Uchambuzi: Tough times never last, Tough people Do!

Uchambuzi: Tough times never last, Tough people Do!

Nanyaro Ephata

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2011
Posts
1,237
Reaction score
1,828
Jina la Kitabu. Tough Times Never Last, But Tough People Do!

Mwandishi. Robert H. Schuller

Mchambuzi. Nanyaro EJ

Utangulizi

Mwandishi anasema kuwa Mwenyenzi Mungu amempa mwongozo mzuri na neema ya kutambua wakati wa kuachia jambo na wakati wa kungangana na jambo. Pia amejaliwa neema ya kujua na kutambua wakati sahihi wa kufanya maamuzi sahihi

Watu wengi wametamani sana kupata hii neema na ni maombi ya watu wengi sana, hiki kitabu kitafungua njia ya kutambua neema hii.. yaani kupitia kitabu hiki maombi yako yatajibiwa!au ndio majibu ya maombi yako.

Kitabu hiki kitakupitisha kwenye matendo magumu ya

A. Kushikilia/Kungangania hadi upenyo utoke, kufanya jambo litokee hata wakati ambako kunaonekana ugumu wa hali ya juu, kutoboa hadi patoboke hata kama ni mwamba imara kiasi gani… (wachimbaji wataelewa kwa urahisi). Kuwatia watu moyo hata wakati ambako wewe binafsi unapita kwenye bonde la uvuli wa mauti, kuleta mabadiliko chanya nyakati ambazo kila moyo wa mmoja umekata tamaa kwenye mazingira ambayo hakuna tena tumaini

B. Kuleta matumaini mapya, na hali ya udhubutu, kubuni nyakati mpya, kutambua kuwa nyakati na majira yamefikia mwisho na mwanzo mpya unahitajika, muhimu kutambua maji yakimwagika hayazoleki… usije ukajikuta unafanya kazi ya kupigia mbuzi gitaa. Kutambua majira na nyakati ni muhimu sana ili kusaidia kuanzisha mbinu mpya za mapambano ya maisha

Mbinu mpya, nguvu mpya, akili mpya, na matokeo tarajiwa
 
Kitabu.Tough Times Never Last, But Tough People Do!
Mwandishi.Robert Schurler
Mchambuzi.Nanyaro EJ


Chapter 1 Tough Times Never Last…

Hata nyakati ambazo umefanya kila njia na kila mbinu..kumbuka kuwa…………bado kuna njia

Mwandishi anasema kuwa mwaka 1982 ilikuwa kama Dunia imerudi kwenye miaka 1920 wakati wa Great Depression,makampuni yalikuwa yanafungwa,biashara hakuna,ajira hakuna.Wakati haya yakitokea huko USA wanasiasa walitumia kama njia ya kujitengenezea,Democratcs walikuwa wanalaumu Republican ambao ndio walikuwa na serikali.Republican walirudisha lawama kuwa ni tatizo waliloridhi kutoka Utawala uliotangulia wa Democratic .

Hapa kila mmoja hakujishughulisha na tatizo bali lawama.Hivo tatizo liliendelea kuwepo na kwa kuwa hakuna kinga kila mmoja aliadhirika kwa kiwango chake

Kila mtu alijua na aliona kuwa Nchi ilikuwa inapitia kipindi kigumu.Tatizo kubwa ilikuwa attitude ya kukabiliana na tatizo la uchumi.Fikra hasi zilikuwa ndio zinaongoza jamii…hapa kila mwanajamii alilaumu badala ya kushughulika na tatizo..fikra hasi zinaenea kwa kasi kuliko moto wa kifuu kupitia neno la mdomo na njia nyingine za mawasiliano ya kijamii

Mwandishi anasema hii mitazamo hasi na fikra hasi za kijamii ndio aliziona kama fursa na akaanza kutoa semina,na mihadhara kwa watu wa kada mbalimbali.Alianza kwa ugumu ila taratibu watu walianza kumwelewa na kubadilika,kuna kipindi alikuwa anahutubia zaidi ya watu laki tatu kwa mara moja,kwenye hotuba zake aliwafundisha kuhusu mtazamo chanya,fikra chanya…mtazamo/fikra chanya ni moja ya njia bora kabisa za kutatua changamoto ya maisha.Hata hivyo mwandishi anakiri ilikuwa nyakati ngumu sana kuwahubiria matumaini watu ambao wamekata tamaa na hawaoni njia yoyote mbele yaohata hivo hakukata tamaa(ni kama vile unaandika jambo la muhimu kwenye ukurasa wako wa FB hupati likes hata moja ila usikate tamaa tamaa wewe usitazame like,endelea kusonga mbele)

Mwandishi anasema ushuhuda una nguvu kubwa sana, mwandishi anasema alikuwa na tabia ya kuandika changamoto na jinsi alivozitatua,njia,na muda wa utatuzi,kisha aliandika ushindi jinsi alivoshinda,hivo alitumia ushuhuda huu kama njia ya kuwatia watu moyo!(hapa tunaona umuhimu wa maandishi).Anashauri jamii kuwa na tabia ya kuandika na ku share na wengine kama mojawapo ya njia za kuhamasisha ujenzi wa fikra chanya.

Mwandishi anasema alikuwa mkulima mdogo ambaye anafahamu changamoto za ukulima,ikiwepo mvua,na bei isiyo na uhakika.Kilimo hakijawai kuwa rahisi lakini haikufanya wakate tamaa,bali kutafuta njia ya kuboresha zaidi.Anasema mchakato wa kilimo ulimbadili fikra sana,kile kitendo cha IMANI cha mkulima kutupa mbegu chini na kuamini kuwa mvua itanyeesha na hiyo mbegu itazaa,kilikuwa kitendo cha IMANI kubwa na kitendo cha kishujaa.Wakulima ni kundi la kijamii lenye imani kubwa sana na fikra chanya.Alimuuliza baba yake mbona unafanya pata potea? Baba yake alimjibu binadamu asiyekuwa na udhubutu wa jambo daima hubaki hapo hapo alipo bila kusogea mbele(Ndugu msomaji wangu chukua hatua,dhubutu kama mkulima haki utavuna)Mkulima anaweza akaotesha mbegu yake ya mwisho kabisa akabaki hana chakula lakini ana matumaini ya kuvuna baada ya muda fulani,ni kwa kuwa ana imani kuwa Tough times never last but tough people do!anasema anakumbuka mwaka fulani ambao mvua hazikunyeesha hivo ikawa vigumu kuvuna,bahati mbaya mwaka huo baba yake alikuwa amekopa bank na kama hawajavuna maana yake wangefilsiwa,ila baba yake alikuwa mtu wa imani kubwa,akaenda bank kuomba nyongeza ya muda wa marejesho,akiwa na matumaini pengine mavuno ya msimu ujayo yatakuwa makubwa,ghafla ikatokea balaa jingine la kimbunga,ilibidi watoroke na gari yeye na wazazi wake kuelekea mwelekeo kinyume cha Kimbunga,walifanikiwa kuokoa maisha yao,ila mazao na nyumba ziliharibiwa vibaya na kimbunga,hii ni nyumba ambayo iliwekwa dhamana bank,na mazao tarajiwa yakawa yameharibiwa.Hata hivo Baba yake hakukata tamaa,ni baba aliyekuwa na imani ya kuhamisha Mlima,imani ya kutembea juu ya Bahari,Imani ya kutatua kila changamoto,Baada ya miaka mitano Baba yake alijenga na kulipa madeni yote……Je tough times ilidumu? Jibu lake hapana…Usiogope

