Unaambiwa kinyang'anyiro cha uchanguzi wa mwaka huu ni Mama Samia vs Salum Mwalim vs Mpina..
Uchaguzi wa mwaka huu ni zaidi ya futuhi ni zaidi ya cheka tu ni zaidi ya sinema zetu kusema kweli ni vichekesho + comedy...nchi hii inadidimia na bado kuna nyumbu na vyura wa kijani unawasikia wakisema octoba tunatiki
Itoshe kusema tu kua njaa mbaya!!
Toa maoni yako
Nimemaliza kumsikiliza pole pole naona taifa linaandaliwa vema kisaikolojia kujisimamia mwaka huu.
Nukuu za Pole pole.
1/ Mama ukichukua form na kugombea Urais utakuwa umetutukana watanzania wote.
2/Mama unataka kugombea na Salum Mwalimu wa chauma, Mama unataka kugombea na Mpina wa Act. Kweli mama unataka kugombea na hawa na moyo wako una amani kabisa?
3/ Kwani Act sisi ccm hatuijuhi? Pole pole anatufumbua macho na kututhibitishia jambo hapa kuhusu Act.
4/ Pole Pole anashauri mama amuachie Mh Lissu bila masharti aende kwenye familia yake. Kisha aitishe muafaka wa kitaifa kabla ya kuingia kwenye uchaguzi. Amesema vyombo vya dola vitajipanga kutokana na maamuzi ya wananchi ambao ndio wenye nchi. Hapa maana yake tume isituambie muda umekwisha. Kila jambo linawezekana waamuzi wa mwisho ni wananchi sio ratiba za serikali na vyombo vyake.
5/ Kuhusu Hayati magufuli sizumgumzii chochote kila mmoja ameelewa code za Pole pole.
6/ Kuhusu Ndugai na kobe wa uvvccm kupandishwa juu ya mti ili kumtukana Ndugai na kumlazimisha ajiuzulu pia sisemi.Mtu yule kutoka kundi la mtandao anayeogopeka na kutisha. Aliyekwenda Dodoma kwa Ndugai na kumwambia jiuzulu na kisha mzee akasema.Nimekosa mimi...Nimekosa sana..Nisameewe huyo naye simzungumzii.Pole pole Amesema kundi hilo linatisha sana.
Hamphrey Pole pole you made my day.
Chadema wako sawa tukatae wahuni kwanza ndipo twende kwenye uchaguzi.This is our country.
Wale mnaodharau msimamo wa chadema muwe na adabu mmeelewa sasa nchi iko wapi.
Wale mnaosema wana chadema wanamezwa na hoja za pole pole muwe na adabu.Huyu jamaa ametujengea nguvu ya mapambano leo kiasi kwamba tunaona kabisa huu ndio mwaka wa mabadiliko.
Kataa wahuni ponyesha Tanzania.