Appriciator na Watanzania,
Nimefuatilia mjadala kwa ujumla. Kwa manufaa ya wengi naomba nitoe taarifa ifuatayo:
1. Awali narudia kauli niliyotoa na imetolewa Mara nyingi na viongozi wa Chadema kuwa ndani ya Chadema hakuna mwenye hati miliki ya Chama, na hivyo maamuzi ya Chadema, kwa mambo yanayohusu chama au nje ya Chama hufanywa kufuata Katiba ya Chama, Kanuni ya Chama na au maazimio ya vikao vya maamuzi yaani Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu.
2. Tumekwishasema kutangaza Mara kadhaa kwenye Press Conference mbalimbali baada ya vikao hivyo, kuwa Chadema imeamua kutekeleza sera yake ya Kanda/Majimbo ndani ya Chama wakati inajiandaa kutekeleza sera hiyo katika muundo wa utawala wa Taifa letu wakati utakapofika. kanda 8 za Bara zimekwisha kuundwa, na Kanda 2 za Zanzibar zinasubiri kuundwa baada ya kujua mwelekeo wa Katiba Mpya. chaguzi za viongozi wa Kanda zilikamilika mwezi Augusti, 2013. Uundwaji huo wa Kanda ambao ulisimamiwa katika Kanda zote na Mhe. Freeman Mbowe ulisimamiwa na Freeman Mbowe(MP), Mwenyekiti wa Chama na uchaguzi wa Viongozi wa kisiasa umefanyika katika ngazi zote. Hatua inayoendelea kukamilika sasa ni uteuzi wa viongozi watendaji yaani Mratibu wa Kanda na Afisa wa Kanda na viongozi wasaidizi. Nafasi hizo zote zimetangazwa kwenye vyombo vya habari na kwenye maeneo yote ya Kanda husika. Ofisi ya Katibu Mkuu imekwisha kuletewa mapendekezo mbalimbali kwa uteuzi wa mwisho, na kazi hii inategemewa kukamilika kufuatana na speed ya kila kanda kukamilisha taratibu zilizo chini ya mamlaka yake.
3. Nilikwisha kutangaza Mara kadhaa, lakini nafafanua ten a kwa manufaa ya watanzania wengi wanaoweza kukwazwa na upotoshwaji unaoendelea.
a) Tulipanga kutoa mafunzo ya kina kuanzia ngazi ya Taifa, Kanda, majimbo na Kata kwa viongozi wetu wapatao 36,000 watakaokuwa injini ya kujenga na kuimarisha mtandao wa chama kwa nchi nzima. Nilitoa Taarifa kuwa kaxini ya wakufunzi hao ni kuunda timu za kufungua misingi ya Chadema ( kwa ccm ni Mashina) ipatayo 250,000 nchi nzima yaani kuwa na msingi wa Chadema kwa kila shina la ccm. Aidha baada ya kutoka kwenye misingi watafanya kazi hiyo pia kuunda na au kuimarisha pale ambapo tayari kuna matawi. Lengo ni kuwa na matawi 18,000 kwa nchi nzima. Yaani kuwa na tawi kila palipo na tawi la ccm, ili tubanane huko huko vijijini. Kazi ya mafunzo ikifanyika kwa ufanisi, na sasa kazi iliyoko ni kufungua misingi na matawi, kaki ambayo kwa formation iliyoko inategemewa kukamilika mwezi wa October. Ni kweli kazi hii imechelewa kwa mwezi mmoja kutokana na mwingiliano wa shughuli mathalan uchaguzi mdogo wa madiwani, zoezi la ukusanyaji wa maoni ya Katiba, mambo ambayo chadema hatuna mamlaka ya ratiba yake.
C) Baada ya kuunda misingi na matawi uundaji na uchaguzi katika ngazi ya kata, majimbo wilaya hadi Taifa itafuata, na ngazi hizo hazina kazi kubwa Kama ngazi ya msingi na matawi kwa vile zina idadi kubwa, lakini pia indigo walk wanachama. Ngazi ya kata kwenda juu ni ngazi za uongozi tu, na wanaohusika kwenye ngazi hizo ni viongozi hivyo kaki inakuwa rahisi zaidi.
Hivyo, watanzania muelewe kuwa Chadema ni chama makini, inafanya kaki zake kisayansi siyo kwa propaganda. Huwezi kuzungumzia uchaguzi bila kufanya kazi ya kujenga chama. Wengi hawajui uzito wa kazi hiyo, kumbukeni Mwl. Nyerere Aliwahi kujiuzulu ili avenge mtandao wa Tanu. Ndipo baada ya kukamilisha kaki hiyo akarudi kuwa Raisi wa kwanza wa Jamhuri ya Tanganyika. Uchaguzi unafanyika baada ya kuwa na chama imara. Ndiyo kazi inayofanyika, na ninawapongeza wale makamanda wote wanaofanya kaki hiyo katika mazingira magumu sana. Nina hakika wote hao wataingia katika historia ya ukombozi wa pili wa Taifa letu.
Ni Imani yangu kuwa baada ya ufafanuzi huu watakaopenda kubishana na kufanya propaganda ni juu Yao. Mwenye kutaka kupokea elimu hii naomba aeleze na kwa wengine pia ili kuwasaidia. Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Chadema.
Ni jambo la kujiuliza mkuu iwapo kila siku tunapiga kelele
juu ya katiba na demokrasia kisha kwenye vyama hatufanyi uchaguzi tunaonyesha picha gani kwa wananchi? kama kweli tunataka kuonyesha njia ni vizuri uchaguzi ukafanyika.