Mwandishi anasema akiwa ni mtu aliyelelewa katika maisha ya ufukara uliopiytiliza yaani chini ya mstari wa ufukara,hakuruhusu hali hiyo iwe mtego kwake,bali aliifanya kuwa sehemu ya historia ya maisha yake yenye mafanikio makubwa.Anasema wakati fulani wazazi wake walikosa hela ya kununua mkaa ili kupasha nyumba joto wakati wa baridi kali huko kwao.Alilazimika kwenda kuokota magunzi na takataka zingine ambazo walizichoma kama njia ya kupasha moto nyumba.

Mwandishi anakuuliza,je unapitia wakati mgumu?kumbuka maisha yako ni mwanga kwa mtu mwingine,hivo usikubali kukaa gizani muda mrefu.Kuna njia inaitwa “The Possibility Thinking Path.” Njia hiiimekuwa na mafanikio makubwa maishani kwa kila anayeitumia.Hakuna mtu wala binadamu aliyeandikiwa kushindwa tu,wanaoshindwa ni wale ambao hawachukui hatua kudhubutu!Udhubutu ni tiba na suluhisho la changamoto za maisha

Mwandishi anasema kuwa kila binadamu ana tatizo/changamoto yake,hakuna maisha bila changamoto.Lazima ujifunze kuelewa changamoto yako na jinsi ya kutafuta suluhisho,hakuna suluhisho linalofanana kwenye kila changamoto,suluhisho hutegemeana na mazingira mahalia.Jambo la msingi ni kuhakikisha kuwa una control changamoto yako,kamwe usiruhusu changamoto yako iku control.Maisha ya wengi yamekuwa na utata mtupu kutokana na watu husika kushindwa ku control changamto zao na kuendeshwa na presha za nje.Lazima uonyeshe uongozi pale unapokuwa kwenye changamoto




Kitabu.Tough times never last,Tough people do!
Mwandishi.Robert Schurller
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Chapter 2: Here’s How You Can Be Tough Too!

Kamwe usiruhusu tatizo/changamoto kuwa sababu au uhalali wa kushindwa kwako
Nini siri ya mafanikio ya watu wanaofanikiwa?Je huwa wanashindaje changamoto ambazo wengine hushindwa?Kwani nini hushinda wakati wengine hushindwa?kwa nini hawazami wakati wengine huzama?
Jibu la maswali yote hayo ni rahisi sana, ni jinsi wanavyotazama tatizo,kwa mtazamo chanya…………….wanalitazama tatizo katika uhalisia wake,na wanaelewa kanuni sita za kutatua changamoto.Hizi ni kanuni sita ambazo ukizizingatia utalishinda tatizo na kuwa mshindi wa maisha yako mwenyewe

1. Every living human beings has problems. Tatizo ni nini? Je unatafuta ajira na hujapata?kama ukiwa na mtazamo hasi utafikiria kuwa kazi ni suluhisho la matatizo yako yote…yaani ukipata ajira utakuwa umemiliki Dunia na Ulimwengu wote.Ukweli ni kuwa walioajiriwa wana matatizo/changamoto pia.Waajiriwa wengi hulalamikia kuwa wanapaswa kuwahi kazini kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa(Baadhi ya Sekta ya Umma)hawana muda wa kufanya jambo lolote,hawa huishia kufanya kazi ili waishi..kazi ya ujira mdogo,They work to live rather than live to work.Matokeo yake hawa waajiriwa huwa hawafanyi kazi kwa weledi wala ubunifu
Je waastafu ndio ambao hawana changamoto? Hapana hata waliostaafu wana changamoto nyingi hasa baada ya kustaafu hutamani kurudi tena kazini,yaani anatamani aamke asubuhi akimbizane…maisha ya kustaafu nayo yana changamoto zake
Je waliofanikiwa?Kimsingi mafanikio ya kiuchumi hayaondoi changamoto,bali huzalisha changamoto mpya
Hakuna mtu wala binadamu ambaye hana changamoto za Maisha
Mwandishi anasema yeye alikuwa na ndoto ya kumiliki kanisa kubwa kabisa,lenye uwezo mkubwa,kwa hesabu zake aliona itamchukua miaka 40 kumiliki hilo kanisa lenye uwezo wa kukaa watu 6000 kwa mara moja.Akaanza kufanyia kazi ndoto yake,ndani ya miaka mitano tayari alikuwa na watu zaidi ya 6000 waumini wa kanisa lake.Anasema hii ilimfundisha kufanyia kazi ndoto yake kwa bidi,na ilimpa somo kuwa kadri unavofanikiwa ndio mahitaji yanaongezeka,alijikuta ana waumini wengi kuliko uwezo wake,na kuliko ndoto yake ya msingi,waumini walifika na kukosa maegesho hali iliyofanya aondoke hata kabla ya kushuka kwenye gari…….Mafanikio huvuta watu zaidi na hivo hitaji huongezeka……

Mfano unaweza ukaanzisha kampuni ya bidhaa fulani,soko likakuendea vizuri sana,ukapata mauzo makubwa,ukajikuta saa tisa mzigo umeisha sokoni,kule kuisha sokoni kutafanya uanze kutafuta njia ya kuongeza uzalishaji na masoko mapya.Hivo hakuna kilele cha mafanikio,kila mara utahitaji zaidi na zaidi
Maisha bila changamoto hayapo na sio maisha,kubali changamoto na songa mbele……………


2. Every problem has a limited life span.
Kila mlima una kilele chake,na kila bonde lina kina chake,ndivo maisha yalivo na mabonde na milima yake,hakuna atakayekaa juu daima,wala hakuna atakayekaa chini milele.Changamoto huisha,na kutoweka.Hakuna hali ya kudumu kwenye maisha,


3. Every problem holds positive possibilities.
Mwandishi ananukuu Bibilia takatifu Mithali 25-2 ambayo inasema Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo,.Kila changamoto huwa na mazuri yake,sio kila chanagmoto ni laana.Shilingi ina sehemu mbili,jambo ambalo ni changamoto kwako ni fursa ya kibiashara kwa mwingine,mfano ukiumwa Malaria ni changamoto kwako,ila kwa mmiliki wa hospital ni fursa ya kutengeneza hela.Kuna vitu kwenye maisha yetu vinalenga kutatua changamoto lakini lazima mtu apate shida,


4. Every problem will change you.
Changamoto huwa haikuachi vile imekukuta,lazima italeta mabadiliko chanya kwenye maisha yako,kuna funzo utapata la maisha.Unaweza ukafutwa kazi kwenye kampuni A ikawa ni njia yaw ewe kupata kazi nzuri zaidi kwenye kampuni B.Kuna nyakati unaweza ukaugua ukaenda hospital kumbe ni nia ya kumpata mwenza/mwenzi wa maisha yako!

