GE2020 Uchaguzi wa mwaka 2020 na maajabu yake

GE2020 Uchaguzi wa mwaka 2020 na maajabu yake

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
21,204
Reaction score
37,555
Heshima sana wanajamvi,

Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 kilikuwa Arumeru kata ya Bangata.
Nakumbuka asubuhi ya saa 2:35 nilikijongelea kituo cha kupiga kura Shule ya Msingi.Nikaanza kutafuta orodha ya majina ambayo yalikuwa yameorodheshwa kwa kufuata alphabet baada ya kuliona jina langu naingia katika darasa lililo na jina langu.

Napatiwa karatasi za kupiga kura ya Diwani,Mbunge na Rais. naelekea katika kibanda cha box kwaajili ya kupiga kura baada ya kumaliza naoelekezwa sanduku la Rais,Mbunge na Diwani naanza zoezi la kudumbuza kura mabox yote yamejaa inabidi nitumie kalamu kusukumiza kura zangu nawauliza wasimamizi mbona mabox yameshajaa na wapiga kura siwaoni wananitazama huku wanatabasamu na wengi kuachia vicheko vya kugugumia.

Sasa naanza kumwelewa Polepole.

Sasa naanza kuwaelewa wasimamizi wa uchaguzi kwanini walikuwa wanajizungusha kutoa barua za mawakala wa vyama vya upinzani.

Sasa naanza kuelewa kwanini Wakurugenzi wa uchaguzi level ya Wilaya ni wezi lakini hawashitakiwa na wakishitakiwa na kufungwa wanatolewa na mamlaka za uteuzi (Rejea DED wa Arusha City Mr Pima alifungwa kwa wizi lakini leo ni mkurugenzi baada ya kufutiwa mashtaka kwasababu mamlaka za utezi hazikutoa kibali cha kushtakiwa).

Sasa naanza kuelewa kwanini Mahakama ilikataza wananchi wakae mbali na vituo vya kupiga kura.Eti ukipiga kura unatakiwa kuondoka mara moja.

Sasa naanza kuelewa kwanini Lissu anashtakiwa na Serekali kwa mashtaka ya uongo (Mchongo) na mahakama kutumika vibaya.

Ngongo nimekaa paleee nawatazama makada wanavyohangaika kuficha ukweli.
 
Ulienda muda gani kupiga kura? Zoezi la sekunde 30 umemaliza unataka kuona msururu mrefu wa nini?
 
Heshima sana wanajamvi,

Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 kilikuwa Arumeru kata ya Bangata.
Nakumbuka asubuhi ya saa 2:35 nilikijongelea kituo cha kupiga kura Shule ya Msingi.Nikaanza kutafuta orodha ya majina ambayo yalikuwa yameorodheshwa kwa kufuata alphabet baada ya kuliona jina langu naingia katika darasa lililo na jina langu.

Napatiwa karatasi za kupiga kura ya Diwani,Mbunge na Rais. naelekea katika kibanda cha box kwaajili ya kupiga kura baada ya kumaliza naoelekezwa sanduku la Rais,Mbunge na Diwani naanza zoezi la kudumbuza kura mabox yote yamejaa inabidi nitumie kalamu kusukumiza kura zangu nawauliza wasimamizi mbona mabox yameshajaa na wapiga kura siwaoni wananitazama huku wanatabasamu na wengi kuachia vicheko vya kugugumia.

Sasa naanza kumwelewa Polepole.

Sasa naanza kuwaelewa wasimamizi wa uchaguzi kwanini walikuwa wanajizungusha kutoa barua za mawakala wa vyama vya upinzani.

Sasa naanza kuelewa kwanini Wakurugenzi wa uchaguzi level ya Wilaya ni wezi lakini hawashitakiwa na wakishitakiwa na kufungwa wanatolewa na mamlaka za uteuzi (Rejea DED wa Arusha City Mr Pima alifungwa kwa wizi lakini leo ni mkurugenzi baada ya kufutiwa mashtaka kwasababu mamlaka za utezi hazikutoa kibali cha kushtakiwa).

Sasa naanza kuelewa kwanini Mahakama ilikataza wananchi wakae mbali na vituo vya kupiga kura.Eti ukipiga kura unatakiwa kuondoka mara moja.

Sasa naanza kuelewa kwanini Lissu anashtakiwa na Serekali kwa mashtaka ya uongo (Mchongo) na mahakama kutumika vibaya.

Ngongo nimekaa paleee nawatazama makada wanavyohangaika kuficha ukweli.
IMG-20250822-WA0006.jpg
 
Ulienda muda gani kupiga kura? Zoezi la sekunde 30 umemaliza unataka kuona msururu mrefu wa nini?

Swali zuri ingawa limeulizwa na mtu mjinga.

Nimekuambia nilikwenda kupiga kura 2:35.hapakuwa na msururu wa wapiga kura.
Vyumba (madarasa) vya kupiga kura vilikuwa kama kumi hivi hapakuwa na foleni hata kidogo zaidi ya kuwaona mtu mmoja mmoja.

Kumbuka muda wa kufungua vituo ni saa 2:00 asubuhi,mimi nilikwenda kupiga kura dakika 35 baada ya vituo kufunguliwa lakini masanduku tayari yalikuwa yamejaa.

Kwa lugha rahisi uchaguzi ulishamalizika kabla vituo havijafunguliwa.
 
Ofisi za ccm pale mkwajuni Dar es Salaam.kura zilipigwa siku mbili yaani ijumaa kabla ya siku ya kupigia kura.
Waliwakusanya vijana mitaani na kuwahidi 5000/= kila mmoja na hawakuwapa.
Waliwapa WALI MAHARAGWE.
Nilikuwepo nikajionea mwenyewe
 
Back
Top Bottom