanyama wakali, maji yaendayo kasi (kufurika kwa mto) mbona yanajengwa mchana kweupe?
 
i once saw in discovery channel na walielezea kuwa madaraja yanajengwa usiku kutokana na mifumo ya upepo..upepo unaovuma usiku nadhan hauna nguvu kubwa kama wa mchana na hii inasaidia katika kulifanya daraja liwe straight,,ni long time sana siwez kuelezea yote waliyosema bt upepo ndio main reason

upepo? Ngoja nikumbuke pressure principles kwanza
 
Kwa sababu usiku watu na magari mengi yanayopita hivyo kupunguza usumbufu

kwa ujenzi wa draja hilo, hapakuwa na daraja la kuvusha magari, watu walitumia kivuko ambacho hata hivyo nilidokezwa hakivushi magari makubwa, watu walitumia magari mawili kwa safari moja, na kivuko kilikuwa pembeni kabisa mbali na sehem draja lilikojengwa
 
Hata ungetumia Kiswahili tungejua kuwa wewe ni msomi
Night-time construction is mainly to avoid traffic congestion and delays that will result from road closures. Heat expansion in metal members is not necessarily the reason since metal will expand regardless be it during construction or operation. Unless if you are dealing with concrete/asphalt where environmental factors (heat,moisture, etc) during placement tend to have an effect on the dry properties(strength,permeability, etc) of the material after placement . A good engineer would take all this into account in their designs (at least that's what my professor says:wink2:). Mchawi mzuri on the other hand will straight up not give a damn and would just roga the p00p out of it.
 
Hata ungetumia Kiswahili tungejua kuwa wewe ni msomi


I think you looked too deep into, my otherwise very innocent explanation and attempt at humor, and somehow concluded that I was looking to show off. Unless if your comment was meant as compliment, rather than a not-so-subtle dig, in which case I say sorry for misunderstanding your comment and thank you for the compliment. Plus I just spent the past three months in a material properties course, Surely you didn't think I was going to let all that newly acquired knowledge go to waste, did you?:wink2:
 
Bahati yako. Kwenye daraja hili kuna kibao kilichoandikwa "USIPIGE PICHA". Kuhusu uchawi nakubaliana na wewe maana kwenye picha zako ulizopiga kuna "ungo" unalinda daraja hilo. Huo mwekundu.
 
Nadhani ujenzi wa usiku haswa kwa madaraja ni kwa sababu ya kuepuka element mbili JUA na UPEPO. Kwani ukaukaji wa cement unahitaji muda maalumu yaani isiwe kwa haraka sana na kusabisha cracks.Labda kwa kuongezea ni kuepusha usumbufu kwa watu na na vyombo vya usafiri
 
Sikujua kuwa ni hadithi za kubuni. Ukiamini kitu usidhani wote wanakiamini kama ufanyavyo. Kirumi na warumi wapi na wapi kama siyo yale ya mfalme wa Oman ana asili ya Kigoma. Wabongo bwana, michosho!
 
Uchawi na ushirikina ni suala ambalo lipo kila kona ya dunia hii. Nimetembelea TARIME, wakati naenda kule nilipita DARAJA LA MTO MARA ambalo kabla ya kujengwa kwake, ilikuwepo PANTON=KIVUKO kilichokuwa kinatumika kuvusha watu toka ng'ambo hadi nyingine.

Serikali iliamua kutengeneza daraja la mto huo, ambapo wakazi wa eneo hilo wanabainisha kuwa WACHINA walichukua kandarasi, lakini kila wakijenga, kesho hawakuti hata nguzo moja waliyoisimamisha, hawakuiti hata alama za ujenzi wowote kufanyika. walijaribu mara kadhaa kabla ya kurudisha tenda kwa serikali wakikiri kushindwa kujenga daraja hilo.

baada ya wachina kushindwa, kandarasi ilichukuliwa na WAKOREA, ambao nao kama wachina walishindwa kujenga daraja hilo kwani yaliyowakuta hayakuwa na tofauti ya yale wachina waliyokumbana nao, hivyo nao walirudisha kandarasi.