5. You can choose what your problem will do to you.
Muda nyakati ngumu huja bila taarifa,lakini ni jukumu lako kushinda hizo nyakati ngumu na kuzibadili kuwa fursa kubwa kwako.Hakikisha hauwi mtumwa wa tatizo,hakuna changamoto yako au huna hakimiliki ya changamoto fulani wala nyakati fulani ngumu.Tambua nyakati na shinda nyakati


6. There is a negative and a positive reaction to every problem.
Watu wenye mafanikio na ambao wameshinda nyakati ngumu…hufanikiwa kutokana na namna wanavotazama nyakati na changamoto zake.Mtazamo hasi au chanya huamua namna ya ushindi! Swala namba moja kuelekea ushindi ni mtazamo chanya,ukweli ni kuwa sio jambo rahisi kama ilivokuandika,ni jambo gumu kuwa na mtazamo chanya kwenye nyakati ngumu na changamoto lukuki,ila lazima kufanya pamoja na ugumu wake!
Mwandishi anatoa mfano wa mtazamo hasi kuwa ni pale ambako umefutwa kazi,unaenda baa kulewa au kuvuta bangi kama sehemu ya suluhisho la changamoto yako!kimsingi hapa unaongeza ukubwa wa tatizo badala ya utatuzi!au wengine huamua kuiba ili kupata ada au matibabu,,utaishia jela kwa kosa la wizi.Mtazamo chanya ni mgumu ila muhimu,unaweza kuwa unadaiwa njia chanya ni kumfuata mdeni wako na kumweleza ukweli,kisha umwombe akupe muda wa kulipa kile unachodaiwa badala ya kukimbia kimbia na kuzima simu au kutopokea simu!

Mwandishi anasema kuna changamoto nyingine unaweza kushindwa kuzitatua ,pale ambako utatuzi umeshindikana angalau hakikisha kuwa una control tatizo..yaani wewe ndio unakuwa juu ya tatizo.Kuna kanuni kumi na mbili za kukabiliana na changamoto/nyakati ngumu


1. Don’t underestimate.
Usidharau wala kupuuzia tatizo,au chagamoto ya maisha,maana huanza kidogokidogo,hatimae huwa kubwa.Changamoto nyingi zimekuwa kubwa baada ya mwanzo kupuuziwa au kutofanyiwa kazi kwa usahihi,unawezakuta mzazi anasema mtoto wangu hafanyi vizuri darasani,lakini atajua tu mbeleni…au naumwa kichwa ila ni kawaida tu kwa kuwa sijanywa maji leo na jana……navuta sigara moja tu hivo siwezi kupata madhara kama wengine…………..matatizo hukua taratibu kama ujauzito…….

2. Don’t exaggerate.
Usikuze changamoto yako na kuifanya ya pekee Duniani.Au usifanye kuwa changamoto yako ndio imeleta balaa zote,na hivo kupata kitu cha kujifichia.Kuna watu huwa wakifiwa tu basi ndio sababu ya kila kitu……akifukuzwa kazi anafanya ndio wa kwanza kufutwa kazi…The one battle most people lose is the batter over the fear of failure… try… start… begin… and you’ll be assured you won the first round.

3. Don’t wait.
Ni kosa kubwa kukaa na kusubiri mambo yatokee…mambo hufanywa kutokea,hayatokei kwa bahati mbaya bali kwa mipango.Kama umefutwa kazi usije ukarudi nyumbani ukakaa kimya bila kuchukua hatua,Mwombe Mwenyenzi Mungu ,kisha chukua hatua….usije ukaketi kusubiria kuitwa kazini tu.Kusubiria muujiza bila kuchukua hatua stahiki kunaweza kupelekea tatizo kuzidi kukua na kuzaliana(Mwenyenzi Mungu ametupa akili ya kufikiri sawasawa na kuchukua hatua)

4. Don’t aggravate.
Usianze kurusha lawama kwa wengine,jamii,kampuni..ukaanza kusema kwa nini meneja amenifuta kazi mimi,huyu meneja yuko hivi ama vile…ukifanya hivo utakuwa unaongeza tatizo! Weka mtazamo chanya tu………

5. Illuminate.
Jiulize maswali kadhaa,je kuna mtu aliwahi kupata tatizo kama langu akalishinda?kuna mtu amewahi kupita kwenye nyakati ngumu kama hizi zangu akashinda?Je nimefukuzwa kazi au nimestaafishwa mapema?Je tatizo lako ni fedha kweli au ni matumizi mabaya ya fedha ulizo nazo hadi unafikiri hazitoshi?pengine unapaswa tu kubadili matumizi yako kisha utapata akiba,



6. Motivate.
Mtazamo chanya hupelekea suluhisho chanya,mfano kuna watu ambao ni walevi wa kupindukia,ulevi wake husababishwa na marafiki zake.Ukitaka kuacha ulevi sharti uachane na hao marafiki zako walevi……….ni swala la uamuzi sahihi kwa matokeo sahihi
Kuna wakati kwenye maisha unahitaji tu kufanya uamuzi sahihi ambao unatibu matatizo yako yote!

