UCHAMBUZI: Ikulu kujiingiza katika kesi ya Msigwa ni matokeo kukosa maarifa?

UCHAMBUZI: Ikulu kujiingiza katika kesi ya Msigwa ni matokeo kukosa maarifa?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
12,151
Reaction score
44,071
Kituko kipya cha karne katika siasa za Tanzania kimeibuka leo, baada ya Ikulu ya Tanzania kuitangazia dunia kuwa, Rais wa nchi amelipa kiasi cha shilingi milioni 38 ili kumlipia faini Mchungaji Peter Msigwa ambaye ni mfungwa wa kisiasa aliyetiwa hatiani kwa makosa ya jinai.

Sina uhakika kama Ikulu ilikuwa inajua kuwa kitendo ilichokifanya leo kilikuwa ni cha kitoto, kijinga na kituko mbele ya macho ya dunia na watanzania wengi.

Sababu za msingi kabisa ni hizi hapa.

1/Mchungaji Msigwa alishtakiwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inaongozwa na Rais wa Tanzania.
(Kwa maneno rahisi kimantiki ni kuwa Rais wa Tanzania alikuwa anamshtaki raia anayeishi Tanzania).

Sasa nini mantiki ya Jamhuri (Raisi) kumshtaki raia ili afungwe na kisha hapo hapo kuja kumlipia faini ili aachiwe huru?

Kwanini Jamhuri ipoteze muda, nguvu kazi ya mawakili wake, mshtakiwa na mahakama katika kuiendesha kesi hiyo kwa zaidi ya miaka 2 mfululizo wakati ikijua fika ilikuwa haina nia ya kumfunga Msigwa gerezani?

2/Rais wa Tanzania kikatiba anayo mamlaka ya kumwachia huru wakati wowote, mfungwa yoyote kutoka kifungoni.
Kwanini Rais akimbilie kumlipia pesa Msigwa badala ya kuamuru aachiliwe huru tu?

3/Mchungaji Msigwa alikuwa akitetewa na mawakili wake kutoka CHADEMA wakati wote wa kesi, na mara baada ya kutiwa hatiani, mawakili hao hao ndio waliweka utaratibu wa namna ya kukusanya pesa kupitia CHADEMA ili mchungaji Msigwa aweze kuachiliwa huru.
Kipi kimewafanya watendaji wa Ikulu kuibuka sasa kumpigania Msigwa baada ya kufungwa gerezani na sio wakati wote wa kuendeshwa kesi dhidi yake?

Nini kimeifanya Ikulu kuukwepa huo utaratibu wa Mawakili wake katika kulipa faini?

Nani kawatuma Ikulu kwenda kujipendekeza kwa Msigwa nje ya utaratibu wa wanasheria wa Msigwa?

Nini kitatokea ikiwa Msigwa atakuja hadharani kuwakana Ikulu?

4/Watanzania wengi wanajua na kuamini kuwa kesi yote hii iliyomtia hatiani Msigwa na wenzake ina mkono wa serikali, vyombo vya dola na CCM.
Sasa hii janja janja ya Ikulu kumlipia faini Msigwa ina lengo gani?
Kulikuwa na ulazima gani kwa Ikulu kuja kujikocha hadharani kwa mtindo wa namna hiyo?

5/Katika mazingira ambayo CHADEMA inarindima katika miamala ya fedha ya kona zote za nchi ili kuchangishana pesa za kuwatoa viongozi wao wote (pamoja na Mashinji ambaye amehama CHADEMA).

Nini mantiki ya Ikulu na CCM ghafla kuibuka na kudai na wao wamechanga pesa ili kuwatoa kifungoni baadhi ya viongozi hao?

Je, Ikulu imeamua kuiga utaratibu wa CHADEMA?

Je, Ikulu ina hofu au wivu kwa huo utaratibu wa CHADEMA?
 
Kitengo cha Propaganda Lumumba kimepwaya sana!Ukiangalia hata yule ndugu yake Peter Msigwa,alikuwa ni kama anaelekezwa cha kusema na Gerson Msigwa!Yaani alikuwa analishwa maneno!Picha limechezwa kwa kiwango cha Bongo movie aisee,wapikaji wamefeli big time!
 
M/Mwenyekiti wa chademaTundu Lissu ameziomba jumuiya za kimataifa kuiwekea vikwazo vya kiuchumi,misaada ya kifedha,,na kuinyima ushirikiano wa wa kidiplomasia, kuitenga Tanzania kwa kile alichodai kuhusika na ukandamizwaji wapinzani wa Rais Magufuli,kudorora haki za binadamu

1584049059601.png


Sababu kubwa ni hii
 
Mtazamo wako

Unaweza kuwa wa kisomi sana

Ila alichofanya JPM amekuwa man of the match kwa raia wengi sana
Kama ni mtu alimshauri afanye uamuzi aliofanya basi namshauri rais wangu asikae apokee tena ushauri kutoka kwa huyo mtu.

Eti man of the match kwa raia wengi,wapi hao? Labda kama unatania au unafanya kejeli.
 
