Ni kweli uchawi upo ila ukikuta mtu anaamini uchawi na kuutegemea, jua tu ya kuwa ukoo wao hata wazazi wao wana Mambo ya mazindiko na uchawi, ukweli ni kuwa Duniani hapa huwezi kufight alone, lazima uwe na nguvu ya ziada, na nguvu zipo mbili tu Nguvu ya Mungu na Ya Shetani (ushirikina), Kwa sababu kumtegea Mungu kunahitaji kujinyima na kujitoa hasa na uvumilivu, wengi hukimbilia cheap option upande wa pili yaan upande wa shetani, Kwa shetani utafanikiwa ndio lakni Kwa mda mfupi na Kwa mateso Sana, kukosa uhuru na kulazimika kutoa makafara na kila adha, na finally kushuka kaburini bila tumaini .....
Kumtumaini Mungu ni option bora kabisa, itakuweka huru sana, Siri yake kuu ni kuacha dhambi, kuomba Mungu, kufanya kazi Kwa bidii na kufanya kila uwezalo kutatua changamoto zinazokukabili kwenye kazi unayofanya alafu sehemu inayobak mwachie Mungu amalizie....
Shida kubwa tuna maisha ya Dhambi, wazembe wa kutatua changamoto, uzinzi, uasherati, utapeli, ufisadi, Roho mbaya n.k, asikudanganye mtu haya Mambo huwa yanazuia nguvu ya Mungu na ndo mana wengi hukimbilia Kwa shetani mana anakupa mafanikio hata kama we ni mzinzi na tapeli,...
Mimi nililima mpunga mwaka 2015, hekari moja, nikascore gunia 18 za dede 10...ndo kijana niliyepiga zaidi kijiji kizima huko usukumani, watu waliniulizia mganga wangu ni yupi...wengine waliniambia ukoo wangu upo strong sirogeki ovyo, nikawaambia Mimi ni Mungu tuu na hakuna kingine....
Mwaka Jana nilikuwa Tabora , nyumba niliyopanga ilikuwa imeshindikana kupangika, ilisemekana ni nyumba yenye mashetani, watu walishangaa kuniona natoka na kuingia kwenye nyumba ile bila was was, siku moja watu wakaniambia hvi una mganga gani anayekufanya uishi kwenye hyo nyumba nikawaambia mi naamini Mungu na hawez kunitupa kwenye ujinga kama huo, waliniogopa Sana , walikuwa wanadai huko nyuma hyo nyumba ilikuwa inawaka Moto usiku ...
Mwaka huu hali ya ukame imeleta shida sana, nililima kidogo tu na sikuvuna sana, nilishia kulima robo hekar nikapata kama nusu gunia, mwaka huu nataka ninunue mashine ya kumwagilia alaf nitafute eneo zuri ili kukabiliana na hali ya ukame alafu na kiwasha tena , nitawapa mrejesho mwaka kesho, Mimi siogopi uchawi, nitashindwa Kwa sababu zingine za kawaida kama ukame na sio uchawi....
Wale manotaka kulima we lima tu usiogope mtu na mtumaini Mungu, achana na Mambo ya kutoa makafara watoto na wazazi au kufanyiwa mambo ya ajabu na waganga, mara utembee usiku huku umebeba mabundi, au kulala na nyoka, ili upate mafanikio, huko ni kujidhalilisha tu.....
Pambana upande wa Mungu ushindi ni hakika cha msingi uwe mvumilivu na uache dhambi