7. Bait.
Mwandishi anasema wakati mwingine unapswa kuwa kwenye sehemu sahihi kupata majibu sahihi,na matokeo tarajiwa,kuna watu kwenye maisha yao wapo sawa na mtu anayesubiria ndege itue baharini.Tambua sehemu sahihi ya kupata majawabu ya changamoto yako! Mfano unapenda kuvua sharti uende kwenye maji,mtoni,ziwani,baharini…huko ndio uvuvi hufanyika,pili unataka kuvua nini samaki gani,uende anakopatikana


8.Date.
Kama huna ajira na unahitaji kuajiriwa nenda katafute ajira kama mtu atafutavyo mchumba.Usijiwekee limit kuwa siku hizi hakuna ajira na zilizopo hadi uwe na fodfather wa kukushika mkono….Jiamini wewe ni godfather wa maisha yako,wewe ni shujaa wa maisha yako mwenyewe…usijikatishe tamaa ukitarajia kuna mtu atakuja kukutia moyo.Lazima utambue kuwa kila siku kuna mtu anastaafu au kuacha kazi hivo usikate tamaa

9. Sublimate.
Mlango mmoja ukifunga mingine inafunguka………..ifanye changamoto yako kuwa ngazi ya kupandia utukufu hadi utukufu


10. Now dedicate.
Watu wengi hushindwa sio kwa kukosa fursa,au kukosa akili au kipaji bali hushindwa kwa kuwa huwa hawashughuliki na tatizo husika bali dalili za tatizo.Ni lazima ushughulike na kiini…lazima uangalie mahali umejikwaa sio mahali umeangukia
Ukijitoa kwenye maisha ni ufunguo muhimu wa kufungua milango yako mingine…ukifanya kazi kokote fanya kwa bidi,na weledi utashangaa vile utafanya watu bora zaidi…unaweza kuwa muhudumu kwa mama ntilie ukamhudumia mteja kwa bidi na weledi kumbe huyu mteja ni mmiliki wa hotel ya nyota tano ukajikuta umepata ajira bila kuandika barua,bidi na weledi na kujitoa kwa moyo wote ni ufunguo tosha!



11. Communicate.
Usijimwambafai! Jifunze lugha bora ya mawasilano yenye mtazamo chanya.Mawasiliano ya kijamii ni moja ya njia bora za kutatua tatizo kwenye jamii.Kuwa mnyenyekevu wakati wote


12. Insulate.
Usijitenge wala kujificha ukiwa kwenye changamoto! Usianze kuwa kwenye mwonekano wa ovyo kwa kuwa tu una changamoto
 
Jina la Kitabu. Tough Times Never Last, But Tough People Do!

Mwandishi. Robert H. Schuller

Mchambuzi. Nanyaro EJ

Utangulizi

Mwandishi anasema kuwa Mwenyenzi Mungu amempa mwongozo mzuri na neema ya kutambua wakati wa kuachia jambo na wakati wa kungangana na jambo. Pia amejaliwa neema ya kujua na kutambua wakati sahihi wa kufanya maamuzi sahihi

Watu wengi wametamani sana kupata hii neema na ni maombi ya watu wengi sana, hiki kitabu kitafungua njia ya kutambua neema hii.. yaani kupitia kitabu hiki maombi yako yatajibiwa!au ndio majibu ya maombi yako.

Kitabu hiki kitakupitisha kwenye matendo magumu ya

A. Kushikilia/Kungangania hadi upenyo utoke, kufanya jambo litokee hata wakati ambako kunaonekana ugumu wa hali ya juu, kutoboa hadi patoboke hata kama ni mwamba imara kiasi gani… (wachimbaji wataelewa kwa urahisi). Kuwatia watu moyo hata wakati ambako wewe binafsi unapita kwenye bonde la uvuli wa mauti, kuleta mabadiliko chanya nyakati ambazo kila moyo wa mmoja umekata tamaa kwenye mazingira ambayo hakuna tena tumaini

B. Kuleta matumaini mapya, na hali ya udhubutu, kubuni nyakati mpya, kutambua kuwa nyakati na majira yamefikia mwisho na mwanzo mpya unahitajika, muhimu kutambua maji yakimwagika hayazoleki… usije ukajikuta unafanya kazi ya kupigia mbuzi gitaa. Kutambua majira na nyakati ni muhimu sana ili kusaidia kuanzisha mbinu mpya za mapambano ya maisha

Mbinu mpya, nguvu mpya, akili mpya, na matokeo tarajiwa
Weka PDF tusome braza

#YNWA
 
Kitabu.Tough times never last,Tough people do!
Mwandishi.Robert Schurller
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Chapter 2: Here’s How You Can Be Tough Too!

Kamwe usiruhusu tatizo/changamoto kuwa sababu au uhalali wa kushindwa kwako
Nini siri ya mafanikio ya watu wanaofanikiwa?Je huwa wanashindaje changamoto ambazo wengine hushindwa?Kwani nini hushinda wakati wengine hushindwa?kwa nini hawazami wakati wengine huzama?
Jibu la maswali yote hayo ni rahisi sana, ni jinsi wanavyotazama tatizo,kwa mtazamo chanya…………….wanalitazama tatizo katika uhalisia wake,na wanaelewa kanuni sita za kutatua changamoto.Hizi ni kanuni sita ambazo ukizizingatia utalishinda tatizo na kuwa mshindi wa maisha yako mwenyewe

1. Every living human beings has problems. Tatizo ni nini? Je unatafuta ajira na hujapata?kama ukiwa na mtazamo hasi utafikiria kuwa kazi ni suluhisho la matatizo yako yote…yaani ukipata ajira utakuwa umemiliki Dunia na Ulimwengu wote.Ukweli ni kuwa walioajiriwa wana matatizo/changamoto pia.Waajiriwa wengi hulalamikia kuwa wanapaswa kuwahi kazini kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa(Baadhi ya Sekta ya Umma)hawana muda wa kufanya jambo lolote,hawa huishia kufanya kazi ili waishi..kazi ya ujira mdogo,They work to live rather than live to work.Matokeo yake hawa waajiriwa huwa hawafanyi kazi kwa weledi wala ubunifu
Je waastafu ndio ambao hawana changamoto? Hapana hata waliostaafu wana changamoto nyingi hasa baada ya kustaafu hutamani kurudi tena kazini,yaani anatamani aamke asubuhi akimbizane…maisha ya kustaafu nayo yana changamoto zake
Je waliofanikiwa?Kimsingi mafanikio ya kiuchumi hayaondoi changamoto,bali huzalisha changamoto mpya
Hakuna mtu wala binadamu ambaye hana changamoto za Maisha
Mwandishi anasema yeye alikuwa na ndoto ya kumiliki kanisa kubwa kabisa,lenye uwezo mkubwa,kwa hesabu zake aliona itamchukua miaka 40 kumiliki hilo kanisa lenye uwezo wa kukaa watu 6000 kwa mara moja.Akaanza kufanyia kazi ndoto yake,ndani ya miaka mitano tayari alikuwa na watu zaidi ya 6000 waumini wa kanisa lake.Anasema hii ilimfundisha kufanyia kazi ndoto yake kwa bidi,na ilimpa somo kuwa kadri unavofanikiwa ndio mahitaji yanaongezeka,alijikuta ana waumini wengi kuliko uwezo wake,na kuliko ndoto yake ya msingi,waumini walifika na kukosa maegesho hali iliyofanya aondoke hata kabla ya kushuka kwenye gari…….Mafanikio huvuta watu zaidi na hivo hitaji huongezeka……