Mtazamo wako

Unaweza kuwa wa kisomi sana

Ila alichofanya JPM amekuwa man of the match kwa raia wengi sana
Nani kabisha hilo? Nani kakataa kuwa miongoni mwa RAIA wapo walio na uwezo mdogo kiasi cha kudanganyika na propaganda mufilisi tuu?
Kama mtu alivutiwa na upigaji push ups tuu atashindwa kuvutiwa na uongo huu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtazamo wako

Unaweza kuwa wa kisomi sana

Ila alichofanya JPM amekuwa man of the match kwa raia wengi sana
Hata Amber Ruti na Gwajma walishawahi kuwa woman and man of the match kwa zile video chafu.

Mantiki ni kuwa, Ikulu ya Tz kama taasisi hawakupaswa kujiingiza kwenye mambo ya vituko, utoto na ujinga ili kumpa credit Rais. Ni mambo ya aibu kubwa kutafuta public attention kwa upuuzi.
 
Kituko kipya cha karne katika siasa za Tanzania kimeibuka leo, baada ya Ikulu ya Tanzania kuitangazia dunia kuwa, Rais wa nchi amelipa kiasi cha shilingi milioni 38 ili kumlipia faini Mchungaji Peter Msigwa ambaye ni mfungwa wa kisiasa aliyetiwa hatiani kwa makosa ya jinai.

Sina uhakika kama Ikulu ilikuwa inajua kuwa kitendo ilichokifanya leo kilikuwa ni cha kitoto, kijinga na kituko mbele ya macho ya dunia na watanzania wengi.

Sababu za msingi kabisa ni hizi hapa.

1/Mchungaji Msigwa alishtakiwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inaongozwa na Rais wa Tanzania.
(Kwa maneno rahisi kimantiki ni kuwa Rais wa Tanzania alikuwa anamshtaki raia anayeishi Tanzania).

Sasa nini mantiki ya Jamhuri (Raisi) kumshtaki raia ili afungwe na kisha hapo hapo kuja kumlipia faini ili aachiwe huru?

Kwanini Jamhuri ipoteze muda, nguvu kazi ya mawakili wake, mshtakiwa na mahakama katika kuiendesha kesi hiyo kwa zaidi ya miaka 2 mfululizo wakati ikijua fika ilikuwa haina nia ya kumfunga Msigwa gerezani?

2/Rais wa Tanzania kikatiba anayo mamlaka ya kumwachia huru wakati wowote, mfungwa yoyote kutoka kifungoni.
Kwanini Rais akimbilie kumlipia pesa Msigwa badala ya kuamuru aachiliwe huru tu?

3/Mchungaji Msigwa alikuwa akitetewa na mawakili wake kutoka CHADEMA wakati wote wa kesi, na mara baada ya kutiwa hatiani, mawakili hao hao ndio waliweka utaratibu wa namna ya kukusanya pesa kupitia CHADEMA ili mchungaji Msigwa aweze kuachiliwa huru.
Kipi kimewafanya watendaji wa Ikulu kuibuka sasa kumpigania Msigwa baada ya kufungwa gerezani na sio wakati wote wa kuendeshwa kesi dhidi yake?

Nini kimeifanya Ikulu kuukwepa huo utaratibu wa Mawakili wake katika kulipa faini?

Nani kawatuma Ikulu kwenda kujipendekeza kwa Msigwa nje ya utaratibu wa wanasheria wa Msigwa?

Nini kitatokea ikiwa Msigwa atakuja hadharani kuwakana Ikulu?

4/Watanzania wengi wanajua na kuamini kuwa kesi yote hii iliyomtia hatiani Msigwa na wenzake ina mkono wa serikali, vyombo vya dola na CCM.
Sasa hii janja janja ya Ikulu kumlipia faini Msigwa ina lengo gani?
Kulikuwa na ulazima gani kwa Ikulu kuja kujikocha hadharani kwa mtindo wa namna hiyo?

5/Katika mazingira ambayo CHADEMA inarindima katika miamala ya fedha ya kona zote za nchi ili kuchangishana pesa za kuwatoa viongozi wao wote (pamoja na Mashinji ambaye amehama CHADEMA).
Nini mantiki ya Ikulu na CCM ghafla kuibuka na kudai na wao wamechanga pesa ili kuwatoa kifungoni baadhi ya viongozi hao?
Je, Ikulu imeamua kuiga utaratibu wa CHADEMA?
Je, Ikulu ina hofu au wivu kwa huo utaratibu wa CHADEMA?
Mpaka October ikulu itajidhalilisha Kwa mengi yanayokuja

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwamba ninyi mnajua zaidi kuliko kundi lote la wataakamu lililoko Ikulu?

Kwamba Oktoba 2020 Upinzani utaingia Ikulu kiulaini. Lakini kwa mwendo huu wa kushabikia matukio kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ni kujifurahisha tu kupunguza shinikizo la damu.

Busara na hekima itawale upinzanu upate agenda za kuwashawishi wapiga kura kampeni zitakapoanza.
 
Achana na huyo mgonjwa wa post brain head injury syndrome. Ni mgonjwa bado. Ubongo wake uliathirika sana baada ya lile shambulio. Wazungu wake wanalijua hilo. Anaendelea na rehabilitation ya ubongo wake. Tuendelee tu kumuombea kwa Mwenyezi Mungu.
Isitoshe Ulaya na Marekani wanahangaishwa na virusi vya CORONA kushughulika na mtu asiyejiheshimu.
 
Back
Top Bottom