Uchawi na kilimo

Uchawi na kilimo

Ujue uchawi upo kwenye kila sekta ya uzalishaji mali, maofisini & majumbani n.k.
Muhimu ni kujiweka sawa tu kuanzia nyumbani wewe pamoja na familia yako & kazini kwako.

Maana mchawi/mwanga lengo lake hasa ni kukurudisha nyuma na kukukomesha yaani akishindwa kukuroga wewe ataroga mke, watoto au yoyote aliyoko kwenye familia yako na akiwakosa wanafamilia atataka kukukomesha katika kazi unayofanya lengo lake hasa upate tabu, shida, maafa na dhiki ili usiendele.
 
Huo mkanda mzima uko wp ss
NIkiwa katika mihangaiko yangu kipindi flani niliamua kuwekeza katika kilimo cha mpunga hapo maeneo ya Mlandizi ila Sasa niliyokuja kuyaona niliamini hakuna Mungu kwenye kulima mana wakati wa kupanda kila Mkulima alikuja na njia zake za kufanikisha kupanda.

Jilani yangu yeye alikuja na vijana wake wakalizunguka Shamba huku wapo uchi na kichwani walikuwa wamebeba chungu kilichojaa majimaji.

Kuangalia upande mwingine wa Shamba naona mtu anaandikiza hilizi kiukweli niliamini kuliacha lile Shamba mana ni mashamba ya kukodi na niliamua kuondoka kabisa baada ya kuulizia habari za eneo lile kipindi cha kilimo inakuwaje nikapewa mkanda mzima
 
TAYAAARI wakimaanisha nn?
Mzee wangu alilima heka 3 za mpunga kule mbalali nilipokuwa darasa la pili.
Sasa baada ya kupiga mpunga vizur akapata gunia kumi na sita tu, na wakati wengine hizo ni kwa heka moja ti.

Siku anatoa tukubai, chini yake alitoka kenge mkubwa sana, na yule kenge hakuwa anakimbia wala nini. Alikuwa anatembea taaaaratibu. Wenyewe wakaropoka tu TAYAAARI .
 
Yani nilipoambiwa mkanda mzima nilimanisha kuwa nilipewa simulizi za eneo lile kuwa kilimo cha pale kinahitaji uwe vyema uende kwa babu akupike mana unaweza kulima ukakuta mwisho wa mavuno umevuna kidogo na wengine huhamisha mazao ya mwenzie kwa njia za kichawi unaweza kuta mpunga umestawi ukajua hapa kwa hrka mbili hizi sikosi gunia 40 mwisho unajikuta unagunia kumi kingine unaweza shangaa Mamba anakuja Shambani kwako analaza mpunga wote ule kisha anaupulula hii niliishuhudia kwa macho yangu mwenyewe
 
Hapa kama kuna ukweli,nina mikorosho km 30 shambani kwangu inatoa maua mengi sana ila siambulii hata gunia moja
nasikiaga wakulima wa korosho wanahamisha Maua na matunda, waeza ona mkorosho wako una mauaa mengi ukajuwa mwaka huu umwe win..... ikifika wakati wa mavunoooo unatoka KAPAAaaaa
 
Uchawi huu ndio umerudisha nyuma maendeleo yetu hapa nchini. Asilimia zaidi ya 90 ya watu kwenye uzalishaji iwe kuchimba madini, kuvua au kulima wanategemea "ndumba" Wasilolijua ni kwamba UKIMTEGEMEA MUNGU ASILIMIA MIA atakulinda na huo uchawi. Hautakupata.
 
Ni kweli kuna vitu lazima tumtegemee Mungu ila katka hili la kilimo kuna vitu vingine niliona niliona naendelea kupoteza mda nitakupa mfano mdogo tu wa yaliyonitokea kule malinyi napo kwenye mpunga .baada ya kulima heka 3 mpunga ulianza kusinyaa na hapo nilikuwa nimeweka na maji ya balaka mule shambani baada ya kwenda kanisani na kueleza matatizo yangu ndio nilipewa hayo maji lakini mpunga ulisinyaa ndipo nikaona isiwe tabu nikaenda sehemu hapa dar nikapewa dawa na kwenda kuweka shambani cha ajabu baada ya wiki mpunga ukanyooka kiasi kwamba kila mtu akawa ananiuliza mi nikawa kimya na kwenye kuvuna nilitoa gunia 75 za debe Saba Saba kitu ambacho kiliwashangaza wakulima wengi sana pale na hata wengine wakawa nikiwasemesha wananuna hasa wenyeji.Sasa vituko siku nimeanika mpunga akaja Mzee akasrma dah mpunga umetoka vyema huu halafu hapo hapo akaanza kuluka salakasi juu ya mpunga niliouanik
Kwann sarakasi na ulinfanyaje
 
Back
Top Bottom