Mfano unaweza ukaanzisha kampuni ya bidhaa fulani,soko likakuendea vizuri sana,ukapata mauzo makubwa,ukajikuta saa tisa mzigo umeisha sokoni,kule kuisha sokoni kutafanya uanze kutafuta njia ya kuongeza uzalishaji na masoko mapya.Hivo hakuna kilele cha mafanikio,kila mara utahitaji zaidi na zaidi
Maisha bila changamoto hayapo na sio maisha,kubali changamoto na songa mbele……………


2. Every problem has a limited life span.
Kila mlima una kilele chake,na kila bonde lina kina chake,ndivo maisha yalivo na mabonde na milima yake,hakuna atakayekaa juu daima,wala hakuna atakayekaa chini milele.Changamoto huisha,na kutoweka.Hakuna hali ya kudumu kwenye maisha,


3. Every problem holds positive possibilities.
Mwandishi ananukuu Bibilia takatifu Mithali 25-2 ambayo inasema Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo,.Kila changamoto huwa na mazuri yake,sio kila chanagmoto ni laana.Shilingi ina sehemu mbili,jambo ambalo ni changamoto kwako ni fursa ya kibiashara kwa mwingine,mfano ukiumwa Malaria ni changamoto kwako,ila kwa mmiliki wa hospital ni fursa ya kutengeneza hela.Kuna vitu kwenye maisha yetu vinalenga kutatua changamoto lakini lazima mtu apate shida,


4. Every problem will change you.
Changamoto huwa haikuachi vile imekukuta,lazima italeta mabadiliko chanya kwenye maisha yako,kuna funzo utapata la maisha.Unaweza ukafutwa kazi kwenye kampuni A ikawa ni njia yaw ewe kupata kazi nzuri zaidi kwenye kampuni B.Kuna nyakati unaweza ukaugua ukaenda hospital kumbe ni nia ya kumpata mwenza/mwenzi wa maisha yako!

5. You can choose what your problem will do to you.
Muda nyakati ngumu huja bila taarifa,lakini ni jukumu lako kushinda hizo nyakati ngumu na kuzibadili kuwa fursa kubwa kwako.Hakikisha hauwi mtumwa wa tatizo,hakuna changamoto yako au huna hakimiliki ya changamoto fulani wala nyakati fulani ngumu.Tambua nyakati na shinda nyakati


6. There is a negative and a positive reaction to every problem.
Watu wenye mafanikio na ambao wameshinda nyakati ngumu…hufanikiwa kutokana na namna wanavotazama nyakati na changamoto zake.Mtazamo hasi au chanya huamua namna ya ushindi! Swala namba moja kuelekea ushindi ni mtazamo chanya,ukweli ni kuwa sio jambo rahisi kama ilivokuandika,ni jambo gumu kuwa na mtazamo chanya kwenye nyakati ngumu na changamoto lukuki,ila lazima kufanya pamoja na ugumu wake!
Mwandishi anatoa mfano wa mtazamo hasi kuwa ni pale ambako umefutwa kazi,unaenda baa kulewa au kuvuta bangi kama sehemu ya suluhisho la changamoto yako!kimsingi hapa unaongeza ukubwa wa tatizo badala ya utatuzi!au wengine huamua kuiba ili kupata ada au matibabu,,utaishia jela kwa kosa la wizi.Mtazamo chanya ni mgumu ila muhimu,unaweza kuwa unadaiwa njia chanya ni kumfuata mdeni wako na kumweleza ukweli,kisha umwombe akupe muda wa kulipa kile unachodaiwa badala ya kukimbia kimbia na kuzima simu au kutopokea simu!

Mwandishi anasema kuna changamoto nyingine unaweza kushindwa kuzitatua ,pale ambako utatuzi umeshindikana angalau hakikisha kuwa una control tatizo..yaani wewe ndio unakuwa juu ya tatizo.Kuna kanuni kumi na mbili za kukabiliana na changamoto/nyakati ngumu


1. Don’t underestimate.
Usidharau wala kupuuzia tatizo,au chagamoto ya maisha,maana huanza kidogokidogo,hatimae huwa kubwa.Changamoto nyingi zimekuwa kubwa baada ya mwanzo kupuuziwa au kutofanyiwa kazi kwa usahihi,unawezakuta mzazi anasema mtoto wangu hafanyi vizuri darasani,lakini atajua tu mbeleni…au naumwa kichwa ila ni kawaida tu kwa kuwa sijanywa maji leo na jana……navuta sigara moja tu hivo siwezi kupata madhara kama wengine…………..matatizo hukua taratibu kama ujauzito…….

2. Don’t exaggerate.
Usikuze changamoto yako na kuifanya ya pekee Duniani.Au usifanye kuwa changamoto yako ndio imeleta balaa zote,na hivo kupata kitu cha kujifichia.Kuna watu huwa wakifiwa tu basi ndio sababu ya kila kitu……akifukuzwa kazi anafanya ndio wa kwanza kufutwa kazi…The one battle most people lose is the batter over the fear of failure… try… start… begin… and you’ll be assured you won the first round.

3. Don’t wait.
Ni kosa kubwa kukaa na kusubiri mambo yatokee…mambo hufanywa kutokea,hayatokei kwa bahati mbaya bali kwa mipango.Kama umefutwa kazi usije ukarudi nyumbani ukakaa kimya bila kuchukua hatua,Mwombe Mwenyenzi Mungu ,kisha chukua hatua….usije ukaketi kusubiria kuitwa kazini tu.Kusubiria muujiza bila kuchukua hatua stahiki kunaweza kupelekea tatizo kuzidi kukua na kuzaliana(Mwenyenzi Mungu ametupa akili ya kufikiri sawasawa na kuchukua hatua)

4. Don’t aggravate.
Usianze kurusha lawama kwa wengine,jamii,kampuni..ukaanza kusema kwa nini meneja amenifuta kazi mimi,huyu meneja yuko hivi ama vile…ukifanya hivo utakuwa unaongeza tatizo! Weka mtazamo chanya tu………

5. Illuminate.
Jiulize maswali kadhaa,je kuna mtu aliwahi kupata tatizo kama langu akalishinda?kuna mtu amewahi kupita kwenye nyakati ngumu kama hizi zangu akashinda?Je nimefukuzwa kazi au nimestaafishwa mapema?Je tatizo lako ni fedha kweli au ni matumizi mabaya ya fedha ulizo nazo hadi unafikiri hazitoshi?pengine unapaswa tu kubadili matumizi yako kisha utapata akiba,



6. Motivate.
Mtazamo chanya hupelekea suluhisho chanya,mfano kuna watu ambao ni walevi wa kupindukia,ulevi wake husababishwa na marafiki zake.Ukitaka kuacha ulevi sharti uachane na hao marafiki zako walevi……….ni swala la uamuzi sahihi kwa matokeo sahihi
Kuna wakati kwenye maisha unahitaji tu kufanya uamuzi sahihi ambao unatibu matatizo yako yote!