Ndipo wakaja WARUMI, hawa kama walivyokuwa wenzao, shughuli zote za ujenzi zilifanyika usiku. Lakini tofauti na wenzao, walinunua mbuzi wengi na kondoo na walikuwa hawaliwi, bali wanachinjwa na damu yake inatolewa sadaka hadi ujenzi wa daraja ukakamilika. Darja walilolijenga WARUMI, ni bora sana, na linaswing endapo kitu kizito kimepita juu.

Baada ya warumi kufanikiwa kujenga daraja hilo, eneo hilo hadi leo panaitwa KIRUMI. Baadhi ya picha kuelekea daraja la kirumi ni kama ifuatavyo:-


View attachment 49989

View attachment 49990

View attachment 49991

View attachment 49992
watu wengi walipoteza maisha hadi daraja hilo kusimama unavyoliona.
tatizo letu kila tusichokifahamu au kukijua badala ya kuchukua muda na juhudi ya kufahamu tunakitupia kwenye kapu la uchawi. na tutaendelea kuwa watumwa wa wenye uwezo wa kufikiri siku zote za uhai wetu na uhai wa taifa letu
 
Mchawi ni nani? mchawi ni mtu asipenda maendeleo ya mwenzake. badala ya yeye kujifunza mwenzake ameendeleaje yeye angependa mwenzake afe. mfano wa mchawi wa Tanzania ni CCM. post yako isingesema duniani maana wenzetu walioendelea hawalogani ili kuzuia maendelea bali wanashikana bila kujali tofauti zao na kuleta maendeleo kwa nchi zao. kuhusu tarime na daraja mimi siamini hizo story maana kama wako fiti ki hivyo si watulogee yanga tusiwe tunatolewa round ya kwanza?
 
maswali ya kujiuliza ni kwamba:-

1. Kwa nini wazungu hupenda kufaya kazi za ujenzi wa madaraja wakati wa usiku na siyo mchana?
2. kuna sababu za kisayansi za wao kufanya hivyo?
Hapo palipo jengwa Daraja sio kwa sababu ya Uchawi mkuu hapo palipo jengwa Daraja pana Mashetani wabaya wa huo Mto ndio waliowazuia hao Wa China na Wa korea

kujenga hilo daraja, mpaka akaja huyo Mrumi aliyejenga usiku Daraja na kutoa Kafara ya mbuzi wengi yaani Damu kamwaga. Zipo baadhi ya nyumba hatu huku ulaya Watu hawawezi kukaa kwa sababu kuna Mashetani ndio

wanaoishi ukilala usiku kwenye hizo nyumba kama ulifunga maji chooni basi utakuta maji yanamwagika kama ulifunga TV kwenye chumba chako cha kufikia wageni Sitting room utakuta TV yako imefunguliwa hiyo TV kwa sauti kubwa,

ukienda kuangalia huko kwenye TV hakuna aliye funguwa hayo sio mambo ya kichawi ni Mambo ya Mashetani wabaya Pepo wabaya waliomo ndani ya hiyo nyumba. Mkuu tofautisha Mchawi na Mashetani. Mchawi ni ni Binadamu anayeonekana ni yule mtu

anayefanya huo Uchawi na Shetani au Mashetani ni Viumbe aliowaumba Mwenyeezi Mungu, wasio onekana kwa macho yetu ingawa tupo nao kwa wakati wowote ule wapo tunaishi nao hao viumbe wa ajabu Mashetani na binadamu na wapo wanaoishi hao mashetani porini kwenye

Miti mikubwa kwenye bahari au mito au chooni au sehemu inayotupwa takataka, sasa mkuu tofautisha mambo ya uchawi na mashetani nakuacha hapo kwa leo.
 
Back
Top Bottom