Uchaguzi ni wa nini basi?

Uchaguzi ni wa nini basi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,092
Reaction score
43,265
Katika nchi ya kidemokrasia uchaguzi unafanyika kwa sababu mbili kubwa.

Kwanza, ni kwa ajili ya wananchi kupima na kutoa hukumu juu ya yale yaliyofanywa katika kipindi kilichopita. Wale wanaomaliza muda wao waliingia na ahadi kadha wa kadha. Je, wametimiza ahadi hizo kwa kiasi gani? Je, wapewe muda mwingine wa kumalizia zile ambazo hazikutimizwa? Je, wanastahili Kuelewa nafasi nyingine?

Hivyo, wananchi wanapewa nafasi ya kufanya uamuzi juu ya uongozi na utawala wa maeneo yao. Endapo wananchi wanakubali na kuridhishwa na kilichofanywa basi watawarudisha viongozi waliopita. Na kama ni la, basi watawaingiza madarakani viongozi wengine.

Sababu ya pili ya kufanya uchaguzi katika nchi ya kidemokrasia inatokana na sababu ya kwanza. Nayo ni kutoa hukumu ya kisiasa juu ya chama tawala. Chama kilichopo madarakani kinaweza kudhania kuwa kinastahili kuwepo madarakani. Hata hivyo ni wananchi ndio wanatakiwa kutoa hukumu hiyo kila baada ya muda fulani, kwa Tanzania ni kila baada ya miaka mitano, kwa Marekani ni kila baada ya miaka minne kwa Urais, miaka miwili kwa wawakilishi na sita kwa maseneta.

Lengo la hili la pili ni kutoa nafasi kwa chama kingine kuja na mwelekeo tofauti na ule wa chama tawala na kuwapa wananchi viongozi wapya nje ya wale wanaomaliza muda wao kutoka chama tawala.

Katika kuhakikisha sababu hizi mbili zinafanikiwa, nchi zenye demokrasia iliyokomaa zimefanya mambo makubwa kadhaa:

1. Kutengeneza na kusimika mfumo wa uchaguzi unaoweka uwezekano wa aliyeko madarakani (incumbent) kushindwa. Mfumo, unahakikisha aliyeko madarakani anaweza kushinda au kushindwa bila dhulma, hadaa, au matumizi ya njia za mkato.

2. Walioko madarakani hawaogopi au kuhofia wapinzani wao walio nje. Kama wanaongoza vizuri na wanatimiza ilani yao, hawahitaji virungu au vurugu kujitangaza. Kazi zao zinajionesha na mafanikio yao yanajipigia panda yenyewe.

3. Ili kuhakikisha kila mtu yuko sawa, nauli zozote au maagizo yoyote yenye kuashiria kutokujiamini au yenye kutaka kuvuruga mfumo wa uchaguzi yatapingwa na kukataliwa. Ukimpa mtu nafasi ya kuchagua vitu vitatu halafu ukamwekea bastola kichwani na kumwambia achague cha kwanza basi kinachofanyika siyo uchaguzi bali uchafuzi wa kidemokrasia! Hakuna uchaguzi mbele ya shurti! Huwezi kuwa huru kuchagua kama familia, mtaa, jamii yako inashikiliwa mateka.

Ni kwa sababu hiyo naamini ukuu wa dhamira na ukweli (the supremacy of conscience and truth) unamtaka mtu kuamua kama anaitaka kushiriki katika uchaguzi au uchafuzi wa kidemokrasia. He, mtu ajiandikishe kupigika kura wakati chama chake hakiko huru kufanya shughuli same za kisiasa? Je, ashikiri huku akijua wasimamizi wamekatazwa kumtangaza mshindi kama akiwa wa chama chá upinzani? Je, ashiriki uchaguzi huku akijua muda yake haitahesabiwa?

Basi katika nchi ya kidemokrasia Ni muhimu sana kuhakikisha kuwa kinachofanyika ni uchaguzi na siyo uchafuzi, na mfumo ni wa demokrasia na siyo demoghasia na kuwa mwisho wa siku watawala hawageuki kuwa watuwala.
 
Baada ya kupata kitambulisho cha Taifa, cha uchaguzi nilikitupa chooni. Matumizi yake halisi yamebadilishwa na Amri za Watuwala.....
Kwa bongoland uchaguzi wa haki bado sana. Kiukweli sioni haja ya kujiandikisha zaidi ya kupata kitambulisho kwa ajili ya shughuli zenye kuhitaji uwepo wa kitambulisho, ila si kwa kupiga kura.
 
Hatari itakuja pale ambapo haki haipatikani katika sanduku la kura, Hivyo Watu wakaamua kutafuta Viongozi kwa njia mbadala,

Lissu amewahi kusema hakuna Kiongozi ambaye ametufudisha thamani ya Utu Kama huyu..

Uchaguzi wa Wabunge waliyounga juhudi ulishatoa picha.. Hata kupoteza Maisha kwa Mwanafunzi Akwilina hakukupewa uzito zaidi ya kunyanyasa Viongozi wa CDM,

Hivi sasa hakuna uchaguzi ni bora liende tu.
 
Wakati wengine walikuwa wanalia na kutokubaliana na mfumo mzima wa uchaguzi pamoja na hitaji kuu la uwepo wa tume huru ya uchaguzi mlijitaidi kukosoa kweli na kujinadi kwamba walikuwa wanalialia ..
Wakilalamika polisi kutumika kimabavu kupendelea chama kimoja mliziba masikio kabisa...
Wqnanchi wamekata tamaa. .wanaona hawana haja ya kupiga kura isiyo na thamani

Yet siku ya kupiga kura uwezekano wa risasi kupotea njia upo..
Watu wapo majumbani jichagueni nyie wenyewe na mjitangaze. .
RIP Akwilina.
 
Haya yanayoendelea kwenye kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi, yamedhihirisha pasi na shaka kile tunachosema kila siku rais na chama chake hawakubaliki, bali hutisha watu ili waonekane wanakubalika.

Haiwezekani useme unakubalika, siasa ufanye mwenyewe ww na chama chako, hujuma ufanyie wapinzani wako, kisha siku ya ukweli wa hiyo hadithi kuwa unakubalika watu hawatokei kupiga kura.

Hii inathibitisha wananchi wana uelewa wa kupima mambo, na wanafahamu fika uhuru na demokrasia yao hauporwi kwa sababu ya uwepo wa vitu.
 
Mzee Mwanakijiji; imebidi niangalie lini uli-post huu uzi. Wewe wa sasa umekuwa tofauti na wewe wa zamani.

Haya; hebu tuambie, kipi kimekusibu hata akili yako ya zamani ikakurudia? Having said that; nakubaliana nawe kwa hiki ulichokiandika. Na ndio maana sitapoteza muda wangu kujiandikisha.
 
Back
Top Bottom