7. Bait.
Mwandishi anasema wakati mwingine unapswa kuwa kwenye sehemu sahihi kupata majibu sahihi,na matokeo tarajiwa,kuna watu kwenye maisha yao wapo sawa na mtu anayesubiria ndege itue baharini.Tambua sehemu sahihi ya kupata majawabu ya changamoto yako! Mfano unapenda kuvua sharti uende kwenye maji,mtoni,ziwani,baharini…huko ndio uvuvi hufanyika,pili unataka kuvua nini samaki gani,uende anakopatikana


8.Date.
Kama huna ajira na unahitaji kuajiriwa nenda katafute ajira kama mtu atafutavyo mchumba.Usijiwekee limit kuwa siku hizi hakuna ajira na zilizopo hadi uwe na fodfather wa kukushika mkono….Jiamini wewe ni godfather wa maisha yako,wewe ni shujaa wa maisha yako mwenyewe…usijikatishe tamaa ukitarajia kuna mtu atakuja kukutia moyo.Lazima utambue kuwa kila siku kuna mtu anastaafu au kuacha kazi hivo usikate tamaa

9. Sublimate.
Mlango mmoja ukifunga mingine inafunguka………..ifanye changamoto yako kuwa ngazi ya kupandia utukufu hadi utukufu


10. Now dedicate.
Watu wengi hushindwa sio kwa kukosa fursa,au kukosa akili au kipaji bali hushindwa kwa kuwa huwa hawashughuliki na tatizo husika bali dalili za tatizo.Ni lazima ushughulike na kiini…lazima uangalie mahali umejikwaa sio mahali umeangukia
Ukijitoa kwenye maisha ni ufunguo muhimu wa kufungua milango yako mingine…ukifanya kazi kokote fanya kwa bidi,na weledi utashangaa vile utafanya watu bora zaidi…unaweza kuwa muhudumu kwa mama ntilie ukamhudumia mteja kwa bidi na weledi kumbe huyu mteja ni mmiliki wa hotel ya nyota tano ukajikuta umepata ajira bila kuandika barua,bidi na weledi na kujitoa kwa moyo wote ni ufunguo tosha!



11. Communicate.
Usijimwambafai! Jifunze lugha bora ya mawasilano yenye mtazamo chanya.Mawasiliano ya kijamii ni moja ya njia bora za kutatua tatizo kwenye jamii.Kuwa mnyenyekevu wakati wote


12. Insulate.
Usijitenge wala kujificha ukiwa kwenye changamoto! Usianze kuwa kwenye mwonekano wa ovyo kwa kuwa tu una changamoto
 
Kitabu.Tough times never last,Tough people do!
Mwandishi.Robert Schurller
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Chapter 2: Here’s How You Can Be Tough Too!




1. Don’t surrender leadership to outside forces.
Mwandishi anasema Mungu anaweza kuchelewa kujibu maombi/dua yako lakini haimaanishi kuwa amekuacha.Muhimu kuwa na imani hadi mwisho.
Uongozi sio kukaa mbele,kuna watu wengi wanaketi viti vya mbele lakini wameshaachia uongozi kwa walio chini yao,au kwa presha za nje.Unawezakuta wewe ni Mwenyekiti wa Bodi lakini kuwa mwenyekiti bado ukaachia mamlaka kwa presha ya nje ya shirika lako!Usi sarende mamlaka yako! Jipe moyo mkuu,ili ufanikiwe futa neno HAIWEZEKANI(impossible) kwenye kamusi yako.
Kiatu huwa hakielekezi mguu jinsi ya mkuu kukua,wala mavazi hayawezi kutaka mwili ukue ili ufike size yake..Mwili ndio hutafuta vazi lilaloutosha,ndio maana kuna mavazi hata ya yule mama wa Mexico ambaye ndio mtu mnene kuliko wote Duniani
Usiwe mtumwa wa mali,majengo,fedha au vitu vya kupita…simamia ndoto yako!kumbuka ndoto yako ni kubwa kuliko kiwango chochote cha fedha
Kumbuka kanuni hii kuwa fedha hufuata mipango mizuri..mipango mizuri ndio mtaji mkubwa kuliko kiwango chochote cha fedha…hii ni kanuni ya asili,kanuni ya Kidunia
Wakati kampuni ya Coca cola inaanzishwa ilikuwa lazima uende kwenye center maalum kununua soda,kama ambavo hufuata maji bombani,yaani unafuata maji bombani/kisimani! Sasa akatokea jamaa mmoja akaona fursa kubwa,akaenda kuuza wazo la chupa kwa kampuni ya Cocacola kwa makubaliano kuwa yeye alipwe asilimia MOJA tu ya mauzo.Kampuni ilinunua hili wazo na kulifanyia kazi na bwana yule amekuwa Milionea kwa kuuza wazo!.Ukiwa na wazo usisite kuliuza kwenye kampuni au shirika
……………………Kuna watu wamekuwa mamilionea kwa kuuza wazo tu……………

2. Don’t surrender leadership to faces.
Watu wengi wameanguka kutokana na kutokana na kutaka kuwafurahisha watu wengine.Unahofu kuwa utakosolewa,una hofu na uamuzi wako,unajikuta unafanya uamuzi batili kwa kuangalia mtu/watu usoni badala ya kusimamia kile unachokiamini!usiache mbachao kwa msala upitao

3.Don’t surrender leadership to farces.
Kuna jamii ambazo hujiona Duni dhidi ya Jamii nyingine,mfano huko USA Negros au Wahindi au Wahispaniola hujiona jamii duni dhidi ya jamii ya Wazungu…huu ni uongo ni hali ya mgandamizo wa jamii ili itawale nyingine.Huku kwetu watu wa Kijijini hujiona duni dhidi ya watu wanaoishi mjini…na huko mijini Watu wa mikoani hujiona duni dhidi ya watu wa Dar,usiruhusu kamwe eneo la kijiografia liamue maisha yako na ndoto zako,usiruhusu mwonekano wako,wa rangi au kabila uamue hatma ya maisha yako

4. Don’t surrender leadership to fences.
Mwandishi anasema kuwa kuna watu wamejijengea ukuta wenyewe…yaani wamekuwa manabii wabaya wa maisha yao wenyewe,au unajiloga mwenyewe..mitazamo kama Mimi siwezi kabisa,hata baba yangu alishindwaga mimi ntawezea wapi! Huu ni ukuta tayari…umejiloga tayari
Mimi hili jambo siwezi,siwezi kumiliki kampuni kabisa..hakuna mtu aliwahi kumiliki kwenye ukoo wetu au kwenye kijiji chetu..umejijengea ukuta wako pekee yako…Mitazamo has huzaa matokeo hasi sina elimu,sina pesa,sina mtaji,mimi sio mtoto wa mtu mzito serikalini,ntaonewa tu na polisi

5.Don’t surrender leadership to frustrations.
Kuna nyakati watu wako wa maana wanaweza kukutenda,kuna nyakati zinaweza kuwa ngumu mno,biashara haziendi,hakuna wateja,umefutwa kazi,unadaiwa na mengine mengi.Kamwe usikubali hali ngumu zikuendeshe,simama imara ukijua neno moja la msingi Tough times never last…….

