Wana JF nawaomba ushauri wenu kuhusiana na jiji la Arusha kuwa chafu kupindukia! hakuna magari ya kubeba uchafu hivyo uchafu umetapakaa kila mahali. kumekuwa na vikao vya wananchi na madiwani wao kuzungumzia suala hilo lakini wale wenye magari wanadai kuwa wananchi hawalipi ada kwa ajili ya huduma hiyo lakini si kweli kwamba wote hawalipi kuna wanaolipa na wasiolipa. Nimekuwa najiuliza utaratibu gani utumike ili kuondokana na kadhia hii. Hali inatisha jamani kila pembe kuna lundo la takataka! Naamini michango yenu itafika kwa wahusika kwani wengi huwa wanachungulia humu.
Wana JF mnaoishi Arusha mtaniunga mkono kwa hili kwani hali halisi mnaijua.
Wana JF mnaoishi Arusha mtaniunga mkono kwa hili kwani hali halisi mnaijua.