6.Don’t surrender leadership to your fantasies.
Pale ambako umepata wazo bora usiruhusu fikra hasi au hofu na mashaka !watu wengi hawasongi mbele kutokana na kujaa hofu mashaka na wasiwasi,unaanza kujiuliza je nikiwekeza kwenye mradi alafu nikafilisika itakuwaje? Ni lazima ujifunze kuchukua risk kubwa ili kupata mafanikio makubwa
Unakuwa na hofu ya kushindwa,je watu watanionaje…hivi mimi na usomi wangu nikalime kweli?Mimi na usomi wangu nifanye hii biashara je nikishindw?

7.Don’t surrender leadership to fears.
Maandiko matakatifu yanasema Mwenyenzi Mungu hakutupa roho ya hofu wala mashaka,bali roho ya nguvu na upendo(2 Timotheo.1.7)uwe na uhakika kuwa hofu sio kusudi la Mungu bali la mwovu shetani na lengo la shetani ni kuharibu
Ukijikuta kwenye hofu na mashaka unapaswa kujiponya,namna ya kujiponya ni kujaribu kufanya kitu kikubwa na kushindwa,kuliko kutofanya chochote na kufanikiwa,bora ujaribu kupanda mlima Kilimanjaro hata kama utarudia njiani kama ile tour iliyoongozwa na waziri wa utalii akiwa ana wasanii,wengi walirudia njiani ila walijaribu kuliko wewe ambaye hata kuwaza kujaribu hujawahi
Mshindwa aliyeshindwa akijaribu kufanya ni mshindi…………
Usiogope unaweza kuwa yule mtu ambaye ungependa kuwa,chukua hatua sasa haujachelewa.Jifunze spirit ya wanasiasa husema sijashindwa uchaguzi bali kura hazijatosha……………….


Failure doesn’t mean you are a failure… it does mean you haven’t succeeded yet. Failure doesn’t mean you have accomplished nothing… it does mean you have learned something. Failure doesn’t mean you have been a fool… it does mean you had a lot of faith. Failure doesn’t mean you’ve been disgraced … it does mean you were willing to try. Failure doesn’t mean you don’t have it… it does mean you have to do something in a different way. Failure doesn’t mean you are inferior… it does mean you are not perfect. Failure doesn’t mean you’ve wasted your life… it does mean you have a reason to start afresh. Failure doesn’t mean you should give up… it does mean you must try harder. Failure doesn’t mean you’ll never make it… it does mean it will take a little longer. Failure doesn’t mean God has abandoned you… ..it does mean God has a better idea!


8. Don’t surrender leadership to fatigue.
Mwandishi anasema kuwa wakati mwingine mwili huchoka,na akili huchoka pia,lakini kamwe usisikilize uchovu ukaacha uongozi.Endela kuwa kiongozi hata wakati ambako mwili na akili vimedhoofu,Rais wa USA Franklin Roosevelt alikuwa mgonjwa mwenye kuendeshwa na kiti cha wagonjwa wakati Japan inaivamia USA na kuua Wanajeshi wanaMaji zaidi ya 4000,licha ya ugonjwa wa Roosevelt alifanya uamuzi mgumu na muhimu kumaliza vita ya pili ya Dunia
Jipe likizo fupi kwa mwaka mara moja kuupa mwili na akili nguvu mpya

9. Don’t surrender leadership to faults.
Wakati mwingine unaweza kuwa na wazo zuri,ila ukakutana na kizingiti cha marafiki,ndugu au wafanyakazi wenzako,wakakosoa wazo lako kwa nguvu kubwa,ooohhh hili wazu litachukua mud asana…..au hili wazo halitekelezeki.Kumbuka kuna watu wameumbiwa kuona kasoro tu kwenye mawazo ya wengine,kazi yao ni kukosoa tu daima…usikate tamaa kumbuka wazo linaweza kupigwa polishi(msasa) likangaa.Ukiona mti porini huwezi kuamini kuwa unaweza kutoa mbao nzuri inayopendeza,mbao hupendeza baada ya kupitishwa mashine kisha hupigwa polishi,piga wazo lako polishi na sio kuliacha
Usifikiri kuwa ni makosa ya wazazi wako wewe kuw hivo ulivo,kuna watu hulaumu wazazi kwa maisha yao,usiruhusu changamoto kuwa excuse yako



10. Don’t surrender leadership to facts.
Usiwe mtumwa wa hali halisi,mfano tatizo la ukosefu wa ajira ni ukweli na ni hali halisi ya nchi,licha ya ukweli huu lakini kamwe usiupigie magoti Dr. Karl Menninger, mmoja wa magwiji wa Sayansi ya jamii aliwahi kusema kuwa “Attitude is more important that facts.” Attitude yako inapaswa kubakiwa kuwa chanya muda wote
Your attitude needs to remain positive and in the control position. Never let yourself be defeated by the facts.

11. Don’t surrender leadership to frenzies.
Wakati mambo ni magumu na yanaenda harijojo,usiharakishe kufanya jambo,tulia kwanza,utulivu wa akili ndio suluhisho

12. Don’t surrender leadership to the fates.
Usiendeshe maisha yako kwa kuzingatia NYOTA na utabiri.Kuna watu maisha yao yote yanaongozwa kwa imani za kishirikina au imani ambazo zina msingi wowote,mfano wa Nyota wale wanaonunua magazeti na kukata kile kipande chenye utabiri wa nyota!


13. Don’t surrender leadership to forecasts.
Kuna kauli kuwa maisha ni magumu,binafsi sijawahi kukutana na mtu aliyesema maisha yana afadhali au yataboreka hasa nchi za Dunia ya Tatu.Kila mara unaambiwa gharama za maisha zinapanda,mambo yanazidi kuwa magumu.Licha ya kauli hizi usiache zikaongoza maisha yako



14. Don’t surrender leadership to your friends.
Sio mara zote rafiki zako watakuunga mkono.Wakati mwingine wanaweza kuwa kikwazo kwako,hata mme/mke anaweza kuwa kikwazo cha ndoto zako.Muhimu kutengeneza mazingira ambayo hata kama watu wako wa karibu hawakubaliani na wewe lakini bado haiwi kikwazo kwa ndoto zako
Hapa panahitajika utengeneze mahusiano na kanuni ambazo utajuikana kwazo,ujenge utamaduni wa kusimamia kile ambacho unakiamini bila kuwa mtumwa.Mwandishi anasema yeye amejiwekea utaratibu na mke wake wa kutoa maksi kwenye jambo ambalo hawakubaliani,kuanzia moja jadi kumi…mwenzako akikataa kwa alama sita basi hapo inaweza kuwa mgogoro
Marafiki wanaweza kukushauri na kutoa mawazo/maoni yao lakini kamwe usiwaache wawe na uamuzi wa mwisho wa maisha yako
………..ishi wewe……….kuwa wewe……………

15. Don’t surrender leadership to the fracturing experiences of life.
Usikubali mabaya ya maisha yaongoze maisha yako,kuna mtu hapandi gari kwa kuwa tu aliwahi kupata ajali na gari…..au kuna mwanamke/mwanamme ambaye amechana na mwenzi/Mwenza na utamkuta anasema Kamwe sitomuamini tena Mwanamke/mwaname kwa yale aliyonitendea………
Amini kwenye ndoto…..kamwe usiamini kwenye maumivu……..usiwe mtumwa wa maumivu
 
Safi Sana Mkuu, ngoja nivae wiwani yangu kwanza.[emoji41]
 
Kitabu.Tough times never last,Tough people do!
Mwandishi.Robert Schurller
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Chapter 2: Here’s How You Can Be Tough Too!

Possibility Thinking

Mwandishi anasema kuna watu ambao hawajajifunza ku control fedha,wengine wanashindwa kwenda na muda,wengine hawawezi wala ku control wenyewe……sasa possibility thinking sio tu kuhusu fedha,nguvu,muda etc bali ni hali ya ku manage wazo chanya
Watu wengine sana wana tatizo kubwa la ku manage WAZO CHANYA kuliko tatizo la ku manage fedha,muda na viti vingine
Kila siku kuna makumi ya maelfu ya mawazo yanayozaliwa kila siku…nidhamu ya kuweza kutofautisha mawazo hasi dhidi ya mawazo chanya ndio nidhamu muhimu
Possibility thinker huchambua wazo kuona uwezakano ndani yake,hufanya huchambuzi wa kina,kisha kuchukua hatua kwenye utekelezaji…kisha mwombe Mungu ndoto/wazo liwe
Daima usidharau/usipuuze dhamani ya wazo hata kama linalonekana ni gumu kutekelezeka,dhamani yake ni kubwa sana,wazo ni kama maji yanayotiririka yanapaswa kuelekezwa kwenye sehemu sahihi ili yalete matokeo chanya
Never reject an idea because it’s impossible! Mara nyingi wazo/ndoto huenekana haitekelezeki pale linapozaliwa,au mwanzo kabisa,ni lazima ugeuze fikra hasi kuwa chanya kwa kuona fursa kwenye kila gumu…….jambo la msingi ni kuhakikisha kuwa wazo/ndoto ni chanya na lina manufaa au kwako,Taifa au kwa kampuni/shirika ukishajiridhisha basi songambele,tengeneza njia pasipo na njia
…..Kumbuka kuna jambo ambalo leo haliwezekani lakini litawezekana kesho………
Kuna mambo ambayo kisheria leo ni haramu lakini kesho sheria inaweza kubadilika ikahalalisha,hivo basi usiache kuwaza,usiache wazo/ndoto kwa kuwa tu ni kinyume cha sheria,sheria hubadilika.
Mwandishi anasema kuwa utekelezaji wa ndoto/wazo hutegemeana sana na nguvu ya ubongo na imani kuliko fedha na msuli,hivo hata kama hauna fedha usiache ndoto yako…..ukiwa na ndoto/wazo lazima kutakuwa na mgogoro au changamoto lakini jifunze namna sahihi ya kukabili changamoto husika,ikiwepo sera sahihi na mipango sahihi,wakati mwingine kuweka silaha chini sio kujisalimisha ni akili ili ujipange upya
Singapore inaagiza 100% ya mafuta lakini uzalishaji wa bidhaa zake ni mkubwa,na inashindana na nchi kubwa kama USA na Ujerumani katika kuuza bidhaa nje,Wasingapore wamefanikiwa kwa kuwa wamefundishwa kuchukua risk kubwa na pia wamefundishwa somo la possibility thinking…..kwao kila kitu ni fursa
Only successful people can help people who are failing. Only winners will survive to give food to the hungry.


7 Count to Ten and Win!
Kuna kanuni ya maisha ya kushinda changamoto za maisha,msingi wa kanuni hii unasema …Unaweza kuwa mtu/binadamu unayetaka kuwa,uamuzi ni wako binafsi,uchaguzi ni wako
Mwandishi anasema ukitaka kushinda sharti uanze (You won’t win if you don’t begin!)Jipangie kuvunja rekodi yako mwenyewe,ukiwa na mtazamo wa kuvunja rekodi huwa huu mtazamo unaongeza hamasa kwenye ubongo na kuondoa hofu
Rule number one: Begin by believing that you possess latent gifts of creativity. You will respect, trust, and admire your own thoughts. Every person can be creative.

Rule number two: Don’t play it alone. Play it with problem-solving people. Play it with possibility-thinking people. Play it with people who have a record of achievement and success. You can play it alone. But a lot of ideas might come from others.
Je umejaribu kuamini na bado unaona ugumu mbele yako?je hauoni mwanga kwenye maisha yako?Imani huwa haimwangushi mtu,mtu huanguka kutokana na kuiangusha imani.
Mwandishi anatukumbusha kuwa Imani ni kama mbegu,lazima ipandwe,kuipanda pekee haitoshi,lazima kuipanda kwenye udongo mzuri,ipate maji ya kutosha,ipate mwanga wa jua,ilindwe ndio mwisho hutoa matokeo tarajiwa!na mbegu huvunwa katika nyakati na majira sahihi.Usipovuna kwa wakati upepo au kitu kingine kinaweza kuifanya ikadondokea sehemu isiyo sahihi!Kuna watu ambao ndoto/mawazo yao huishia hewani kama mbegu ambayo ahikupandwa sehemu mwafaka,wengine hufanana na mbegu ambayo haikupata udongo wala maji ikakauka,wengine huwa kama mbegu iliyoota vizuri ila haikuvunwa kwa wakati mwafaka hivo ikapeperushwa na upepo

…………………kila mtu ni mbunifu……………………………

I’ll make the most of today. There will never be another me—I’ll make the most of myself.

Don’t trust the clouds—trust the sunshine. Don’t set your compass by the flash of lightning—set it by the stars. Trust the sun—don’t trust the shadows. Believe in your dreams—don’t believe in your despairing thoughts. Have faith in your faith—and doubt your doubts. Trust in your hopes—never trust in your hurts.
 
Back
Top Bottom